Naacha kazi serikalini

Naacha kazi serikalini

Habari wakuu wote wa jf
nawapenda sana hasa kwa mambo mazur nnayopata
Mmi ni mtumishi wa serikali kada ya elimu (mwl)

Sababu hasa ni hizi
1.interest au hob
Kiukweli hii kazi siipendi niliisomea bada ya kuwa sina otenative najitaidi niikubali but inashindikana so naona kama napoteza muda

2.kipato
Najua kuwa watumishi weng hasa awamu hii ya 5 weng wanalalamika hali ya uchumi but mmi naona hii yangu ni too much

Kiukweli najitahidi sana kujibana ila naona nashindwa, nashindwa kufanya hata mambo ya kawaida tu nikiwa kama baba natamani familiar yangu angalau iishi standard hata kias tu but huku nliko naona kama ndoto
Yan labda uwe mzee wa topup jambo ambalo naona pia ntaongeza ufukara mana ukiisha ndo utataabika kama nnavyoona wengine

Lengo la uzi huu ci kuwatangazia msimamo wangu bali ni kuwaomba wale ambao walishachukua maamuzi kama yangu au wanaotarajia hivyo waendlee kunipa moyo pia wote ambao watakua na wasaa basi wanisaidie kimawazo nifkie lengo langu

Naomba kuwaslisha

NB: Pls nmejitaidi kutumia lugha nzuri naomba bro o sister kama unanishaur bas lugha iwe ya kunielewesha isiwe ya kebehi au kunitusi kwan kuyaheshimu maamuzi ya mtu ni jambo la busara
Nimeipenda Sana hii. Ngoja nisome comment maana kama tulikua wote vile. Nataka kuukimbia utumwa.
 
Hajasema hicho ulichoandika wewe. Hebu soma vizuri mpe ushauri
Naona wengi mliorudishwa kufundisha shule za msingi mmepagawa sana!
Punguza stress wape madogo elimu kwani mshahara si ulele uliotoka nawo secondary!
 
Kabla hujaacha kazi hakikisha una mhimili wa kukuwezesha wewe na familia yako kusurvive.. Baada ya kujihakikishia hilo piga chini kacharike kivingine.

Bila kuzingatia hilo utazikumbuka zile 500 ulizokuwa ukizipata nwisho wa mwezi.
Chukua ushauri huu
 
Kama hali ndio hiyo we acha kazi kafanye mambo mengine, kuuliza watu si tija we nenda kapambane soon utaitwa oligarchy
 
Daah, kweli wewe una uzoefu wa hii kazi,umeongea ukweli mtupu,umeongelea yote ninayopitia na ninayoyaona. Mungu akubariki kwa kweli.
Acha kazi mara moja, roho yako inayo kuongoza haiwezi kukupoteza, nilifanya huko kazi lakini mafanikio niiyapata kwa rushwa tu, tena rushwa ndefu, bila rushwa mshahara wao hautoshi, tena wanakubana sana kila asubuhi uko kazini, hata muda wa kufikiri huna, kariakoo unaisahau. sasa ningeishije kwa wizi ?mpaka lini? nikayakoroga yasije nikuta

Ujue hao wanaopata raha serikalini wana ma-godfather wao wana tanua sana, au kama unaweza ujipendekeze sana kiasi cha kujidhalilisha, na kufanyiwa ya hovyo,

Wale wenye godfather wanapewa semina na mishahra ina panda kama kawa, wanapanda madaraja, wanapewa nafasi nzuri hata wa chini yako anawezakuwa na mshahara mkubwa kuliko wewe ilimradi tu ana godfather. wakiona umemenunua gari, umejenga umeenda kusoma, wanakuzushia tu ili uhame au

wanakukatia mshahara kwa muda usojulikana bila sababau ilimradi tu utumie resources zako zote,

kwa kufidia pengo la mshahra, utafuatilia mpaka miguu iote kutu, na usisubili hayo yakukute ondoka mara moja, huko serikalini imejaa misukule mitupu, yana visukari, ma high BP, ni shida sana huko. labda magufuli ayaondoe kwa sasa.

Top layer ya serikalini itakupenda Kama unaishi kwa shida shida sana, huna mpango wa kwenda kujiendeleza (kusoma), mfano mlevi, teja( mlandukaji), mgonjwa wa ukimwi, hapo hutoki, lkn eti kijana una afya yako mjanja unadundulize hela yako unapojua mwenyewe, ujenge nyumba gari weeee! utaona kila rangi ya fitina.

Navyo kuona wewe tayari ni mjanja, umeshtuka ka mshahara kadogo, ina maana utatengeneza vyanzo vingine vya pesa, wakikujua tu tegemea hayo hapo juu, Yaani wanaweza lengesha rushwa tu, kuna mawili godfather akutose, au aendelee kukuunga mkono hivohivo, akihamishwa umeumia.
UKIKAA KAA KI MAGUTU SANA ISIVO KAWAIDA. yangu ni hayo!

kila la kheri!
 
Ukiishi katika uoga hakika hautafanikiwa katika Maisha haya.
uoga ni adui mkubwa wa mafanikio.
Pia ujinga ni kung'ang'ana na kitu ambacho hakikunufaishi wala kukuletea mfanikio yoyote.
Fikiria umefanya kazi 5yrs but hauna hata nyumba wala gari.
Maisha yako kila kukisha yanazidi kuwa magumu sana.
But unazidi kung'ang'ana hukohuko. Huo ni ujinga mkubwa sana. Njoo tufanye ujasiriamali mkuu.
utateseka mwaka mmoja ila after 3ys utakuwa Tajiri mkubwa sana mwenye kipato kizuri sana.
Wekeza katika mambo madogo madogo mfano mradi wa chips, mgawahawa , sehemu ya kuuza pombe pamoja na kitimoto , ukumbi wa kuangalia mpira etc uone utakavyokuwa uaningiza hela mpaka utajuta kupoteza muda huko uliko.
Wewe unafanya kipi kati ya hivyo? Na status yako ya maisha ipoJe?
 
Mkuu Sauti uisikiayo kutoka nafsi yako ndio usahihi wako...


Mara zote public opinions za mambo yasioyo na ukawaida huwa ni negative .. Kwa maana kuwa haijazoeleka kuona mtu akiacha kazi na kufanya issues zake ... Tegemea kukutana na vitisho na kuvunjwa moyo..



Ila amini nakwambia kuajiriwa ni utumwa na hautakuja kuishi maisha ya ndoto yako kwa kuajiriwa. Utaishia saaaaNa kuishi maisha MAZURI na sio BORA.

Maisha Bora ni kuwa free na familia yako , kupata muda Wa kuumzika etc..



Ushauri wangu ni Sikiliza nafsi yako... Hakuna anaejua hali yako .. Wewe ndio unajijua Gap lako la maisha likoje kuwa kama ukiacha kazi utalifill vipi na kwa muda gani ...


Nakuomba utafute shughuli ya kufanya kabla ha kuacha kazi atleast miezi sita kabla ya kuacha kazi ... Katika kipindi hicho fanya Reformations za unavyoishi ili uanze kuadapt utakavyoishi kwa kujiajiri.. Kama ulikuwa kwa mwezi unatumia 200,000 kwa matumizi ya nyumbani jitahidi upunguze ..


Nunua friji uwe unanunua vifaa vyote kwa mwezi , gharama isiwe hiyo 200,000... Kama ulikuwa unakaa katikati ya mji na unalipa kodi kubwa , jitahidi uhamie nje ya mji kuna nyumba nzuri sana kwa bei nafuu sana na unaweza kupata hata sehemu kubwa ya kuanzisha mradi Wa ufugani Kuku na mayai ...


KwA ufupi nifanyie self assessment yako halafu njoo na Work plan yako ...



Amini nakwambia utapitia uchungu kwa kipindi kifupi ila utamu wake utakuwa Wa muda mrefu kuliko walioajiliwa ambao wanakuona hujielewi ..



Please Follow Where Your Heart Tells You To Follow.
Moja kati ya ushauri bora na mzuri kuliko zote katika thread hii

Nakupa kongolee mkuu
 
Mim naungana na baadhi ya washauri waliopita. kuwa chamsingi isikilize ile sauti ya moyo wako inavyokwambia kwa upole kabsaa" Lakin pia achana na "uwoga" wengi wetu tumekuwa watumwa kimawazo kuwa "serikalin ni serikalini" lakin kimsingi serikalin kuna ugumu wake hasa sisi ambao tunafanya kaz kwenye local govmnt halafu huna ukuu wa kitengo. natolea mfano mim ni muuguzi lakin pia mtoa dawa za usingiz hapa nilipo nafikiria kuondoka govment then naingia private sector huku nikiwa na lengo la kuwa karibu na biashara yangu. Hakuna sababu ya kubaki sehemu ambayo hakuna maslahi na wew.
Unaweza kushauriwa fanya subra. Ila watu hawajui kutofautisha kati ya subira na kupoteza mda. Waweza kujiona unafanya subira kumbe unapoteza mda.

Tupambane kaka mda ndo huu.
 
Hivi watu mnawezaje kuishi kwa kusoboneka ?? Hivi watu mnawezaje kuishi kwa kuteseka ??


Jamani tunaishi mara 1 duniani usiruhusu kuteseka Kisa kazi .. Maisha kwangu huwa siyaogopi kabisa ... Niliacha kazi account Yangu INA laki 3 and Niko fresh tu .. Sipendi kuamrishwa amrishwa hovyo kazini .. Sipendi makato ya hovyo kwenye salary.. Hizo ni sababu chache zilizofanya nijione sina vigezo vya kuajirika licha tangu nimemaliza chuo nilikuwa nimeajiriwa sehemu kadha wa kadhaa ..



Jamani Uoga ndio umasikini wako ... Endeleeni kusubiri mishahara ya tarehe 30 tu
 
Hivi watu mnawezaje kuishi kwa kusoboneka ?? Hivi watu mnawezaje kuishi kwa kuteseka ??


Jamani tunaishi mara 1 duniani usiruhusu kuteseka Kisa kazi .. Maisha kwangu huwa siyaogopi kabisa ... Niliacha kazi account Yangu INA laki 3 and Niko fresh tu .. Sipendi kuamrishwa amrishwa hovyo kazini .. Sipendi makato ya hovyo kwenye salary.. Hizo ni sababu chache zilizofanya nijione sina vigezo vya kuajirika licha tangu nimemaliza chuo nilikuwa nimeajiriwa sehemu kadha wa kadhaa ..



Jamani Uoga ndio umasikini wako ... Endeleeni kusubiri mishahara ya tarehe 30 tu
Ni tarehe 25 mkuu
 
Kuna Jamaa Siku anaacha kazi huko kwenye Taasisi mshahara ukaongezeka mara dufu mwezi uliofuata! Mi nakushauri uache kwa sababu na wewe unaweza kuwa unawazibia wenzako...
 
Binafsi sijawahii kuexperience situation kama hii lakini kama ingekuwa ndo naipitia basi ningechora mipangho yangu kama ifwatavyoo.
1.plan for my long term goals
hapa najua kabisa apart from this job nataka kuwa nani au napendelea kuwa nani ,so kwa wakati huo nipo kazini ningejikita zaidi kuhakikisha naanda vema sana njia yangu ya kufika huko napotaka kuwa,so ntakaa chini ntajipanga kisaikolojia,kiuchumi,kiafya na kiimani ili kuimarisha na kuhakikisha sipungukiwi power au kupata kikwazo cha aina chochote

mfano plan zako zikiwa kuwa mfanyabiashara na ww ndo unaajira eyo hapo ambayo unataka kuiacha,kwa plan namna hii lazima uanze kujikita katika kutambua fursa za biashra unayoota kuwa zinapatikana wapi,nini kinahitajika kuifanya,uanze wapi na uishie wapi,vikwazo na namna ya kuvitatua vikwazo

2.know how much time and budget needed
kama una uhakika wakupataa mkate wako hapo kila siku inakuwa ni rahsii sana kujipanga zaidi mdogo mdogo kuelekea katika ndoto yako ambapo utakuwa unajua kabisa nini chahitajika,kutokana na ile reserach yako ulioifanya mwanzo hapo .Mfano ushajua kuwa sasa unaweza kuanza biashara ya retail shop ,so hapo unaanza kujipanga na business cost na namna ya kuwekeza meaning the frame work ya eyo biashara .

Hakuna kitu chakuzingatia kama muda,unapoutumia muda vizuri utavuna kuliko kawaida , ila unavyoutumia tofauti na mavuno huwa kunyume na mategemeo.so point yangu kuu ni kuplan utatumia muda gani kufanikisha unajenga msingi wako.. ni miezi 6,9 au 12...

vitu vya kuzingatia

skills and mindset are necessary for success ,pia i do beleieve that prosperity can be archieved by anyone.

lastly success does not require a great deal of money,what requires is the belief and willingness to make a conscious investment in oneself
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom