Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 87,326
- 150,813
Upo sahihi mkuu unachotakiwa ni kutoa njia kwa vijana wafanye nini ili wafike huko na kuishi bila kuvunja sheria kama unajua kama haujui tulia tuu watapata njia maana hakuna lisilowezekana wala msiwakatishe tamaa kabisa...
Kuna mtu kaomba kujua process ya kupata immigrant visa. Nimempa "from the horses mouth".
Mimi baharia ingawa wa nchi kavu na sikuwepo ughaibuni enzi za mtoto wa Gorbachev Vale wa Pereas, lakini nishawahi kusaidia mpaka watu waliofika nchi za watu kibichibichi hawana sehemu za kufikia miji mikubwa, kwa hiyo habari za kuoneshana njia kwetu ni utamaduni, hata kwetu Dar Wasukuma waliokuwa wanakuja mara ya kwanza mjini hawana pakufikia walifikia sana.
Sina roho ya Kangi Lugola, ningekuwa na roho hiyo ningekuwa bongo nasota bado.
Kwa hiyo kupigiana mapande watu kusafiri si kitu ambacho sikijui. Ila nasisitiza tu dunia imebadilika, zile safari za kiskauti skauti za 1997 mpaka 2000, enzi ya kabla ya 9/11 masharti nafuu kujichanganya rahisi, kwa sasa hata ukifika US, bila makaratasi ya kueleweka sisemi huwezi kufanikiwa, kuna vichaa kibao wanakomaa, ila utapata tabu sana na unaweza kuona tabu hazina maana, au ukaishia jela.
Kwa hivyo sitaki kuonekana navunja watu moyo.
Tunahitaji kuongeza wanajeshi huku.
Ila safari inabidi ipangwe kwa akili na si kukurupuka,unaweza kufanya mistake moja tu katika mipango yako ikaku cost siku zote.