Zitto Kabwe, na wenzako mnaoendelea kusambaza thread hii, With due respect to you, let us debate on Agendas, National issues and NOT PERSONALITIES. My collegemate, my agemate, my felloweconomist, mwanadamu mwenzangu: Where is the limit?
Nimesoma thread yako, na nimesoma kipengele cha Katiba ulichokitaja. AMBAYO IKO KWENYE THREAD; "Ni muda mwafaka SASA Baraza la Mawaziri kutumia Ibara ya 37(2) ya Katiba. Kwenye Katiba, maudhui ya Ibara hiyo ni"
37(2), Endapo Baraza la Mawaziri litaona kuwa Rais hawezi kumudu kazi zake kwa sababu ya Maradhi ya MWILI au AKILI, laweza kuwasilisha kwa Jaji Mkuu azimio la kumwomba Jaji Mkuu athibitishe kwamba kwa sababu ya Maradhi ya Mwili au ya Akili hawezi kumudu kazi zake. " .......
.......
Mwanzo nilidhani ID feki, pili nikadhani wamekulisha maneno, but sijaona ukikanusha. Well ukiwa na jazba unaweza kuandika hivyo na yeyote mwenye jazba anaweza kufurahia hicho. But let us get back to the sense of humanity;
1) Taifa linapita kwenye janga, limepoteza watu, watu wako kwenye majonzi, Kiongozi ambaye ndio anadhamana ya watu wote yuko kwenye kipindi cha kupoteza watu kwenye janga hilo, msiba huo ni wake, wewe badala ya kumpa pole, any word of hope, unaweka neno ambalo impliedly unataka kuaminisha watu kuwa Rais anaumwa, maradhi ya mwili au ya akili. The timing and allegation haina chembe ya ubinadamu.
2) Hata kama, kuna mapungufu kwenye kuruhusu watu kupanda au vyovyote, ustaarabu wetu unatuonesha TUWAHIFADHI KWANZA NDUGU ZETU, NDIO TUANZE KUGOMBANA, kama ni kusingiziana au mirathi, nk, SOTE TUTAKUFA SIKU MOJA, hata sasa, Hii sio sherehe, badala ya kuwafariji ndugu, jamaa na wote waliokutwa na janga hili, we feel tumepata mwanya wa kupenyeza maneno. Hatuwatendei haki wale walio kwenye deep pain ya janga hili.
3) Hata kama kwenye siasa kuna kusemana, hata kama kwenye siasa kuna kushambuliana, hata kama kwenye siasa kuna kuchukiana, Maneno yanayolenga personalities za aina hii, tena za maswala ya kiafya, kwa kiongozi, maneno yanayoweza kusababisha taharuki kwenye familia, kwa wananchi na maneno yanayojeruhi personalities, ni adui mkubwa wa uhuru wa kuongea na ustawi wa demokrasia unaopiganiwa.
4) Mimi najua status ya afya yangu, mke wangu na watoto wangu, Je nina haki ya kujua status ya afya yako Zitto? Ni haki ya kuifanya public na nije kuwashauri wapiga kura wako? Brothers and sisters lets observe humanity.
5) Nini tafsiri sahihi ya kipengele hicho cha Katiba,? Hujakielewa, au unatumia Katiba kutukana, kudhalilisha, kuaminisha kitu kisicho na ukweli.
"KITU NISICHOTAKA KUTENDEWA HUWA SITAKI NA MWINGINE ATENDEWE, Huyu ni Kiongozi wetu, Huyu ni Baba yetu kwa umri, Hii ni nembo yetu as a Nation, can you just say like that? can you just wish like that? Oooh No!
Dkt Mwigulu Nchemba, (MB) Iramba.