Mods, naomba msiunganishe hii mada.
Brother Mwigulu, si sahihi kabisa kuhusisha tweet ya Zitto kuhusu ibara hiyo ya katiba na swala zima la ajali ya kivuko cha Mv.Nyerere.
Watu wengi hawaelewi kuwa ile tweet Zitto aliipost tarehe 20/09//2018 saa saba na dakika thelathini na mbili mchana (1:32 PM) wakati ajali ilitokea saa nane kamili mchana kwa mujibu wa RPC (someni uzi wa ajali ulioko hata hapa JF kuona kauli hiyo ya RPC).
Binafsi ile tweet ya Zitto niliona siku moja kabla haijaletwa hata hapa JF na kwa mazingira ya siku ile, inaonyesha Zitto aliguswa na document fulani ambayo wengi iliwashitua na hata hapa JF iliibua mjadala mzito kuhusu maswala ya family planning.
Brother Mwigulu, kama ungeongelea ile tweet ya Zitto kuhoji kuhusu maswala ya kununua Dreamliner, maSGR, n.k hapo ungekuwa unaongelea tweet sahihi iliyohusiana na maswala ya ajali lakini sio ile tweet yake kuhusu ibara ya 37 (2).
Tuweke kumbukumbu sawa na tuache kutafuta huruma kutoka kwenye jamii.