Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,232
- 12,733
Tafsiri ya kitabu The Autobiography of Malcom X. Unaweza kukisoma ndani ya Maktaba app.
Muandishi: Malcom X(Alex Haley), 1965.
Mtafsiri: Pictus Publishers ltd
Email: pictuspublishers@gmail.com.
Whatsapp: 0715278384
©Pictus Publishers Ltd2023.
Akisimama sehemu ambayo waliweza kuona hali yake ya ujauzito, aliwaambia kuwa alikuwa peke yake na wanawe watatu wadogo, na kuwa baba yangu alikuwa amesafiri, ameenda kuhubiri huko Milwaukee. Watu wale walitoa vitisho na onyo wakisema ni vyema tukahama mji haraka kwa sababu “Wakristo wema wa Kizungu” hawatavumilia kuona baba yangu “akifanya uchochezi” kati ya Manegro “wema” wa Omaha kwa kutumia mahubiri ya “kurudi Africa” ya Marcus Garvey.
Baba yangu, mchungaji Earl Little alikuwa ni mchungaji wa kanisa la Baptist, mfuasi mtiifu wa chama cha Marcus Aurelius Garvey, U.N.I.A(Universal Negro Improvement Association(Chama cha Kuwainua Watu Weusi Duniani)). Kwa msaada wa mitume kama baba yangu, Garvey kutoka katika makao yake makuu huko Harlem, New York-alikuwa akitoa mwito juu ya ubora wa watu weusi na akiuhimiza umma wa watu weusi kurudi Afrika, nyumbani kwa mababu zao-kampeni iliyomfanya Marcus Garvey kuwa mtu mweusi mtata zaidi dunaini.
Huku wakiendelea kutoa vitisho, wabaguzi wale waliamrisha farasi wao kukimbia kuizunguka nyumba huku wao wakivunja vioo vyote vya madirishani kwa vitako vya bunduki. Kisha wakaenda zao, mioto yao iking’aa gizani kama walivyokuja.
Baba yangu aliporudi alikasirika sana. Aliamua kusubiri mpaka nitakapozaliwa-na wakati ulikuwa karibu, kisha ahamishe familia yake. Sijajua kwa nini alifanya uamuzi huu maana hakuwa Mnegro muoga kama ambavyo wengi walikuwa nyakati hizo, na bado wengi wako hivyo hadi hii leo.
Baba yangu alikuwa na mwili mkubwa, urefu wa futi sita na nchi nne na mweusi ti. Alikuwa na jicho moja tu zima. Mpaka leo sijajua nini kililipata lile lingine. Alikuwa ni mzaliwa wa Reynolds, Georgia ambako aliacha shule baada ya darasa la tatu au la nne. Aliamini-kama alivyoamini Marcus Garvey, kuwa mtu mweusi hawezi kupata uhuru, kujitegemea na kujiheshimu ndani ya Marekani, hivyo inampasa mtu mweusi kumuachia mtu mweupe Marekani na yeye kurudi Afrika alikotokea. Moja ya sababu iliyofanya baba yangu kutumia muda wake na kuhatarisha maisha yake kusambaza falsafa hii kati ya watu wake ni kuwa alikuwa ameshuhudia kaka zake wanne kati ya sita wakiuawa kikatili. Watatu kati yao wakiuawa na wazungu, akiwemo mmoja kwa kuuliwa na umati. Kitu ambacho baba yangu hakujua wakati ule ni kuwa, kati ya watatu waliobaki, yeye akiwemo, ni mmoja tu-mjomba Jim ndiye atakufa kifo cha kawaida kitandani.
Baadaye, polisi wa kizungu wa kaskazini ya Marekani walimpiga risasi mjomba wangu Oscar. Na mwishowe baba yangu mwenyewe alikufa kwa mikono ya wazungu.
Siku zote imekuwa ni imani yangu kuwa mimi pia nitakufa kikatili. Nimefanya kila niwezalo kujiandaa.
Nilikuwa mtoto wa saba kwa baba yangu. Alikuwa na watoto wengine watatu kutoka kwenye ndoa yake ya kwanza, Ella, Earl na Mary walioishi Boston.
Alikutana na kumuoa mama yangu huko Philadelphia, na huko ndiko mtoto wao wa kwanza, kaka yangu mkubwa Wilfred alizaliwa. Walihama kutoka Philadelphia kwenda Omaha ambako Hilda na Philbert walizaliwa.
Kisha nikafuata. Mama yangu alikuwa na miaka ishirini na nane nilipozaliwa tarehe 19/5/1925, kwenye hospitali huko Omaha. Kisha tukahamia Milwaukee ambako Reginald alizaliwa.
Toka uchanga wake amekuwa na aina fulani ya ugonjwa wa ngiri ambao ulimsumbua maisha yake yote.
Mama yangu, Louise Little alizaliwa huko Grenada, British West Indies. Mama yangu alionekana kama mwanamke wa kizungu. Baba yake alikuwa ni mzungu.
Alikuwa na nywele ndefu nyeusi, na ongea yake haikuwa kama ya mtu mweusi. Sijui chochote juu ya baba yake mzungu zaidi ya kuwa alijisikia aibu kuzaliwa naye. Nakumbuka kumsikia akisema kwamba hajawahi kumuona. Na ni kwa sababu yake ndiyo maana nina rangi hii ya ngozi na nywele.
Nilikuwa ndiye mtoto mweupe zaidi katika familia yetu(Baadaye maishani nilipokuwa huko Boston na New York, nilikuwa kati ya mamilioni ya watu weusi ambao walikuwa wehu hadi kufikiri kuwa ilikuwa ni aina fulani ya hadhi kuwa na weupe-na kuwa mtu alikuwa na bahati kuzaliwa hivyo. Lakini badaye zaidi nilikuja kuchukia kila tone la damu ya mzungu yule mbakaji ndani yangu).
Familia yetu haikukaa sana huko Milwaukee maana baba yangu alitaka kuishi sehemu ambayo tungepanda vyakula vyetu wenyewe na ambako angeweza kuanzisha biashara, na kuishi kulingana na mafundisho ya Marcus Garvey ya kutotegemea wazungu. Kwa sababu fulani, tulienda Lansing, Michigan.
Baba yangu alinunua nyumba, na ndani ya muda mfupi, kama kawaida yake, akaanza kujitolea kuhubiri kwenye makanisa ya kibapstisti ya watu weusi yaliyokuwepo eneo letu, na siku za juma alikuwa akizunguka akitangaza maneno ya Marcus Garvey.
Alikuwa ameanza kutunza pesa kwa ajili ya duka ambalo siku zote alikuwa ametamani kumiliki, kisha, kama kawaida, watu weusi fulani wapumbavu wa jamii ya Uncle Tom(Vibaraka) wakaanza kupeleka maneno kwa wazungu juu ya muelekeo wake wa kimapinduzi. Safari hii kitisho cha kutakiwa kuhama mji kilitoka kwa kikundi cha wabaguzi kilichoitwa the Black Legion, hawa walivaa kanzu nyeusi badala ya nyeupe. Haikuchukua muda ikawa kila mahali ambako baba yangu alikwenda, wanachama wa Black Legion walikuwa wakimfuata ili kumuumbua kama mnegro “mwenye kujifanya” kwa sababu ya kutaka kwake kufungua duka, kwa kuishi nje ya eneo la Lansing lililotengwa kwa ajili ya watu weusi na kwa kuchochea vurugu na uasi kati ya watu “weusi wema.”
Kama ilivyokuwa Omaha, wakati huu mama yangu alikuwa mjamzito tena, wakati huu ilikuwa mimba ya dada yangu mdogo. Muda mfupi baada ya Yvonne kuzaliwa, ulifika usiku wa kutisha wa mwaka 1929, kumbukumbu yangu ya kwanza ambayo bado ipo. Nakumbuka ghafla kubebwa juu juu katikati ya vurugu za milio ya bastola, kelele, moshi na moto. Baba yangu alikuwa akifoka na kupiga risasi kuelekea wazungu wawili waliokuwa wamewasha moto na sasa wakikimbia. Nyumba yetu ilikuwa ikiungua.
Tulikuwa tukikanyagana na kugongana tukijaribu kujiokoa. Nusura nyumba imuangukie mama yangu akiwa na mtoto mkononi, alikimbia kupitia mlango wa uani huku nyuma yake nyumba ikianguka na kurusha cheche huku na kule. Nakumbuka tukiwa nje usiku tukiwa na nguo zetu za ndani, tukilia na kupiga kelele. Polisi na askari wa zimamoto wa kizungu walifika na kusimama wakiangalia nyumba ikiteketea hadi chini.
Marafiki kadhaa walimsaidia baba yangu kutupa hifadhi na nguo kwa muda; kisha akatuhamishia kwenye nyumba fulani pembezoni mwa Mashariki ya Lansing. Wakati huo watu weusi hawakuruhusiwa kuwepo katikati ya Lansing Mashariki baada ya giza kuingia.
Huko ndiko ambako chuo kikuu cha Jimbo la Michigan kilikuwepo: nilisimulia haya yote nilipozungumza na wanafunzi wa chuo hicho mwezi wa kwanza mwaka 1963(Na nilikutana na mdogo wangu Robert baada ya kipindi kirefu cha kutoonana, alikuwa pale akichukua masomo ya juu ya saikolojia).
Niliwaeleza jinsi ambavyo Lansing Mashariki ilitunyanyasa hadi tukalazimika kuhama tena, wakati huu tukienda maili mbili nje ya mji. Huko ndiko ambako baba yetu kwa mikono yake mwenyewe alitujengea nyumba ya vyumba vinne.
Huko ndiko nilikoanza kukumbuka mambo, hiyo ndiyo nyumba niliyokulia.
Nakumbuka baada ya tukio la moto, baba yangu aliitwa na kuhojiwa juu ya kibali cha bastola ambayo alifyatulia wazungu wawili waliowasha moto.
Nakumbuka mara nyingi polisi walikuwa wakifika nyumbani kwetu na kurusha vitu huku na kule, wakitafuta bastola. Bastola waliyokuwa wakiitafuta, ambayo hawakuwahi kuipata, na ambayo hawangeweza kumpa baba yangu kibali cha kuimiliki-ilikuwa imeshonewa ndani ya mto.
Lakini bunduki ya baba yangu na gobole lake vilikuwa peupe tu; kila mtu alikuwa navyo kwa ajili ya kuwindia ndege, sungura na wanyama wengine.
Baada ya hapo, kumbukumbu zangu ni juu ya mizozo kati ya baba na mama yangu.
Ilionekana kama walizozana muda wote. Wakati mwingine baba yangu alimpiga mama. Pengine ilitokana na kuwa mama yangu alikuwa na elimu nzuri.
Sijui alikoipata, lakini nafikiri mwanamke mwenye elimu hawezi zuia kishawishi cha kumsahihisha mwanaume asiye na elimu. Mara moja moja alikuwa akimsahihisha naye baba hakusita kumkunja.
Baba yangu alikuwa pia mkali sana kwa watoto wake wote isipokuwa mimi. Ndugu zangu wakubwa walipigwa kikatili kila walipovunja sheria zake-na alikuwa na sheria nyingi hivyo haikuwa rahisi kuzifahamu zote.
Karibu vipigo vyangu vyote vilitoka kwa mama yangu. Nimejiuliza sana kwa nini? Naamini kabisa kuwa, pamoja na kuwa baba yangu alikuwa mpinga wazungu, lakini kwenye akili yake alikuwa ameathirika na mtazamo wa wazungu kiasi kwamba alipendelea watoto weupe, na kati ya watoto wake mimi ndiye niliyekuwa mweupe zaidi.
Wazazi wengi weusi wa wakati huo walikuwa wakiwatendea watoto weupe kwa upendeleo kuliko wale weusi. Hii ilitoka moja kwa moja wenye utamaduni wa wakati wa utumwa kuwa “chotara” kwa sababu alikuwa anafanana na mtu mweupe kwa karibu, basi alikuwa bora.
Kumbukumbu zangu nyingine mbili juu ya baba yangu ni nje ya nyumbani. Moja ni juu ya kazi yake kama mhubiri wa Kibapstisti. Hakuwahi kuwa mchungaji mwenye kanisa lake mwenyewe; siku zote alikuwa ni “mhubiri mualikwa” nakumbuka mahubiri yake maarufu aliyopendelea sana, “treni ndogo nyeusi inakuja. . . na ni vyema ukaweka mambo yako yote sawa!” Nadhani kuwa hili lilihusiana na kampeni ya Marcus Garvey ya kurudi Afrika, ikiwa na kaulimbiu, “Treni nyeusi kuelekea nyumbani.” Philbert, kaka yangu ambaye alikuwa amenipita umri kidogo tu, alipenda sana habari za kanisa, lakini mimi zilinichanganya na kunishangaza.
Nilikuwa nikikaa nimemtumbulia macho baba yangu akiruka na kufoka alipokuwa akihubiri huku kanisa zima likiruka na kupiga kelele nyuma yake, likiwa limejitoa roho na mwili kwenye kuimba na kusali.
Hata katika umri huo mdogo, sikuweza kuamini dhana ya Wakristo kuwa Yesu ana uungu. Na hakuna mtu yeyote wa kidini, hadi nilipokuwa mtu mzima wa miaka ishirini-na baadaye nikiwa gerezani, aliyeweza kunieleza chochote.
Niliwaheshimu kidogo sana watu waliowakilisha dini.
Ni kupitia kazi yake hii ya uhubiri ndipo baba yangu aliweza kukutana na watu wengi weusi walioishi Lansing.
Niamini ninapokuambia kuwa Manegro wale walikuwa na hali mbaya sana wakati huo. Bado hata sasa wana hali mbaya-japo ni kwa namna nyingine. Kwa kusema hivyo, namaanisha kuwa sijawahi kuona mji ambayo una asilimia kubwa zaidi ya watu weusi wanaoitwa wa “daraja la kati” walioridhika na waliopotoshwa –watu weusi watafuta hadhi na kuchangamana.
Hivi karibuni nilikuwa nimesimama kwenye sehemu ya mapokezi ya Umoja wa Mataifa nikiongea na balozi kutoka nchi ya Afrika na Mke wake. Mtu mweusi mmoja alinifuata na kusema, “Unanifahamu?”
nillifedheheka kidogo sababu nilifikiri labda ni mtu ninayepaswa kumfahamu. Kumbe ni mmoja wa wale Manegro wa “daraja la kati” wanaojisifu na kuridhika kutoka Lansing. Sikujisikia vizuri.
Alikuwa ni aina ya mtu mweusi ambaye kamwe hangeweza kujihusisha na Afrika hadi pale kitendo cha kuwa na rafiki wa kiafrika kilipokuwa kama fasheni kati ya watu weusi wa “daraja la kati.”
Zamani nilipokuwa nakua, watu weusi wa Lansing waliokuwa na “mafanikio” walikuwa ni wahudumu na wang’arisha viatu.
Kuwa mfanya usafi kwenye duka fulani mjini ilifanya mtu aheshimike sana. Watu wa “maana,” “wakuu,” “wasemaji wa watu weusi,” walikuwa ni wahudumu wa Lansing Country Club na wang’arisha viatu kwenye makao makuu ya jimbo.
Watu weusi pekee waliokuwa na pesa kiukweli walikuwa ni wachezesha kamari au ambao kwa namna fulani waliishi kwa kunyonya masikini zaidi, na masikini walikuwa wengi sana. Wakati ule hakuna mtu mweusi aliyeajiriwa na kiwanda cha magari cha Lansing au kiwanda cha Reo. (Unakumbuka magari ya Reo? Yalitengenezwa Lansing na R. E. Olds, mtu ambaye yaliitwa jina lake, aliishi Lansing. Vita ilipoingia, waliajiri wafanya usafi kadhaa weusi.) Sehemu kubwa ya watu weusi ilitegemea msaada wa serikali, au W.P.A(Works Projects Adminstration)., au iliteseka kwa njaa.
Siku ilifika ambayo familia yetu ilikuwa masikini hadi tulikula tundu la donati; lakini wakati huo tulikuwa na hali nzuri kidogo kulinganisha na watu weusi wengine. Sababu kubwa ni kuwa tulizalisha sehemu kubwa ya chakula chetu wenyewe huko nje ya mji tulikokuwa.
Tulikuwa na afadhali kuliko watu weusi wa mjini ambao walipiga kelele, kama baba yangu alivyosema kwenye mahubiri yake, juu ya keki angani na mbingu yao baadaye wakati mzungu anayo yake hapahapa duniani.
Nilifahamu kuwa michango ambayo baba yangu alipata kwenye kazi yake ya kuhubiri ndiyo hasa ilitulisha na kutuvisha, na pia alifanya kazi zingine za ajabu, lakini picha yake inayofanya nijivunie zaidi ni harakati na upambanaji wake juu ya maneno ya Marcus Garvey.
Pamoja na udogo wangu niliokuwa nao, nilifahamu kutokana na niliyosikia kwamba baba yangu alikuwa akiongea mambo yaliyomfanya awe “shupavu.” Nakumbuka mwanamke mzee mmoja akitabasamu na kumwambia baba yangu, ‘Unawaogopesha wazungu, wako karibu kufa.’
Moja ya sababu zinazofanya nihisi kuwa baba yangu alikuwa akinipendelea ni kuwa, kulingana na kumbukumbu zangu, ilikuwa ni mimi tu ndiye aliyenichukua kwenda naye kwenye mikutano ya chama cha Garvey, U. N. I. A ambayo aliifanya kwa siri kwenye nyumba za watu tofautitofauti. Mikutano hiyo haikuwa na watu wengi, hawakuzidi ishirini.
Lakini hao walikuwa ni wengi sana kwenye sebule ya mtu. Nilitambua walivyokuwa tofauti wakati wa mikutano hii japo ni watu walewale waliokuwa wakiruka na kupiga kelele kanisani. Kwenye mikutano hii, wote-kutia ndani baba yangu, walikuwa makini sana, wenye akili zaidi na wanyenyekevu. Hili lilinifanya nami nijihisi namna hiyohiyo.
Nakumbuka kusikia, “Adam alifukuzwa kwenye bustani ya Eden kwenda kwenye mapango ya Ulaya,” “Afrika kwa waafrika,” ‘Waethiopia amkeni!” Kisha baba yangu angeongea kwamba haitachukua muda mrefu Afrika yote itaongozwa na mtu mweusi. Alipendelea kutumia neno “mtu mweusi” badala ya Negro.
“Hakuna anayejua wakati ambao saa ya ukombozi wa afrika itafika. Ipo kwenye upepo inakuja. Siku moja, kama tufani itafika.”
Nakumbuka kuona picha kubwa za kung’aa za Marcus Garvey zikipitishwa kwa kupasiana mikononi. Baba alikuwa na bahasha kubwa ya kuzihifadhi ambayo mara zote aliibeba kwenye mikutano hii. Kwenye picha zile, niliona kama mamilioni ya watu weusi wakiwa wamesongamana nyuma ya Marcus Garvey aliyekuwa amepanda gari zuri sana.
Mtu mweusi mkubwa akiwa amevalia sare nadhifu iliyokuwa na mapambo ya dhahabu, na pia alivalia kofia nzuri ikiwa na manyoya marefu. Nakumbuka nilisikia kuwa ana wafuasi weusi si tu katika Marekani bali duniani kote, na nakumbuka jinsi mikutano ilivyoisha mara nyingi kwa baba yangu kusema, huku watu wakimfuatisha; “Simama ewe mtu mkuu, utatimiza unachotaka!”
Sijawahi elewa kwanini baada ya kusikia mambo haya, kwa namna fulani, wakati huo; sikufikiria juu ya watu weusi wa Afrika. Picha yangu juu ya Afrika wakati huo ilikuwa ni washenzi walio uchi, wala watu, nyani, simba na misitu yenye joto.
Kwenye ziara zake baba yangu alitumia gari yake kuukuu iliyokuwa na rangi nyeusi, wakati mwingine alinichukua na tukaenda wote kwenye maeneo mbalimbali yaliyozunguka Lansing. Nakumbuka mkutano mmoja wa mchana(Mikutano mingi ilifanyika usiku) kwenye mji wa Owosso, umbali wa maili arobaini kutoka Lansing, mji ambao watu weusi waliuita “Mji mweupe” (Jambo kubwa ambalo Owosso ilijivunia ni kuwa mji wa Thomas. E. Dewey).
Kama ilivyokuwa East Lansing, watu weusi hawakuruhusiwa kutembea usiku, ndiyo sababu ya kufanya mkutano mchana. Na ukweli ni kuwa, miji mingi ya Michigan ilikuwa hivyo wakati huo. Kila mji ulikuwa na watu weusi wachache walioishi hapo. Wakati mwingine ilikuwa ni familia moja tu, kama ilivyokuwa kwenye makao makuu ya county, Mason. Huko kulikuwa na familia moja tu ya watu weusi, familia ya Lyon. Bwana Lyon alikuwa ni mcheza mpira maarufu wa shule ya sekondari ya Mason, aliheshimika sana huko Mason. Sa sasa alikuwa akiishi mjini humo akifanya vibarua vya hapa na pale.
Wakati huo mama yangu alionekana kama vile muda wote alikuwa akifanya kazi, akipika, akifua, akipiga pasi, akisafisha nyumba na kupigishana kelele na sisi watoto wake nane, na kawaida alikuwa akibishana au amenuniana na baba yangu. Moja ya chanzo cha mizozo yao ilikuwa ni mama yangu kuwa na msimamo mkali juu ya vitu ambavyo hataki kula, na wala hataki sisi tule, mfano nguruwe na sungura, vitu ambavyo baba yangu alivipenda sana.
Alikuwa ni mtu mweusi kutoka Georgia na aliamini katika kula vya kutosha chakula ambacho hapa Harlem tunaita “Chakula cha roho.”
Nimesema kuwa mama yangu ndiye aliyekuwa akinichapa-Lakini ilimbidi kufanya hivyo wakati ambao angeepuka aibu kutoka kwa majirani ambao wangeweza dhani kuwa alikuwa akitaka kuniua.
Kila alipojaribu kuinua mkono kunichapa, nilifungua mdomo na kupiga kelele za kufanya dunia yote ijue. Kama kuna mtu alikuwa anapita barabarani, basi angehairisha au angenichapa fimbo chache tu.
Nikiwaza kuhusu hilo leo, nahisi kuwa, kama ambavyo baba yangu alinipendelea kwa kuwa mweupe kuzidi wengine, mama yangu aliniadhibu vikali kwa sababu hiyohiyo.
Yeye mwenyewe alikuwa mweupe lakini aliwapendelea watoto waliokuwa weusi zaidi. Nafahamu kuwa kipenzi chake alikuwa ni Wilfred.
Nakumbuka alikuwa akiniambia nitoke ndani na “Acha miale ya jua ikupige ili upate rangi kidogo.”
Bidii yake katika kunifanya nisijihisi bora kutokana na rangi yangu ilivuka mipaka. Nina hakika alinitendea hivi kutokana na jinsi yeye mwenyewe alivyopata kuwa mweupe.
Nilijifunza mapema maishani kuwa kupiga kelele kunaweza kusaidia. Kaka zangu wakubwa na dada yangu walikuwa wameanza shule, wakati mwingine walikuwa wakirudi toka shule na kuomba biskuti zenye siagi au kitu fulani, kwa mkato mama yangu aliwajibu hapana. Lakini mimi nikikataliwa nililia na kufanya fujo mpaka nipate ninachotaka. Nakumbuka vizuri mama yangu akiniuliza kwa nini siwi mtoto mwema kama Wilfred; lakini nilijiambia mwenyewe, Wilfred kwa kuwa mwema na mkimya kulimfanya ashinde njaa mara nyingi. Hivyo basi, ingali bado mdogo sana nilijifunza kuwa kama unataka kitu fulani ni vyema ukapiga kelele.
Hatukuwa tu na bustani kubwa, bali pia tulifuga kuku. Baba yangu alinunua vifaranga na mama alivilea. Sote tulipenda kuku. Hicho ndicho chakula pekee ambacho hakukuwa na ubishani kati ya mama na baba. Kitu kimoja ambacho kinanifanya nimshukuru mama yangu ni hiki, siku moja nilimfuata na kumuomba niwe na bustani yangu na akaniruhusu kuwa na kitalu changu mwenyewe.
Nilikipenda na nilikihudumia vizuri sana. Nilipenda zaidi kupanda njegere. Nilijivuna sana tulipozila mezani petu. Niling’oa magugu kwenye bustani yangu kwa mikono mara tu yalipochomoza.
Nilikagua matuta nikiwa nimepiga magoti kuangalia minyoo na wadudu. Niliwaua na kuwazika. Wakati mwingine ambapo kila kitu kilikuwa safi na sina cha kupanda, nililala katikati ya matuta na kuangalia anga la bluu na mawingu yanayosafiri huku nikiwaza mambo mbalimbali.
Baada ya kufikisha miaka mitano nami pia nikaanza shule, nikiondoka nyumbani asubuhi pamoja na Wilfred, Hilda na Philbert. Shule yetu ilianzia chekechea hadi darasa la nane.
Ilikuwa umbali wa maili mbili kutoka mjini, nafikiri hakukuwa na shida sisi kusoma pale kwa sababu tulikuwa ndiyo watu weusi pekee kwenye eneo lile.
Kipindi hicho wazungu wa kaskazini walikuwa na kawaida ya”kuasili” watu weusi wachache kwenye jamii yao; hawakuwaona kama kitisho. Watoto wa kizungu hawakutufanyia ubaguzi mkubwa. Walituita “nigger” “weusi” na “Rastus” mara nyingi kiasi kwamba tulidhani hayo ndiyo majina yetu ya asili. Lakini hawakusema hivyo wakiwa na lengo la kututusi, ni namna tu waliyofikiria kutuhusu.
Muandishi: Malcom X(Alex Haley), 1965.
Mtafsiri: Pictus Publishers ltd
Email: pictuspublishers@gmail.com.
Whatsapp: 0715278384
©Pictus Publishers Ltd2023.
Sura ya kwanza
JINAMIZI
Mama yangu alinisimulia kuwa alipokuwa na mimba yangu, usiku mmoja kundi la wabaguzi wa rangi la Ku Klux Klan lilifika kwa farasi nyumbani kwetu huko Omaha, Nebraska. Waliizingira nyumba yetu huku wakionyesha bunduki zao, walipiga kelele wakimtaka baba yangu atoke nje. Mama yangu alienda mlangoni na kufungua.JINAMIZI
Akisimama sehemu ambayo waliweza kuona hali yake ya ujauzito, aliwaambia kuwa alikuwa peke yake na wanawe watatu wadogo, na kuwa baba yangu alikuwa amesafiri, ameenda kuhubiri huko Milwaukee. Watu wale walitoa vitisho na onyo wakisema ni vyema tukahama mji haraka kwa sababu “Wakristo wema wa Kizungu” hawatavumilia kuona baba yangu “akifanya uchochezi” kati ya Manegro “wema” wa Omaha kwa kutumia mahubiri ya “kurudi Africa” ya Marcus Garvey.
Baba yangu, mchungaji Earl Little alikuwa ni mchungaji wa kanisa la Baptist, mfuasi mtiifu wa chama cha Marcus Aurelius Garvey, U.N.I.A(Universal Negro Improvement Association(Chama cha Kuwainua Watu Weusi Duniani)). Kwa msaada wa mitume kama baba yangu, Garvey kutoka katika makao yake makuu huko Harlem, New York-alikuwa akitoa mwito juu ya ubora wa watu weusi na akiuhimiza umma wa watu weusi kurudi Afrika, nyumbani kwa mababu zao-kampeni iliyomfanya Marcus Garvey kuwa mtu mweusi mtata zaidi dunaini.
Huku wakiendelea kutoa vitisho, wabaguzi wale waliamrisha farasi wao kukimbia kuizunguka nyumba huku wao wakivunja vioo vyote vya madirishani kwa vitako vya bunduki. Kisha wakaenda zao, mioto yao iking’aa gizani kama walivyokuja.
Baba yangu aliporudi alikasirika sana. Aliamua kusubiri mpaka nitakapozaliwa-na wakati ulikuwa karibu, kisha ahamishe familia yake. Sijajua kwa nini alifanya uamuzi huu maana hakuwa Mnegro muoga kama ambavyo wengi walikuwa nyakati hizo, na bado wengi wako hivyo hadi hii leo.
Baba yangu alikuwa na mwili mkubwa, urefu wa futi sita na nchi nne na mweusi ti. Alikuwa na jicho moja tu zima. Mpaka leo sijajua nini kililipata lile lingine. Alikuwa ni mzaliwa wa Reynolds, Georgia ambako aliacha shule baada ya darasa la tatu au la nne. Aliamini-kama alivyoamini Marcus Garvey, kuwa mtu mweusi hawezi kupata uhuru, kujitegemea na kujiheshimu ndani ya Marekani, hivyo inampasa mtu mweusi kumuachia mtu mweupe Marekani na yeye kurudi Afrika alikotokea. Moja ya sababu iliyofanya baba yangu kutumia muda wake na kuhatarisha maisha yake kusambaza falsafa hii kati ya watu wake ni kuwa alikuwa ameshuhudia kaka zake wanne kati ya sita wakiuawa kikatili. Watatu kati yao wakiuawa na wazungu, akiwemo mmoja kwa kuuliwa na umati. Kitu ambacho baba yangu hakujua wakati ule ni kuwa, kati ya watatu waliobaki, yeye akiwemo, ni mmoja tu-mjomba Jim ndiye atakufa kifo cha kawaida kitandani.
Baadaye, polisi wa kizungu wa kaskazini ya Marekani walimpiga risasi mjomba wangu Oscar. Na mwishowe baba yangu mwenyewe alikufa kwa mikono ya wazungu.
Siku zote imekuwa ni imani yangu kuwa mimi pia nitakufa kikatili. Nimefanya kila niwezalo kujiandaa.
Nilikuwa mtoto wa saba kwa baba yangu. Alikuwa na watoto wengine watatu kutoka kwenye ndoa yake ya kwanza, Ella, Earl na Mary walioishi Boston.
Alikutana na kumuoa mama yangu huko Philadelphia, na huko ndiko mtoto wao wa kwanza, kaka yangu mkubwa Wilfred alizaliwa. Walihama kutoka Philadelphia kwenda Omaha ambako Hilda na Philbert walizaliwa.
Kisha nikafuata. Mama yangu alikuwa na miaka ishirini na nane nilipozaliwa tarehe 19/5/1925, kwenye hospitali huko Omaha. Kisha tukahamia Milwaukee ambako Reginald alizaliwa.
Toka uchanga wake amekuwa na aina fulani ya ugonjwa wa ngiri ambao ulimsumbua maisha yake yote.
Mama yangu, Louise Little alizaliwa huko Grenada, British West Indies. Mama yangu alionekana kama mwanamke wa kizungu. Baba yake alikuwa ni mzungu.
Alikuwa na nywele ndefu nyeusi, na ongea yake haikuwa kama ya mtu mweusi. Sijui chochote juu ya baba yake mzungu zaidi ya kuwa alijisikia aibu kuzaliwa naye. Nakumbuka kumsikia akisema kwamba hajawahi kumuona. Na ni kwa sababu yake ndiyo maana nina rangi hii ya ngozi na nywele.
Nilikuwa ndiye mtoto mweupe zaidi katika familia yetu(Baadaye maishani nilipokuwa huko Boston na New York, nilikuwa kati ya mamilioni ya watu weusi ambao walikuwa wehu hadi kufikiri kuwa ilikuwa ni aina fulani ya hadhi kuwa na weupe-na kuwa mtu alikuwa na bahati kuzaliwa hivyo. Lakini badaye zaidi nilikuja kuchukia kila tone la damu ya mzungu yule mbakaji ndani yangu).
Familia yetu haikukaa sana huko Milwaukee maana baba yangu alitaka kuishi sehemu ambayo tungepanda vyakula vyetu wenyewe na ambako angeweza kuanzisha biashara, na kuishi kulingana na mafundisho ya Marcus Garvey ya kutotegemea wazungu. Kwa sababu fulani, tulienda Lansing, Michigan.
Baba yangu alinunua nyumba, na ndani ya muda mfupi, kama kawaida yake, akaanza kujitolea kuhubiri kwenye makanisa ya kibapstisti ya watu weusi yaliyokuwepo eneo letu, na siku za juma alikuwa akizunguka akitangaza maneno ya Marcus Garvey.
Alikuwa ameanza kutunza pesa kwa ajili ya duka ambalo siku zote alikuwa ametamani kumiliki, kisha, kama kawaida, watu weusi fulani wapumbavu wa jamii ya Uncle Tom(Vibaraka) wakaanza kupeleka maneno kwa wazungu juu ya muelekeo wake wa kimapinduzi. Safari hii kitisho cha kutakiwa kuhama mji kilitoka kwa kikundi cha wabaguzi kilichoitwa the Black Legion, hawa walivaa kanzu nyeusi badala ya nyeupe. Haikuchukua muda ikawa kila mahali ambako baba yangu alikwenda, wanachama wa Black Legion walikuwa wakimfuata ili kumuumbua kama mnegro “mwenye kujifanya” kwa sababu ya kutaka kwake kufungua duka, kwa kuishi nje ya eneo la Lansing lililotengwa kwa ajili ya watu weusi na kwa kuchochea vurugu na uasi kati ya watu “weusi wema.”
Kama ilivyokuwa Omaha, wakati huu mama yangu alikuwa mjamzito tena, wakati huu ilikuwa mimba ya dada yangu mdogo. Muda mfupi baada ya Yvonne kuzaliwa, ulifika usiku wa kutisha wa mwaka 1929, kumbukumbu yangu ya kwanza ambayo bado ipo. Nakumbuka ghafla kubebwa juu juu katikati ya vurugu za milio ya bastola, kelele, moshi na moto. Baba yangu alikuwa akifoka na kupiga risasi kuelekea wazungu wawili waliokuwa wamewasha moto na sasa wakikimbia. Nyumba yetu ilikuwa ikiungua.
Tulikuwa tukikanyagana na kugongana tukijaribu kujiokoa. Nusura nyumba imuangukie mama yangu akiwa na mtoto mkononi, alikimbia kupitia mlango wa uani huku nyuma yake nyumba ikianguka na kurusha cheche huku na kule. Nakumbuka tukiwa nje usiku tukiwa na nguo zetu za ndani, tukilia na kupiga kelele. Polisi na askari wa zimamoto wa kizungu walifika na kusimama wakiangalia nyumba ikiteketea hadi chini.
Marafiki kadhaa walimsaidia baba yangu kutupa hifadhi na nguo kwa muda; kisha akatuhamishia kwenye nyumba fulani pembezoni mwa Mashariki ya Lansing. Wakati huo watu weusi hawakuruhusiwa kuwepo katikati ya Lansing Mashariki baada ya giza kuingia.
Huko ndiko ambako chuo kikuu cha Jimbo la Michigan kilikuwepo: nilisimulia haya yote nilipozungumza na wanafunzi wa chuo hicho mwezi wa kwanza mwaka 1963(Na nilikutana na mdogo wangu Robert baada ya kipindi kirefu cha kutoonana, alikuwa pale akichukua masomo ya juu ya saikolojia).
Niliwaeleza jinsi ambavyo Lansing Mashariki ilitunyanyasa hadi tukalazimika kuhama tena, wakati huu tukienda maili mbili nje ya mji. Huko ndiko ambako baba yetu kwa mikono yake mwenyewe alitujengea nyumba ya vyumba vinne.
Huko ndiko nilikoanza kukumbuka mambo, hiyo ndiyo nyumba niliyokulia.
Nakumbuka baada ya tukio la moto, baba yangu aliitwa na kuhojiwa juu ya kibali cha bastola ambayo alifyatulia wazungu wawili waliowasha moto.
Nakumbuka mara nyingi polisi walikuwa wakifika nyumbani kwetu na kurusha vitu huku na kule, wakitafuta bastola. Bastola waliyokuwa wakiitafuta, ambayo hawakuwahi kuipata, na ambayo hawangeweza kumpa baba yangu kibali cha kuimiliki-ilikuwa imeshonewa ndani ya mto.
Lakini bunduki ya baba yangu na gobole lake vilikuwa peupe tu; kila mtu alikuwa navyo kwa ajili ya kuwindia ndege, sungura na wanyama wengine.
Baada ya hapo, kumbukumbu zangu ni juu ya mizozo kati ya baba na mama yangu.
Ilionekana kama walizozana muda wote. Wakati mwingine baba yangu alimpiga mama. Pengine ilitokana na kuwa mama yangu alikuwa na elimu nzuri.
Sijui alikoipata, lakini nafikiri mwanamke mwenye elimu hawezi zuia kishawishi cha kumsahihisha mwanaume asiye na elimu. Mara moja moja alikuwa akimsahihisha naye baba hakusita kumkunja.
Baba yangu alikuwa pia mkali sana kwa watoto wake wote isipokuwa mimi. Ndugu zangu wakubwa walipigwa kikatili kila walipovunja sheria zake-na alikuwa na sheria nyingi hivyo haikuwa rahisi kuzifahamu zote.
Karibu vipigo vyangu vyote vilitoka kwa mama yangu. Nimejiuliza sana kwa nini? Naamini kabisa kuwa, pamoja na kuwa baba yangu alikuwa mpinga wazungu, lakini kwenye akili yake alikuwa ameathirika na mtazamo wa wazungu kiasi kwamba alipendelea watoto weupe, na kati ya watoto wake mimi ndiye niliyekuwa mweupe zaidi.
Wazazi wengi weusi wa wakati huo walikuwa wakiwatendea watoto weupe kwa upendeleo kuliko wale weusi. Hii ilitoka moja kwa moja wenye utamaduni wa wakati wa utumwa kuwa “chotara” kwa sababu alikuwa anafanana na mtu mweupe kwa karibu, basi alikuwa bora.
Kumbukumbu zangu nyingine mbili juu ya baba yangu ni nje ya nyumbani. Moja ni juu ya kazi yake kama mhubiri wa Kibapstisti. Hakuwahi kuwa mchungaji mwenye kanisa lake mwenyewe; siku zote alikuwa ni “mhubiri mualikwa” nakumbuka mahubiri yake maarufu aliyopendelea sana, “treni ndogo nyeusi inakuja. . . na ni vyema ukaweka mambo yako yote sawa!” Nadhani kuwa hili lilihusiana na kampeni ya Marcus Garvey ya kurudi Afrika, ikiwa na kaulimbiu, “Treni nyeusi kuelekea nyumbani.” Philbert, kaka yangu ambaye alikuwa amenipita umri kidogo tu, alipenda sana habari za kanisa, lakini mimi zilinichanganya na kunishangaza.
Nilikuwa nikikaa nimemtumbulia macho baba yangu akiruka na kufoka alipokuwa akihubiri huku kanisa zima likiruka na kupiga kelele nyuma yake, likiwa limejitoa roho na mwili kwenye kuimba na kusali.
Hata katika umri huo mdogo, sikuweza kuamini dhana ya Wakristo kuwa Yesu ana uungu. Na hakuna mtu yeyote wa kidini, hadi nilipokuwa mtu mzima wa miaka ishirini-na baadaye nikiwa gerezani, aliyeweza kunieleza chochote.
Niliwaheshimu kidogo sana watu waliowakilisha dini.
Ni kupitia kazi yake hii ya uhubiri ndipo baba yangu aliweza kukutana na watu wengi weusi walioishi Lansing.
Niamini ninapokuambia kuwa Manegro wale walikuwa na hali mbaya sana wakati huo. Bado hata sasa wana hali mbaya-japo ni kwa namna nyingine. Kwa kusema hivyo, namaanisha kuwa sijawahi kuona mji ambayo una asilimia kubwa zaidi ya watu weusi wanaoitwa wa “daraja la kati” walioridhika na waliopotoshwa –watu weusi watafuta hadhi na kuchangamana.
Hivi karibuni nilikuwa nimesimama kwenye sehemu ya mapokezi ya Umoja wa Mataifa nikiongea na balozi kutoka nchi ya Afrika na Mke wake. Mtu mweusi mmoja alinifuata na kusema, “Unanifahamu?”
nillifedheheka kidogo sababu nilifikiri labda ni mtu ninayepaswa kumfahamu. Kumbe ni mmoja wa wale Manegro wa “daraja la kati” wanaojisifu na kuridhika kutoka Lansing. Sikujisikia vizuri.
Alikuwa ni aina ya mtu mweusi ambaye kamwe hangeweza kujihusisha na Afrika hadi pale kitendo cha kuwa na rafiki wa kiafrika kilipokuwa kama fasheni kati ya watu weusi wa “daraja la kati.”
Zamani nilipokuwa nakua, watu weusi wa Lansing waliokuwa na “mafanikio” walikuwa ni wahudumu na wang’arisha viatu.
Kuwa mfanya usafi kwenye duka fulani mjini ilifanya mtu aheshimike sana. Watu wa “maana,” “wakuu,” “wasemaji wa watu weusi,” walikuwa ni wahudumu wa Lansing Country Club na wang’arisha viatu kwenye makao makuu ya jimbo.
Watu weusi pekee waliokuwa na pesa kiukweli walikuwa ni wachezesha kamari au ambao kwa namna fulani waliishi kwa kunyonya masikini zaidi, na masikini walikuwa wengi sana. Wakati ule hakuna mtu mweusi aliyeajiriwa na kiwanda cha magari cha Lansing au kiwanda cha Reo. (Unakumbuka magari ya Reo? Yalitengenezwa Lansing na R. E. Olds, mtu ambaye yaliitwa jina lake, aliishi Lansing. Vita ilipoingia, waliajiri wafanya usafi kadhaa weusi.) Sehemu kubwa ya watu weusi ilitegemea msaada wa serikali, au W.P.A(Works Projects Adminstration)., au iliteseka kwa njaa.
Siku ilifika ambayo familia yetu ilikuwa masikini hadi tulikula tundu la donati; lakini wakati huo tulikuwa na hali nzuri kidogo kulinganisha na watu weusi wengine. Sababu kubwa ni kuwa tulizalisha sehemu kubwa ya chakula chetu wenyewe huko nje ya mji tulikokuwa.
Tulikuwa na afadhali kuliko watu weusi wa mjini ambao walipiga kelele, kama baba yangu alivyosema kwenye mahubiri yake, juu ya keki angani na mbingu yao baadaye wakati mzungu anayo yake hapahapa duniani.
Nilifahamu kuwa michango ambayo baba yangu alipata kwenye kazi yake ya kuhubiri ndiyo hasa ilitulisha na kutuvisha, na pia alifanya kazi zingine za ajabu, lakini picha yake inayofanya nijivunie zaidi ni harakati na upambanaji wake juu ya maneno ya Marcus Garvey.
Pamoja na udogo wangu niliokuwa nao, nilifahamu kutokana na niliyosikia kwamba baba yangu alikuwa akiongea mambo yaliyomfanya awe “shupavu.” Nakumbuka mwanamke mzee mmoja akitabasamu na kumwambia baba yangu, ‘Unawaogopesha wazungu, wako karibu kufa.’
Moja ya sababu zinazofanya nihisi kuwa baba yangu alikuwa akinipendelea ni kuwa, kulingana na kumbukumbu zangu, ilikuwa ni mimi tu ndiye aliyenichukua kwenda naye kwenye mikutano ya chama cha Garvey, U. N. I. A ambayo aliifanya kwa siri kwenye nyumba za watu tofautitofauti. Mikutano hiyo haikuwa na watu wengi, hawakuzidi ishirini.
Lakini hao walikuwa ni wengi sana kwenye sebule ya mtu. Nilitambua walivyokuwa tofauti wakati wa mikutano hii japo ni watu walewale waliokuwa wakiruka na kupiga kelele kanisani. Kwenye mikutano hii, wote-kutia ndani baba yangu, walikuwa makini sana, wenye akili zaidi na wanyenyekevu. Hili lilinifanya nami nijihisi namna hiyohiyo.
Nakumbuka kusikia, “Adam alifukuzwa kwenye bustani ya Eden kwenda kwenye mapango ya Ulaya,” “Afrika kwa waafrika,” ‘Waethiopia amkeni!” Kisha baba yangu angeongea kwamba haitachukua muda mrefu Afrika yote itaongozwa na mtu mweusi. Alipendelea kutumia neno “mtu mweusi” badala ya Negro.
“Hakuna anayejua wakati ambao saa ya ukombozi wa afrika itafika. Ipo kwenye upepo inakuja. Siku moja, kama tufani itafika.”
Nakumbuka kuona picha kubwa za kung’aa za Marcus Garvey zikipitishwa kwa kupasiana mikononi. Baba alikuwa na bahasha kubwa ya kuzihifadhi ambayo mara zote aliibeba kwenye mikutano hii. Kwenye picha zile, niliona kama mamilioni ya watu weusi wakiwa wamesongamana nyuma ya Marcus Garvey aliyekuwa amepanda gari zuri sana.
Mtu mweusi mkubwa akiwa amevalia sare nadhifu iliyokuwa na mapambo ya dhahabu, na pia alivalia kofia nzuri ikiwa na manyoya marefu. Nakumbuka nilisikia kuwa ana wafuasi weusi si tu katika Marekani bali duniani kote, na nakumbuka jinsi mikutano ilivyoisha mara nyingi kwa baba yangu kusema, huku watu wakimfuatisha; “Simama ewe mtu mkuu, utatimiza unachotaka!”
Sijawahi elewa kwanini baada ya kusikia mambo haya, kwa namna fulani, wakati huo; sikufikiria juu ya watu weusi wa Afrika. Picha yangu juu ya Afrika wakati huo ilikuwa ni washenzi walio uchi, wala watu, nyani, simba na misitu yenye joto.
Kwenye ziara zake baba yangu alitumia gari yake kuukuu iliyokuwa na rangi nyeusi, wakati mwingine alinichukua na tukaenda wote kwenye maeneo mbalimbali yaliyozunguka Lansing. Nakumbuka mkutano mmoja wa mchana(Mikutano mingi ilifanyika usiku) kwenye mji wa Owosso, umbali wa maili arobaini kutoka Lansing, mji ambao watu weusi waliuita “Mji mweupe” (Jambo kubwa ambalo Owosso ilijivunia ni kuwa mji wa Thomas. E. Dewey).
Kama ilivyokuwa East Lansing, watu weusi hawakuruhusiwa kutembea usiku, ndiyo sababu ya kufanya mkutano mchana. Na ukweli ni kuwa, miji mingi ya Michigan ilikuwa hivyo wakati huo. Kila mji ulikuwa na watu weusi wachache walioishi hapo. Wakati mwingine ilikuwa ni familia moja tu, kama ilivyokuwa kwenye makao makuu ya county, Mason. Huko kulikuwa na familia moja tu ya watu weusi, familia ya Lyon. Bwana Lyon alikuwa ni mcheza mpira maarufu wa shule ya sekondari ya Mason, aliheshimika sana huko Mason. Sa sasa alikuwa akiishi mjini humo akifanya vibarua vya hapa na pale.
Wakati huo mama yangu alionekana kama vile muda wote alikuwa akifanya kazi, akipika, akifua, akipiga pasi, akisafisha nyumba na kupigishana kelele na sisi watoto wake nane, na kawaida alikuwa akibishana au amenuniana na baba yangu. Moja ya chanzo cha mizozo yao ilikuwa ni mama yangu kuwa na msimamo mkali juu ya vitu ambavyo hataki kula, na wala hataki sisi tule, mfano nguruwe na sungura, vitu ambavyo baba yangu alivipenda sana.
Alikuwa ni mtu mweusi kutoka Georgia na aliamini katika kula vya kutosha chakula ambacho hapa Harlem tunaita “Chakula cha roho.”
Nimesema kuwa mama yangu ndiye aliyekuwa akinichapa-Lakini ilimbidi kufanya hivyo wakati ambao angeepuka aibu kutoka kwa majirani ambao wangeweza dhani kuwa alikuwa akitaka kuniua.
Kila alipojaribu kuinua mkono kunichapa, nilifungua mdomo na kupiga kelele za kufanya dunia yote ijue. Kama kuna mtu alikuwa anapita barabarani, basi angehairisha au angenichapa fimbo chache tu.
Nikiwaza kuhusu hilo leo, nahisi kuwa, kama ambavyo baba yangu alinipendelea kwa kuwa mweupe kuzidi wengine, mama yangu aliniadhibu vikali kwa sababu hiyohiyo.
Yeye mwenyewe alikuwa mweupe lakini aliwapendelea watoto waliokuwa weusi zaidi. Nafahamu kuwa kipenzi chake alikuwa ni Wilfred.
Nakumbuka alikuwa akiniambia nitoke ndani na “Acha miale ya jua ikupige ili upate rangi kidogo.”
Bidii yake katika kunifanya nisijihisi bora kutokana na rangi yangu ilivuka mipaka. Nina hakika alinitendea hivi kutokana na jinsi yeye mwenyewe alivyopata kuwa mweupe.
Nilijifunza mapema maishani kuwa kupiga kelele kunaweza kusaidia. Kaka zangu wakubwa na dada yangu walikuwa wameanza shule, wakati mwingine walikuwa wakirudi toka shule na kuomba biskuti zenye siagi au kitu fulani, kwa mkato mama yangu aliwajibu hapana. Lakini mimi nikikataliwa nililia na kufanya fujo mpaka nipate ninachotaka. Nakumbuka vizuri mama yangu akiniuliza kwa nini siwi mtoto mwema kama Wilfred; lakini nilijiambia mwenyewe, Wilfred kwa kuwa mwema na mkimya kulimfanya ashinde njaa mara nyingi. Hivyo basi, ingali bado mdogo sana nilijifunza kuwa kama unataka kitu fulani ni vyema ukapiga kelele.
Hatukuwa tu na bustani kubwa, bali pia tulifuga kuku. Baba yangu alinunua vifaranga na mama alivilea. Sote tulipenda kuku. Hicho ndicho chakula pekee ambacho hakukuwa na ubishani kati ya mama na baba. Kitu kimoja ambacho kinanifanya nimshukuru mama yangu ni hiki, siku moja nilimfuata na kumuomba niwe na bustani yangu na akaniruhusu kuwa na kitalu changu mwenyewe.
Nilikipenda na nilikihudumia vizuri sana. Nilipenda zaidi kupanda njegere. Nilijivuna sana tulipozila mezani petu. Niling’oa magugu kwenye bustani yangu kwa mikono mara tu yalipochomoza.
Nilikagua matuta nikiwa nimepiga magoti kuangalia minyoo na wadudu. Niliwaua na kuwazika. Wakati mwingine ambapo kila kitu kilikuwa safi na sina cha kupanda, nililala katikati ya matuta na kuangalia anga la bluu na mawingu yanayosafiri huku nikiwaza mambo mbalimbali.
Baada ya kufikisha miaka mitano nami pia nikaanza shule, nikiondoka nyumbani asubuhi pamoja na Wilfred, Hilda na Philbert. Shule yetu ilianzia chekechea hadi darasa la nane.
Ilikuwa umbali wa maili mbili kutoka mjini, nafikiri hakukuwa na shida sisi kusoma pale kwa sababu tulikuwa ndiyo watu weusi pekee kwenye eneo lile.
Kipindi hicho wazungu wa kaskazini walikuwa na kawaida ya”kuasili” watu weusi wachache kwenye jamii yao; hawakuwaona kama kitisho. Watoto wa kizungu hawakutufanyia ubaguzi mkubwa. Walituita “nigger” “weusi” na “Rastus” mara nyingi kiasi kwamba tulidhani hayo ndiyo majina yetu ya asili. Lakini hawakusema hivyo wakiwa na lengo la kututusi, ni namna tu waliyofikiria kutuhusu.
***