Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
Mtunzi Boniphance Ngumije sehemu ya 01
“Babu…” sauti ya mtoto ilisikia.
“Naam mjukuu wangu.” Ilijibu sauti nzito ya mtu mzee.
Kisha wanaonekana watu wawili wakiwa wameketi kwenye gogo la mti wakiwa wamejianika pembeni ya moto uliyokokwa na kuwapa mwanga usiku huo.
Mtu mmoja alikuwa ni mwanaume mzee, mweusi na mrefu, mwenye nywele nyingi na alikuwa amejitanda mashuka ya kimasai mwilini mwake yenye rangi ya bluu na nyekundu huku chini mguuni akiwa amekanyagia viatu vilivyotokana na mpira wa tairi la gari.
Mbele ya mwanaume huyo mzee alikuwa ameketi kijana mdogo mwenye miaka kumi na moja, mwembamba aliyekuwa amejitanda pia shuka la kimasai lenye rangi nyekundu yenye weusi kwa mbali.
Wawili hawa walikuwa kwenye mazungumzo na kijana yule aliendelea;
“Azra Malama ndiye nani?” Alimuuliza babu yake.
“Umemsikia wapi?” Babu yake alijibu kwa swali.
“Jina lake linatajwa kila mahali!”
“Azra Malama alikuwa Mfalme wa Swadege ya Rwadege.” Hatimaye babu yule alimjibu mjukuu wake.
“Imekuwaje mpaka akafa na kwa nini anazungumziwa kila mahali?”
“Kuhusu yeye mpaka kifo chake ni historia ndefu mjukuu wangu.”
“Naomba unisimulie.”
Yule mzee alimtazama mjukuu wake na kutabasamu, kisha akaokota kuni na kutupa kwenye moto mbele yake, akajitanda shuka lake la kimasai vizuri na kumtupia macho tena mjukuu wake.
Ukimya ulitawala wa sekunde chache, kisha yule mzee aliamua kuuvunja ukimya huo kwa kuanza kumsimulia mjukuu wake kile ambacho alikuwa anahitaji kusikia.
“Kama nilivyokwambia Azra Malama alikuwa ni Mfalme wa Swadege ya Rwadege, kisiwa ambacho kipo Afrika Mashariki na kimezungukwa na visiwa vya Zanzbar, kusini na Madagaska, kaskazini.
Mwishoni mwa karne ya 19, katika kisiwa hiki kabla ya Azra Malama kuwa mfalme, vipande vya ganda la dunia viliachana na kusababisha volkeno kali iliyoibuka juu ya ardhi ikiwa na gesi, majivu yenye joto kali pamoja na tetemeko la ardhi vilivyopelekea maafa makubwa sana.
Watu wote walikufa kisiwani hapo, mimea ikakauka na hakukuwa na kiumbe hai kilichosalia. Likabaki kuwa eneo tupu lililotelekezwa.
“Babu…” sauti ya mtoto ilisikia.
“Naam mjukuu wangu.” Ilijibu sauti nzito ya mtu mzee.
Kisha wanaonekana watu wawili wakiwa wameketi kwenye gogo la mti wakiwa wamejianika pembeni ya moto uliyokokwa na kuwapa mwanga usiku huo.
Mtu mmoja alikuwa ni mwanaume mzee, mweusi na mrefu, mwenye nywele nyingi na alikuwa amejitanda mashuka ya kimasai mwilini mwake yenye rangi ya bluu na nyekundu huku chini mguuni akiwa amekanyagia viatu vilivyotokana na mpira wa tairi la gari.
Mbele ya mwanaume huyo mzee alikuwa ameketi kijana mdogo mwenye miaka kumi na moja, mwembamba aliyekuwa amejitanda pia shuka la kimasai lenye rangi nyekundu yenye weusi kwa mbali.
Wawili hawa walikuwa kwenye mazungumzo na kijana yule aliendelea;
“Azra Malama ndiye nani?” Alimuuliza babu yake.
“Umemsikia wapi?” Babu yake alijibu kwa swali.
“Jina lake linatajwa kila mahali!”
“Azra Malama alikuwa Mfalme wa Swadege ya Rwadege.” Hatimaye babu yule alimjibu mjukuu wake.
“Imekuwaje mpaka akafa na kwa nini anazungumziwa kila mahali?”
“Kuhusu yeye mpaka kifo chake ni historia ndefu mjukuu wangu.”
“Naomba unisimulie.”
Yule mzee alimtazama mjukuu wake na kutabasamu, kisha akaokota kuni na kutupa kwenye moto mbele yake, akajitanda shuka lake la kimasai vizuri na kumtupia macho tena mjukuu wake.
Ukimya ulitawala wa sekunde chache, kisha yule mzee aliamua kuuvunja ukimya huo kwa kuanza kumsimulia mjukuu wake kile ambacho alikuwa anahitaji kusikia.
“Kama nilivyokwambia Azra Malama alikuwa ni Mfalme wa Swadege ya Rwadege, kisiwa ambacho kipo Afrika Mashariki na kimezungukwa na visiwa vya Zanzbar, kusini na Madagaska, kaskazini.
Mwishoni mwa karne ya 19, katika kisiwa hiki kabla ya Azra Malama kuwa mfalme, vipande vya ganda la dunia viliachana na kusababisha volkeno kali iliyoibuka juu ya ardhi ikiwa na gesi, majivu yenye joto kali pamoja na tetemeko la ardhi vilivyopelekea maafa makubwa sana.
Watu wote walikufa kisiwani hapo, mimea ikakauka na hakukuwa na kiumbe hai kilichosalia. Likabaki kuwa eneo tupu lililotelekezwa.