Mzee Kawawa afariki dunia!

Mzee Kawawa afariki dunia!

Inasikitisha..Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi Amina.
Tumuombe Mungu asiruhusu wanajimu wetu uchwara kukihusisha kifo cha Mzee kawawa na ushindi wa CCM 2010 kama wlivyochawia kifo cha Lawrence Masha...ahh sory Lawrence Gamma
 
Ulale pema SIMBA WA VITA. Nitakukumbuka daima kwa yale yote uliyojitolea kuyafanya kwa ajili ya taifa letu.
 
RIP simba wa vita nakutakia maisha mema poponi tafadhali usiwasimulie Nyrere na Moringe uliyo yaacha huku duniani(Tanzania) kama ufisadi kwani watahuzunika sana mungu akulaze pema ppeponi


Nimeipenda sana hii
 
Program ya Kawawa inaendelea TBC, kumbe Mwalimu Nyerere alifundisha Tabora St. Marys na sio Tabora School. Kawawa akiwa mwanafunzi Tabora School ndipo alipomuona Mwalimu kwa mara ya kwanza mwaka 1948 alipokuja Tabora School kwenye debate ya Elimu ni bora kuliko Mali, Nyerere alimwaga nondo ukumbi mzima ukishangilia na yeye akaanza kumstaajabia.

RIP SIMBA WA VITA.
 
Simba wa Vita anaendelea kuunguruma TBC, anazungumzia mapambano akiwa kiongozi wa wafanyakazi, aliitisha mgomo wa wafanyakazi wa ndani mwaka 55, kulazimisha kuongezwa mshahara toka Shilingi 5 kwa mwezi hadi 20. Fedha zilpatikana baada ya Kawawa kuitwa London kwenda kunegotiate.
Makange na Baghdelah walitiwa ndani baada ya kuandika makala kuhusu dharau za DC wa Geita kwenye gazeti la Mwafrika.

Pia anasema japo uhuru ulpatikana bila kumwaga damu, kuna damu za watanzania zilimwagika katika mapambano na wakoloni.

Program inaendelea.

RIP RASHIDI MFAUME KAWAWA.
 
Tanzania and CCM in particular has lost a brave hero aho has stood against 'mafisadi' in his party. If JK is to honour him well, grave as he looked at him on his deathbed, should purge Mafisadis from CCM.
Rest In Peace Mzee Kawawa, we wish other elders will emulate your devotion and principled character.
 
Kawawa anazungumzia kuanzishwa kwa Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na Operesheni Vijiji. Anakiri ilitumika nguvu kubwa, watu walikuwa hawataki kuhama, 'tulikuwa wakali', hatukuwa na mchezo mchezo, ilifikia mahali wakisikia Kawawa yuko kijiji fulani, vijiji vinavyofuata, walihama usikuusiku kabla hajawafikia.

Anazungumzia Ujamaa, anasema nia Ujamaa ni njema, kila kitu ni mali ya umma, hakuna matajiri na masikini, kila kitu ni bure, maji bure, elimu ure, hospitali bure. Hata hivyo anasikitikia kufikia mahali ujamaa umeshindwa, serikali aiwezi tena kutoa huduma za bure.

Anamalizia kwa kutoa wito kuishika sana elimu kama mkombozi wa kweli kwa Mtanzania, ni kusoma ili ujitegemee. Kosoma ni kuamsha elimu ili uweze kuona mbali, ujitegemee sio kusubiri kajiriwa.

Program inaendelea TBC.

RIP RASHIDI MFAUME KAWAWA.
 
Jamani, give me a break. We already have too many holidays. Katika siku ya Kawawa tutafanya nini? Tutamkumbuka nini? Siku ya Nyerere watu wanafanyaga nini? Ya Karume je? Hata watoto wetu hatuwaambii tunakumbuka nini siku hizo, basi watu kazi yao ni kulewa na kulala tu. Jamani, itakuwa aibu tukifanya jambo hili. Mimi nadhani tungekuwa na siku moja tu ya waasisi wa taifa, tukawakumbuka wote kwa pamoja, tuache kuongeza siku za uvivu, tuchape kazi.

Many thanks Chupaku and others for the challenge. Sikuwa na maana kuwa hiyo siku iwe ya mapumziko. Binafsi ningependa sana siku za Nyerere na Karume ziwe ni siku za kazi.

Lamsingi kama taifa tukubaliane nini hasa tufanye siku hizo za waasisi wakuu wa taifa letu--Kambarage; karume na Kawawa. Sokoine japo hakuwa mmoja wa waasisi wa taifa letu, anastahili kuwa mmoja wa mashujaa wetu wa kukumbukwa kila mwaka.

Hongera sana kwa wazo la kuwa na siku moja ya kipekee ya kuwakumbuka waasisi wetu.
 
Tumepoteza mmoja waasisi na viongozi shupavu wa Taifa letu.

Pole Mh. Vita Kawawa, poleni wana familia wote.

Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi - Ameen
 
Babu yetu Kawawa hatutakuwa na we kimwili lakini daima tutakuwa nawe kiroho. Tunakuombea pumziko la amani huko uendako. Raha ya Milele umpe ee bwana, na Mwanga wa Milele umwangazie, Astarehe kwa amani AMINA
 
Kumbe Mzee Kawawa ndie aliyekuwa Mtanzania wa Kwanza kuhojiwa na TBC ya mkoloni mwaka 1955. Akaambiwa awe mtangazaji, eti aliambia sauti yake inakwaruza sana!

Anashangaa kumbe filamu zake zilipigwa marufuku na serikali!

Ameomba msamaa Watanzania, kuwa ni kweli alikuwa mkali sana lakini ni kwa nia njema katika kutekeleza maagizo ya chama, lakn yeye sio katili.

Pia anazungumzia kuhamishwa hamishwa toka Waziri Mkuu, mpaka waziri asiye na wizara maalumu, kwake anasema ilikuwa Cheo ni dhamana, hivyo chochote unachopewa unakubali. 'he was really humble'.

Program imemalizika, David Wakati ameaga.

Imeingia video nyingine ya Kawawa kwenye mkutano mwingine.

Unafortunately, hakuna back annoucement yoyote toka TBC kusema ni lini na wapi, ila nimesikia Kidumu chama cha Mapinduzi, kwa jinsi alivyo kijana hii lazima itakuwa ni mwaka 1977.

RIP SIMBA WA VITA.
 
Mi kusema kweli ni kwamba kuhusu Kawawa mi nimeishia kumsoma tuu,yaani kama story za kina malcom x na wengineo,sijawahi kumjua ktk maisha yake,but all in all may almighty God rest his lovely soul in everlasting life!!
 
Amemaliza ng'we yake..
Mungu ampumzishe kwa Amani..
Nashangaa baadhi ya viongozi wanaweza kupata maombolezo kama haya???
 
Mi kusema kweli ni kwamba kuhusu Kawawa mi nimeishia kumsoma tuu,yaani kama story za kina malcom x na wengineo,sijawahi kumjua ktk maisha yake,but all in all may almighty God rest his lovely soul in everlasting life!!

Kuna haja ya kutengeneza DVD maalum inayohusu Maisha yake na nini alichoifanyia nchi yetu. TBC naamini wakishirikiana na JF tunaweza kupata DVD nzuri sana kwa ajili ya Watanzania wenzetu na hasa wanafunzi katika ngazi mbalimbali za elimu nchini. Wanafunzi wetu wapate fursa ya kuangalia wakiwa shuleni.

Kwa upande mwingine, tuvipe changamoto vituo vyetu vya televisheni na redio (vya umma na binafsi) kuwa na programu maalum kila wiki kwa ajili ya Waasisi wa taifa letu. Saa moja kila wiki inatosha kwa kuanzia.
 
Kutokana na Umuhimu wa huyu Mzee,
Inatakiwa Serikali Iandae msiba wake kufanyika Uwanja wa Taifa, Ili Watanzania Wapate Muda wa kutoa Salaam Zao za Mwisho.
Sasa Sijui Waislam miongozo yao inasemaje?
Ila Anastahili heshima ya namna hiyo.
Na ikiwezekana wampeleke pale nyumbani Songea Uwanja Wa Majimaji ili mpaka bibi zetu wapate nafasi ya kumuaga

Benno
+255713092952
+255755387572
 
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un
To Allah we belong and to Him we shall return
Sisi ni wa Mwenyezi Mungu Na Kwake Hakika Tutarejea

“Oh Uncle Rashid is not with us anymore... Insha'Allah, soon or letter this will happen to all of us,
our life on earth is like a loan.
We have to remember that one day, Allah will take us as well.”

Rabbana Aatina fii'd dunia hasanatu'n wafil aakherat hasanatu'n
wakin azaaban naar...!

 
Mzee Kawawa ni kati ya viongozi waliolijenga taifa letu. Wengi wao wametuondoka. Tumebakiwa na wachache kutoka miaka ile.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.
 
Back
Top Bottom