Mzee wa Upako amchana live TB joshua

you are 100% correct sir,the problem with people criticizing Prophet T.B. Joshua is that they do not know that a prophet is there to serve GOD as a Go-between information Agent,he is there to explain the unfoldind issues of GOD before them as they are not entitled to such a power of a Prophet granted by GOD.They want Prophet to fulfill their wishes as the way they want while GOD is not like that.

Tell them
Wanafikiri Mungu mganga w kienyeji
Wanataka afanye wanavyotaka wao.
Mungu wetu ni wa utaratibu
 
Ni kweli kabisa ndugu, yani nimekua nikimsikiliza tb joshua, sikuwahi kumsikia akikashifu mtumishi yoyote wa Mungu au kujibu mashambulizi anayoyapata toka sehemu mbalimbali. Ana hekima ya ajabu sana mtu huyu.

Halafu cha ajabu huwa anawaombea
Wengi wameshaenda kuomba msamaha na akawaambia sio wao ni roho iliyopo ndani yao ndo imetenda hayo na mwisho wa siku wanafunguliwa na anawasapoti kwenye huduma zao.
Neno lake kubwa huwa anasema 'we a team'.
 
Lakini Yesu tunaye msoma kwenye Bible alikuwa hatoi huduma ambayo ni Money oriented mfano kuuza Annointed Oil.... Fikiria Chukua Hatua.

God can use any medium kuponya.
Ss km una Roho Mtakatifu atakushuhudia kuwa hii ni kweli hii hapana.
Soma biblia uone njia ambazo Mungu alitumia mfano
2wafalme 6:1-7, 2:19-22
Joshua 6:15-16
Matendo ya mitume5:12-15
1 Samwel 17:49

Hyo inatosha
So wether mtumishi/mchungaji anatumia chochote km kweli ni maelekezo ya Mungu hakuna tatizo.
Biblia inasema manabii wa uongo wapo so hakuna cha ajabu bt shida ni utajuaje? Only Roho Mtakatifu ndo atakushuhudia
 
Ni kwel Yesu alikuwa hatoi huduma ambayo ni money oriented but kumbuka zile anointing oil and anointing water TB Joshua ananunua na anapark ktk chupa na anasafirisha...so ulitegemea zigaiwe bure??hyo Huduma ingekuwepo had Leo??kumbuka dunia ya sasa bila pesa huwez kufanikisha kitu..

Yaani mkuu kuna watu wanashangaza kweli.
Kwahiyo walitaka agawe bure
 
Ni udhaifu kupambana na mtu ambae hana time na wewe. Lusekelo hata hujishtukii! We ndo kila siku unamfatilia Tb, unaangalia tv yake.jiulize kama yeye anajua km unaexist chini ya jua.

Hahahaa haaaa
Umenifurahisha mkuu
 
Wajinga ndio waliwao!

Ni kweli wajinga ndio waliwao. Wapo waliojiita mitume lakini wamefanya mapenzi na watoto wa miaka 6, wakafanya ngono na mateka wa kivita, lakini pia wakasema hawajui hatima zao lakini bado wana wafuasi wengi duniani. Hapa hawajui hatima yao lakini wana wafuasi Qur'an 46:9 Say, "I am not something original among the messengers, nor do I know what will be done with me or with you. I only follow that which is revealed to me, and I am not but a clear warner."To be forgiven sin
 
KUna hoja nzito hapa
Hili la boko haram na wasichana mbona Mungu wa Joshua kala bunda
 
Lusekelo ni mwizi ,na fisadi kama wengine tu tofauti yy kajipambanua kupitia madhabahu ya bwana na ole wake
 
hii ni vita ya sadaka, enzi ya babu wa samunge sadaka zilipunguwa sana kwenye haya makanisa ya ndombolo, na babu alipigwa vita hasa.

nadhani sasa adui yao mpya ni tb joshua maana scoan wana agents Tanzania sasa hivi, inawezekana mafungu ya 10 yamepunguwa ndio hasira zote hizi.

huyu mzee wa upako anayetunzwa pesa jukwaani utazani muimbaji wa ngwasuna anapata wapi credibility ya kunyoshea wengine vidole?

Babu naye si ni walewale tu kwani ni mchungaji yule ila yeye aliamua kuja na style tofauti kidogo ndo maana akatoka fasta, na sasa baada ya kupiga pesa ndefu ya uzeeni katulia zake samunge kimyaaaa, kama vile hayupo.
 
Na wakati anatabiri Zambia kuchukua Kombe la mataifa afrika alipewa na CIA, kufa kwa Atta Mills rais wa ghana mbona haviingii kichwani kasomeni Yer 31:31.
 
Kwa uelewa wa kawaida usio wa "elimu ya bongo ya tests na kukaa vitini" kama ilivyotamkwa hapo juu, sidhani kama tuliowengi tumeyasoma mawazo ya mtoa mada na kwenda zaidi ya kutoa hoja zetu. Suala la TB Joshua kuwa nabii huku maafa makubwa yakitokea ndani ya nchi yake mwenyewe bila hata kuyazuia ama kutabiri kuwa yangetokea nadhani ndo ilikuwa hoja ya Mzee wa Upako kujustify unabii hewa wa TB Joshua na wengine wenye jina la nabii. Lakini kwa upande wa pili wa shilingi, mzee wa "Upako" amesahau kuwa yeye mwenyewe yuko katika kikaango kilekile kwa watu kuanza kulizungumzia hata jina lake na maana halisi ya neno UPAKO kama ni sahihi ama la na humaanisha nini. Kwa uelewa wangu wa kawaida (wa kushika Biblia na vitabu vingine vya dini kwa matukio), neno "upako" limetokanana na kile kinachoaminika kuwa ni nguvu za Mungu kwa namna alivyowavuvia ama kuwapaka mafuta (anointment) watumishi wake ambao kwa neno jingine huitwa "Manabii" (prophets). Kama yeye pia si mmoja wa manabii ama wale wanojiita jina hilo ningeona ni busara kama angefafanua hilo kwanza kisha akaanza itupia mawe nyumba ya jirani yake. Ni upako upi huo ambao yeye anao na wengine wameukosa??? Hoja ya kutoweza kuzuia maafa ndani ya nchi yake na hata sehemu nyingine nje ya eneo lake, hazimfanyi TB Joshua kutokuwa nabii kwani hata Yesu pia hakuzuia baadhi ya mambo yasitokee bali kuyaacha yatimie kwani ilikuwa ni sehemu ya mpango wa Mungu kuonesha utukufu wake mf. kusalitiwa na Yuda (alilijua mapema), kifo cha Lazaro, mateso na hata kifo chake n.k vyote hivi alivijua lakini hakuvizuia (nisiulizwe juu ya kutekwa kwa mabinti wa kinaijeria kama ni mpango wa Mungu ama wa Boko kharam). Siwezi sema kati ya hawa wawili yupi ni nabii wa uongo ama la kwani kumtaja mmoja kati yao ni ku-take side ama kujipa 'unabii' wa aina yangu hivyo suala la nani alitabiriwa ni wa uongo ama la ninaliacha kwenu. Mzee wa Upako anasahau kuwa yeye pia ni nabii ukiachilia kuwa hajiiti jina hilo (kutolitumia haina maana siye) kwani a "PROPHET is a person who is believed to have a special power which allows them to say what God or a god wishes to tell people, especially (not necessarily) about things that will happen in the future". Yeye pia huwatabiria watu kuwa watakuwa matajiri, kupona magonjwa yao na mengine makubwa in no time na kwa shuhuda za "wanae" kama awaitavyo, yale aliyoyasema yali/yametimia tena double-double kama si zaidi ya hapo, hivyo ni nabii pia. Kazi ya nabii ni "kuyatimiza yale anayoagizwa na aliyemtuma (be it God or a god of its own kind) na si kufanya chochote ili watu waone kuwa amefanya". Uwezo wa kuyafanya hayo yote hutoka kwa aliyemuagiza na si vile apendezwavyo yeye vinginevyo hata Yesu angetengeneza makontena ya mikate kumuonesha shetani kuwa anaweza. Mimi napita tu!
 
Nice. Ila imeandikwa "....huwajua walio wake". Hekima hapa ni maombi na kumwabudu Mungu katika roho na kweli. Kibinadam ni ngumu sana. Shetani ni mdanganyifu sana unaweza kuona hata jinsi alivyowapiga watu upofu wameconcentrate kumuomba Mama bikira .... na kumuweka mwanae ambaye ndiye Mungu kuwa subsidiary au secondary instead ya kuwasiliana naye yeye moja kwa moja kwa maombi kupitia roho wake mtakatifu. Yaani duniani tunayo dhiki. Ni kumuomba Mungu hekima na utambuzi wa kiroho.
 
TB Joshua ni mtumishi na si msaka maisha na umaarufu. Lusekelo hana la kujilinganisha kwa TB Joshua.
 
Back
Top Bottom