Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 16
“Sikiliza Azra,” Mzungu mwingine aliyekuwa amekaa aitwaye Smith, alizungumza akisimama, akaendelea;
“Sisi kuwa weupe na wewe kuwa mweusi haimaanishi hatuwezi kuwa mtu na kaka zake, sisi ni ndugu na ili kudumisha undugu wetu imetupasa tukupe kazi ya kufanya itakayokupa uhuru.”
“Simwagi damu ya binadamu tena!” Azra alijibu kwa mkazo.
“Ha! Ha! Haaa!” Wale Wazungu walicheka.
“Inashangaza kuona binadamu anakimbia kivuli chake.
Hata hivyo miguu hii haijakufuata hapa kwa kazi ya kumwaga damu ya ndugu zako, tunahitaji kukusaidia kurudi kwenu Swadege ya Rwadege ukatawale na kuwa mfalme, bila shaka umefurahi kusikia taarifa hii!” Smith alimwambia Azra.
Azra alibaki ametoa macho akitafakari maneno yale ya huyo Mzungu aliyekuwa amesimama mbele yake.
Kauli hiyo ilimkumbusha azma yake ya muda mrefu ya kurudi kwao Swadege ya Rwadege, ambako marehemu baba yake mzazi aliwahi kumwambia kwamba ni sehemu nzuri kuliko mahali popote pale duniani.
“Jua la nyumbani ni zawadi nzuri na ya kujivunia ambayo Mungu alitubariki, Swadege ya Rwadege ni mfano wa gadeni ya Hedeni, nyumbani hakuna ugonjwa wala uzee, kuna maisha yenye uhai usio na kikomo kwani hata wafu huishi pamoja nasi,” Azra alikumbuka maneno ya baba yake.
Lakini akiwatazama Wazungu wale alipata swali kwamba nini watu hao walikuwa wanahitaji kupata ndani ya Swadege mpaka watafute mtu akatawale. Azra aliwafahamu Wamarekani, wasingeweza kufanya jambo lisilo na manufaa kwao.
Hata hivyo alipokubali kukaa chini na kusikiliza nini hasa aliitiwa mahali hapo, Smith alimwelewesha lengo lao la kumsaidia kurudi kwao Afrika na kwenda kuwa Mfalme wa Swadege ya Rwadege.
Smith aliongeza kumwambia kwamba walifikia uamzi huo wakiwa wamelenga kuyapata mazao ya uhai yanayopatikana kwenye kisiwa hicho hata kuyasaidia mataifa mbalimbali duniani, kutibu wagonjwa, kuboresha teknolojia, lakini zaidi kutoa msaada kwenye mambo tofautitofauti.
Azra Malama baada ya kusikiliza kwa makini na kutafakari hicho alichokuwa ameambiwa, alikubali kuifanya kazi hiyo lakini kwa sharti moja tu. Jaji Steven Kessy atolewe gerezani pia, jambo ambalo lilitekelezwa mara moja!
“Siamini Azra!” Mzee Kessy alimwambia Azra siku aliyotolewa gerezani.
“Sikiliza Azra,” Mzungu mwingine aliyekuwa amekaa aitwaye Smith, alizungumza akisimama, akaendelea;
“Sisi kuwa weupe na wewe kuwa mweusi haimaanishi hatuwezi kuwa mtu na kaka zake, sisi ni ndugu na ili kudumisha undugu wetu imetupasa tukupe kazi ya kufanya itakayokupa uhuru.”
“Simwagi damu ya binadamu tena!” Azra alijibu kwa mkazo.
“Ha! Ha! Haaa!” Wale Wazungu walicheka.
“Inashangaza kuona binadamu anakimbia kivuli chake.
Hata hivyo miguu hii haijakufuata hapa kwa kazi ya kumwaga damu ya ndugu zako, tunahitaji kukusaidia kurudi kwenu Swadege ya Rwadege ukatawale na kuwa mfalme, bila shaka umefurahi kusikia taarifa hii!” Smith alimwambia Azra.
Azra alibaki ametoa macho akitafakari maneno yale ya huyo Mzungu aliyekuwa amesimama mbele yake.
Kauli hiyo ilimkumbusha azma yake ya muda mrefu ya kurudi kwao Swadege ya Rwadege, ambako marehemu baba yake mzazi aliwahi kumwambia kwamba ni sehemu nzuri kuliko mahali popote pale duniani.
“Jua la nyumbani ni zawadi nzuri na ya kujivunia ambayo Mungu alitubariki, Swadege ya Rwadege ni mfano wa gadeni ya Hedeni, nyumbani hakuna ugonjwa wala uzee, kuna maisha yenye uhai usio na kikomo kwani hata wafu huishi pamoja nasi,” Azra alikumbuka maneno ya baba yake.
Lakini akiwatazama Wazungu wale alipata swali kwamba nini watu hao walikuwa wanahitaji kupata ndani ya Swadege mpaka watafute mtu akatawale. Azra aliwafahamu Wamarekani, wasingeweza kufanya jambo lisilo na manufaa kwao.
Hata hivyo alipokubali kukaa chini na kusikiliza nini hasa aliitiwa mahali hapo, Smith alimwelewesha lengo lao la kumsaidia kurudi kwao Afrika na kwenda kuwa Mfalme wa Swadege ya Rwadege.
Smith aliongeza kumwambia kwamba walifikia uamzi huo wakiwa wamelenga kuyapata mazao ya uhai yanayopatikana kwenye kisiwa hicho hata kuyasaidia mataifa mbalimbali duniani, kutibu wagonjwa, kuboresha teknolojia, lakini zaidi kutoa msaada kwenye mambo tofautitofauti.
Azra Malama baada ya kusikiliza kwa makini na kutafakari hicho alichokuwa ameambiwa, alikubali kuifanya kazi hiyo lakini kwa sharti moja tu. Jaji Steven Kessy atolewe gerezani pia, jambo ambalo lilitekelezwa mara moja!
“Siamini Azra!” Mzee Kessy alimwambia Azra siku aliyotolewa gerezani.