Mzee Butiku: Tukubali tunaye Rais

Mzee Butiku: Tukubali tunaye Rais

Kuwe na uchaguzi, kusiwe na uchaguzi, anayeziweka serikali za mataifa ni Mungu pekee!. Hata serikali za kidikiteta, hata serikali za kidhalimu, ni Mungu ndie huweka serikali za mataifa yote!. Je, wajua japo Mungu huweka Serikali za Mataifa kuna Serikali/Viongozi wa Mungu na Shetani? Tusiruhusu Ushetani kwa kuchagua mashetani

P
Kwa hiyo Mungu, muweza wa yooote alishindwa kufuata njia nyingine yoyote ila kuruhusu yatokee yaliyotokea October 29.

Ili tu amuweke samuya madarakani???
 
Mimi nakubali kwamba tuna Rais, japo nataka nione utu tuliohimiza kwenye kampeni tuuone live bila chenga!

Ifikie mahali tufanye tulichokihubiri Kwa watu waliotuchagua japo Kwa sarakasi nyingi!!
 
Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku, amewataka Watanzania kukubaliana na uhalisia kwamba nchi tayari ina Rais aliye tayari kwa maridhiano.

Butiku ametoa kauli hiyo leo Machi 4, 2026, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Maridhiano (Maridhiano Day) yaliyofanyika katika ukumbi wa Kwa Tunza, wilayani Ilemela, mkoani Mwanza.

Akizungumza katika hafla hiyo, amesema kuwa tume iliyoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeongezewa muda hadi mwezi Aprili, na kuwataka wananchi kuwa na subira.

“Nimesikia tume iliyoundwa na Rais Samia imeongezewa muda mpaka mwezi wa nne (Aprili). Tukubali tusubiri aje atuambie jambo na lije litusaidie kwenye mazungumzo,” amesema Butiku.

Aidha, amewataka viongozi wa dini nchini kuendelea kuhimiza haki na amani kwa wakati mmoja, akisisitiza kuwa hakuna amani ya kweli bila haki.

Huu ujumbe wapewe wale wa kanisa la mitume maana hawana Cha kumfanya na huyo ndio Rais Hadi 2030.

Utawasikia wanahubiri msamaha harafu wao Wameshindwa kusamehe 😂😂😂😂😂

Bora na mara 100 wale wa kulipa kisasi wako real kuliko Hawa waigizaji.

Kila siku nakwambia hizo dini zenu ni miradi kama biashara zingine
 
Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku, amewataka Watanzania kukubaliana na uhalisia kwamba nchi tayari ina Rais aliye tayari kwa maridhiano.

Butiku ametoa kauli hiyo leo Machi 4, 2026, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Maridhiano (Maridhiano Day) yaliyofanyika katika ukumbi wa Kwa Tunza, wilayani Ilemela, mkoani Mwanza.

Akizungumza katika hafla hiyo, amesema kuwa tume iliyoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeongezewa muda hadi mwezi Aprili, na kuwataka wananchi kuwa na subira.

“Nimesikia tume iliyoundwa na Rais Samia imeongezewa muda mpaka mwezi wa nne (Aprili). Tukubali tusubiri aje atuambie jambo na lije litusaidie kwenye mazungumzo,” amesema Butiku.

Aidha, amewataka viongozi wa dini nchini kuendelea kuhimiza haki na amani kwa wakati mmoja, akisisitiza kuwa hakuna amani ya kweli bila haki.

Anajitahidi kulazimisha afanane na Mwalimu Nyerere kuanzia Kuhutubia, kujenga Hoja na kuvutia Hadhira ila kote hapatii na anaharibu tu.

Angekuwa na Akili angetulia tu kama Wazee wenzake wengine waliofanya makubwa nchi hii walivyoamua kutulia ila kulinda Heshima zao.

Kifupi anaboa sana tu na sijui kwanini hajishtukii au hata wanafamilia wake hawamwambii atulie. Analazimisha mno aonekane ndiyo Nyerere wa sasa Tanzania wakati hana na kamwe hatokuwa na uwezo kama aliokuwa nao Mwalimu Nyerere japo ana Undugu nae kupitia Mama zao.
 
Kwani nani anabisha?
Amalize muda wake aondoke zake.
 
Kwa hiyo Mungu, muweza wa yooote alishindwa kufuata njia nyingine yoyote ila kuruhusu yatokee yaliyotokea October 29.

Ili tu amuweke samuya madarakani???
Kuna maovu mengi yanatokea duniani, kwa kumruhusu shetani kufanya yake,
Mungu hajaweka hii serikali bali ni shetani ingawa naye shetani kaumbwa na Mungu.
Anayeweka serikali za mataifa ni Mungu tuu, ila humruhusu shetani kuwarubuni watu wa Mungu na kutenda mambo ya kishetani!.

P
 
Kuna maovu mengi yanatokea duniani, kwa kumruhusu shetani kufanya yake,

Anayeweka serikali za mataifa ni Mungu tuu, ila humruhusu shetani kuwarubuni watu wa Mungu na kutenda mambo ya kishetani!.

P

Tunatofautiana kwa hilo serikali hii ya Samia ya sasa imewekwa na mashetani nantuombe Mungu atuepushe na mashetani. Watu binafsi inawezekana wametubu kivyao na ni watu wa Mungu lakini hii serikali ni ya mashetani. Wewe baki na msimamo wako na mimi wangu
 
Hii anawajibu Katoliki jinsi walivyo mtendea sa100. Nadhani hawa wazee wanang'ata na kupuliza wao wenyewe hawapendezwi na huyu mama ni basi
 
Back
Top Bottom