Smart911
Platinum Member
- Jan 3, 2014
- 165,917
- 184,691
.Daaah kwa hiyo unataka kuniambia haya yote ninayoyaona ni kwamba hayapo ila tu nimefanywa kuyaona hivyo? Hapana! Waafrika tupo nyuma kwenye kila kitu. Najaribu kutazama juhudi zilizotumika wakati wa kudai uhuru na yake yaliyofanywa na viongozi mara baada ya kupata uhuru. Natazama rasilimali tulizo nazo na umasikini tulio nao. WAAFRIKA ni tatizo hapa duniani
Siyo kweli. Tunaaminishwa tujione ni tatizo. Nenda nchi za watu ujionee, kuna wafrica wengi sana ni mabingwa wa fani mbali mbali. Lakini tayari washapewa uraia wa huko ili wasikumbuke wala kurudi makwao na kuendeleza. Angalia vitu kama Facebook, instagtam,whastsapp, ni za kawaida sana lakini, zinavyopewa promo na kuwa habari ya dunia mzima. Lakini angalia app zilizotengenezwa Africa/na waafric nikikuambia unitajia hata kumi hufikishi. Lakini zipo nyingi na nzuri sana. Africa tunaweza na tunafanya makubwa sana. Tatizo mfumo. Huo mfumo umefanya hadi sisi kwa sisi tujione wajinga hatuwezi na kurudishana nyuma.