Mwisho wa Azra Malama

Mwisho wa Azra Malama

SEHEMU YA 31

Siku zilizidi kusonga mbele lakini hadi mwezi mmoja unakatika akiwa anaishi mahali hapo hakuwahi kuulizwa jambo lolote na wazee hao, kuhusu asili yake pamoja na mambo mengine.

Jambo hili lilimshangaza kwani mategemeo yake ilikuwa ni kuulizwa maswali ili aweze kufahamu wazee hao walikuwa wanawaza nini juu yake.

Hata hivyo yote tisa- kumi jambo lililomshangaza zaidi, kila siku usiku majira ya saa kumi, alikuwa akisikia watu wakizungumza kwenye vyumba vya nje ya kile alichopewa kuishi na baada ya hapo alisikia milango ikifunguliwa na hatua za watu wakiondoka.

Alipochungulia kupitia kidirisha kidogo cha chumba hicho anachoishi aliona wazee watatu, mmoja wao alikuwa ni mzee Makimbi, aliyempokea na wawili ni rafiki zake, wakiwa wamejifunga mashuka ya kimasai na waliondoka wakiwa pekupeku.
Suala hili lilimpa wasiwasi mno Azra. Alijiuliza watu hao walikuwa wanakwenda wapi kila siku usiku lakini hakuweza kupata jibu.

Ndipo siku moja alipoamua kujifunga mkanda kuwafuatilia ili aweze kufahamu ni wapi wanakwenda.
Kweli kama alivyopania hazikuchukua hata siku mbili za kutekeleza zoezi lake toka alipopata mawazo hayo.
Siku hiyo alijipanga.

Hakusinzia kabisa. Alilala akikapua mpaka yalipofika majira ya saa kumi za usiku. Kama kawaida alisikia milango ikifunguka na baada ya muda watu wakizungumza nje na hatua zilisikika watu hao wakiondoka.

Azra alikuwa anafuatilia vizuri kila kilichokuwa kinaendelea akiwa chumbani kwake. Baada ya wazee hao kupotea kwenye upeo wa macho yake, Azra alitoka kwenye chumba alichokuwa analala kisha kwa tahadhali kubwa alianza kuwafuatilia wale wazee.

Hakika ilikuwa siyo safari ya kawaida. Azra alitembea kuliko alivyowahi kutembea huko kabla. Saa zima lilikatika akitembea akiwafuatilia wale wazee mpaka walipofika eneo ambalo lilionekana ndiyo mwisho wa safari yao.

Baada ya kufika katika eneo hilo Azra akiwa amejibanza sehemu akiwafuatilia kwa macho wazee hao watatu, kiukweli alibaki ameduwaa haamini alichokuwa anakiona.

Eneo hilo lilikuwa ni sawa na kijiji kipya chenye watu wengi lakini hakukuwa na nyumba hata moja. Kilichomshangaza zaidi kila aliyemuona mahali hapo alfajiri hiyo alikuwa bize na shughuli fulani anafanya.
 
32

Baada ya kufika katika eneo hilo Azra akiwa amejibanza sehemu akiwafuatilia kwa macho wazee hao watatu, kiukweli alibaki ameduwaa haamini alichokuwa anakiona.

Eneo hilo lilikuwa ni sawa na kijiji kipya chenye watu wengi lakini hakukuwa na nyumba hata moja. Kilichomshangaza zaidi kila aliyemuona mahali hapo alfajiri hiyo alikuwa bize na shughuli fulani anafanya.

Wapo waliyoonekana wanapika na wengine walionekana wamekaa huku wameunganisha viganja vyao vya mikono kifuani na wameinamisha kichwa, wengine walikuwa wanafua nazi, wengine wanakamua maziwa ya ng’ombe, wengine wanalima na moshi ulitanda kila kona ya eneo hilo.

Azra alipotazama kwa makini aligundua sura za watu hao zilikuwa ni tofauti na zile alizozoea kuziona kwenye kisiwa cha Swadege ya Rwadege, zenye furaha muda wote na maisha.

Sura alizoziona hapa zilikuwa na uhaba wa matumaini pamoja na shahuku, lakini mahali hapo aliona mpaka Wazungu, watu ambao toka afike Swadege hakuwahi kuwaona hata mmoja wao. Alibaki ndani ya butwaa isiyoelezeka.

“Pengine hawa ndiyo wachawi ambao mama yangu alikuwa ananisimulia kwamba wanapatikana Afrika?” Azra alijiuliza kwa sauti.

“Hapana siyo wachawi!” Mara alisikia sauti kutoka nyuma yake ikizungumza.
Azra alishituka kiasi kwamba mapigo ya moyo wake yakawa yanakwenda kasi kuliko kawaida. Utadhani yalikimbizwa na mwanariadha maarufu Tanzania, Alphonce Simbu.

Azra, aligeuza shingo haraka kumtazama huyo aliyekuwa nyuma yake, macho yake yalikutana ana kwa ana na mzee Makimbi.

“Huyu mzee nimemuona muda mchache tu kajichanganya na hao watu, huku kafikaje na amefahamu vipi nipo hapa?” alijiuliza moyoni lakini kabla ya kupata jibu mzee huyo alizungumza.

“Hawa ni watu wema wanaotafuta amani ya mioyo yao!”
“Amani ya mioyo yao?” Azra aliuliza kwa mshangao.

“Ndiyo, kwa nini unashangaa?”
“Sijakuelewa, nifafanulie zaidi.
“Oh! Kabla sijakufafanulia niambie unafanya nini hapa?”

Mzee huyo alimhoji Azra na kutega sikio kusikia atakachosema. Azra alishikwa kigugumizi, hakuwa na namna aliamua kuwa muwazi.
 
Sehemu ya 33

“Mzee samahani niliwafuatilia?” Alimwambia mzee Makimbi.

“Samahani, umesema…?”
“Niliwafuatilia.”
“Kina nani?”
“Nyie.”

“Kwa nini?”
“Niliingiwa na hofu kusikia kila alfajiri mnatoka. Nilipenda kufahamu ni wapi mnakwenda.”
“Vyema kijana.

Napenda watu wadadisi kama wewe, ambao wapo tayari kujifunza hata kama hawaitwi darasani. Huku ndiko tunakuja kila alfajiri. Nifuate pengine na wewe unaweza kuambulia lolote na kuipata amani ya moyo wako.”

Yule mzee alimwambia Azra. Kijana huyo alisita, mapigo ya moyo wake yalikuwa bado yanakwenda mbio nje ya kontroo kwa sababu moyoni aliwaza baada yam zee huyo kugundua kwamba aliwafuatilia, alikasirika na angemtendea jambo boya. Akizidi kuwaza mzee Makimbi alimsisitiza amfuate.

Azra alipiga moyo konde kisha akaanza kumfuata mzee huyo na baada ya kuingia kwenye eneo hilo mshangao aliokuwa nao mwanzo uliongezeka mara mbili.

Azra alijiuliza hao watu walitoka wapi? Mbona walikuwa wamechoka sura zao namna hiyo. Wengine walikuwa ni kama walevi, wangine walionekana kama mateja waliyobobea kwenye dawa za kulevya na wengine watu wasiyo na matumaini kabisa na maisha.

Mzee Makimbi aliendelea kumzungusha kwenye eneo hilo na kadiri alivyokuwa anazidi kumzungushwa ndivyo alivyozidi kumshangaa.

“Hawa watu wametoka wapi?” alimuuliza mzee Makimbi.

“Sehemu mbalimbali dunia.” alijibu mzee huyo. “Azra kitu ambacho hufahamu ni kwamba Swadege ya Rwadege ni kisiwa kilichobarikiwa.

Ni sehemu hii tu duniani ambayo mtu anaweza kuja na akarudisha tumaini kwenye maisha hata kama amepoteza dira kiasi gani.
“Hawa watu unaowaona hapa kila mmoja anatatizo lake.

Wapo mateja, wauza unga wastaafu, majambazi wastaafu, washirikina na watu wabaya wa aina zote duniani unaowafahamu wewe ambao kwa namna moja au nyingine walikuwa wamekata tamaa kutokana na maisha yao huko nje.

“Wameamua kuja hapa kwa ajili ya kupata amani ya mioyo yao, kuzaliwa upya na kubatizwa kwa mmea wa uhai kutoka Swadege ya Rwadege. Kisha wakirudi huko walikotoka wanakuwa ni watu wapya.”

Mzee Makimbi alizungumza hayo akiwa bado anamtembeza Azra.
 
Sehemu ya 34

“Sasa amani ya moyo na hizi shughuli wanazofanya mbona ni maji na mafuta? Inaonekana kama mnawatumikisha.”
“Hapana wanajitumikia,” Mzee Makimbi alisema akisimama, akamgeukia Azra na kumshika begani.

Kisha akamwambia;
“Hakuna kitu kikubwa ambacho mtu anaweza kufanya kwa ajili yake kama kuwekeza kwenye ufahamu, mabadiliko ya akili na mtazamo wa maisha yake kwa jumla.”

“Una maanisha nini?” Azra alimuuliza. “Ninamaanisha nilipokuwa kijana mdogo nilikuwa mtukutu sana.

Mwizi na nisiyewasikiliza wazazi wangu. Marehemu mama yangu alipenda kuniambia methali ya kwamba asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.

“Maneno yake nilihisi ni kelele za mbinja na zumari masikioni mwangu, lakini maneno hayohayo yaliweza kuwa na maana kwenye maisha yangu pale niliponusurika kuuawa na wananchi kutokana na wizi. Niliokolewa na polisi na niliishi muda mrefu jela.

Nikiwa jela nilipitia mateso makubwa sana. Ni mateso ambayo mwanzoni yalinifanya nijute juu ya kila kitu nilichofanya kwenye maisha yangu na nikumbuke maneno ya mama yangu.

“Siku moja nikiwa gerezani nililia mno. Akaja mzee mmoja na kuniuliza nilikuwa ninalilia nini.

Nilimweleza juu ya maisha hayo ya gerezani tuliyokuwa tunapitia kwamba sikuyazoea na kwangu yalikuwa ni mateso makubwa.

“Mzee huyo aliniambia nisijali. Akanitaka kuacha kulia na kwamba kila kitu kwenye maisha hutokea kwa sababu. Ilikuwa ni lazima nipitie mateso hayo ili kubadilika na kufahamu wapi nilikosea maishani mwangu. Zaidi aliniambia nilikuwa ninawekeza kwa ajili ya maisha yangu na njia ipi niifuate.

Toka hapo nilibadilisha mtazamo na nilipotoka gerezani niliamua kubadilika na kwenda kuishi na wazee wa Swadege, wakanifundisha mambo mengi na leo nipo hapa ninasaidia maisha ya watu wengine,” mzee Makimbi alimaliza kumweleza Azra.

“Simulizi yako nimeisikia lakini ninahisi sijaielewa vizuri.” “Kwa shughuli wanazofanya hawa watu wanawekeza kwa ajili ya maisha yao. Huwezi kubadili mtazamo na namna ya kufikiri bila ya kuwa mzalishaji.

“Lakini kitu kingine nilichokufundisha kwenye maneno yangu ni kwamba siku zote makosa yanatoa nafasi ya pili ya mtu kufahamu ipi ni njia sahahihi ya kufuata.”
“Mh!”

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 35

“Lakini kitu kingine nilichokufundisha kwenye maneno yangu ni kwamba siku zote makosa yanatoa nafasi ya pili ya mtu kufahamu ipi ni njia sahahihi ya kufuata.”
“Mh!”

“Ndiyo hivyo. Adui yako anaweza kuwa ndiye rafiki yangu wa damu Azra! Unaweza kufanya kosa na ukajuta, mtu mwingine kupitia makosa anajifunza.” “Bado siioni pointi yako mzee wangu.

Uwezo wa kufikiri, kujifunza kupitia makosa una uhusiano gani na kazi hizi za suruba, kutembea peku, kupika kwenye kuni na shughuli zote hizi zinazoendelea hapa?”

“Nimekwisha kwambia Azra…jambo la kwanza kwenye kubadilika katika mtazamo wako na kuboresha akili yako ni lazima uwe mzalishaji. Uzalishaji ni pamoja na kufanya shughuli hizi unazoziona.

Hili ni darasa wakitoka hapa watafanya mambo makubwa zaidi na kutimiza ndoto zao.”

Azra alibaki kimya akimkodolea macho mzee Makimbi. Mzee huyo naye alimtazama na kutabasamu kisha akaanza kupiga hatua;

“Azra nina fahamu hali inayokukuta, ni lazima unielewa taratibu, hata hivyo ndivyo elimu inavyotakiwa kuingia kichwani kwa mtu lakini kadiri tunavyoendelea kuwa wote utanielewa zaidi.”

“Naomba nikuulize swali mzee Makimbi…”
“Endelea?”

“Mbali na hayo uliyoyasema, hatua nyingine ya kutimiza ndoto zangu ni ipi?”
“Kufanya yale unayoyapenda kwa bidii, ni hivyo, rahisi tu.”
“Samahani…”

“Najua ulitegemea kusikia kitu kikubwa zaidi. Lakini ni hivyo. Kama unapenda kuwa mwanasoka maarufu duniani, tafuta muda wa kucheza hata kama unabanwa na shughuli zako kwa kiasi gani kisha cheza soka kwa bidii.

Kama unapenda kuwa mwanamuziki imba kwa bidii. Kujiajiri, usiogope anza kujiajiri.”
“Kabla ya hatua hii hakuna jambo lingine…”
“Oh! Jambo lingine?”
“Ndiyo.”

“Yote hayo niliyokwambia na yote unayotamani ni lazima yawe moyoni, muda wote, dakika zote, kiasi kwamba ukipumua unasikia kile unachokipenda, ukifumba macho unaona kile unachokipenda na kutamani kwenye maisha hilo ndilo jambo la kabla.”

Azra alitikisa kichwa kumaanisha alikuwa ameelewa yale yote ambayo mzee Makumbi alikuwa anamweleza.
Lakini akiwa kimya mzee huyo alimrudia tena;
 
SEHEMU YA 36

“Kuna jambo nilikuwa sijakwambia…”

“Jambo gani?” Azra aliuliza. “Umekwisha wahi kuona au kusikia mtu ambaye mbele za watu hanywi pombe halafu akiwa peke yake anajifungia ndani na kunywa pombe?”
“Nilishasikia. Baba yangu alikuwa mmoja wao.”

“Mtu wa namna hii anakuwa anafanya vitu kwa kuwafurahisha watu wengine. Nje anaonekana hanywi pombe lakini ndani yake anakunywa.

Huu ni mfano tu, lakini ninajaribu kukuonyesha picha ya ambacho tunakitibu hapa. Ni kuwasaidia watu kujitambua. Kuwa wao. Kuishi maisha ya kwao na kila kinachoonekana nje kiwe kinamaanishwa kutoka ndani pia. Siyo mtu wa ndani awe tofauti na yule anayeonekana nje.

“Na hiyo ni siri nyingine ya shughuli hizi zinazoendelea mahali hapa. Mtu hawezi kujitambua juu ya uwezo wake wote utakaomfanya apate mabadiliko na mafanikio ya kufurahia maishani mwake bila kuunganisha nguvu mbili. Nguvu ya dunia na nguvu yako ya asili.

“Nguvu hizo unaweza kuziunganisha pekee kwa kufanya vitu vya asili na kiunganishi kwenye haya yote ni akili. Nakueleza zaidi, unaona hao wanaolima?’
“Ndiyo.”

“Hao na wengine wote katika hicho wanachokifanya wanatakiwa kuweka akili yao hapohapo kwa muda wote wanaolima.

Ni kweli unapozingatia kwenye jambo moja mawazo mengine yanakuja kwa sababu binadamu wa kawaida anawaza mpaka mawazo 60, 000, kwa siku na asilimia 95 ya mawazo hayo ni yaleyale anayoyawaza kila siku.

“Lakini akili ni kama kiungo cha mwili. Jinsi unavyoifundisha na kuituma ndivyo inafanya kazi na kukomaa zaidi, ambavyo hata mkono ukiufanyisha mazoezi unakomaa zaidi.

Mawazo yanapokuja mengine wanatakiwa kuyaondoa na kurudisha kwenye hicho wanachokifanya. Taratibu wanakwenda wanakomaa na itafika hatua watakuwa na uwezo wa kuwaza jambo moja kwa muda wa robo saa mpaka zaidi huku wakiwa wanalima.” Alisema mzee Makumbi.

Mzee huyo aliendelea kumwambia Azra kwamba akili ya binadamu ikisha komaa inaweza kumpa kila anachokitaka kwenye maisha na kuwa vile anavyotaka kuwa.
“Ni lazima kila tajiri au mtu mwenye mafanikio apitie haya?” Azra aliuliza.
 
SEHEMU YA 37

“Si lazima. Utajiri au mafanikio yanamaana tofauti kwa kila mmoja wetu.

Kila mtu ana chaguo lake kwenye maisha. Lakini hapa tunachofanya ni kujumuika zawadi yetu Mungu aliyotubariki pamoja na watu wengine.

Zawadi ya mtu kutambua juu ya uwezo wake wa akili na kwamba akili inaweza kufanya chochote kile, kupata majibu yote magumu na kutazama kila aina ya fursa ambazo zimetuzunguka kwenye maisha yetu ya kawaida.

“Lakini pia zawadi yetu Waswadege itamfanya mtu afahamu nini maana ya furaha, heshima, kuwa na busara, kutumia vipaji alivyozawadiwa na Mungu, matumaini, utajiri na kuishi miaka mingi kama ambavyo sisi tunaishi.

Haya ndiyo mafanikio kwetu na mtu yeyote akitumia njia zetu nilizokueleza anaweza kuishi kama sisi.”

Mazungumzo hayo yalifanyika wakati Azra Malama na mzee Makumbi wanazidi kukatiza katikati ya watu wale ambao kila mmoja alikuwa amekazana kwenye kile alichoambiwa afanye.

Wakizidi kukatiza mara kuna mtu Azra alimuona na kumfananisha. “Ngoja…” alimwambia mzee Makumbi. Kisha akamsogelea mtu yule aliyemfananisha kwa tambo ndefu.

“Jaji Kessy!” aliita kwa mshangao baada ya kuminya macho yake kutazama vizuri zaidi na kugundua kwamba yalikuwa hayamdanganyi. Huyo mwanaume aliyekuwa analima alikuwa ni Jaji Kessy waliyekutana kwenye Gereza la Guantanamo.

Mwanaume huyo aligeuza shingo na kumtazama.
“Azra Malama,” aliita pia na kuliachia jembe likidondoka chini kisha wawili hao wakakimbiliana na kukumbatiana.

Waliendelea kukumbatiana kwa takribani sekunde hamsini kisha wakaachiana.
“Jaji Kessy sikutegemea kabisa kukuona huku!” Azra alimwambia.
“Hata mimi sikutegemea.” Jaji huyo alijibu.

“Umefuata nini?” Azra alimuuliza.
“Nimefuata kile ulichofuata wewe.”
“Ha! Ha! Haaa!” Azra Malama kidogo afe kwa cheko.

Hakikuwa kicheko cha furaha moja kwa moja, bali alimcheka mzee huyo kwani alikuwa na uhakika hafahamu kile kilichompeleka hapo Swadege ya Rwadege ingawa ndicho kilichomsaidia mpaka yeye akatoka jela pia.
Wakati mazungumzo hayo yakiendelea tayari mzee Makumbi alikuwa amekwisha wasogelea wawili hao.

Akiwa karibu yao kabla ya kuzungumza neno lolote, mara kuna mtu mwingine aliibuka kutoka upande aliokuwa anatazama Azra na kuita jina la Azra!
 
sehemu ya 38

Azra alikaza macho kutazama ni nani alimuuita na alikuwa akimfahamu katika eneo hilo geni.

Baada ya kutupa macho Azra alistaajabu kwa alichokiona na ilikuwa ni sawa na miujiza.

Mtu mweusi, mwenye misuli mingi, mfupi wa wastani na aliyekuwa amefuga rasta kichwani aliyemuona alimtambua sawasawa, ingawa walikuwa wamepotezana takribani miaka nane iliyopita.

“Kaka ni wewe?” Yule mtu alimuuliza.
“Ni mimi Michael. Upo huku?”
“Ndiyo kaka, hubadiliki Azra?”
Azra alijitazama kisha akamjibu; “Hata wewe hubadiliki, umeongeza tu rasta kichwani.”

“Ha! Haa! Bado ni mcheshi vilevile. Aisee, nimefurahi sana kukuona.”
“Hata mimi Michael.”
“Ndiyo unafika leo?” “Ndiyo.”
“Hongera sana kwa maamuziki yako ya busara.

Hakuna kama Swadege ya Rwadege, huku ndiyo utafahamu nini maana ya maisha ambayo kila mwanadamu anatakiwa kuishi.

Utafahamu nini maana ya ndoto zako, utaanzia wapi mpaka ufanikishe na mengine mengi. Karibu sana kaka.”
“Asante Michael.”

Azra alijibu huku akiwa bado ameduwaa akihisi pengine alikuwa ndotoni kwa kukutana na watu wale wawili kisiwani hapo aliowafahamu.

Azra na Michael Ndassa walikuwa ni marafiki miaka ya nyuma sana.

Wawili hawa walifahamiana wakiwa Marekani kutokana na shughuli zao walizokuwa wanafanya.

Azra alipokuwa muuaji na mtekaji, Michael alikuwa ni jambazi sugu aliyefanya unyang’anyi kwa kutumia silaha.

Urafiki wao ulidumu kwa miaka kadhaa lakini kilichowatenganisha ilikuwa ni baada ya Michael kumuua askari polisi na kuikimbia Marekani.

Azra hakuwahi kufahamu alikimbilia wapi mpaka alipokwenda jela kwa kesi ya mauaji na toka Michael alipopotea Marekani hiyo ndiyo ilikuwa siku yao ya kwanza kukutana huko Swadege ya Rwadege.
 
sehemu ya 39

“Nyie wote mnafahamiana?” Mzee Makumbi aliuliza wakiwa bado wamesimama.

“Ndiyo.” Azra alijibu. “Hawa wote ni rafiki zangu. Huyu Mzungu anaitwa Jaji Kessy na huyu ni Michael.”
“Wote kutoka Marekani?”
“Ndiyo. Lakini usisahau damu yangu ina asili ya Swadege ya Rwadege”
“Ha! Haaa! Ni kweli siwezi kusahau.

Kikubwa hongereni kwa uamuzi mzuri mliyofanya kwa ajili ya maisha yenu. Wamarekani wengi huko nyuma walikuwa wanafikiria kuingia kwenye taifa letu ili watutawale, angalau nyie mnafikiria kujikomboa kwenye maisha yenu.”
“Asante sana.”

Toka siku hiyo, Azra Malama alikuwa anaamka asubuhi na mapema kisha anaambatana na wazee wa Swadege kufika kwenye eneo hilo kwa ajili ya kujifunza mambo mengi mapya aliyokuwa hayafahamu ambayo yalikuwa yanaendelea kisiwani hapo.

Harakati za kuitawala
Swadege ya Rwadege

Michael na Jaji Kessy ndiyo walikuwa rafiki wapya wakubwa wa Azra Malama kisiwani hapo.

Hata hivyo pamoja na yote yaliyokuwa yanaendelea, bado azma yake ya kukitawala kisiwa hicho kama ambavyo alitumwa na Wamarekani, ilikuwa palepale.

Hakuwa na mswalia mtume katika hilo. Hiyo ndiyo ilikuwa ndoto yake kubwa na alikuwa tayari kufa akiipambania. Kuhusu ndoto Azra aliamini kwamba ni kile kitu ambacho mtu anahitaji kukitimiza maishani mwake kwa namna yoyote ile.

Kwake haikujalisha kiwe kizuri kwa watu fulani au kibaya, ilimradi tu kwake ilikuwa ni sawa na ndiyo kiu ya moyo wake, basi alijiona mwenye haki ya kujifunga mkanda na kukipambania mpaka kieleweke.

Pamoja na hivyo, kitu kingine kilichompa furaha Azra Malama ilikuwa ni kukutana na watu hao wawili aliowafahamu Michael na jaji Kessy, moyoni alipanga kuwashawishi wawili hao ili aweze kushirikiana nao kwenye azma yake hiyo ya kuitawala Swadege na kusafirisha mazao ya uhai kwenye mataifa mengine.
 
SEHEMU YA 40

“Michael…” Azra aliita. Ilikuwa ni siku moja alipopata nafasi nzuri ya kuzungumza na Michael baada ya shughuli za siku hiyo kwenye eneo la Amani walikokuwa wanakwenda kila siku.

“Nambie kaka…” Michael aliitika.
“Unakumbuka juu ya ndoto zetu kipindi tupo pamoja Marekani.”
“Ha! Ha! Haa! tafadhali usinirudishe huko.”

“Hapana sina nia ya kukurudisha. Ninakuuliza tu.”
“Ndiyo, ninakumbuka. Tulikuwa na ndoto nyingi.”

“Kubwa kuliko zote ilikuwa ni ipi?”
“Azra usinivute masikio unafahamu wazi.”
“Naomba unikumbushe.”

“Kufanya matukio makubwa ya kuishangaza dunia. Hata tukiondoka siku moja duniani vizazi na vizazi vitukumbuke. Ndiyo zilikuwa ndoto zetu!”

“Kweli unakumbuka.” Azra alimsogelea Michael karibu zaidi usoni na kumkazia macho kisha akamwambia; “Huu ndiyo muda Michael wa kutimiza ndoto zetu.”
“Azra una…”

“Hapana.” Azra alimkatisha Michael kabla hajamaliza alichokuwa anataka kuzungumza huku akiendelea kumtazama kwa macho yenye mkazo.

“Michael nisikilize kwa makini. Hakuna tutakacho vuna hapa. Hawa wazee wapo mahali hapa kwa ajili ya kupumbaza watu akili na kutengeneza ulimwengu wa watu waoga.

“Wanafahamu dunia inafahamu wazi juu ya siri ya mazao yao ya uhai. Lakini hawapo tayari kuona yanatoka na kwenda kwenye mataifa mengine.

Njia pekee ya kuyalinda wameona watumie hii ya kuwafanya watu wajinga kwa elimu isiyo na maana na kuwatumikisha. Michael funguka akili rafiki yangu…funguka…tumekuja duniani kuandika historia, tuwe tofauti na watu wengine.”

Michael alimsikiliza Azra kwa makini lakini bado ni kama alionekana hamuelewi rafiki yake huyo kutokana na yale aliyokuwa anamueleza.
“Hapana Azra sijakuelewa bado.”
“Unaona…” Azra aling’aka.

“Huyu siye Michael rafiki yangu ninayemfahamu. Huyu ni mtu mwingine kabisa. Kaka ina maana hawa watu wameingia akilini mwako kiasi kwamba huwezi kuona fursa yoyote ile mbele yako?

“Huoni kile ambacho siku zote tulitamani na kuota kiweze kutimia kwenye maisha yetu. Kaka, tunaishi mara moja na kufa mara moja, hii mara moja tunayoishi ni lazima itoshe, lazima majina yetu yaandikwe kwenye historia.”

“Kwa hiyo unataka tufanye kipi?”
“Hili ndilo swali nililokuwa ninalisubiri muda mrefu. Michael, hiki kisiwa kinatakiwa kuwa
 
SEHEMU YA 41

“Huyu siye Michael rafiki yangu ninayemfahamu. Huyu ni mtu mwingine kabisa. Kaka ina maana hawa watu wameingia akilini mwako kiasi kwamba huwezi kuona fursa yoyote ile mbele yako?

“Huoni kile ambacho siku zote tulitamani na kuota kiweze kutimia kwenye maisha yetu. Kaka, tunaishi mara moja na kufa mara moja, hii mara moja tunayoishi ni lazima itoshe, lazima majina yetu yaandikwe kwenye historia.”
“Kwa hiyo unataka tufanye kipi?”

“Hili ndilo swali nililokuwa ninalisubiri muda mrefu. Michael, hiki kisiwa kinatakiwa kuwa chetu…”
“Kivipi?”
“Tukitawale.”

“Azra. Inawezekanaje? Kwanza sisi ni wageni hapa na tunawezaje kubadili mfumo mzima wa maisha wanayoishi hawa watu na kuwatawala?”

“Hakuna mwenyeji duniani. Wote ni wageni na wote ni wasafiri. Kuhusu kuwatawala inawezekana, kikubwa tu ni utayari wako.”

Michael alibaki ameduwaa akimtazama Azra bila kupata neno la kuzungumza. Kijana huyo alitikisa kichwa kana kwamba mtu aliyekuwa anakataa jambo fulani, alifanya hivyo akiwa amefumba macho na kung’ata lipsi za chini za mdomo wake, kisha alifumbua macho na kumwambia Azra ampe muda wa kufikiria juu ya suala hilo.

Wakati Michael akitaka muda zaidi wa kufikiria juu ya hilo, Azra hakuwa na muda wa kupoteza zaidi, aliamua kumtafuta Jaji Kessy ili aweze kumueleza pia juu ya suala hilo na kuona kama anaweza kumpa sapoti. ***

“Kipi unaweza kumlipa mtu aliyeokoa maisha yako?” Azra alimuuliza jaji Kessy, alipopata nafasi ya kukutana naye kwa ajili ya mazungumzo.

“Naweza kumfanyia lolote lile ilimradi liwe ndani ya uwezo wangu,” Jaji Kessy alijibu.
“Kweli?”

“Ndiyo, nategemea kuna jambo linakuja baada ya swali lako.”
“Kabisa, upo karibu na ukweli.”
“Ni nini hasa?”
“Kuna jambo ninataka tusaidiane.”
“Tusaidiane?”

“Ndiyo tusaidiane.”
“Ninakusikiliza…”
Azra hakuwa na muda wa kupoteza zaidi ya kumwaga mchele mbele ya kuku.

Alimweleza kila kitu Jaji Kessy, kuanzia namna Wamarekani walivyomfanyia mpango akatoka gerezani lakini pia juu ya azma yao ya kukitawala kisiwa hicho kisha kuchukua mazao ya uhai na kuyasambaza sehemu mbalimbali duniani.
 
SEHEMU YA 42

Kwa upande wa Jaji Kessy habari hizo zilikuwa ni za kushitua mno. Ni jambo ambalo hakulitegemea kwamba Azra alikuwepo kisiwani hapo kwa ajili ya kazi maalumu aliyotumwa na Wamarekani.

Kwa sekunde kadhaa, jaji huyo aliyewahi kuwa na heshima kubwa Marekani alibaki akimtazama Azra, kisha akatikisa kichwa mfano wa mtu aliyekuwa anasikitika.
“Mbona unasikitika?”

Azra alimuuliza.
“Nimeamini hakuna wema wa bure duniani, nilijiuliza sana wakati unanitoa gerezani, malipo ya wema huo ni kitu gani na nitaulipa wakati gani lakini sikuweza kupata jibu.”

“Jaji Kessy...hebu acha hayo maneno. Sisi ni marafiki na ningeweza kufanya jambo lolote lile kwa ajili ya urafiki wetu, wala sikukutoa gerezani ili siku moja nikutumie,”

Azra alimjibu jaji huyo.
Hata hivyo kwa upande wa Jaji Kessy ingawa Azra alijitahidi kumwelezea kwa kina kila kitu juu ya azma hiyo ya Wamarekani, lakini ilikuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa kwa mategemeo acheze. Jaji Kessy hakuelewa wala kukubaliana na lolote lile.

Zaidi alitishia kama Azra angeendelea na mawazo hayo basi angemshitaki kwa wahusika.
Mapokeo ya jaji Kessy juu ya suala lake yalimfanya Azra ahisi kuishiwa nguvu.
Zaidi apatwe na hasira!

Kwa mara ya kwanza alipokutana na mzee huyo kisiwani hapo alifurahi sana na kufahamu alikuwa amekutana na rafiki ambaye wangesaidiana kutimiza ndoto zake.

Lakini mambo yalikuwa yanaonekana kwenda kinyume na matarajio, kuna wakati ulifika Azra akawa anajuta ni kwa nini ameamua kuchukua uamuzi wa kumueleza mzee huyo juu ya suala hilo.

Kwa maana alifahamu kwa vyovyote kukataa kwake ilimaanisha kulivujisha suala hilo pale ambapo ataanza harakati zake za wazi za kuitawala Swadege ya Rwadege.
Mawazo ya kumuua yakaaingia kichwani mwake!

Hatimaye wawili hao walimaliza mazungumzo na kuachana. Baada ya shughuli zao kila mmoja alielekea mahali anapoishi.

Akiwa chumbani usiku wa siku hiyo Azra kichwani alikuwa na mawazo chungu nzima na yote aliyokuwa anayawaza ilikuwa ni namna gani anaweza kupata sapoti kutoka kwa rafiki zake za kukitawala kisiwa hicho.
 
SEHEMU YA 43

Akiwa amezama kwenye mawazo hayo, akifikiria kwa kina mara kuna jina la mtu liliingia kichwani mwake.
Jemima!

“Yes,” alijikuta akitamka kwa lugha ya Kingereza.

Aliwaza Jemima alikuwa ni miongoni mwa watu sahihi wa kushirikiana nao kwenye suala hilo kwa sababu msichana huyo alikuwa anaifahamu Swadege ya Rwadege vizuri zaidi kuliko hata rafiki zake Michael na Jaji Kesssy.

Hata hivyo Azra aliufahamu udhaifu wa mwanamke ulikuwa wapi. Kwenye mapenzi!
Lakini pia aliifahamu nguvu ya mwanamke.

Alifahamu mwanamke akiamua kufanya jambo harudi nyuma. Hasa pale akiwa anafanya kwa sababu ya mtu anayempenda, huwa tayari kufanya lolote lile ilimradhi kumridhisha na kuonyesha upendo wake.

Akawaza kumshawishi Jemima kuwa mpenzi wake. Aliona hiyo ndiyo njia pekee ya kumshirikisha msichana huyo kwenye ndoto hizo alizokuwa nazo.

Kulipopambazuka, majira ya alfajiri wakati mzee Makimbi akijiandaa kwenda kwenye eneo la Amani, aligonga kwenye chumba cha Azra ili waongozane, alimkuta Azra anasali. Akamsubiri!
“Leo siendi huko,” Azra alimwambia mzee Makimbi baada ya kumaliza kusali.
“Kwa nini?”

“Kuna sehemu nataka niende.”
Mzee Makimbi alitabasamu.
“Umekuwa mwenyeji sasa,” alimtania huku uso wake ukiwa bado kwenye tabasamu. “Ni wapi huko?”

“Kwa mama Cecillia.” Azra alimjibu. “Nimejikuta nimemkumbuka sana mama yangu, naomba nikaonane naye.”
“Sawa.”

Mzee Makimbi aliondoka.
Jua lilipochomoza Azra aliishika njia na kuelekea moja kwa moja mpaka nyumbani kwa mama Cecilia.

Ilikuwa tabu kufika kwa maana ilikuwa ni sehemu ambayo hakuwahi kufika, lakini alichokifanya ilikuwa ni kwenda maeneo ya mpakani akakutana na kundi la Shebo, walinzi wa mpaka, akawaeleza nia yake ya kukutana na mama Cecilia, vijana hao kwa kuwa hawakuwa wanamtilia tena shaka na wakati huu walikuwa wanamhesabu kama mmoja wao walimpeleka.
Mama Cecilia alifurahi kumuona Azra Malama.

“Mwanangu,” Alisema mama huyo alipomtia machoni.
“Mama,” Azra alijinasibu.
Wakakumbatiana.
“Mzima?” Azra alimuuliza.
“Mzima, wewe?”

“Mzima pia.” Baada ya mazungumzo ya hapa na pale baadaye Azra pia alikutana na Jemima. Pia walifurahi kuonana kwa kuwa muda mwingi walikuwa hawajaonana.
 
SEHEMU YA 44

Siku hii Azra alishinda nyumbani hapo akizungumza mambo mbalimbali na familia hiyo, jioni alipotaka kuondoka alisindikizwa na Jemima.

“Nafurahi kuwa nyumbani Jemima,” Azra alimwambia Jemima wakipiga hatua.
“Hujakoma tu kufurahi?”
“Siwezi.”
“Siku zote utafurahi.”
“Hata hivyo kuna ofa napenda kukuomba.” Azra alimwambia.

“Ofa gani?” Jemima aliuliza huku akisimama na kumtazama kwa makini Azra. Azra naye alisimama na kumtazama Jemima machoni.
“Nahitaji unitembeze maeneo mbalimbali ya kisiwani hapa, kila siku.”

“Ooh!” Jemima alitoa sauti ya mshangao kisha akaendelea kutembea. Azra naye alianza kutembea. “Kumbe hivyo. Haina shida, ila Jumatatu, sitakutembeza, tutakuwa kwenye Gereza la Koba kwa ajiri ya kuhudumia wagonjwa.”
“Kwa siku utakazo tenga zitakuwa zinatosha kabisa.”

Baada Jemima kumsindikiza mpaka sehemu ambayo alihisi ilikuwa inatosha waliweza kuagana. Azra akaondoka. Lakini wakiahidiana siku iliyofuata wangekutana kwa ajili ya Jemima kumtembeza maeneo mbalimbali ya kisiwa hicho.

*** Baada ya Azra kurejea nyumbani kwa mzee Makimbi na wazee wangine wa Swadege ya Rwadege, akiwa ametulia peke yake wazo la kumuondoa Jaji Kessy bado lilikuwa linaendelea kutembea akilini mwake.

Azra alifahamu kumuacha mzee huyo ni sawa na kuupuuzia ugonjwa mdogo mwilini, bila kujua ugonjwa hukua na baadaye unaweza kusumbua ukisha komaa.

Lazima nimuue! Alizidi kuwaza.
Lakini akiwaza jambo hilo swali lingine lilikuwa linaingia akilini mwake.
Nitamuua vipi?

Jambo hili ndilo lilimtatiza zaidi.
Baada ya kuwaza kwa muda na kushindwa kupata majibu ya namna ambavyo anaweza kutekeleza jambo hilo, Azra aliamua kuachana nalo kwa muda, ili kuupa ubongo wake muda wa kufikiri kutekeleza mauaji hayo.

Azra aliamini asingekosa njia ya kufanya mpaka azma aliyonayo ikatimia.

Amewahi kufanya mauaji huko nyuma katika mazingira magumu kuliko hata hayo ambayo alikuwepo, kwa hiyo kichwani mwake alifahamu kutekeleza mauaji ya Jaji Kessy, lilikuwa suala la muda tu.
 
SEHEMU YA 45

***
Siku iliyofuata kama ambavyo alikuwa ameahidiana na Jemima walikuwa pamoja kwa ajili ya msichana huyo kumtembeza maeneo mbalimbali ya Swadege ya Rwadege.

Safari yao ilianzia kwenye mipaka ya kisiwa hicho.

Akiwa mpakani Azra aliweza kujifunza jambo moja. Kwamba kulikuwa na ulinzi mkali kuliko kawaida.
Watu wa Swadege walilinda mipaka yao, kuliko hata roho zao.

Kwa sababu walifahamu hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee ambayo adui zao wangeitumia kuwavamia na kuchukua kila walichokitaka.

Jemima pia alimpeleka Azra mpaka kwenye mashamba ya mazao ya uhai. Azra alistaajabu mno baada ya kufika mashambani hapo.

Kilichomstaajabusha ni ukubwa wa mashamba hayo na namna ambavyo yalikuwa yanalidwa.
Katika matembezi hayo, Azra mambo mengine alikuwa anajifunza kwa kumuuliza Jemima.

Hakusita kumuuliza kwa nini Swadege hakukuwa na kiongozi. Binti huyo alimjibu kwamba, watu wengi walifahamu hivyo, kwamba hakukuwa na kiongozi lakini haikuwa hivyo.
Jemima alisema watu wote kisiwani hapo waliyaabudu mazao ya uhai.

Hayo ndiyo yaliwaongoza maana hata kulipokosekana mvua, kulipotokea majanga na mambo mengine mabaya, waganga wa kienyeji walitumika kwenda kwenye mashamba yenye mazao hayo kuomba kile walichokihijati na walipata kweli.

Siku tano zilipita, kila siku Azra akiwa na Jemima wakizunguka sehemu mbalimbali za kisiwa hicho.

Baada ya kuhakikisha kwamba katika siku hizo alipata kuyafahamu mambo mengi, Azra alijifungia chumbani kwake katika siku ya sita na na kuandika kitabu kilichoeleza kila kitu alichokiona.
Aliichora pia ramani ya Swadege, mipaka yake na hata mashamba ya uhai yalipokuwa.

Katika kitabu hicho alieleza pia juu ya tabia za watu wa Swadege, namna walivyoendesha majeshi yao, udhaifu waliyokuwa nao na mengine mengi aliyohisi yangeisaidia Marekani, kukitawala kisiwa hicho.

Baada ya kuimaliza kazi hiyo Azra alipumzika. Alifahamu kazi yake ya kwanza kuelekea kwenye azma ya kuitawala Swadege ilikuwa imekamilika.
 
SEHEMU YA 46

***
Hata hivyo huku yeye akifurahia mafanikio yake hayo ya kwanza ya kuingia kisiwani humo na kujifunza mengi juu ya kisiwa hicho, upande wa pili Kalega, kaka yake Jemima alikuwa hafurahii ukaribu kati ya Azra na dada yake Jemima.

Mara kwa mara alikuwa akimwambia mama yao, mama Cecilia juu ya suala hilo, lakini mama huyo alilipuuzia kwani aliona lilikuwa ni suala la kawaida tu na alimchukulia Azra kama kijana wa familia yake.
Kumbe alikuwa gizani.

Kama ambavyo Kalega alikuwa anahisi pengine kuna jambo baya lilikuwa linapangwa na Azra, kwa kupitia dada yake, ndiyo ukweli wenyewe ulivyokuwa. ***

Azma ya Azra ya kuanzisha uhusiano na Jemima hakutaka ichukue muda mrefu kukamilika. Katika kipindi hiki baada ya kuzoeana, alianza kumtania Jemima kwa maneno matamu yenye kumfurahisha.
“Jemima,” aliita Azra.

Ilikuwa siku moja wakiwa peke yao kwenye Mlima wa Iboni, ambako Jemima alimpeleka Azra, kutazama maua na mimea ya kuvutia iliyostawi mahali hapo.

Vilevile kileleni walipokuwa wamesimama, ilikuwa ni sehemu ambapo mtu akisimama anakiona Kisiwa cha Swadege ya Rwadege na mandhari yake kwa uzuri zaidi au kuliona jua wakati linazama.
“bee.” Aliitika.

“Naomba nifahamu kuhusu familia yako, hasa baba yako?” Azra alimwambia Jemima.

Jemima alibaki kimya kwa sekunde kadhaa akimtazama kijana huyo machoni kisha akamueleza;

“Alikuwa ni mwanaume tofauti sana. Jasiri na mwenye upendo wa dhati. Alikufa kwa ajili ya Swadege, kwenye mapigano baina yetu na wavamizi wetu.

Siku zote upendo wake umebaki ukiishi moyoni mwangu, sura yake haibanduki akilini mwangu….shiiiiii….” baada ya kutamka hayo Jemima alishusha pumzi ndefu na kuonekana hana raha tena.
“Pole sana,” Azra alimwambia.
“Nishapoa,” alijibu binti huyo. “Naomba unitazame.”

Azra alimwambia tena Jemima huku akinyoosha mikono yake na kushika ya Jemima, binti huyo aliinua macho yake taratibu na kumtazama Azra. “Jemima,” Azra alianza kuzungumza.

“Uzuri wa uso wako unanivutia sana, upole wako ndiyo unanifanya niwe hoi bin taaban. Nimejizuia kwa muda mrefu kukweleza haya, toka tuonane mara ya kwanza kwenye Gereza la Koba.
 
SEHEMU YA 47

“Nimetokea kukupenda Jemima, tena sana, naomba unikubalie niwe nawe, nikubalie nikuoe, niurudishe upendo wa baba yako kwenye maisha yako.”

Jemima alitoa macho na kumtazama Azra. Maneno ya kijana huyo yalimshangaza japokuwa yalikuwa matamu.

“Azra, unataka kunioa mimi,” Jemima alihoji akijigusa kifuani kwa kiganja cha mkono wake wa kulia.
“Ndiyo Jemima.” Azra alimjibu kwa uhakika.

“Ndugu zangu hawatanielewa.”
“Ni wewe kukubali tu Jemima, mimi nitafanya juu chini mpaka hili lifanikiwe.”
Baada ya Azra, kumaliza kuzungumza maneno hayo Jemima alijinasua kwenye mikono yake, akasimama na kuanza kukimbia.

“Jemima…” Azra aliita. “Jemima usikimbie…Jemima…”
Azra aliendelea kuita akimfuata msichana huyo lakini hakusimama. Aliendelea kukimbia.

Hata hivyo juu ya suala hilo Azra Malama hakukomea hapo. Mara kwa mara alipopata nafasi hakuacha kumsisitizia Jemima, juu ya ombi lake hilo. Baada ya kumsisitiza zaidi Jemima hakuwa na namna alimkubalia. Wakawa wachumba!

*** “Mkh khkhhhhh….Roliwe…. Mkh khkhhhhh…Roliwe, ayeee…” Ilisikika sauti laini ya mwanadada aliyekuwa anaimba. Aliendelea kuimba kwa sekunde kadhaa, akijisikiliza na kutabasamu.

Lakini akiendelea kufurahia sauti yake aliyobarikiwa na Mungu mara alisikia sauti ikimwambia; “Hebu acha kuimba.” Jemima aligeuka, akakutanisha macho na mama yake aliyekuwa ameingia chumbani humo alipokuwa akipiga pasi nguo zake.

“Furaha ya kuimba huku unatabasamu mchana huu inatoka wapi?” alihoji mama Cecilia. Jemima, alimtazama mama yake, akajikuta akishindwa kuzuia tabasamu kuchanua usoni kwake.

“Nimempenda kijana mama kwa mara ya kwanza,” Jemima alimueleza mama yake. Mama Cecilia alimtazama kwa kumkazia macho.

“Navutiwa kusikia binti yangu kapenda, lakini usiamini uhusiano wa kwanza,” alimwambia.

“Hapana mama, amekuja na ombi.” Jemima alizungumza akitabasamu.
“Kukuoa?” Mama Cecilia aliuliza.
“Ndiyo.” Jemima alijibu.

“Ni jogoo la mzee yupi?” aliuliza mama Cecilia huku uso wake ukichanua kwa tabasamu laini.

“Hajakulia Swadege ya Rwadege, amekuja hivi karibuni.”
“Azra?” mama Cecilia alihoji kwa mshangao.

“Ndiyo mama.”
“Jemima mwanangu.” Mama Cecilia alizungumza kwa kusisitiza. “Kwa nini unataka kunitia aibu, unawezaje kukubal
 
SEHEMU YA 48

Baada ya kuzungumza maneno hayo mama Cecilia akiwa amemtolea macho makali Jemima, aliendelea;
“Hawezi kukuoa, nimekataa.” Alizungumza kwa herufi kubwa kisha akaondoka kwenye chumba hicho akimuacha binti yake ameishiwa pozi.

Baada ya kutoka kwenye chumba hicho, moja kwa moja mama Cecilia alikwenda na kumueleza kila kitu Kalega, juu ya ombi la Azra Malama kwa Jemima.
Mama huyo alimwambia Kalega hakufurahishwa na kitendo hicho, zaidi alimuomba kama inawezekana wamfukuze Azra kisiwani hapo hata kwa nguvu, kabla hajamteka akili zaidi Jemima.

Suala hilo ni kama Kalega alikuwa analisubiri kwa hamu, hakuchelewa, mara moja alitoka mbiombio mpaka nje alipokuwa amemfunga farasi wake, akampanda na kwenda naye moja kwa moja mpaka lilipokuwa kundi la kina Shebo, mpakani. Aliwaeleza kilichojiri na akaomba waungane kwenda kumtimua Azra Malama.

Msako ulianza, baada ya saa mbili waliweza kumpata Azra akiwa ametulia kwenye Kilima cha Uwandani, akipanga mipango yake ya kukitawala kisiwa hicho.

Akiwa ameketi kilimani hapo, alisikia milio ya farasi wakitinga eneo hilo kutoka nyuma yake, aligeuka na kuona kundi la watu likiingia katika eneo hilo, akasimama na kuwasubiri vijana hao ambao baada ya kumkaribia walishuka kwenye farasi.

“Mmarekani…” Kalega alizungumza akipiga hatua mpaka alipokuwa amesimama Azra Malama, kisha alianza kumzunguka. “Unataka kumuoa dadaangu sindiyo?” Alimhoji, huku akiendelea kuzunguka.

“Ndiyo, ninampenda Jemima,” Azra alijibu kwa kujiamini. Vijana wale wote wakaangua kicheko.

“Unakipi cha kunipa kama mahari…eeh…labda almasi, dhahabu au mazao ya uhai…kipi unacho cha kunipa…?” Kalega alizidi kuhoji.

“Hana chochote huyo labda ategue kitendawili…” Ilisikika sauti ya Shebo aliyekuwa nyuma ya Kalega pamoja na vijana wengine. Vijana wote walicheka tena. Ha! Ha! Haaa!

“Wanasema utegue kitendawili tukupe mke,” Kalega alizungumza kwa dharau akimtazama Azra machoni. “nitafanya kama walivyoomba.

Lakini tunaweka makubaliano haya, ukifanikiwa kutegua kitendawili tunakupa mke, ukishindwa muda wako wa kuishi Swadege ya Rwadege ndiyo unakuwa umeishia hapo…”

Azra alikuwa anamtazama tu Kalega.
“Hujibu unanitolea tu macho,” Kalega alisema akimtazama Azra, kisha aka
 
SEHEMU YA 49

“Tegaa…” vijana wale wa nyuma yake waliitikia.
“Ninaonekana usiku bila kuitwa, ninafurahiwa, lakini mchana naondoka bila kufukuzwa, je, mimi ni nani?”
Ukimya ulitawala kama dakika moja hivi, Azra alikuwa akitafakari juu ya kitendawili hicho lakini hakuweza kupata jibu.

“Inaonekana kitendawili kigumu kwani kimya kinaonyesha huna jibu.” Kalega alizungumza kwa dharau huku anamkazia macho Azra. “Sasa muda wako wa kuishi Swadege umemalizika.”

Baada ya maneno hayo, Kalega akiwa ameshika rungu lake mkononi alimvaa, Azra, wakaanza kupigana. Japo Azra, hakuwa na silaha mkononi lakini alikuwa anajiweza.

Kalega alirusha rungu, Azra akalikwepa. Alirusha tena Azra akakwepa na kuruka sarakasi za nyuma kama tatu pamoja na mkuchu.

Kundi lote la Shebo, nalo lilimzungumza na kuanza kumchangia.
Kichapo kilitembea ikawa piga nikupige maana kumpiga Azra, ilikuwa si kazi rahisi kwa kundi lile. Jamaa alikuwa hapigiki, kila walipojaribu kurusha mateke aliruka sarakasi, ngumi alizipangua na zaidi yeye ndiye alikuwa anawapa kichapo watu wale.

Baada ya kuona wanazidiwa na Azra, mmoja wao alipuliza pembe la ng’ombe walilokuwa wanalitumia kwa kutoa taarifa kwa makundi mengine ya wapambanaji kisiwani hapo hasa pale wanapokuwa wamevamiwa na maadui zao.
Baada ya hapo haukupita muda, ghafla makundi mengine ya wapambanaji yaliingia katika eneo hilo kama mvua, yakiwa kwenye farasi..

Baada ya kuona hivyo Azra alifahamu wazi kwamba mambo yamekwisha haribika na asingeweza kuwapiga watu wengi namna ile kama sisimizi. Aligeuka nyuma na kuanza kukimbia.

Kundi lile likipiga kelele kila mmoja wao akiwa kwenye farasi wake lilianza kumkimbiza Azra. Kijana huyo aliendelea kukimbia, lakini baada ya kufika mbele zaidi kwenye kilima hicho cha Uwandani, hakukuwa na njia ya kukimbilia zaidi maana mbele yake kulikuwa na bonde kubwa lenye maporomoko ya maji.
Azra alibaki amesimama akishindwa afanye nini.

Kusema aruke, alihofia kufikia kwenye miamba na kupasuka vipandevipande, alipogeuka nyuma na kulitazama kundi lile, aliwaona watu wenye hasira na uchu wa kumuua. Alibaki njia panda!
 
SEHEMU YA 50

AZRA Malama, alibaki ameganda, akishindwa achukue uamuzi gani, hata hivyo kadiri alivyochelewa kufanya uamuzi ndivyo kundi lile lilivyozidi kumzunguka.

Kijana huyo akajikuta katikati, hakuwa tena na nafasi ya kufanya uamuzi wowote wala kupambana. Walikuwa ni wengi sana.

Alipiga magoti na kuinama chini.
Akaingia mikononi mwa Waswadege, watu ambao walikuwa na hasira naye kwelikweli kutokana na maafa aliyokuwa ameyasababisha.

Kundi hilo la wapambanaji lilimfunga Azra kamba, kisha wakamuunganisha kwenye farasi na kuanza kumburuza huku wanaelekea sehemu maalumu ya kutesea, ili wakampe mateso makali kijana huyo. ***

Wakati kijana huyo akikamatwa, upande wa pili vilio vilikuwa vimetawala katika kisiwa cha Swadege ya Rwadege.

Madhara aliyokuwa ameyasababisha Azra Malama, kwenye mapambano kati ya kundi la Shebo lililomfuata Uwandani likiongozwa na Kalega, yalikuwa ni makubwa. Watu wengi walikuwa wamepoteza maisha.
Zaidi ya watu ishirini!

Hiyo ilikuwa ni idadi kubwa mno ya watu kupoteza maisha kwenye pambano la mtu mmoja, ambalo kwa Swadege lilihesabika ni pambano dogo na la kihistoria.
Kutokana na hali hiyo watu wa Swadege walitokea kumchukia mno kijana huyo Azra Malama.

Walimchukia kuliko njaa, jua kali linaloharibu mazao au mafuriko.
Hata hivyo chuki haikuishia kwa Azra, peke yake. Ilikwenda mpaka kwa mama Cecilia na binti yake Jemima, waliyomleta kijana huyo Swadege.

Ndugu waliyopoteza watu wao waliamini kama si mama Cecilia na Jemima, maafa hayo yasingetokea, jambo lililowafanya ndugu hao kushika mapanga, mikuki na vijiti vya moto, wakiwa kwenye farasi na kwenda mpaka nyumbani kwa mama Cecilia kwa ajili ya kuchoma makazi hayo kwa moto.

Walipofika walimkuta Kalega, mama Cecilia na binti yake Jemima, wakiwa ndani. Baada ya kusikia fukuto la farasi, Kelega alitoka ndnai na kusimama uwanjani kwao, mama na dada yake wakiwa nyuma yake, kulisikiliza kundi hilo lilitaka nini, baada ya kufika.

“Hatuwezi kukubaliana na alichokifanya mama yako,” mmoja wa watu wale aliyeitwa Bonza, alimwambia Kalega.
“Hakuna aliyekuwa anamhitaji Azra,” Kalega alijibu.

“Lakini mama na dada yako ndio waliomleta!” Bonza aliongeza kwa msisitizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom