Ohhhh thanks.
That will be easier
Oukey acha kwa kifupi nishirikishe moja ya safari nilizoenda nje ya Tanzania. Ilikuwa miaka mingi tuu huko nyuma na nilienda Italy eneo la Milano au Milan.
Nilikuwa mwenyewe, safari niliiandaa kwa mwaka mzima kwa maana ya booking ya ndege nilitumia KLM, hoteli nilibook online nikachagua hoteli zilizokuwa na offer. Nilienda msimu wa mwezi wa 12 hivyo kubook mapema ilinisaidia kupata hoteli ya bei rahisi. Mara nyingi huwa napenda kukaa eneo ambalo naweza kutumia usafiri wa uma kutoka airport ili nijionee mambo na kujifunza na kushangaa humohumo bin kutoa ushamba.
Nilikaa kule kwa wiki mbili kamili yaani siku 14 ukitoa siku za kusafiri na nilifanikiwa kufika miji mingine ya Italy kwa kutumia usafiri wa Treni.
Kitu kikubwa ni kuzingatia afya yako, pamoja na kukata bima ya afya ya muda ila huwa natengda hata dola 200 kwa ajili ya matibabu incade unagonjweka.
Na mwezi mmoja kabla ya safari nafika zahanati za serikali wananifanyia vipimo kujihakiki niko fit kusafiri (hasa kwa sie umri ulioenda maana waweza kaa kwenye ndege mkifika miguu hainyanyuki kumbe misuli imekakamaa kwa kukaa mkao mmoja muda mrefu eehehehehe) hapa ndo utatambua umuhimu wa business class na first class.
Japo huwa najiuliza mbona kwenye ndege hakunaga second class??
Tuachane nalo, mnaona siweki gharama maana nimejaribu kutafuta nyaraka sizioni na sikumbuki jumla ilinigharimu kiasi gani.
Ila kupanga safari mwaka mmoja kabla au miezi sita kabla unasevu gharama kubwa tuu.