Mwingira atangaza mwisho wa CCM 2015

Ili mradi hamlazimishi mtu kwenda kanisani kwake sioni tatizo, watu dhaifu hujipeleka na kuliwa, usikute hata huyo alomegewa wife bado ni mwana kondoo wake. Jamaa liko kisanii/kibiashara zaidi. Wajinga ndio waliwao
 
Mungu usamehe makosa ya mtu. Hata kama umefanya dhambi kiasi gani unapoenda kwake kwa toba ya kweli ufuta dhambi zako. Mwingira kama ametubu na aendelei na mchezo mchafu bila shaka amesamehewa. Tujadili thread wakuu
 
hivi mtu akisema CCM mwisho 2015 anakuwa amevunja sheria gani ya nchi?

mimi si nabii na mimi nasema CCM mwisho 2015 na kila Mtanzania Mkweli na Mpenda Haki ni wakati wa kusema
NIMEJITAMBUA, CCM ILITOTAWALA KWA MIAKA 50 BILA MAFANIKIO, HAICHAGULIKI 2015
 
Hawa ndo walikuwa viongozi wengine kwishney

206295_201872893167465_3289548_n.jpg
 
Watu wengine waongo...binafsi sikusikia km mwaka 2015 ulitajwa
 
we Ritz utashangaa nini wakati unajua kabisa amewatoroka. nadhani M4C inaelekea pazuri mpaka kwa wachangiaji wa kijani
 
Mkuu inawezekana amesema ukweli lakini tatizo amesemea kanisani, wengi watazani anawapigia kampeni chama fulani.
Kama mtumishi wa Mungu ambaye anawaumini chini yake ana ruhusa kufanya alichofanya
 
Ndio hawa wale manabii wa uongo waliotajwa kwenye vitabu.

Si nilisikia juzi kati alichochea waumini wake wafanye fujo! au ndio hasira ya kukamatwa na polisi waumini wake naona amesema hapo wapiga mabomu. Yeye alitaka achome moto kiwanda cha watu aachwe tu!
 
Hii ni dhahiri mwisho wa ccm kuwa madarakani ni 2015.
Watu wameshaona mbali na ndio wakati wakujichukulia ujiko wa buure, kwa kutabiri kifo cha mgonjwa baada ya kumuona anapumulia mashine.
 
Alitangaza mwisho wa CCM au mwisho wa wanaodhulumu?

Unabii wa mwisho wa wanaodhulumu ulishasemwa siku nyingi ba haijalishi wako chama gani yaani ni Koranic & Biblical!
 
Hukumu ni juu ya Mungu wala si kazi yetu. Kama nimemwelewa vema mleta thread hii hakusema Mwingira ametabiri na wala hakusema ni unabii, bali anasema Mwingira amesema kama mtumishi wa Mungu. Ningepata shida kama ungekuwa ni unabii lakini kama amesema tuu, sio tatizo sana inategemea alikuwa ansisitiza nini katika mahubiri yake au moyoni mwake amebeba nini. Kuhusu kumhukumu tumwachie Mungu aliyemwita katika huduma hiyo kwani hata nyie mnaomhukumu je mko safi? Usiangalie tu na kujifariji kwamba, kwakuwa wewe sio mtume au nabii au mtumishi wa Mungu una haki ya kutenda dhambi na yeye kwa sababu ni mtumishi wa Mungu hawezi kutenda dhambi. Dhambi ni dhambi tu ifanywe na mtumishi ni dhambi ifanywe na wewe ni dhambi na hukumu yake ni moja. Usione kibanzi kwenye jicho la mwenzio wakati boriti liko kwenye jicho lako. Unachotakiwa wewe kufanya kama una hakika na umethibitisha kweli anafanya au alifanya dhambi mnazozisema ni kumwombea ili Mungu amsamehe na aweze kuifanya kazi ya Mungu kwa uaminifu. Kama huna uhakika, jihadhari kuwawekea watumishi wa Mungu maneno ya uongo ni moto kwako.
 
Kipindi Live TRENET: Mtume na Nabii Josephat Mwingira katika mahubiri yake ameeleza kuwa yeye kama mtumishi wa Mungu anatangaza kuwa walioko madarakani mafisadi na wapiga mabomu mwisho wao ni 2015 kama alivyoitabiria KANU ya Kenya...!! ametoa mifano kadhaa ya Biblia kuhusu Shedrack, Meshack na Abednego waliotupiwa kwenye moto lakini hawakuungua. ameeleza kwa ujasiri sana kuwa watawala wa Tanzania wataharibikiwa mambo yao kutokana na maovu wanayowafanyia waTz..!

my take:
naona hz ni hasira za kupigwa mabomu pale kanisani kwake...!

Bolded is a truth!!! Wananchi wenyewe wamechoka!!! Watafanya mageuzi.
 
Back
Top Bottom