Eric Cartman
JF-Expert Member
- May 21, 2009
- 11,967
- 11,212
Kwa mantiki hiyo JK, Nape, Mukama na wanachama wengine wa CCM ni mwili wa nyoka ambaye anaweza kuotesha magamba. Tumuue nyoka ili asiendelee kutuuma ( utawala mbovu, uwizi wa maili ya umma)- Ukitaka kumua nyoka unaanzia kichwani kwanza! hawa mapacha watatu ndio hasa kichwa cha nyoka na magambas!
William @ NYC, USA.
- baba yangu hahusiki na anything kama huna cha kuchangia kwenye mjadala wa taifa ni bora ukakaa pembeni ukaachia wanaotaka kuelimishana, kama una tatizo na baba yangu wewe ni kumfungulia topic yake! ha! ha! siku njema sana mkuu!
William @ NYC, USA.
William,
kuliwahi kuzuka tetesi kuwa Patel yule mmoja wa wachota hela za EPA alifinance haruc ya mzee wako na hapo ndipo anapohusishwa na yeye kuwa mmoja wa walionufaika na pesa za EPA, je hili unalisemaje, kama ulishawahi kulijibu sio vibaya ukirudia mkuu
Na-hope huko tunakokwenda hatutatakiwa kudhibitisha au kukanusha tuuma za wazazi/ndugu zetu ambao wako hai na wanaweza kujibu shutuma zao wenyewe. Kama tukifanya hivi tutakua tunanyamazisha independent voices. Na vile vile chochote atakachosema William ni wazi very few if not all of us will doubt because of conflict of interest. Naomba pia nitoe angalizo:tusije ku-assume watoto ambao wazazi wao wanaonekana walikua wazalendo wakweli ndio wenye haki yaku-voice their opinions. Uliyeuliza swali unaweza kuwa una-good intentions as I also believe in freedom of speech. Lakini I also believe we should judge people as individuals wanapotoa maoni yao otherwise tutaanza kupoteza mweleko wa thread ikaishia kuwa too personal ambayo haitusaidii kwenye mustakabali wa nchi yetu.
NN unapokuwa rais ni issue nyingine hasa kwa nchi zetu hizi.
Lakini hali imekuwa mbaya kiasi hata mawaziri, makatibu wakuu nao wanaiba zaidi ya alichoiba rais . Kwangu Binafsi bora fisadi awe mmoja tu rais wengine hawaruhusiwi.
Tukimaliza tatizo la ufisadi la mwaziri na watendaji ndo tunahamia kwa hicho cheo amabcho kiko above the law. Alkini hawa kina mkapa, Mwinyi na JK tuwaweke pmbeni tu.
Willy,
Mkuu wangu shukran sana kwa kuweka ukweli huu ambao hauna ushabiki labda tu mtu apende kushabikia..Sisi wote hapa tunaomba hawa mapacha watiwe ndani kama walivyotangulia kina Yona na Mramba kwani tuna ushahidi mkubwa zaidi dhidi yao na mahla pekee panapoweza kuthibitisha kwamba wao ni innocent/Guilty ni mahakamani na as long as they are presumed innocent hakuna sheria inayokataza kukamatwa kwao.Hatuwezi kukataa ukweli huu kwa sababu ati kuna Mafisadi wengi CCM ama nchini kwani kama ingekuwa hivyo tusinge wakamata hata wezi maanake wapo wengi.
Nakumbuka wakati JK anaingia madarakani alisafisha Polisi na kukamata majambazi kiasi kwamba tuliweza kusafiri, kulala na kutembea kwa amani ingawa sii majambazi wote walokamatwa isipokuwa ilitoa onyo kali kwa majambazi. Na katika majambazi hao wapo walioshinda kesi zao na wengine kupelekwa lupango ndivyo sheria inavyo operate.
Na hata walipokamatwa Yona na Mramba, mkuu wangu rushwa iliogopwa kama ukimwi na kwa mara ya kwanza ilikuwa ukienda ofisi za serikali utahudumiwa haraka na bila kutoa rushwa. Lakini pamoja na yote haya hivi vilikuwa vita vya Titans, kumbe ilikuwa kugombea nafasi za Kufisadi lakini toka Lowassa ameondolewa madarakani serikali ya JK imekwenda likizo, yaonyesha JK hawezi kuongoza pasipo Lowassa na mtandao. Serikali hii imekuwa sii ya kufuatilia utekelezaji wa maagizo Ujambazi na Ufisadi umerudi tena kwa kasi baada ya serikali kwenda rikizo.
CCM na JK kama kweli mnataka kujuvua magamba kukomesha Ufisadi basi ile ile dawa ya Lowassa na Sokoine itumike kupambana na Ufisadi kwani inawezekana. Sumu ya nyoka pia ni snake venom antidote!
William,
..na ufisadi uliotumika kumuingiza JK madarakani unaushughulikia namna gani?
..JK,Lowassa,na Rostam, wameunda mtandao ambao ni chama ndani chama[ccm].
..katika kufanya hivyo wametumia fedha chafu, mbinu chafu na fitina dhidi ya wenzao ndani ya CCM, rushwa na hongo ktk uchaguzi n.k n.k.
..haya mambo mlitakiwa myashughulikie tangu mwaka 1995 lakini hamkufanya hivyo. kuyashughulikia sasa hivi wakati mtandao wameshashika chama ndiko kunakusababisha muwe na kigugumizi.
..UGUMU WA KUWAFUKUZA LOWASSA NA ROSTAM NI KWAMBA MWENYEKITI NAYE NI MDAU KTK UFISADI MWINGI WALIOUFANYA.
NB:
..na kile kitendo cha Mwenyekiti wa Chama kuwapigia kampeni za waziwazi hivi hakistahili hata kutolewa karipio?
..hivi kitendo kile siyo dalili za wazi kwamba Mwenyekiti anawaunga mkono mafisadi?
..let me explain: Takukuru iko chini ya Ofisi ya Raisi. Sophia alikuwa waziri wa nchi Utawala Bora. Kwa msingi kisheria Waziri wa Utawala Bora, and particularly Takukuru, ni Raisi. sasa Raisi alipokuwa anawapigia kampeni watu wanaoshitakiwa na Takukuru kweli mnamuelewa. Halafu Takukuru ni chombo cha ulinzi na usalama, na Raisi ndiye amiri jeshi mkuu.
..sasa JK siyo kama haelewi uzito wa Amiri Jeshi Mkuu kufanya kitendo kama kile dhidi ya askari wake walio ktk medani ya kupambana na Rushwa. JK amepitia mafunzo ya kijeshi, ni senior commander mstaafu mwenye cheo cha Luteni Kanali.
Nafikiri Willie ama unakebehi watu ama haujaielewa CCM....kwanza nikuulize mafisadi CCM ni hao watatu tu?..Well kama una uvivu wa kuujua ama kuutafuta ukweli,ama kama umetekwa na cover la kitabu cha kujivua gamba unaweza sema ndio...CCM kamwe haiwezi kuwafukuza mafisadi hao watatu wala wale wengine,maana ukweli ufisadi hawakuufanya wao peke yao..ufisadi ulifanywa na CCM kwa manufaa ya CCM ili waendelee kuinyonya asali ya Tanzania..Kifupi Ufisadi na CCM havitengamani...sinema hii wanayoicheza CCM mimi nafananisha na mtandao wa maambukizi ya Ukimwi katika jamii fulani au kundi fulani then ikaamuliwa watatu wenye ukimwi wauae ili kuzuia maambukizi zaidi,wakati walioambukizwa ni 50..sasa ukiua watatu hawa 47 hawataendelea kuwaambukiza walio bado?.. Willie baba kuwa CCM siyo kigezo cha wewe kijana mwenye ufahamu kukumbatia CCM na mabaya yake....Taifa la kesho si CCM,amka sasa na acha kuendekeza magamba jiunge na CHADEMA kulikomboa Taifa...na bahati mbaya mzee wako naye anatajwa kuhusika na ufisadi...sorry for that lakini si lazima na wewe uunywe ufisadi eti kwa sababu mzee ni wale wale...Welcome CHADEMA!!
Heshima kwako W J Malecela.
Mkuu wangu niliwahi kukupa tahadhari kipindi fulani ulianzisha thread yako ya kushangilia kujivua gamba CCM nikakuonya hukutaka kusikia kabisa ukajiaminisha na kuwaamisha baadhi ya watu wenye mioyo ya kuku kwamba CCM itajivua gamba! .Nakumbuka nilikupa sababu kadhaa lakini moja kubwa ni kukosa msimamo kwa mwenyekiti wenu Rais J M Kikwete.Kama umefuatilia sakata zima lilivyoripotiwa na baadhi ya magazeti ya Raia Mwema ,Mwanahalisi na baadae kuthibitishwa na Mwananchi utagundua jambo moja muhimu sana "ukosefu wa msimamo madhubuti wa Mwenyekiti wa CCM taifa". Mwenyekiti wenu bado hajaonyesha msimamo wa kuchukia ufisadi na washiriki wa ufisadi kwa dhati,Washirika wakuu wa ufisadi walimsaidia sana kufika hapo alipo bado anawaonea aibu hata ingekuwa ni wewe ingekupa shida[dhambi ya kushirikiana na waovu].
Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali vya habari Rais Kikwete alikutana na Lowassa kabla hajakutana na Mzee Msekwa.Mazungumzo baina ya Rais na Lowassa yaelekea hayakugusia kabisa suala la Lowassa kujivua gamba hata kama yaligusia huko yaelekea kabisa Lowasaa aliweza kupangua hoja zote kwa ukamilifu kabisa tofauti na alivyoshindwa kupangua hoja wakati Mheshimiwa Dr Mwakyembe alipowasilisha hoja za RICHIMOND mjengoni [ni siri baina yao].Yamkini yalikuwa ni mazungumzo ya kawaida sana pengine Lowasa alimkumbusha Rais Kikwete jinsi alivyomsaidia hadi akaukwa urais wa JMT,jinsi alivyoratibu ukusanyaji wa fedha hadi kufikia kukwapua fedha kibao Benki Kuu [BOT],jinsi alivyopambana na wapinzani wake waliokuwa wakitishia nafasi yake pengine alimwambia Kikwete unakumbuka tulivyompakazia Salimu A Salimu kwamba alihusika na mauaji ya Sheikh A Karume kwamba yeye ni HIZBU,unakumbuka tulivyonunua vyombo vya habari na nk.Baada ya siku kadhaa Lowasa anaitwa na makamu mweyekiti Mzee Msekwa na kuambiwa mambo ya ajabu eti ajivue gamba mara ohooo achana na ndoto za urais hata kama ni wewe lazima ushangae iweje mkuu wa nchi na Mwenyekiti wa chama ashindwe kukuambia msimamo wa chama amwachie jukumu hilo Mzee Msekwa !.Mkuu wangu W J M wewe nimtu mzima sana hakuna ubishi kwamba Mwenyekiti wako akiwa na Lowasa anazungumza masuala tofauti na akiwa na Makamu Mwenyekiti wake.Kauli za katibu wa Itikadi Bwana Nape na Katibu Mkuu Bwana Mukama zilitosha kabisa kukupa ujumbe kwamba kujivua gamba ni aina ya maigizo yasiyokuwa na mwongozaji,kila mmoja anaamua namna ya kuigiza apendavyo.
TANU/CCM chini ya uongozi madhubuti Mwl J K Nyerere iliwahi kujivua gamba mara kadhaa na wananchi wa kawaida wakalishuhudia kwa macho yao tofauti na huu usanii wa sasa.Mwaka 1967 TANU baba wa CCM ilijivua gamba kwa kuanzisha Azimio la Arusha[Miiko ya uongozi iliasisiwa na hili azimio].Mwaka 1984 CCM ilijivua gamba kwa kumwondosha aliyekuwa Rais wa Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.Mwaka 1987 CCM ilijivua gamba kilipobaini vyombo vya serekali na taasisi za kiuchumi zilikuwa zimeshindwa kuwahudumia watanzania ipasavyo,Mawaziri na wakuu wa mashirika ya umma kama ATC,NASACO na TIB walikwenda na maji.
CCM chini ya uongozi lege lege haiwezi kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya taifa.
Mkuu W J Malecela ni wakati wako wa kufanya maamuzi sahihi sasa kwakuwa naamini wewe ni mtu mzima umeona mengi si vibaya ukaachana na CCM ukaelekeza nguvu zako sehemu nyingine.Muasisi wa CCM Mwl Nyerere aliwahi kutamka hadharani kwamba CCM si Mama wala Baba yake baada ya kuchoshwa na uoza usiokwisha ndani ya chama alichokianzisha[kadi namba moja hadi leo hajapewa mwanachama mwingine bado anaendelea kuimiliki hata kama ameshatangulia mbele ya haki].Najua ni uamuzi mgumu sana kwako hasa ukizingatia umekulia huko,umekuzwa huko na sehemu ya mafaniko yako yameanzia huko ni wakati wako sasa kuachana na siasa za udanganyifu dunia ya leo watu wanataka haki,wanataka kumiliki uchumi wao katika hali ya usawa umeona mwenyewe yaliyotokea na yanayotokea Mashariki ya kati.
William, do you think matatizo ya nchi yetu yametokana na mapacha watatu? Kwa maneno mengine, unadhani kwamba gamba la CCM na serikali ni mapacha watatu au Kikwete mwenyewe? Hawa mapacha watatu hawana madaraka yoyote makubwa serikalini yanayoweza kuathiri utendaji wa serikali. Cha ajabu hali ya nchi na maisha ya watanzania yanazidi kuwa magumu na yenye kukatisha tamaa.
Je mapacha watatu wana influence gani kwenye ugumu wa maisha ya watanzania kwa sasa? Labda ninaweza kusema Rostam ana impact kiasi fulani kutokana na kushikiria njia kuu za uchumi wa nchi. Lakini the rest, sioni kama wana madhara makubwa sana kwa nchi. Otherwise gamba kuu na gumu kwa CCM na serikali kwa ujumla wake ni Kikwete. Kushindwa kwa CCM na kushindwa kwa serikali hakujasababishwa na mapacha watatu, bali Kikwete. Mimi na wanaCCM wengine tunatakiwa tuache unafiki na tusema wazi kwamba gamba letu kuu ni Kikwete, tufanye kama ANC tumuombe ajiuzulu kama alivyofanya Mbeki. Uwezo huo kama wanaCCM tunao, lakini tatizo kubwa linalotusumbua ni unafiki. Tunakazana tu kuwataja akina Lowassa kwa kuwa hawana impact kwetu tunaacha kumtaja Kikwete kwa kuwa ameshika lungu na tunaogopa makali ya upanga wake.
Tuwe wawazi katika hoja zetu tuache unafiki, Kikwete ndiye aliyeshindwa kuendesha nchi na ndiye aliyeshindwa kusimamia misingi ya utawala bora na wa sheria.
Naomba ninukuu sehemu ya tano ya "Azimio la Arusha na siasa ya TANU ya Ujamaa na Kujitegemea" iliyotolewa na Idara ya Habari ya TANU,1967.
SEHEMU YA TANO
AZIMIO LA ARUSHA
Kwa hiyo basi,Halmashauri Kuu ya Taifa iliyokutana katika Community Centre ya Arusha kuanzia tarehe 26/1/67 mpaka 29/1/67,inaazimia ifuatavyo:-
A. VIONGOZI
1.Kiongozi wa TANU au wa serikali sharti awe mkulima au mfanyakazi na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au kikabaila.
2.Asiwe na hisa katika makampuni yoyote.
3.Asiwe mkurugenzi katika kampuni ya kikabaila au kibepari.
4.Asiwe na mishahara miwili au zaidi.
5.Asiwe na nyumba ya kupangisha.
6.Viongozi tunaofikiria hapa ni wajumbe wa Halmashauri kuu ya taifa,Mawaziri,wabunge,wakuu wa vyama vilivyoshirikishwa na TANU,Wakuu wa mashirika ya kiserikali.Viongozi kutokana na kifungu chochote cha katiba ya TANU,madiwani,na watumishi wa serikali wenye vyeo vya kati na vya juu.(Kwa mujibu wa kifungu hiki kiongozi ni mtu au mtu na mkewe au mke na mumewe).
B. SERIKALI NA VYOMBO VINGINE
3.Inahimiza serikali kutengeneza mipango yake kwa kutegemea uwezo wa nchi hii kuiendesha mipango hiyo na wala isitegemee mno mikopo na misaada ya nchi za ng'ambo kama ilivyofanya katika mpango wa maendeleo wa miaka mitano.Halmashauri kuu ya Taifa inaazimia mpango huo urekesishwe ili ulingane na siasa ya kujitegemea.
5.Serikali itilie mkazo sana njia za kuinua maisha ya wakulima.
Mwisho wa kunukuu.
Kuthibitisha kuwa azimio la arusha ni moja ya nguzo za katiba ya CCM,tuangalie katiba ya CCM section 1,5(3):-
"To promote the building of Socialism and self reliance on the basis of the Arusha Declaration".
MY OPINION:
Katiba ya CCM imeonyesha wazi ni watu wa aina gani wanatakiwa wawe viongozi wa chama na serikali,sehemu ya kwanza ibara ya 5,kuanzia kifungu cha 3 na kuendelea vinaonyesha bayana kuwa uongozi uliokuwepo haufuati katiba na kanuni za chama na tukiungana wanachama tunaweza kuwapeleka mahakama kuu, ku question na ultimately dissolve their leadership based on contitutionality.
NAWASILISHA!
Zak Malang, unasema CCM ni kama vile haina viongozi imara..., naomba kukuuliza, unaposema ni kama vile haina, unamaanisha wapo, kama wapo, wataje ni wepi?. Kwa maoni yangu, ondoa neno 'ni kama', lililobaki ndilo jibu halisi kuhusu CCM sasa!....CCM sasa hivi ni kama vile haina viongozi imara wa kuweza kutoa maelekezo/amri na kusikilizwa mara moja -- chama kimebakia kubembelezana katika masuala yoote!!