Mzee Faraj Katalambula Amefariki Dunia

Mungu amrehem mzee huyu ambaye kwangu mimi kupitia vitabu vyake vya hadithi niliweza kujenga reading culture. RIP mwanafasihi mahili na mmoja wa magwiji wetu wa fasihi na utunzi. Upumzike kwa amani. AMINA
 
Kezilahabi, Mkerewe yuko Botswana sasa. Alipigwa ban na Kanisa Katolic kuhusu kitabu hicho cha Rosa Mistika. Nakumbuka sana kitabu chake cha 'Dunia uwanja wa fujo.

Hakika msiba wa Mzee Katalambula umefufua mengi! Nilikuwa natafuta jina la nani mtunzi wa Rosa Mistika maana nilisoma kitabu hicho katika umri wa barehe basi nilikuwa na fantasize vitu lukuki nikisoma kitabu hicho!

Kizazi kipya wanajua kunukuru (sina hakika na kiswahili changu kwenye neno fasaha) tungo za mapenzi na upuuzi mwingine na KUANDIKA RIWAYA ndio aibu tupu!

Sidhani hata kama wanajua (watunzi na waandishi wetu wa kizazi kipya) kuwa walikuwepo watunzi na waandishi ambao walivyotupatia kamwe havitotoka katika vichwa vyetu kwa ufasaha na umahiri walioutumia!
 
I believe Pili Pilipili was and to me is the best Play, yaani ukiisoma ile kitu huwezi weka chini hadi last page, tumepoteza shujaa wengi wa waliobakia ni wale wa kukopi na kupesti hadithi toka kwenye mtandao..... sorry kwa wanaomfahamu vizuri hivi ndie huy huyu alieandika na ile riwaya ya SIRI ya SIFURI???

Siri ya Sifuri iliandikwa na Mohamed Said Abdula (Mhusika mkuu wa vitabu vyake ni bwana Msa).

RIP Mzee Katalambula.
 
Poleni wote jamani alini~Insipire saaaana jamani PUMZIKA KWA AMANI Faraj Katalambula...

Hivi Kezilahabi aliyetunga ROSA MISTIKA...yu wapi? Nakumbuka kipande cha Hadithi yake " Tulikuwa tukisikiliza NEGRO SUCESS NA MATONDO YA BEYA"

Euphrase Kezilahabi, Mkerewe wa Namagondo, Nansio.

Web: www.litprom.de/littrans.detail.php ; University of Botswana, Gaborone.

Napenda kazi zake kama:

Riwaya: Rosa Mistika (1971), Dunia uwanja wa fujo (1975), Gamba la nyoka (1979), Kichwamaji (1974), Nagona (1990),
Mzingile (1991)

Mashairi: Kichomi, Dhifa n.k.

Tamthiliya: Kaptula la Marx
 
Hakika msiba wa Mzee Katalambula umefufua mengi! Nilikuwa natafuta jina la nani mtunzi wa Rosa Mistika maana nilisoma kitabu hicho katika umri wa barehe basi nilikuwa na fantasize vitu lukuki nikisoma kitabu hicho!

Kizazi kipya wanajua kunukuru (sina hakika na kiswahili changu kwenye neno fasaha) tungo za mapenzi na upuuzi mwingine na KUANDIKA RIWAYA ndio aibu tupu!

Sidhani hata kama wanajua (watunzi na waandishi wetu wa kizazi kipya) kuwa walikuwepo watunzi na waandishi ambao walivyotupatia kamwe havitotoka katika vichwa vyetu kwa ufasaha na umahiri walioutumia!

Ni kweli mkuu usemayo. Zamani kidogo tulikuwa na : Balaa (Hammie Rajab) ), Watanitambua (S.A.M Kitogo), Tabu (Anthony Komanya), Pashkuna, Mapenzi kwa kaya, Shuga Dedi, Operesheni tajiri ( Kassim Mussa Kassam) n.k.
Watunzi wa vitabu, mashahiri na riwaya sijaona wakati huu watu kama hawa hapo juu, wenye mvuto sana ktk jamii yetu. Kulikoni?

 
FAMBO wa riwaya ya SIMU YA KIFO! Ilikuwa ni kifupisho cha Francis Andrew Mbozia..

R.I.P. Mzee Katalambula
Sterling alikuwa ni Inspector Wingo.
Jina kamili ni Faraj Hussein Hassan Katalambula.

Enzi hizo ukiondoa magazeti ya Spear ya Kenya, jarida lake la Filam Tanzania, ndio lililokuwa jarida la kwanza la mapicha nchini, baadae likafuatiwa na Sani!. 'Simu ya kifo' ndio ilikuwa novo kali ya upepelezi enzi hizo kabla ya Musiba kuibuka na 'Kufa na Kupona'.

RIP F.H.H.KATALAMBULA!.
 
FARAJ KATALAMBULA KUZIKWA MKOANI TABORA




Aliyekuwa mtunzi mahiri wa vitabu vya hadithi na riwaya nchini marehemu Faraj Katalambula (kulia) anatazamiwa kuzikwa kesho Isevya mkoani Tabora majira ya saa kumi jioni.

Faraj Katalambula alifariki juzi saa kumi na mbili jioni katika hospitali ya rufaa Muhimbili. Faraj Katalambula ambaye ni mmoja wa watunzi wa vitabu mahiri kupata kutokea atakumbukwa zaidi kwa utunzi wake wa kitabu kilichosomwa sana cha ' Simu ya Kifo'. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa John Katalambula mwanae marehemu.

Ewe Mwenyezi Mungu ilaze Mahali Pema Peponi roho ya marehemu, Amen.
From: g sengo

NB: Nimeambiwa kuwa atazikwa leo huko Isevya, TABORA. R.I.P. Faraj Katalambula.

Bwana Alitoa Na Bwana Ametwaa, Jina L a Bwana Lihimidiwe....Pole Tanzania, Pole Tabora na Pole waandishi wa Vitabu na Riwaya..
Bwana Alitoa Na Bwana Ametwaa, Jina L a Bwana Lihimidiwe....Pole Tanzania, Pole Tabora na Pole waandishi wa Vitabu na Riwaya..
 
I believe Pili Pilipili was and to me is the best Play, yaani ukiisoma ile kitu huwezi weka chini hadi last page, tumepoteza shujaa wengi wa waliobakia ni wale wa kukopi na kupesti hadithi toka kwenye mtandao..... sorry kwa wanaomfahamu vizuri hivi ndie huy huyu alieandika na ile riwaya ya SIRI ya SIFURI???

Hapana, Siri ya Sifuri kiliandikwa na Mohammed Said Abdullah.
Faraji Hussein Hassan Katalambula ni maarufu kwa kitabu cha riwaya ya Simu ya Kifo.
Katalambula alitunga pia, Buriani na Pili Pilipili.
Magazeti yake ya Film Tanzania yalitoa tamthilia kwa njia ya picha. alikuwa very creative.
Filamu pekee ya bongo inayotazamika ni ile ya Simu ya kifo iliyokuwa based kwenye kitabu chake.
Itafuteni ni nzuri, mtayarishaji wake ni marehemu Hammie Rajab aliyewahi kuwa gwiji la utunzi nchini.
Kilicho haribu hiyo filamu kidogo ni uwepo wa Mrisho Mpoto aliyeigiza kama dokta Francis Mbozia aka Fambo.
RIP FHHK
 
Mungu Aiweke Pema Roho yake.

Kwa nini mgomo usihusike na ikiwa amefariki Juzi, madakitari wameanza kazi leo.

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Madaktari siyo Mungu! Kifo ni hadi Mungu apende.Madaktari hufanya kazi kwa mapenzi ya Mungu.
 
Dah! Faraji namfahamu sana, siyo ndugu yangu ila ninamfahamu kwa karibu mno tangu utotoni akiwa anaishi pale Tabora miaka ile ya sabini na baadaye tukakutana naye hapo Dar akiwa anaishi Sinza pamoja na mdogo wake Profesa Katalambula wa hapo UDSM.

Faraji alikuwa mtu mwenye akili sana ila nadhani hakupata mazingira mazuri ya kutumia akili hiyo. Tangu alipoandika majarida ya Film Tanzania mwishoni mwa miaka ya sitini na mwanzoni mwa miaka ya sabini akiwa na characters za akina Unyeke, Tojo, Hamisa na Amina kabla hajamalizia na ile ya Simu ya Kifo, hakujatokea watunzi wengi wenye mvuto wa aina hiyo zaidi ya yule mtunzi wa Kuli, na labda na Profesa Kezilahabi. Akina Musiba, na wengineo wote walikuwa ni wanafunzi tu mbele ya nguli huyu; kitabu chake cha Simu ya Kifo kilitumika katika kutoa elimu ya uandishi wa vitabu vya kiswahili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Mungu ailaze pema peponi roho ya merehemu.
 
mungu mlaze mahali pema peponi mzee faraja katalambura.kitabu chake cha simu ya kifo nimekisoma mara zaidi ya mia mbili tangia nikiwa darsa la tatu mpaka namaliza master hapa USA. moja ya vitu muhimu nilivyotaka kuja navyo marekani ni kitabu cha Allan quarteman na simu ya kifo. kweli huyu alikuwa na kipaji kikubwa sana sana cha usanii. msiba huu umenishtua na mimi namuona Faraj kama ndugu yangu wa karibu kwa jinsi nilivyokuwa namshabikia. He is going to meet his maker!
 
RIP Mzee wetu. Asante kwa mchango wako na kuiacha dunia pazuri kuliko ulivyoikuta! Nasi tutajitahidi kuacha japo mchango kidogo kuiboresha zaidi
 
Huyu jamaa kumbe ni Prof. sasa? Una maanisha Hassan Katalambula? Nakumbuka kuwasiliana naye miaka ya 90 wakati Tanzanet imeanzishwa na kuanza kukutanisha Watanzania dunia nzima.

Katalambula uandishi wake hadi leo nashindwa kujua kama alisoma sana vitabu vya James Hadley Chase au alikuwa akiangalia sana film za kijasusi za USA. Kwa kweli jamaa aliweza sana kutunga kitabu ambacho kingeliweza sana kutokea kwenye mazingira yetu kwa wakati ule. Tofauti na Musiba ambaye aliingiza sana vikorombwezo ambavyo labda kwa leo ndiyo ungelisema vinawezekana na kuwa jambo la kawaida ila si kwa miaka ile.

Nina imani kuna siku atakuja FILM Director mzuri na kutengeneza film yenye hadhi ya KATALMBULA.

Kama jamaa angeliwezeshwa, nisingelishangaa kuwa angelikuwa kachukuliwa Hollywood au Bollywood kuandika film.
Dah! Faraji namfahamu sana, siyo ndugu yangu ila ninamfahamu kwa karibu mno tangu utotoni akiwa anaishi pale Tabora miaka ile ya sabini na baadaye tukakutana naye hapo Dar akiwa anaishi Sinza pamoja na mdogo wake Profesa Katalambula wa hapo UDSM.

Faraji alikuwa mtu mwenye akili sana ila nadhani hakupata mazingira mazuri ya kutumia akili hio. tangu alipoandika majarida ya Film Tanzania mwishoni mwa miaka ya tisini na mwanzoni mwa miaka ya sabini akiwa na characters za akina Unyeke, Tojo, Hamisa na Amina kabla hajamalizia na ile ya Simu ya Kifo, hakujatokea watunzi wengi wenye mvuto wa aina hiyo zaidi ya yule mtunzi wa Kuli, na labda na Profesa Kezilahabi. Akina Musiba, na wengineo wote walikuwa ni wanafunzi tu meble ya nguli huyu; kitabu chake cha simu ya Kifo kilitumika katika kutoa elimu ya uandishi wa vitabu vya kiswahili kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Mungu ailaze pema peponi roho ya merehemu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom