Hata uandike kurasa 100 binafsi siwezi kuamini kwamba chadema hawajahusika maswali ni mengi hayana majibu, kama ulivyouliza ni wapi chadema wangetoa silaha hata mimi nauliza kama Serikali na machinery yake wangetaka kumuua kweli Tundu Lisu wangeshindwaje? Unajua ni nani aliyempa Tundu Lisu huduma ya kwanza? Walishindwa nini pale Dodoma kummalizia kama hilo ndiyo lilikuwa lengo la Serikali yetu? Hivyo kuanzia kupotea kwa Saanane mpaka kumficha dereva aliyekuwepo kwenye crime scene ambaye sasa wamemhamishia Ubelgiji kote huku kunanifanya niamini kwamba chadema wanahusika na hata Tundu Lisu mwenyewe anahusika pia!
Unaanza siasa za kichadema za kudhani bila ushahidi.
Sijasema kuwa serikali imehusika mana sina ushahidi .
Nimesema Mamlaka zinazohusika kuchunguza tukio la Lisu wametuambia kuwa watu waliofanya tukio hilo hawajukikani .
Wamesema ni watu wasiojulikana.
Na Mimi nimekubaliana na uchunguzi wa serikali mana ndiyo yenye jukumu hilo.
Sasa hayo ya kina Mwita Waitara ni uchochezi na unalenga kuichafua nchi bado mana unaitangaza nchi kuwa imeshindwa kudhibi watu wanaofahamika kumiliki na kutumia silaha za kivita kuuana hadharani mchana kweupe.
Kipi rahisi kwa Mbowe kushindwa kumuua Lisu wakati amemuuguza takribani mwezi mzima huko Nairobi au wale wahalifu wasiojulikana ambao wametumia risasi 38 na huenda waliamini kabisa kua hakuna aliyetoka hai sio Dereva wala Lisu.
Nadhani Kumuua MTU asiye na hatia yoyote direct USO kwa USO ni ngumu sana hasa pale ambapo anayeua sio mhalifu na hana dai lolote binafsi kwa mlengwa. Mara nyingine Ndio maana utakuta risasi zinarushwa bila mpangilio.
Kuhusu Dereva wa Lisu iko wazi kuwa waliomtorosha wametumia busara mana kwa vyovyote kama angebaki humu nchini hao wahalifu au Majambazi wangemmaliza kwa wasiwasi kuwa amewaona na angeweza kuwataja.
Ni kawaida kwa wahalifu hata wanapovamia benki hawataki MTU awaangalie usoni na wakigundua kua umewafaham au unawafaham watakuua.
Kwa hiyo hao wahalifu kwa vyovyote hawakujua kua wahanga ndani ya gari wamepona hivyo lazima wangekua na kazi ya kuwatafuta au kumtafuta Dereva aliyetoka mzima kwa hofu ya kuwa huenda aliwafahamu. Pamoja na kwamba uwezekano wa kuwafaham ni mdogo kulingana na hofu ya risasi na paniki.