Naamini kwa dhati kabisa nguvu ya Makonda haitokani na kuwa kwake katibu mwenezi wa CCM, lazima kuna chanzo kingine kinampa kujiamini kiasi hiki

Mawaziri na watendaji wanaolalamikiwa ni wateule/waajiriwa wa serikali ya CCM. Chama kimejaza mawaziri na bureaucracy kubwa serikalini. Hiyo ndiyo maana sahihi ya chama kuwa kazini; ndivyo chama kinavyodhibiti na kusimamia serikali. Kawaida, si sahihi kwa viongozi wa chama (except Rais) kuwa na mawasiliano ya moja kwa moja ya kikazi na watendaji wa serikali bali kupitia wateule wake wa kisiasa serikalini (mawaziri, RCs, DCs, etc.) nje ya ofisi za umma.

May seem complicated to many lakini huo ndio usahihi wenyewe.

Sasa hii ya Katibu Mwenezi wa CCM kutembea na misafara mikubwa na kuitisha mikutano ya hadhara yenye gharama kubwa kusikiliza malalamiko ya individuals dhidi ya viongozi na watendaji wa serikali ya CCM, ni ufujaji mkubwa wa hazina ya taifa usiokuwa na tija yoyote zaidi ya kupeana faraja ya kisaikolojia kwa watu wenye uwezo mdogo sana wa kufikiri.
Sasa wewe unadhani yeye hajui.inachoongea? Hao wanaoutwa wateule hakuna Cha maana wanafanya kumsaidia Rais ndio maana kampa Rungu Makonda.

Tumuone Sasa wa kumbishia
 
Mawazo huru!

Dola itakua imemwambia mama hatoshi,Kuna mtu anahitajika afanye kazi yako ,mtu kivuli,yaani Raise kiutendaji lakini sio kikatiba!!

Ndio makonda akaonekana anafaa na yeye ndio ana sauti nani apite au akatwe hapo 2025!!

Makonda ni Raid kivuli kabla hajawa Rais rasmi!

Source:- trust me broo!
Mchango wa Makonda katika watu kupotea na kutekwa na hata kuuwawa wakati wa Uraisi wa Magufuli unajulikana. Watu kama USA wana ushahidi wote ambao serikali iliambiwa kama wakibisha wako tayari kuuweka hadharani, wakaufyata mkia.

Ndio maana Samia alipokuwa raisi, pamoja na uhusiano wake wa karibu sana na Makonda, alimshauri Makonda asubiri kwanza hadi watu wasahau kidogo yaliyofanyika akiwa "Mkuu wa Mkoa" wa Dar es Salaam, japo Makonda alitaka apewe nafasi immediately.

Sasa kama kuna mwenda wazimu atafikiria Makonda anaweza kupewa nafasi ya uraisi, mtu ambaye ana tuhuma nzito za mauaji, basi siku hiyo ikitokea nitakuwa wa kwanza kushawishi watu kwamba demokrasia nchini haifanyi kazi tena na ni afadhali serikali itakayosimikwa kwa namna hiyo iondolewe madarakani hata kwa nguvu.

Hakuna sehemu popote kwenye vitabu vya uongozi panaposema kiongozi muuaji akichaguliwa kidemokrasia basi ni sawa tu aachwe asifanywe kitu. Hapana, dikteta yeyote, hata kama alichaguliwa kidemokrasia, anastahili kuondolewa kwa nguvu. Uchaguzi wa kidemokrasia ni wa siku moja, lakini uongozi wa kiongozi aliyechaguliwa ni wa miaka mitano. Huwezi kumvumilia kiongozi dikteta muuaji kwa miaka mitano eti kwa sababu alichaguliwa kidemokrasia. Alichaguliwa aue watu? Ondoa uchafu huo hata kwa mtutu wa bunduki.
 
Sasa umeanza kujipendekeza kwa Makonda ukitegemea kwamba labda kuna siku atapitishwa kuwa Raisi? Tuombe uhai, maana nachelea unaweza kufa kwa kuvunjika moyo. Samia anaweza kuwa alilazimisha Makonda kuwa katibu mwenezi japo alipingwa sana na viongozi wa CCM na wengine kutaka hata kumziria chama, lakini Samia akitaka kujua Watanzania bara wakoje aje ajaribu kulazimisha eti Makonda awe mteule wa CCM kugombea uraisi. Utaona mambo yatakayoanikwa hadharani.

Makonda hata azunguke vipi, kuna siku wanaomlinda watakapoondoka, atasimama kizimbani kujibu mauaji yote ya raia wasio na hatia aliyoyaplan na kuyasimamia.
 
Kwanza naunga mkono hoja, kuwa Mwenezi ni very powerful extra ordinarily, hiyo power anaipata kutoka kwa YEYE!. Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

Kuhusu anguko la CCM, naomba kutofautiana na wewe, badala ya CCM kuanguka, Makonda ameifanya CCM iamke, CCM sasa inapata!. Pongezi Paul Makonda kuifufua CCM kwa amsha amsha. Twende mdogomdogo ngoma ikivuma sana inakaribia kupasuka!
P
Pascal, nimekuelewa nadhani. Kwa tafsiri yangu nguvu ya YEYE inaweza kuwa ni abstract, kwa sababu binadamu tunaweza kuwa na nguvu na control juu ya mtu mwingine kutokana na nguvu ambazo ziko ndani yetu, ambazo sio lazima zianishwe kikatiba. Ni nguvu zinakuwa very powerful kiasi kama mtu anaweza kuwa hana kauli mbele ya influence ya hizo nguvu, kama vile kuwa chini ya hypnosis.

Pili, ni kweli kabisa CCM inapeta kwa sasa, na Makonda anachangia sana katika kupeta huko na hizo amsha amsha. Lakini pia tukumbuke amsha amsha inaweza ikawa amsha amsha inayoleta ngoma iliyovuma sana kupasuka. Mara nyingine watu wanasema usimwamshe mtu aliyelala, kwa sababu alipolala hakuwa conscious na lolote katika comfort zone ya usingizi wake, na akiamka anakuwa katika state ya kujiuliza na kufanya maamuzi

Mwalimu wangu wa physics, wakati tukisoma work done = force x distance, alisema ukijitwisha gunia la kilo 50 kichwani, ukatulia nalo sehemu moja hata kwa masaa kumi, hujafanya kazi. Baada ya Makonda kumaliza ziara zake za mikoa 20 (sidhani kama atathubutu kwenda Zanzibar), itakuwa kama gunia la kilo 20 alilojitwisha amelitua bila kuwa amelisogeza hata milimita moja. Gunia hilo ni matatizo ya watanzania yanayotokana na uongozi usiosimamia watendaji wa serikali ya CCM kuwajibika katika majukumu yao.

Workdone ya Makonda = Force x distance = 0,

japo force itakayokuwa imetumika ni kubwa sana. Sijaona namna yeyote tunayoweza kusema Makonda ametatua matatizo ya wananchi. Ukienda Shinyanga alikopita tayari, je hawana matatizo tena yanayotokana na uongozi wa mkoa usiowajibika? Labda tum-assess katika kuonyesha kwamba serikali iko mbali na wananchi katika kutatua matatizo yao, kitu ambacho Fereshi, in a very pathetic and mediocre way, amaejaribu kuki address.
 
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.

Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo wengine huko nyuma, lakini ni mara ya kwanza tunapata katibu mwenezi wa CCM ambae anaonyesha kujiamini kupita mamlaka yanayostahili ya katibu mwenezi wa CCM.

Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.

Leo hii katibu mwenyezi apewe bajeti, misafara ya magari, kuliko inavyokuwa kwa makamu mwenyekiti wa CCM au katibu mkuu wa CCM, kwa sababu gani? Kwamba katiba ya CCM imebadilishwa kisiri na hawa wote wameambiwa kuanzia sasa bosi wenu ni katibu mwenezi wa CCM? Pamoja na mawaziri? Wakuu wa mikoa? Mwanasheria Mkuu? Wenyeviti wa CCM wa mikoa?

Sote tunajua msemaji mkuu wa chama chochote anasema yale chama kilichoamua katika vikao vyake rasmi. Kuwa msemaji wa chama haina maana wewe ndio unakuwa unakisemea chama, hata siku moja. Kuwa katibu mwenyezi sio katika mpangilio wa vyeo vya chama, ni nafasi tu. Huwezi hata kusema katibu mwenezi wa CCM ni mkubwa kuliko mwenyekiti wa CCM wa mkoa. Lakini sio hivyo kwa Makonda. Yeye amejipa madaraka ambayo nadhani yanazidi hata ya kuwa makamu mwenyekiti wa CCM, au katibu mkuu wa CCM. Kujiamini huko kunatoka wapi? Mamlaka haya yanatoka wapi? Kwamba siku zote hatukujua kuwa katibu mwenezi wa chama ni mtu mkubwa namna hii? Ni kweli?

Nyie watu wa CCM, nyie mawaziri, nyie wakuu wa mikoa, tuambieni ukweli. Kinachowafanya muufyate Makonda akiunguruma ni nini hasa, Ukatibu mwenezi wa CCM? Na kwa nini sasa wenye akili tukiwauliza mbona mambo yako hivi, mnaishia kutabasamu tu bila kusema lolote? Kuna kitu gani msichotuambia?

Na niwaambie wazi nyie watu wa CCM. Kama nguvu ya Makonda sio ya kikatiba ndani ya CCM, kama kuna chanzo kingine kisicho rasmi kinampa nguvu na kujiamini kiasi hiki, basi anguko la CCM liko karibu sana!
Bashite kwa ubora wake. Baba kamrithisha mwanae toka kuzimu.
 
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.

Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo wengine huko nyuma, lakini ni mara ya kwanza tunapata katibu mwenezi wa CCM ambae anaonyesha kujiamini kupita mamlaka yanayostahili ya katibu mwenezi wa CCM.

Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.

Leo hii katibu mwenyezi apewe bajeti, misafara ya magari, kuliko inavyokuwa kwa makamu mwenyekiti wa CCM au katibu mkuu wa CCM, kwa sababu gani? Kwamba katiba ya CCM imebadilishwa kisiri na hawa wote wameambiwa kuanzia sasa bosi wenu ni katibu mwenezi wa CCM? Pamoja na mawaziri? Wakuu wa mikoa? Mwanasheria Mkuu? Wenyeviti wa CCM wa mikoa?

Sote tunajua msemaji mkuu wa chama chochote anasema yale chama kilichoamua katika vikao vyake rasmi. Kuwa msemaji wa chama haina maana wewe ndio unakuwa unakisemea chama, hata siku moja. Kuwa katibu mwenyezi sio katika mpangilio wa vyeo vya chama, ni nafasi tu. Huwezi hata kusema katibu mwenezi wa CCM ni mkubwa kuliko mwenyekiti wa CCM wa mkoa. Lakini sio hivyo kwa Makonda. Yeye amejipa madaraka ambayo nadhani yanazidi hata ya kuwa makamu mwenyekiti wa CCM, au katibu mkuu wa CCM. Kujiamini huko kunatoka wapi? Mamlaka haya yanatoka wapi? Kwamba siku zote hatukujua kuwa katibu mwenezi wa chama ni mtu mkubwa namna hii? Ni kweli?

Nyie watu wa CCM, nyie mawaziri, nyie wakuu wa mikoa, tuambieni ukweli. Kinachowafanya muufyate Makonda akiunguruma ni nini hasa, Ukatibu mwenezi wa CCM? Na kwa nini sasa wenye akili tukiwauliza mbona mambo yako hivi, mnaishia kutabasamu tu bila kusema lolote? Kuna kitu gani msichotuambia?

Na niwaambie wazi nyie watu wa CCM. Kama nguvu ya Makonda sio ya kikatiba ndani ya CCM, kama kuna chanzo kingine kisicho rasmi kinampa nguvu na kujiamini kiasi hiki, basi anguko la CCM liko karibu sana!
Naona unazinguka Sana : Makonda ni Mtoto wa Familia za Kawaida Kabisa za Kitanzania na anajua uchungu wa kuumizwa na Mafisadi papa na anajua wako wanaoendelea kuumia zaidi na zaidi kwasababu ya kupumbazwa na Taarifa za Fedha wakati Mwananchi wa Kawaida anachotaka kukiona ni Mazingira rafiki ya yeye kuishi. Na Ukiona Makonda una nongwa kwa Makonda jua ni sehemu ya kundi linalosababishia Wengine umasikini.
NB: Makonda anatakiwa kutiwa Moyo kwa Mambo makubwa anayoyafanya ya kuwakumbusha Watendaji mbalimbali wa Serikali (Wauza Duka) maana yeye ni sehemu ya Wenye Duka (CCM).
Na Kwa Mwendo wa Makonda naona Picha ya JPM na ndoto zake kwenda kutimia awamu hii ya 6. Samia hoyeeeee, Tanzania Hoyeeeee, Mkonda hoyeeeeee. Nisema tu Piga kazi Mpaka wakasirike
 
Sasa wewe unadhani yeye hajui.inachoongea? Hao wanaoutwa wateule hakuna Cha maana wanafanya kumsaidia Rais ndio maana kampa Rungu Makonda.

Tumuone Sasa wa kumbishia
Sijui kama unaelewa unachosema hapa? Jaribu kuweka mantiki katika hoja unayotoa. Not this.

Una maana Rais anateua mamia ya watu kufuja mabilioni ya serikali bila kufanya kazi ya maana hadi Makonda ategemewe kutenda hiyo “miujiza” yake kwa gharama kubwa zaidi?

Tunatangaziwa mara kwa mara Rais akiteua na kutengua. All in vain?

Anyway kwa vile Watanzania wameamua kutulia katika ujinga, acha CCM iendelee kuwacheza shere hadi kiama.
 
NB: Makonda anatakiwa kutiwa Moyo kwa Mambo makubwa anayoyafanya ya kuwakumbusha Watendaji mbalimbali wa Serikali (Wauza Duka) maana yeye ni sehemu ya Wenye Duka (CCM).
Na Kwa Mwendo wa Makonda naona Picha ya JPM na ndoto zake kwenda kutimia awamu hii ya 6. Samia hoyeeeee, Tanzania Hoyeeeee, Mkonda hoyeeeeee. Nisema tu Piga kazi Mpaka wakasirike
Kwa hiyo baada ya ziara ya Makonda Mbeya, mwezi ujao nikitembelea Mbeya nitakuta wananchi wa Mbeya hawana matatizo, kwa sababu Makonda alipita?

Unajua kuna watu hamna kabisa uwezo wa kutafakari, mnaona vitu kwa ukaribu sana? Wazungu wanasema "you don't see further than the end of your nose"
 
Sasa ulitaka makonda aje nyumbani kwako?au ni chuki na wivu umekujaa

Tarizo hamkutegemea makonda atapewa tena cheo ,Mlikuwa mnatembea na hukumu zenu mfukoni
Jambo moja ninakuunga mkono 100% ni kwamba hatukutegemea Makonda atapewa tena cheo, kama ilivyokuwa kwa wengi tu ndani ya CCM na ndio maana Samia alipata wakati mgumu kidogo kulazimisha Makonda ateuliwe. Watu wenye busara walimshauri lakini alikataa, na labda kwa sababu ya influence ya Makonda juu ya Samia pia. Hatujui kwa nini Samia aling'ang'ania sana lazima Makonda arudi.

For your information, hata watu kama ubalozi wa USA walishangaa sana. Si unakumbuka, walisema Makonda enzi za Magufuli alikuwa akiwanyima watu haki yao ya kuishi, na walikuwa na ushahidi. Unajua nikikunyima haki yako ya kuishi maana yake nitakufanya nini?
 
Anyway sina jibu lakini Makonda angalau anaonyesha njia kwamba kuinyoosha hii nchi inawezekana. Imagine tuna raisi, Makamu wa rais, Waziri mkuu, spika wa bunge na mawaziri na makatibu wakuu pamoja na wakuu wa mikoa na wenyeviti wa chama wenye ujasiri kama wa Makonda hii nchi ingenyooka tu. Tuendelee kumwombea Makonda na si kumponda.
 
Mimi binafsi yangu nitakua wa mwisho kuamini kile anachofanya mwenye cheo cha ukatibu mwenezi hadi pale zile kero zinazosemekana kwamba anaziskiliza kutoka kwa wananchi na kwamba anazichukulia hatua.
Ni muendelezo wa kile kinachoaminika kwamba sisi watanzania ni rahisi sana kusahau unapewa kofia ya "wananchi" halafu unapigia kura chama tawala
Yaani tumeshasahau swala la bandari, katiba, sasa tuko na makonda aaaaagh!!!!!
 
Naona sasa mmeanza kuweweseka kama kawaida yenu. Hata kabla ya kuwa mkuu wa wilaya na baadaye mkuu wa mkoa kila mmoja hakufahamu majukumu ya nafasi hizo, pamoja na mamlaka yake katika kuchochea maendeleo.ni mpaka alipoteuliwa mwamba mwenyewe Mheshimiwa Makonda kijana jasiri kusini mwa jangwa la sahara.

Mheshimiwa Makonda ni kijana jasiri na anayetambua majukumu yake.afanyayo ni majukumu yake kabisa. Chama ndicho kilichounda serikali na siyo serikali iliyounda chama. Ni chama kinachokwenda kwa wananchi kuomba kura na siyo serikali inayokwenda. Ni CCM Ndio itakayoulizwa maswali majukwaani na wananchi na siyo serikali.serikali ikiharibu kinachochukiwa ni chama kilichounda serikali na ndicho kitakacho adhibiwa kwenye sanduku la kura wakati wa uchaguzi.

Sasa kwa akili yako unataka chama kikawa kimya? Unataka chama kinyamaze bila kuwasemea watanzania? Unataka chama kisiende kwa wananchi kuwasikiliza kero zao na kuwapa majibu? Unataka wananchi wasipelekee kero zao kwa chama walichokichagua wao wenyewe?

Kwa akili yako hiyo hiyo unafirikiri chama kikianguka hao wakuu wa mikoa watabaki? Hao mawaziri watakuwepo ? Hao madc na na Ded watabakia? Sasa kwanini wasikiheshimu chama kilichowapa nafasi hizo kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM? Kwanini wasikumbushwe wajibu wao na majukumu yao katika kuwatumikia wananchi?
Kwa maelezo yako ni wazi kwamba Makonda ana baraka zote za Rais. Rais baada ya kuona hana ubavu wa kuwakoromea watendaji aliamua kumtafuta mtu wa kaliba ya Magufuli ila ambaye anammudu pia. Rais hakuwa ana uwezo wa kummudu Magufuli, ila anammudu vizuri Makonda. Kwa njia hii, Rais anafurahia tu kazi yake na milakati yake
 
Makonda ana kitu cha tofauti ndani yake, wakati ambapo watu wengi tulitarajia kwamba amepotea kwenye siasa, kaibuka na ndio gumzo sasa.

Kila nafasi atayopata hata ikiwa udiwani atang'aa sio kwasababu anafanya jambo la kipekee kuliko wengine, ila ana neema au charisma inayofanya awake.

Chadema wana vijana wengi makini kuliko Makonda, lakini wamelala, nakumbuka harakati za Marehemu kamanda Mawazo hakukaa kinyonge, he was vocal and bold, hata ukisikiliza hotuba zake utaona hilo.
 
Kawakojolea Chadema? Umeona katika ziara hata moja Makonda kawapigia simu Chadema? Anawakojolea watu wake hao hao wa CCM, mawaziri, wakuu wa mikoa nk, anaowaamrisha kesho uwe hapa, bila kujua huyo mtu kesho anaweza kuwa na appointment na raisi. Ndio maana kuna mmoja alisema mimi huyu hawezi kabisa kuniamrisha, ambapo ni kama kusema huyu hawezi kabisa kunikojolea!

Makonda anachofanya katika ziara zake ni kuonyesha udhaifu wa serikali ya CCM katika kusimamia uongozi wa nchi na kutatua matatizo ya wananchi. Lakini ni watu wenye akili tu kama kina Ftama Karume wanaona hilo, sio watu kama wewe na wengine wanaoshabikia hizi ziara. Wao hawaoni tatizo bali wanaona Makonda anasuluhisha.

Yaani Makonda akipita Mwanza na kusikiliza watu wawili au wanne, anakuwa ametatua matatizo yote ya wananchi wa Mwanza ndio maana anaenda Shinyanga? Hivi watu mmesoma shule gani?
👏👏👏👏✅✅✅✅
 
Makonda ananguvu zaidi ya Mama Abdul kwasasa.Ndio anakwenda hivyo,
Nihivi!!Makonda hafai hata kidogo lakini kwasasa nibora Makonda mara 100 kuliko Ccm yoote na baraza zima la Mawaziri.Sisemi Bunge mana bado ndani ya Bunge wapo wabunge wachache wenye nafuu zaidi ya Makonda.

Sent from my SM-A107M using JamiiForums mobile app
 
Deep state wamemweka hapo kuvunja nguvu ya Msoga at al.
Mkuu ulichoandika ndiyo ukweli wenyewe. Hata mimi simkubali Makonda kabisa na nina threads zangu nyingi humu.

Ila nilichokiona ni kwamba awali Mama alichukua watu wote alioelekezwa na Mstaafu wa Msoga na akawapa kazi kama akina Januari, Mchechu, Maharage, Nape, nk

Lakini watu hawa hawajamsaidia Rais Samia katika kufanya kazi, mfano ĥali ya TANESCO na giza tulilonalo.

Worse enough akaonekana Katibu Mkuu wa zamani Chongolo akiwa ana conspire na Team Msoga kutaka waweke mgombea mwingine mwaka 2025.

Kwa Tanzania ya sasa hatukubali tena Mstaafu wa Msoga ashiriki kutuonyesha nani anafaa kuwa Rais kwa kuwa hana uwezo na Samia kishajua hiyo conspiracy.
 
Back
Top Bottom