Mzee Kikwete, leo ndiyo leo; msituangushe

Mzee Kikwete, leo ndiyo leo; msituangushe

Wewe sema ulikuwa haumpendi magufuli. Hayo mengine ilikuwa tu njia ya kuonesha chuki zake kwake.
Kila siku ulikuwa unapiga kelel kuhusu barakoa mara lock down lakini leo kimyaa.
Kama hatupendi mtu unafiki unatoka wapi?

Wanafiki umewasahau?

Wengine hujawaona wanavaa barakoa sasa baada ya mwenzetu kufa.
 
Huyu mama namuona ni kiongozi mzuri mwenye busara nani Raisi ambae anauwezo wakuendeleza pale alipoishia magu ila sasa hawa wakora watamuandama kinoma naisi hatafanya kwa weledi wake zaidi hawa wakora watamzibiti... Mungu akusaidie raisi mama samia suluhu hasani ukapate wasaidizi wa kweli wasiwe mamluki" Mungu ibariki Tanzania, RIP JOHN MAGUFULI
 
Ndiyo Polepole awe VP? mmm haya sawa endelea kumuombea ili nyota yake iendelee kung'aa

Kwa maoni yangu huyo hapana. Huyo ni Chatto Inc. ndiyo waliotufikisha hapa tulipo kwenye mifarakano hii.

Ndiyo waliokuwa mstari wa mbele kuifagilia Corona inayotusambaratisha.

Hawakukemea lolote katika mengi fyongo waliyokuwa wanayaona.

Waliangalia matumbo yao tu.
 
Mh. Rais mstaafu Jakaya Kikwette tunayo matumaini makubwa kwenu kuwa ule muda ambao taifa hili limeusubiri mno hatimaye umewadia.

Ni wazi kuwa kila mtu katika nchi hii angalipendelea tuishi sote kwa usawa na haki. Utashi wa viongozi wa juu katika kufanikisha hayo ni jambo la muhimu sana.

Kufanya maamuzi magumu yatakayorejesha imani ya wananchi kwa nchi yao itakuwa jambo la msingi mno kwa sasa labda kuliko jambo lolote lile.

Pana watu wakiwamo watia nia wengi waliojaribu kuutaka urais na kura kuwa hazikutosha hali nafasi ni moja wakiwamo akina:

1. Asha Rose Migiro
2. Mzee Mwandosya
3. Bernard Membe
4. Mizengo Pinda
5. Frederick Sumaye
6. Edward Lowassa
7. Abdulhaman Kinana
8. Philip Mangula
9. Anna Mghwira
10. Dkt. Slaa
11. Dkt. Nchimbi
12. Nk nk

Watu ambao hawakuwamo ndani ya establishment ya sasa au wale waliokuwa na maoni tofauti kuhusiana na establishment ya sasa kwa hakika wangetufaa sana.

JK tupeni raha kwa kuandaa mustakabala mwema utakaotuletea mwanzo mpya.
Unategemea JK akupe raha? JPM alionesha jinsi awamu ya 4 na 3 zilivyozingua halafu bado unataka kurudi nyuma.
 
Kazi imekolea jamani
Siasa hizo watu ni wale wale jaman
Hivi hakuna wengine eti
Haya mambo ya kujaribu kuleta ''Candidates''wapya matokeo yake ndio mnatuletea watu kama Jiwe.Yaani mtu anakiri,''Uraisi haukuwepo kwenye malengo yangu,nilijaribu''.Tunatakiwa tuletewe watu waliojipanga kuwa maraisi kwa muda mrefu!
 
Unategemea JK akupe raha? JPM alionesha jinsi awamu ya 4 na 3 zilivyozingua halafu bado unataka kurudi nyuma.

JPM alidai hata awamu ya kwanza ilizingua.

Kwa JPM kila kitu kilikuwa ni uzinguaji isipokuwa chake.

Huyu hata aliwaona malaika ni wazinguaji akatamani kuwa kiongozi wao.

Siyo hivyo?
 
Huyu mama namuona ni kiongozi mzuri mwenye busara nani Raisi ambae anauwezo wakuendeleza pale alipoishia magu ila sasa hawa wakora watamuandama kinoma naisi hatafanya kwa weledi wake zaidi hawa wakora watamzibiti... Mungu akusaidie raisi mama samia suluhu hasani ukapate wasaidizi wa kweli wasiwe mamluki" Mungu ibariki Tanzania, RIP JOHN MAGUFULI

Pana wakora wanajiita Chatto Inc. hao ni wa kuogopa kuliko ukoma!
 
JPM alidai hata awamu ya kwanza ilizingua.

Kwa JPM kila kitu kilikuwa ni uzinguaji isipokuwa chake.

Huyu hata aliwaona malaika ni wazinguaji akatamani kuwa kiongozi wao.

Siyo hivyo?
Natamani ningekuwa na nguvu ya kujibu hoja zako lakini sina wewe tambua soon utajua mwelekeo wa serikali ya Rais Samia kwasasa you can speculate as much as you want.
 
Mh. Rais mstaafu Jakaya Kikwette tunayo matumaini makubwa kwenu kuwa ule muda ambao taifa hili limeusubiri mno hatimaye umewadia.

Ni wazi kuwa kila mtu katika nchi hii angalipendelea tuishi sote kwa usawa na haki. Utashi wa viongozi wa juu katika kufanikisha hayo ni jambo la muhimu sana.

Kufanya maamuzi magumu yatakayorejesha imani ya wananchi kwa nchi yao itakuwa jambo la msingi mno kwa sasa labda kuliko jambo lolote lile.

Pana watu wakiwamo watia nia wengi waliojaribu kuutaka urais na kura kuwa hazikutosha hali nafasi ni moja wakiwamo akina:

1. Asha Rose Migiro
2. Mzee Mwandosya
3. Bernard Membe
4. Mizengo Pinda
5. Frederick Sumaye
6. Edward Lowassa
7. Abdulhaman Kinana
8. Philip Mangula
9. Anna Mghwira
10. Dkt. Slaa
11. Dkt. Nchimbi
12. Nk nk

Watu ambao hawakuwamo ndani ya establishment ya sasa au wale waliokuwa na maoni tofauti kuhusiana na establishment ya sasa kwa hakika wangetufaa sana.

JK tupeni raha kwa kuandaa mustakabala mwema utakaotuletea mwanzo mpya.
Hapo Dr Mchimbi anafaa
 
Wewe sema ulikuwa haumpendi magufuli. Hayo mengine ilikuwa tu njia ya kuonesha chuki zake kwake.
Kila siku ulikuwa unapiga kelel kuhusu barakoa mara lock down lakini leo kimyaa.

Huku sasa ndiko kunakoitwa kujishebedua.

Hatupendi mtu. Yenye kutukera tulikuwa wazi hakutusikia.

Kutelekezea watu gonjwa baya hili yeyote halitamwacha salama.
 
CCM asilia inarudi ulingoni,sio masalia tena. Membe kwa mbali anapasha... Covid 19 et al itabidi mtafute sehemu yenu.. Wenye chama wamekuja
 
Baada ya kumaliza kusoma nimejikuta nimekasirika Sana kuona upeo wako wa hali ya chini hivi na nyumbani unategemewa Kama kibaba
emoji848.png
emoji34.png

Nakubaliana na wewe Chatto Inc. Hii ni habari mbaya sana kwenu. Wasukuma ni muda wa kupumzika na kujitafakari. Hasira hazitawasaidia.

Mjini wanasema: "imeisha hiyo!"

Chatto Inc. big NO!
 
na samia asipofanya mnayotaka si mtamchukia?.
Maisha bila UNAFIKI HAYAENDI
Huku sasa ndiko kunakoitwa kujishebedua.

Hatupendi mtu. Yenye kutukera tulikuwa wazi hakutusikia.

Kutelekezea watu gonjwa baya hili yeyote halitamwacha salama.
 
Hakuna jipya ndani ya zimwi liitwalo CCM, halikuli ukakwisha, uozo ni uleule tu.
Katiba mpya ndio mwiba wa yote haya, na ndio maana mwendazake hakutaka kabisa kusikia kitu hiki.

Hakuna anayepinga ila mwanzo wa ngoma jombi.
 
Kwa hiyo kikwete ndiye unategemea akuletee Tanzania mpya? Mbona hiyo Tanzania mpya alishindwa kuileta kipindi akiwa rais? Wewe ni ngumbalu mkondo B! Usijiabishe mbele ya Kadamnasi ficha japo ufinyu wa uwezo wako wa kufikiri.

Aliyeileta ndani ya kipindi chake yuko wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom