njiwa
JF-Expert Member
- Apr 16, 2009
- 12,360
- 5,474
Karibu Alliance in Motion GLOBAL tufanye biashara
Hahahahaha matapeli mshaanza mnatafuta watu desperate kama hawa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Karibu Alliance in Motion GLOBAL tufanye biashara
Ngedere, kabla ya kuacha tawi, HUWA ANAJUWA ANAKWENDA KUDANDIA TAWI LIPI. Maamuzi hayo ya kudandia tawi lipi huwa anayafanya kabla hajaachia tawi alilolishika wakati anafikiri....Habari wakuu wote wa jf
nawapenda sana hasa kwa mambo mazur nnayopata
Mmi ni mtumishi wa serikali kada ya elimu (mwl)
Sababu hasa ni hizi
1.interest au hob
Kiukweli hii kazi siipendi niliisomea bada ya kuwa sina otenative najitaidi niikubali but inashindikana so naona kama napoteza muda
2.kipato
Najua kuwa watumishi weng hasa awamu hii ya 5 weng wanalalamika hali ya uchumi but mmi naona hii yangu ni too much
Kiukweli najitahidi sana kujibana ila naona nashindwa, nashindwa kufanya hata mambo ya kawaida tu nikiwa kama baba natamani familiar yangu angalau iishi standard hata kias tu but huku nliko naona kama ndoto
Yan labda uwe mzee wa topup jambo ambalo naona pia ntaongeza ufukara mana ukiisha ndo utataabika kama nnavyoona wengine
Lengo la uzi huu ci kuwatangazia msimamo wangu bali ni kuwaomba wale ambao walishachukua maamuzi kama yangu au wanaotarajia hivyo waendlee kunipa moyo pia wote ambao watakua na wasaa basi wanisaidie kimawazo nifkie lengo langu
Naomba kuwaslisha
NB: Pls nmejitaidi kutumia lugha nzuri naomba bro o sister kama unanishaur bas lugha iwe ya kunielewesha isiwe ya kebehi au kunitusi kwan kuyaheshimu maamuzi ya mtu ni jambo la busara
Hapo alipo anateseka na familia alafu unamwambia akiachakazi atateseka. Mimi namshauli kwamba kama ameweza kuvumilia maisha ya ualimu basi anaweza kufanya kazi yoyote akapata pesa. Acha hiyo kazi kwa vike uipendi na haina maslahi na anzisha biashara ya chapati, uji, chain sehemu zenye msongamano mwingi wa watu na hiyo kazi ifanye 24 hours uwe unalala hapo kwasababu wateja ndo hao hao watu wanaoingia na kutoka. Tafuta sehemu kama mbezi mwisho, tegeta nyuki, au mikoani nenda stendi za mabasi. Wasafiri wengi hawana hela ya lodge na chakula akipata chapati/uji ndo imetoka. Hii biashara inapesa ila wanaoifanya kwavile wamepiguka hawana malengo ela inaishia hivyo hivyo lakini nafahamu watu wenye uhakika was kuingiza hata 80,000 kwa siku kama umejipanga na huna aibu utaajili wadada jinsi kijiwe kinavyochanganyaPole sana mkuu, ningekushauri kabla ya kuacha uwe umeshaimarisha kipato chako na una njia nyingine mbadala ama sivyo utaitesa familia yako na wewe mwenyew
Ushauri wa kweli kabisa usio hata chembe moja ya unafiki.Acha kazi mara moja, roho yako inayo kuongoza haiwezi kukupoteza, nilifanya huko kazi lakini mafanikio niiyapata kwa rushwa tu, tena rushwa ndefu, bila rushwa mshahara wao hautoshi, tena wanakubana sana kila asubuhi uko kazini, hata muda wa kufikiri huna, kariakoo unaisahau. sasa ningeishije kwa wizi ?mpaka lini? nikayakoroga yasije nikuta
Ujue hao wanaopata raha serikalini wana ma-godfather wao wana tanua sana, au kama unaweza ujipendekeze sana kiasi cha kujidhalilisha, na kufanyiwa ya hovyo,
Wale wenye godfather wanapewa semina na mishahra ina panda kama kawa, wanapanda madaraja, wanapewa nafasi nzuri hata wa chini yako anawezakuwa na mshahara mkubwa kuliko wewe ilimradi tu ana godfather. wakiona umemenunua gari, umejenga umeenda kusoma, wanakuzushia tu ili uhame au
wanakukatia mshahara kwa muda usojulikana bila sababau ilimradi tu utumie resources zako zote,
kwa kufidia pengo la mshahra, utafuatilia mpaka miguu iote kutu, na usisubili hayo yakukute ondoka mara moja, huko serikalini imejaa misukule mitupu, yana visukari, ma high BP, ni shida sana huko. labda magufuli ayaondoe kwa sasa.
Top layer ya serikalini itakupenda Kama unaishi kwa shida shida sana, huna mpango wa kwenda kujiendeleza (kusoma), mfano mlevi, teja( mlandukaji), mgonjwa wa ukimwi, hapo hutoki, lkn eti kijana una afya yako mjanja unadundulize hela yako unapojua mwenyewe, ujenge nyumba gari weeee! utaona kila rangi ya fitina.
Navyo kuona wewe tayari ni mjanja, umeshtuka ka mshahara kadogo, ina maana utatengeneza vyanzo vingine vya pesa, wakikujua tu tegemea hayo hapo juu, Yaani wanaweza lengesha rushwa tu, kuna mawili godfather akutose, au aendelee kukuunga mkono hivohivo, akihamishwa umeumia.
UKIKAA KAA KI MAGUTU SANA ISIVO KAWAIDA. yangu ni hayo!
kila la kheri!
Karibu Alliance in Motion GLOBAL tufanye biashara
Acha kumtia uogaUtaililia hiyo kazi nakuhakikishia
Ki kwenye ugumu ndio kuna chanceMshahara ni mtamu sana na ni wa uhakika kila mwezi.
Mimi sikushauri uache kazi , ila kama una wazo la biashara unaweza kufungua biashara yako na ukaweka msimamizi, huku ukitoka kazini unapitia kukagua.
Ila kuacha kazi , tena kama ni serekalini usiache , maisha ya biashara msimu huu wa Magu ni magumu sana.
Ajaribu aone,nakuakikishia atakuja Lia apa au kugugumia mwenyeweAcha kumtia uoga
Naungana na wenzangu wanakushauri vizuri sana pia kwa kuzingatia hali halisi.Yaani wamesimama kana kwamba ni wao wanataka kufanya kama wewe.Nawapongeza kwa kukujali.Kama kuupata mhimili kwasasa ni shida nakushauri usiache kazi. Ukiwa na kazi opportunities zinakuwa nyingi ila usipokuwa na kazi mambo yanagoma.
Cha kukushauri jaribu kutafuta namna ya kuongeza kipato ukiendelea na hiyo ajira yako ya sasa.