Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,620
- 46,261
Nimemsikia na kumtazama mara kadhaa katika redio na TV, huyu bwana anafanya vihoja vyote alivyokuwa akifanya mwendazake TB Joshua.
Shuhuda kutoka kwa wafuasi wake ni zile za mambo ya ajabu yasiyomithilika "outlandish claims" za watu kuharisha vyura, kutolewa ndege machoni, vifo vya paka wa uchawi n.k
Kama alivyokuwa mwendazake TB Joshua na wanaojiita manabii wote hawa wa kisasa, Mwamposa pia hana mafundisho rasmi ya kanisa lake. Ibada nzima imetawaliwa na madai ya miujiza ya ajabu kuhusu afya, uchumi, vyeo n.k
Pia kupitia biashara ya kanisa ameweza na ameendelea kujikusanyia ukwasi mkubwa wa utajiri.
Haya ndio yanayoonekana hadharani kwa sasa, nafikiri ni suala la muda kabla ya mengi ya huko gizani kuibuliwa wakati fulani.
Shuhuda kutoka kwa wafuasi wake ni zile za mambo ya ajabu yasiyomithilika "outlandish claims" za watu kuharisha vyura, kutolewa ndege machoni, vifo vya paka wa uchawi n.k
Kama alivyokuwa mwendazake TB Joshua na wanaojiita manabii wote hawa wa kisasa, Mwamposa pia hana mafundisho rasmi ya kanisa lake. Ibada nzima imetawaliwa na madai ya miujiza ya ajabu kuhusu afya, uchumi, vyeo n.k
Pia kupitia biashara ya kanisa ameweza na ameendelea kujikusanyia ukwasi mkubwa wa utajiri.
Haya ndio yanayoonekana hadharani kwa sasa, nafikiri ni suala la muda kabla ya mengi ya huko gizani kuibuliwa wakati fulani.