hahahaaaaaaa chaku unanifanya nianze kuwa private investigator
Sijui kama wote wanaujasiri kama wa GP.Naomba akina HE wote humu jeiefu igeni mfano wa GP.
mkuu nilikua natumia sana tuu, kwakua ninampenda si unajua tena magonjwa mengi siku hizi.
Mkuu ingependeza kama waraka huu angekuwa anatumiwa wife nadhani licha ya roho kumuuma angekuhurumia vilevile
nimeamua kuja kwa wapya na mabinamu mnishauri kwanza kabla sijajikusanya na kuanza kumwambia. inaniuma sanaaaaa jamani naandika kwa uchungu sana hapa, akili yote na mawazo yako kwake ukizingatia siku hizi ameongeza upendo kwangu mara dufu, sometimes nahisi sijui kanistukia?, yani hapo ndo naumia balaa. sio siri lazima nikonfess mbele yake
Bravo shemeji.
But some secrets are made to remain secrets. Usimwambie bali badilika tu na umwonyeshe kuwa umebadilika na UACHE kweli kucheat. You never know ukimwambia anaweza akaipokea na kukusamehe ndio but imani yake haitakuwa imeshake ? siku mkikinzana lugha kidogo tu atajua bado unaendelea. Duh sijui ni sawa maana hata sijui nikushaurije!
shemeji yangu kipenzi kwanza naanza kusema kuwa nimesikitishwa sana na kuhuzunishwa sana!!
Huyu uliyemcheat niyule uleyekuja kutoa ushauri hapa kwamba umemwambia kuwa mkapange akakwambia kuwa jipange kwanza kabla ya kwenda kwenye maamuzi hayo?
Pili huyu uliyemcheat ni yule uliyemsema kuwa bado yuko chuo na amemaliza juzijuzi engineering?
Tatu huyu uliyemcheat ni yule uleyesema kuwa ukimtumia credit hana haja hata ya kusema asante wala kukupigia pindi anapokuwa anakuhitaji?
Nne huyu uliyemcheat ni yule uliyeniambia kuwa kila anapokuwa na safari lazima akupe taarifa kukuondoa shaka?
Tano huyu uliyemcheat niyule aliyekuwa anayetoka out na mshikaji wake ambaye wamesoma wote enzi hizo za nyuma mchana wakati wa lunch na wewe kuumia?
Sita huyu uliyemcheat ni yule uliyekwenda naye vacation na ukaja kuaaga jf?
Ukinijibu nami nitanena.
George_Porjie watu wanakumbukumbu duh haya ukijimix tu umekwisha utaonekana chovya chovya.
Lakini twendeni mbele na kurudi nyuma kina kaka huwa mnawaza nini mnapoamua kuwacheat wenzi wenu? Kwa wale walio na familia
Kwa mke unapata
-Mapenzi ya kweli ya dhati
-Anakujali kwa shida na raha (ukiumwa yeye ndo wa kukuhangaikia)
-Amekuzalia warithi wa jina lako, anawalea na kuhakikisha wako salama just for you
- Ndiye mwenye kukujua hasa kula yako, vaa yako hata lala yako.
-Mshauri wako mkuu
-mshirika katika mambo ya fedha na uchumi wa familia
-Ngono unaipata anakupa kwa moyo wote -inawezekana ikawa si exciting kama ambavyo ungependa
Kwa kimada unapata
- ngono haramu ingawa inakuwa exciting
- na nini tena maana hata sijui mnachopata huko zaidi ya hii!!
mimi George Porjie, nikiwa na akili timamu na wala sijalazimishwa na mtu yoyote, najitokeza mbele yenu wanajamii wote wa JF na wengineo, ili muwe mashahihidi wangu. leo kwa dhati kabisa toka ndani ya moyo wangu pasina kushurutishwa na mtu yoyote, kwani moyo wangu umekua ukiniuma sana hasa pale nimuonapo mai waifu wangu kwamba kuna kipindi nilikua namchiti. roho ilinimua sana tena inaniuma sana kuona napata na ninapewa kila nikitakacho toka kwake (yale yaliyo halalishwa only) na mengine ni zaidi na matamu kuliko huko vichochoroni, nimekuja kugundua kwamba mwisho wa siku ladha, utamu na mengineyo ni sawa sawa kwa wanawake wote, kwani simu ni simu tu mambo ya kwamba ina kamera, ina slide au ina bluututhi hizo ni mbwembwe tuu!!.
napenda pia kuchukua fursa hii kutubu kwa mai waifu wangu popote alipo kwamba anisamehe sana na nina ahidi kuanzia leo kwamba mimi na yeye ni kufa na kuzikana. na wala sitarudia tena kumchiti.
wanaJF wenzangu, mabinamu, mashemeji na wazee wa kujiexpress jamani nyama ni nyama, tutamaliza mabucha but nyama ni ile ile, tubadilike.
nimeamua kubadilika kuanzia sasa.
oui, j'ai décidé de me changer, parce que la charité commencent à la maison .
eeeh Mwenyezi Mungu nisamehee kwa kumchiti mai waifu wangu.
mbona hujanijibu kabla ya kukupa ushauri nina maushauri yaani yapo mengi sana kwa tukio kama lako nijibu kwanza niyuleyule au kule ulikuwa unazuga tu
https://www.jamiiforums.com/mahusia...250-nini-maana-ya-kujipanga-na-kujijenga.html
shost mbona umejichanganya mwenyewe kwenye hiyo red?
Yaani na wewe unasema kuwa kule wanapata ngono iliyojuu kuliko ya nyumbani?
basi kama ndo hivyo basi ndo jibu lenyewe?