Hili shambulizi walilipanga wenyewe ni inside job chadema na Tundu alikuwa sehemu ya mpango mzima na alijua lkn likaenda ndivyo sivyo yaani Mungu akawaumbua, lkn walitaka wafanye assasination attempt ili waishitumu Serikali yetu!
Tutumie akili zetu sawa jambo baya tuliite baya na tulilaani na zuri tuliite zuri na tulipongeze.
Huo ndio ubinadam na malengo yote mazuri ya binadam yanapaswa yawe furaha kwa watu sio huzuni.
Siamini kuwa kuna mtu ndani ya Chadema anamiliki silaha ya kivita halafu asikamatwe.
Mbaya zaidi aitumie kwa kumpiga mbunge ndani ya eneo la nyumba za serikali mchana kweupe. Atokomee kusikojulikana bila kukamatwa.
Yani Chadema wamiliki silaha za kivita wafanye mauaji au wapigane risasi mchana kweupe halafu serikali ichafuke dunia nzima kuwa imejaribu kumuua Tundu halafu wakati huo huo waachwe bila kukamatwa mpaka leo.
Waitara nimemdharau sana.
Tuache tu ibaki kuwa ni watu wasiojulikana mana ndilo jibu la serikali baada ya uchunguzi.
Sasa kama mamlaka zenye jukumu la uchunguzi wamesema kuwa ni watu wasiojulikana iweje Waitara aseme ni Chadema na Dereva wao.
Sura ya MTU hua inareflect roho yake wakati mwingine.
Waitara ni MTU laghai na mwenye Roho mbaya. Labda kama tumeamua kujenga taifa la kiidiamini idiamini ndio tutakubaliana na watu wenye roho mbaya za kushangilia roho za wenzao kunyofolewa.
Mkuu wa Nchi mwenyewe aliagiza kuwa waliopiga Tundu Lisu risasi wasakwe mpaka wapatikane sasa iweje Waitara asiende polisi kutoa taarifa na maelezo yake yakaandikwa ili baadae atoe ushahidi?
Hii ni mojawapo wa kumsaidia rais aliyetoa wito wa kuwasaka na kuwakamata wote waliohusika.
Siasa za Tanzania zinakua za hovyo sana kwa sababu ya kujitafutia umaarufu kwenye mambo ambayo ni ya kudhani tu badala ya uhalisia.
Chacha wangwe alikufa kwa ajali na vyombo vinavyohuiska na uchunguzi wakathibitisha hivyo na Dereva aliyehusika na ajali hiyo akahukumiwa kwa kuendesha gari kwa mwendo wa hatari na kusababisha kifo lakini cha ajabu Ajali imegeuzwa mtaji wa siasa za kuchafua watu.
Mbowe chama kimemshinda lakini ni dhambi kubwa kumuhusisha na vitu bila ushahidi.
Kauli ya kusema eti amesema kuwa atashughulikiwa hivyo amehusika na Kifo cha Wangwe ni upuuzi.
Neno kushughulikiwa kisiasa linatumika kwenye vyama vyote na Mara nyingi ni kufukuzwa kwenye Chama na hilo limefanyika kwenye vyama vyote. Lakini hili la kupigana Risasa hadharani ni geni ndio maana wahusika walitakiwa wakamatwe ili hali hiyo isijirudie na isitumike kama kama njia ya kisiasa au hata kihalifu au visasi.
Kama kweli Chadema wanaweza kupanga mashambulizi kwa kutumia zana za kivita na kuingia kwenye eneo la Serikali lenye ulinzi na kujaribu kumuua mbunge mchana kweupe bila kukamatwa wala kujulikana basi ni hatari sana hata kwa usalama wa watu wengine akiwemo huyo anayewatuhumu.