Mzee wa Upako aishukia serikali

Mzee wa Upako aishukia serikali

kwa nini asimlalamikie aliyempa huo upako ili atambulike na serikali. Ikiwa alipewa upako na Mungu wasiwasi wake unatokana na nini? Mungu huyo huyo aliyempaka upako atamfungulia milango anayoitaka. Yeye amtumikie tu aliyempa upako.
 
Mzee wa upako ni misheni town, hana lolote zaidi ya kutaka utajiri na kujikweza. Hawa wahubiri/wakole walio wengi kama si wote ni wafuasi wa makanisa ya katoloki/Lutherani baada ya kuasi ndio wametumbukia huko. Yeye anasema makanisa ya katoloki na lutheran hayajui kuhubiri. Nani kamdandanganya kwamba yeye yuko juu upande wa kuhubiri kupita katoliki/Lutheran, Kupayuka na kupiga kelele ndio kuhubiri?
 
kweli sasa napata maana ya mengi yaliyoandikwa kwenye biblia. Eti huyu naye anadiriki kusema wengine hawajui kuhubiri...! Hivi kwa kweli kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kuongea hilli kwenye public? Nina wasiwasi na elimu ya huyu bwana. Nimemsikia leo nikahisi kichefuchefu.
 
haihitaji kuumiza kichwa kabla ya kujua kwamba he's is just another conman,siphoning sick souls pockets...
 
My take.

Mtandao wa makanisa ya Lutherani na Katoliki ni mkubwa sana na umeenea karibu kila sehemu Tanzania.Madhehebu ya akina Mzee wa upako yako mengi sana lakini yako disorganise kiasi kwamba serekali inapata taabu sana jinsi ya kuwasiliana nayo.Utakuta mtumishi wa Mungu anaongoza kanisa lisilokuwa hata jengo [anatumia majengo ya shule] anajiita Askofu na anataka heshima anazopewa Askofu wa kanisa katoliki/Lutherani.Mwingine unakuta kaanzisha kanisa nyumbani kwake kaamua kujita nabii xyz,kanisa lake lina waumini 100 atataka naye kujifaninisha na kina Pengo au Malasusa kwa kweli serekali ipo sahihi kabisa.Makanisa mengine ukiyatazama kwa makini utagundua ni mali ya viongozi,makanisa ya jinsi mara nyingi yanasambaratika wakati viongozi wao wanapofariki au wanapojitokeza baadhi ya waumini wajuaji watakaohoji mambo ambayo viongozi/waanzilishi hawataki kuyaweka wazi.

Makanisa yanayoongozwa na kina mzee wa upako na Askofu Z Kakobe yatatetereka sana siku viongozi wake watakapotangulia mbele ya haki kwasababu misingi yake imejikita zaidi katika vipaji vya uongozi ukilinganisha na makanisa ya Lutherani na Katoliki.

Mzee wa upako ameenda mbali zaidi kwa kusema kwamba wahubiri wa makanisa ya Lutherani/Katoliki hawajui kuubiri wamebaki kubusu pete tu.Mimi ni muumini wa madhehebu ya Lutherani kila j2 na kwenda kanisani kusali kama ningekutana na mahubiri mabovu/hovyo kwa vyovyote ningekubali kupoteza muda wangu nadhani mzee wa upako kaamua kubwabwaja tu labda ana jambo lingine kaamua kulificha.


Huwa naamini katika maneno 100 ya mjinga basi naweza kupata moja au mawili ya kweli.

Ndugu Ngongo, point yako ya kuwa kuna makanisa disorganised sidhani kama ina mantiki hapa.Mzee wa upako anasema serikali inayakumbatia madhehebu ya wakatoliki na walutheran, na umekubali na kusema ni sahihi kabisa.

Kwanza nina wasiwasi sana urafiki huu wa serikali na haya makanisa, nasema nina wasiwasi, kwa sababu akina Malasusa leo ndio wasemaji wa Lowassa na wewe ni Mlutheri na ulikaa kimya, na katu hautamgusa Malasusa katika hilo. Kwa hiyo urafiki huu wa serikali na makanisa ni mbaya kwa maana ya kuwa makanisa yanatakiwa yawe makali kukemea ufisadi lakini kwa sababu ya hizo attention za hapa na pale basi wanakaa kimya.

Urafiki wa serikali na katoliki huwa unawaconfuse wengi kwani vatican ni serikali na wao ni wakatoliki, so usije kukuta hii notion ndio inawafanya wengi waamini serikakali inawakumbatia wakatoliki

Kwa kifupi uarfiki waserikali na makanisa ni wrong, kama serikali itasimama kama serikali, divide and rule ya viongozi wazembe serikalini huwa wanapitia kwenye hizi dini kuwapata walio wao. Ishu ya mahakama ya kadhi ni wazi ni failure ya JK kushindwa kuongoza na kutaka kufavour watu fulani, is the same concpet applies na huku kwenye haya madhehebu. KAnisa inabidi lisimame kama Yohana mbatizaji , Eliya, Shadrack, meshack and Abednego kukataa na kupinga maovu yote.

To my knowledge sijaona kama haya makanisa yamefika level ya juu kiasi cha kupendelewa na serikali, ila napata picha kwamaneno ya Lusekelo na confirmation yako.

Pili si kweli kuwa Lutheran na Katoliki ndio wana netwrok kubwa sana, sijaona ukilitaja Moravian,wasabato,SDA,Angalican, EAGT, TAG,FGBF,.Haya makanisa huwezi kuyadharau hata kidogo, si kwa population wala network.

Unawataja wa makanisa machanga kama ya akina Lusekelo ndio wako wengi zaidi, lakini hii haiipi kibali serikali kuwa iwape attention baadhi ya makanisa, serikali yetu haina dini kabisa. Bungeni tuna askofu Lwakatare hawa ni baadhi ya watu wenye single churches lakini wako powerful. Kuna akina Kakobe-style ya uongozi katika massive population kama ile si ya kuchezea, na ukiacha makanisa mengine mapya, huyu jamaa kanisa lake halina history ya ku-split, kanisa lake la DSM ndio kubwa kuliko yote EAST africa. Mwangalie Mwingira, Gamanywa n.k these are emerging but powerful churches ambapo wakisema wote waseek attention ya serikali ni mbaya sana. Na wanawachukua watu kutoka huko huko Lutheran and catholic, so organisation here without power is nothing!

Sasa imagine haya manisa yote yawe organised (kama unavyotaka ) and then wa seek attention ya serikali!!

Swala la watu kujiita maaskofu , manabii yatakuumiza kichwa as far as faith reigns. Tatizo ni kuwa the very same reformation that happens during Luther it is still going on! Kosa lilishafanyika zile zama za (dark ages) nadhani unafahamu. Kwa kifupi; haya makanisa mapya yanatokea wapi? si yanazaliwa kutoka kwenye existing churches? kuna nini humo mpaka wakimbie? whats wrong? utakuta ni mambo ya Imani.Problem ni kuwa kuna tatizo la kurithi hizi imani without exploring, nalo naliona kwako.Hujajua hasa ukristo na nafasi yake katika jamii.unachosema ni organisation zinazojiita za kikristo.Ndio maana kwa mfano kanisa la Lutheran unalosema liko organised ndio weak kabisa,Kanisa moja utamkuta mchungaji Mlokole na yuko strictly, na lingine utamkuta mchungaji mlevi na mzembe, within same church hakuna universal law ya kuwatambulisha walutheri,Leo hii kuna walutheri walokole na wasio walokole!

Mwisho, kwa knowledge yangu ya ulokole na walokole, sijaona sehemu yoyote katika biblia inayompa kibali Anthony Lusekelo aseme aliyoyasema.Biblia inasema Mungu atakupigania, atakuinua. Kwa hiyo haraka haraka hapa ni kuwa Lusekelo ameviolate divine rule ndogo sana ya kuwa Mungu ndie atakayempigania. Sasa napata picha who is he?

Kama anataka awe sawa na Lutheran, wakatoliki , basi he belong to the same group and class,Katika Biblia viongozi wa dini wako juu sana ya marais, simply kwa sababu walijaa nguvu za Roho mtakatifu na kuwa watakatifu kweli, Siku hizi tunaona maigizo ya vongozi wa dini. Hili ndio linasababisha makanisa kuzaliwa kila siku, If Lutheran and Catholic would have stood in the right path of God, kusingekuwa na huu utitiri wa makanisa. Believe me ndani ya Lutheran na Catholic still today kuna watu wamesimamia kweli ya Mungu.Ni hawa wachache tu akina Malasusa na Pengo ambao kwako unawaona wako sahihi!

Yes kuna ukweli wa walichosema na ukweli ni huu, serikali haina dini. urafiki huu ni wa nini?
 
Mzee wa upako ni misheni town, hana lolote zaidi ya kutaka utajiri na kujikweza. Hawa wahubiri/wakole walio wengi kama si wote ni wafuasi wa makanisa ya katoloki/Lutherani baada ya kuasi ndio wametumbukia huko. Yeye anasema makanisa ya katoloki na lutheran hayajui kuhubiri. Nani kamdandanganya kwamba yeye yuko juu upande wa kuhubiri kupita katoliki/Lutheran, Kupayuka na kupiga kelele ndio kuhubiri?

Please try to find the history.

Lutheran walijitoa kutoka Roman Catholic

Roman Catholic walijitoa(waliliua) kutoka Catholic

Catholic means universal, miaka 1000 baada Tangu Yesu alipoondoka Ulimwenguni kulikuwa na just Christian church, ambalo warumi waliita Catholic.

Fuatilia ili kanisa la umoja(universal) lilipotelea wapi, na nani aliyelipoteza. Usiseme kana kwamba haya makanisa yametokea sayari ya mars au mwezini kunadocumented historical facts

So usiwaite wenzako waasai ndio raha ya kuwa na uhuru wa kuamua, offcourse huo uhuru kwenye biblia haupo! maana tuna Mungu mmoja, ubatizo mmoja, njia moja,injili moja .....

kwa hiyo kama uasi uusemao wewe woote hao ni waasi!!!
 
Aidha, aliwatahadharisha viongozi wa serikali kukumbuka yaliyotokea Rwanda ambako kwa asilimia kubwa kanisa lilichochea mauaji ya kimbari hali iliyosababisha washitakiwa wakuu katika kesi ile kuwa viongozi wa dini.



Hivi ni kweli makanisa yalchochea mauwaji? basi inabidi hawa viongozi wa Dini hizi za makanisa zidhibitwe sana, kwasababu sio kuwa Yesu anatumiwa kibiashara naona pia kwa uchochezi
 
Kuna siku nilimwambia rafiki yangu natafuta mtaji nami nianzishe kanisa langu ntaenda Nigeria kupata yale mambo yetu then naanza kujinadi Star Tv na CH Ten.
Kma serikali itaanza kujari kila dhehebu linaloibuka Mbeya yako zaidi ya 300 mbona watakuwa matajiri.
 
Kanisa la Gospel Revival Centre linajulikana kwasababu kaamua kutumia channel 10.Juzi juzi nilikuwa natazama kipindi chake anataka tumchangie 100,000/= au zaidi umtajie mambo yako matano akuombee.Kwa maana hiyo basi usipokuwa na hizo 100,000/= hawezi kukuombea kweli siku hizi Yesu kawa biashara nzuri.

Hii kali ya kuanzia mwaka. kuombewa mpaka utoe pesa?. Yesu alipita huku na kule kuwaombea watu na kuihubiri injili bure, na isitoshe aliwaambia wanafaunzi wake enendeni mkaihubiri injili bure na wala msichukue malipo yoyote. Sasa huyu askofu kama ni kweli alisema anataka pesa ndipo awaombee watu nasindwa kuelewa kwanini alifanya hivyo. Mbarikiwe sana.
 
Kwa huyu mzee wa Upako huwa napata shida sana kuangalia kipindi chake pamoja na mama yangu (over 60 years) Kuna wakati anaonyesha wazi upotoshaji wa hali ya juu. Mimi huwa nasonya na mama ananikanya kila mara. Mama anasema hata akikosea yeye ni kiongozi wa dini tumweshimu tu. Kuna baadhi ya mambo anayosema ambayo yanamwanika wazi hata kwa mtu mwenye akili ya kawaida tu. Wakati mwingine busara ya kawaida inapotea katika mahubiri / maneno yake. Wakati wa mjadala wa kadhi kwa wale walioangalia watakuwa waliona ukweli huu. Hata hivyo katika BIBLIA TAKATIFU kuna sehemu yasema "MTAWATAMBUA KWA MATUNDA YAO". Nashukuru kwa mjadala huu ingekuwa vizuri kama mama angesoma mawazo mengi mazuri yaliwekwa hapa.
 
Jana nilibahatika kumwangalia katika channel ten huyo mzee wa upako kama anavojiita, alichokuwa anafanya ni kituko na allegetion kama za kibwetele,ovyo sana huyo!
 
Watu wengine bana. Akipewa kipawa na Mwenyezi anataka akitumie kutawala kila mtu. Anayoyawasilisha Mzee wa upako ni mambo yake binafsi ila anataka ionekane ni suala la halaiki. Halafu ndio tuseme anaitishia usalama serikali au?

Kwani nani kasema huko serikalini na usalama wa Taifa hakuna watumishi wa Mungu nani? Hekima ya Mungu ndiyo inawaongoza viongozi wa serikali kujua namna ya kumchukulia kila mmoja wao. Na kwa hili serikali iko sahihi.

Halafu aache kumpaka Rais mafuta kwa mgongo wa chupa. Eti anamfagilia huku anamponda. Mzee wa upako hiyo ni dhambi ya uongo na unafiki.

Somesheni viongozi wenu ili wajue kutofautisha ya Mungu na ya Kaisari.
 
Huwa naamini katika maneno 100 ya mjinga basi naweza kupata moja au mawili ya kweli.

Ndugu Ngongo, point yako ya kuwa kuna makanisa disorganised sidhani kama ina mantiki hapa.Mzee wa upako anasema serikali inayakumbatia madhehebu ya wakatoliki na walutheran, na umekubali na kusema ni sahihi kabisa.

Kwanza nina wasiwasi sana urafiki huu wa serikali na haya makanisa, nasema nina wasiwasi, kwa sababu akina Malasusa leo ndio wasemaji wa Lowassa na wewe ni Mlutheri na ulikaa kimya, na katu hautamgusa Malasusa katika hilo. Kwa hiyo urafiki huu wa serikali na makanisa ni mbaya kwa maana ya kuwa makanisa yanatakiwa yawe makali kukemea ufisadi lakini kwa sababu ya hizo attention za hapa na pale basi wanakaa kimya.

Urafiki wa serikali na katoliki huwa unawaconfuse wengi kwani vatican ni serikali na wao ni wakatoliki, so usije kukuta hii notion ndio inawafanya wengi waamini serikakali inawakumbatia wakatoliki

Kwa kifupi uarfiki waserikali na makanisa ni wrong, kama serikali itasimama kama serikali, divide and rule ya viongozi wazembe serikalini huwa wanapitia kwenye hizi dini kuwapata walio wao. Ishu ya mahakama ya kadhi ni wazi ni failure ya JK kushindwa kuongoza na kutaka kufavour watu fulani, is the same concpet applies na huku kwenye haya madhehebu. KAnisa inabidi lisimame kama Yohana mbatizaji , Eliya, Shadrack, meshack and Abednego kukataa na kupinga maovu yote.

To my knowledge sijaona kama haya makanisa yamefika level ya juu kiasi cha kupendelewa na serikali, ila napata picha kwamaneno ya Lusekelo na confirmation yako.

Pili si kweli kuwa Lutheran na Katoliki ndio wana netwrok kubwa sana, sijaona ukilitaja Moravian,wasabato,SDA,Angalican, EAGT, TAG,FGBF,.Haya makanisa huwezi kuyadharau hata kidogo, si kwa population wala network.

Unawataja wa makanisa machanga kama ya akina Lusekelo ndio wako wengi zaidi, lakini hii haiipi kibali serikali kuwa iwape attention baadhi ya makanisa, serikali yetu haina dini kabisa. Bungeni tuna askofu Lwakatare hawa ni baadhi ya watu wenye single churches lakini wako powerful. Kuna akina Kakobe-style ya uongozi katika massive population kama ile si ya kuchezea, na ukiacha makanisa mengine mapya, huyu jamaa kanisa lake halina history ya ku-split, kanisa lake la DSM ndio kubwa kuliko yote EAST africa. Mwangalie Mwingira, Gamanywa n.k these are emerging but powerful churches ambapo wakisema wote waseek attention ya serikali ni mbaya sana. Na wanawachukua watu kutoka huko huko Lutheran and catholic, so organisation here without power is nothing!

Sasa imagine haya manisa yote yawe organised (kama unavyotaka ) and then wa seek attention ya serikali!!

Swala la watu kujiita maaskofu , manabii yatakuumiza kichwa as far as faith reigns. Tatizo ni kuwa the very same reformation that happens during Luther it is still going on! Kosa lilishafanyika zile zama za (dark ages) nadhani unafahamu. Kwa kifupi; haya makanisa mapya yanatokea wapi? si yanazaliwa kutoka kwenye existing churches? kuna nini humo mpaka wakimbie? whats wrong? utakuta ni mambo ya Imani.Problem ni kuwa kuna tatizo la kurithi hizi imani without exploring, nalo naliona kwako.Hujajua hasa ukristo na nafasi yake katika jamii.unachosema ni organisation zinazojiita za kikristo.Ndio maana kwa mfano kanisa la Lutheran unalosema liko organised ndio weak kabisa,Kanisa moja utamkuta mchungaji Mlokole na yuko strictly, na lingine utamkuta mchungaji mlevi na mzembe, within same church hakuna universal law ya kuwatambulisha walutheri,Leo hii kuna walutheri walokole na wasio walokole!

Mwisho, kwa knowledge yangu ya ulokole na walokole, sijaona sehemu yoyote katika biblia inayompa kibali Anthony Lusekelo aseme aliyoyasema.Biblia inasema Mungu atakupigania, atakuinua. Kwa hiyo haraka haraka hapa ni kuwa Lusekelo ameviolate divine rule ndogo sana ya kuwa Mungu ndie atakayempigania. Sasa napata picha who is he?

Kama anataka awe sawa na Lutheran, wakatoliki , basi he belong to the same group and class,Katika Biblia viongozi wa dini wako juu sana ya marais, simply kwa sababu walijaa nguvu za Roho mtakatifu na kuwa watakatifu kweli, Siku hizi tunaona maigizo ya vongozi wa dini. Hili ndio linasababisha makanisa kuzaliwa kila siku, If Lutheran and Catholic would have stood in the right path of God, kusingekuwa na huu utitiri wa makanisa. Believe me ndani ya Lutheran na Catholic still today kuna watu wamesimamia kweli ya Mungu.Ni hawa wachache tu akina Malasusa na Pengo ambao kwako unawaona wako sahihi!

Yes kuna ukweli wa walichosema na ukweli ni huu, serikali haina dini. urafiki huu ni wa nini?




Heshima kwako Waberoya,

Ndugu Waberoya ni kweli makanisa yanayongozwa na kina Mzee wa Upako/ Askofu Mkuu Z Kakobe yako disorganised.Kuendelea kuwapo kwa makanisa yao kunategemea zaidi na uwepo wao binafsi.Ukienda kwenye makanisa mengine eg Katoliki,Lutheran,Anglican,AIC,Morovian na nk organisation structure inafuatwa na inaeleweka kirahisi na taasisi za kisekali na zisizo za kiserekali,ukienda kwa Mzee wa upako na Zakaria Kakobe huwezi kukutana na hii kitu.


Kanisa Katoliki na kanisa la Lutheran [KKKT] ni makanisa ambayo yamejikita zaidi kumhudumia mwanadamu kiroho na kimwili.Madhehebu ya kikatoli na Lutheran yamefungua miradi mingi inayotoa huduma za afya,elimu na malezi ya watoto yatima na wazee.Kimsingi shughuli zote hizi zilipaswa kufanywa na serekali lakini kanisa baada ya kugundua serekali haina uwezo wa kutosha kumhudumia kila mwananchi lenyewe likachukua jukumu hili kubwa.Uhusiano baina ya serekali na madhehebu haya mawili makubwa Tanzania unaanzia hapa na si vinginevyo kama Mzee wa Upako na watu wengine wanavyotaka kupotosha.Hospital za KCMC na Bugando ni mfano hai jinsi madhehebu haya yalivyojitoa kumsaidia mwananchi kimwili bila kujali dini au dhehebu.

Ndugu yangu kama ulivyokiri mwenyewe katika bandiko lako serekali haina dini,serekali inashirikiana na madhehebu ya KKKT & Kanisa Katoliki kwasababu nilizitaja [Elimu & Afya] na si mambo yanayohusiana na imani.Madhehebu ya Kina mzee wa upako na Askofu Mkuu Z Kakobe yamejikita zaidi kumhudumia mwanadamu kiroho na kuacha mambo ya mwili.Ikiwa serekali itashikiana na madhehebu ya jinsi hii itakuwa inaingilia mambo ya imani na hivyo kuvunja katiba ya nchi.Mzee wa Upako kama anataka kutambuliwa na serekali ajenge hospital,vyuo vikuu na nk,kinyume cha hapo aendelee kulalama kwenye channel ten.

Attention ya serekali anayeita si mimi au wewe bali ni Mzee wa Upako,tena kwa kuwavurumishia maneno ya kejeli viongozi wa kanisa katoliki na Lutheran ambao kwa namna yoyote hawakuilazimisha serekali iwape attention.

Umesema nilikaa kimya wakati Askofu Mkuu Malasusa alipokuwa msemaji wa familia ya Lowassa tafadhali fuatilia hilo bandiko hapa jamvini uangalie niliandika nini !.Kwa kweli nilimpinga sana na wala sikuishia hapo nilimawandikia email,hata Askofu wangu Thomas Laiser aliposhiriki kumpokea Lowassa alipojiuzulu/zira uwaziri mkuu naye pia nilimlaumu kwa kitendo chake cha kulidhalilisha kanisa.

Sijayazungumzia madhehebu mengine kwasababu Mzee wa upako hakuyazungumzia kabisa pengine alikuwa na sababu zake.







 
Heshima kwako Waberoya,

Ndugu Waberoya ni kweli makanisa yanayongozwa na kina Mzee wa Upako/ Askofu Mkuu Z Kakobe yako disorganised.Kuendelea kuwapo kwa makanisa yao kunategemea zaidi na uwepo wao binafsi.Ukienda kwenye makanisa mengine eg Katoliki,Lutheran,Anglican,AIC,Morovian na nk organisation structure inafuatwa na inaeleweka kirahisi na taasisi za kisekali na zisizo za kiserekali,ukienda kwa Mzee wa upako na Zakaria Kakobe huwezi kukutana na hii kitu.

Kanisa Katoliki na kanisa la Lutheran [KKKT] ni makanisa ambayo yamejikita zaidi kumhudumia mwanadamu kiroho na kimwili.Madhehebu ya kikatoli na Lutheran yamefungua miradi mingi inayotoa huduma za afya,elimu na malezi ya watoto yatima na wazee.Kimsingi shughuli zote hizi zilipaswa kufanywa na serekali lakini kanisa baada ya kugundua serekali haina uwezo wa kutosha kumhudumia kila mwananchi lenyewe likachukua jukumu hili kubwa.Uhusiano baina ya serekali na madhehebu haya mawili makubwa Tanzania unaanzia hapa na si vinginevyo kama Mzee wa Upako na watu wengine wanavyotaka kupotosha.Hospital za KCMC na Bugando ni mfano hai jinsi madhehebu haya yalivyojitoa kumsaidia mwananchi kimwili bila kujali dini au dhehebu.

Ndugu yangu kama ulivyokiri mwenyewe katika bandiko lako serekali haina dini,serekali inashirikiana na madhehebu ya KKKT & Kanisa Katoliki kwasababu nilizitaja [Elimu & Afya] na si mambo yanayohusiana na imani.Madhehebu ya Kina mzee wa upako na Askofu Mkuu Z Kakobe yamejikita zaidi kumhudumia mwanadamu kiroho na kuacha mambo ya mwili.Ikiwa serekali itashikiana na madhehebu ya jinsi hii itakuwa inaingilia mambo ya imani na hivyo kuvunja katiba ya nchi.Mzee wa Upako kama anataka kutambuliwa na serekali ajenge hospital,vyuo vikuu na nk,kinyume cha hapo aendelee kulalama kwenye channel ten.

Attention ya serekali anayeita si mimi au wewe bali ni Mzee wa Upako,tena kwa kuwavurumishia maneno ya kejeli viongozi wa kanisa katoliki na Lutheran ambao kwa namna yoyote hawakuilazimisha serekali iwape attention.

Umesema nilikaa kimya wakati Askofu Mkuu Malasusa alipokuwa msemaji wa familia ya Lowassa tafadhali fuatilia hilo bandiko hapa jamvini uangalie niliandika nini !.Kwa kweli nilimpinga sana na wala sikuishia hapo nilimawandikia email,hata Askofu wangu Thomas Laiser aliposhiriki kumpokea Lowassa alipojiuzulu/zira uwaziri mkuu naye pia nilimlaumu kwa kitendo chake cha kulidhalilisha kanisa.

Sijayazungumzia madhehebu mengine kwasababu Mzee wa upako hakuyazungumzia kabisa pengine alikuwa na sababu zake.




Hii ni kibiblia kabisa. Mathew 22:37-40. 'You shall love the LORD your God with all your heart, with all your soul, and with all your mind.'

Kina 'mzee wa upako' ikifika kwenye 'mind' wanatoka hola kabisa. Wao ni shandaraba karabako shondororiba.

Jamani eeh siyo roho tu ebo. Mwishoni ndo mnageukaga vibwetere. roho haina akili jamani! Mwanadamu ni roho, anayo nafsi na anaishi katika mwili.

Ndo mana narudia tena nendeni shule. Wengi wenu unakuta darasa la pili unusu lakini eti askofu. DUH!Na kibiblia Askofu maana yake ni mwangalizi sasa utaweza kuwa mwangalizi wa karne hii kweli na darasa lako la pili unusu kasorobo???????????
 
Hafai kuwa kiongozi wa dhehebu lolote ni mbinafisi na sasa amaota mapepe yamemzidi
 
Duh ama kweli level ya kuelewa mambo jamiiforums ni kubwa kuliko nilivyo fikiri,laiti watanzania tungekuwa na uwezo wa kuchanganua mambo hakika JK asingekatiza uchaguzi mkuu.Mzee wa Upako kadri siku zinavyosonga mbele ndio anazidi kuwa kichekesho namshauri atafute biashara nyingine huku kwenye dini watu wameshamstukia.
 
tafadhali rekebisha kauli yako akuna aliyeokoka ambaye amechanganyikiwa pls omba radhi kwa hilo


Walokole wengi wamechanganyikiwa ina maana hujui mkuu mbona tumeona mifano kibao au wewe bado ujagudua.nasema wengi wao wamechanganyikiwa ingawa si wote.Nawaomba radhi wale wote ambao hawajachanganyikiwa,waliochanganyikiwa mtanisamehe bado msimamo wangu uko pale pale.
 
Heshima kwako Waberoya,

Ndugu Waberoya ni kweli makanisa yanayongozwa na kina Mzee wa Upako/ Askofu Mkuu Z Kakobe yako disorganised.Kuendelea kuwapo kwa makanisa yao kunategemea zaidi na uwepo wao binafsi.Ukienda kwenye makanisa mengine eg Katoliki,Lutheran,Anglican,AIC,Morovian na nk organisation structure inafuatwa na inaeleweka kirahisi na taasisi za kisekali na zisizo za kiserekali,ukienda kwa Mzee wa upako na Zakaria Kakobe huwezi kukutana na hii kitu.

Kanisa Katoliki na kanisa la Lutheran [KKKT] ni makanisa ambayo yamejikita zaidi kumhudumia mwanadamu kiroho na kimwili.Madhehebu ya kikatoli na Lutheran yamefungua miradi mingi inayotoa huduma za afya,elimu na malezi ya watoto yatima na wazee.Kimsingi shughuli zote hizi zilipaswa kufanywa na serekali lakini kanisa baada ya kugundua serekali haina uwezo wa kutosha kumhudumia kila mwananchi lenyewe likachukua jukumu hili kubwa.Uhusiano baina ya serekali na madhehebu haya mawili makubwa Tanzania unaanzia hapa na si vinginevyo kama Mzee wa Upako na watu wengine wanavyotaka kupotosha.Hospital za KCMC na Bugando ni mfano hai jinsi madhehebu haya yalivyojitoa kumsaidia mwananchi kimwili bila kujali dini au dhehebu.

Ndugu yangu kama ulivyokiri mwenyewe katika bandiko lako serekali haina dini,serekali inashirikiana na madhehebu ya KKKT & Kanisa Katoliki kwasababu nilizitaja [Elimu & Afya] na si mambo yanayohusiana na imani.Madhehebu ya Kina mzee wa upako na Askofu Mkuu Z Kakobe yamejikita zaidi kumhudumia mwanadamu kiroho na kuacha mambo ya mwili.Ikiwa serekali itashikiana na madhehebu ya jinsi hii itakuwa inaingilia mambo ya imani na hivyo kuvunja katiba ya nchi.Mzee wa Upako kama anataka kutambuliwa na serekali ajenge hospital,vyuo vikuu na nk,kinyume cha hapo aendelee kulalama kwenye channel ten.

Attention ya serekali anayeita si mimi au wewe bali ni Mzee wa Upako,tena kwa kuwavurumishia maneno ya kejeli viongozi wa kanisa katoliki na Lutheran ambao kwa namna yoyote hawakuilazimisha serekali iwape attention.

Umesema nilikaa kimya wakati Askofu Mkuu Malasusa alipokuwa msemaji wa familia ya Lowassa tafadhali fuatilia hilo bandiko hapa jamvini uangalie niliandika nini !.Kwa kweli nilimpinga sana na wala sikuishia hapo nilimawandikia email,hata Askofu wangu Thomas Laiser aliposhiriki kumpokea Lowassa alipojiuzulu/zira uwaziri mkuu naye pia nilimlaumu kwa kitendo chake cha kulidhalilisha kanisa.

Sijayazungumzia madhehebu mengine kwasababu Mzee wa upako hakuyazungumzia kabisa pengine alikuwa na sababu zake.








Mkuu ulichosema ni sahihi kabisa, rejea post yangu ,naona na wewe umesimamia hapo, kwa ufahamu wako ni kuwa huduma za jamii zinafanyika na Lutheran na Katoliki tu, nimekueleza si kweli, kuna makanisa hata ya design ya akina Lusekelo nao wanatoa miasaada katika jamii , nao wana shule, vituo vya kulelea yatima n.k

My take hapa ni kuwa kama uhusiano wa serikali na hayo madhehebu huko katika misingi ya huduma za jamii sawa ni vizuri.

Ila picha inayoonekana ni kuwa kuna zaidi ya hapo, na reference ni Malasusa, hatujasema kuhusu Pengo na wengine. hao wengine is even worse

JK na askofu Gamanywa ni marafiki sana, na sidhani kama uhusiano wao unatokana na Gamanywa kuwa na huduma za jamii!!

Serikali ina uhusiano sana na Moses Kulola askofu mkuu wa EAGT, na huyu askofu kila leo ,mpaka leo, achilia mbali kuwaambia waumini wake JK chaguo la Mungu! EAGT haina huduma za jamii kama Lutheran na wengineo! na huyu nadhani Anthony Lusekelo alisahau kumtaja najua anamwogopa! na huyu askofu ana heshimiwa na serikali! huu uhusiano ua walakini! wakati Ngongo unaamini kuwa uhusiono wao uko decent wengine wanaona mbali sana, pengine Anthony alitaka aseme hivi, ila kaogopa, maana na yeye ana yake million!

Note that I am not supporting Lusekelo,nataka tujadili katika dimension tofauti, tusitetee tu na vitu ambavyo kesho tunaweza kujuta.


Kweli kabisa haya makanisa wanatoa huduma nzuri katika jamii, na sio lutheran tu mengi, kanisa la moraviana wana chuo kikuu huko mbeya na sijasikia,(pengine haumjui kiongozi wa moravian Tanzania)!!

Uhusiano huu umepitiliza basi, na swali ni kwa nini? Malasusa kuwa msemaji wa Lowassa kunatokana na huduma za jamii? kama Malasusa amekosea, watu ataaminije hao wengine?

Au unaweza kutuwekea dalili na namna gani ya kutambua huu uhusiano ni mzuri na huu uhusiano una walakini?
 
Back
Top Bottom