Mwendelezo wa Mgomo, Kiongozi wa Wafanyabiashara Kariakoo adai kuna kikundi kina maslahi binafsi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Kariakoo, Martin Mbwana amesema mgomo unaoendelea leo unasababishwa na kikundi cha watu wachache wenye maslahi yao binafsi huku akiomba wachukuliwe hatua na kuahidi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya usalama.

Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 16, 2023 wakati akizungumza na Mwananchi kufuatia baadhi ya maduka kuendelea kufungwa, licha ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jana kuwataka wafanyabiashara hao kusitisha mgomo huku akiahidi kushughulikia kero zao kikao cha kesho Jumatano ya Mei 17, 2023.

Mbwana amesema kilio chao kama wafanyabiashara ilikuwa ni kusikilizwa na Rais Samia Suluhu Hassan, na katika kuonyesha kuwa amewasikia alimtuma Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

"Alipokuja aliwaomba wafanyabiashara wafungue maduka na kuahidi kuwasiliza siku ya Jumatano. Nashangaa wafanyabiashara kuwa hawana imani na Waziru Mkuu," amesema

Amesema shida ni kikundi cha watu wachache wanaoonekana kuwa na manufaa na mgomo huo huku akieleza kuwa ameomba msaada kwa vyombo vya usalama kuwachukulia hatua na kusema yupo tayari kutoa ushirikiano.

POLISI WATOA TAMKO
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema wapo tayari kuimarisha usalama kwa wafanyabiashara wa soko la Kariakoo watakaofungua maduka yao huku akiwatahadharisha watakaoleta vurugu.

Muliro ametoa kauli hiyo leo Jumanne Mei 16, 2023 alipotembelea wafanyabiashara wa Kariakoo.

“Tupo kuimarisha usalama watakaofunga wafunge nasema ole wake atakeyekwenda kumsumbua atakayefungua tayari Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Jana alitoa maagizo na maelekezo yake yameeleweka” amesema Muliro na kuongeza,

“Watu wanaofungua maduka tunawahakikishia usalama, tumeshaweka askari mbalimbali mtu anayetaka afunge lakini anayetaka kufungua afungue usalama upo.

“Mtu yeyote atakayefungua biashara wafanye na natoa onyo kali atakayekwenda kufanya fujo hatua kali zitachukuliwa.”


Chanzo: Mwananchi
 
Miongoni mwa style za Shujaa Magufuli nilizozikubali ni ile ya Tumbua Tumbua na Ile ya " Utemi" ya Tembeeni kifua mbere

Utakuta hapo Kariakoo ni Wanasiasa Uchwara wachache tu ndio wanaotesa Watu kushindwa kujipatia Mkate wa kila siku kwa siku ya pili leo

Shujaa Magufuli angenyooka nao mchana kweupe

Fikiria Wafanyabiashara Kutoka Rwanda, Burundi, Comoro na Congo wanatesekaje na mgomo huu!!
 
Duuh mi naona kama kiongozi wao ange-side na wafanyabiashara hii ni 'betrayal'
 
Naomba kufahamu hoja haswa za wanyabiashara wa kariakoo ni nini na mapendekezo yao ni nini kutatua huu mgogoro
1.kamatakamata ya task force
2.rushwa
3.kodi ambazo hazieleweki
4.mikakati ya kusajili stoo
5.TRA kwa ujumla wake wanafanya mazingira ya kufanya biashara kuwa magumu sana kwa wafanyabiashara Kariakoo na Tanzania kwa ujumla.
 
1.kamatakamata ya task force
2.rushwa
3.kodi ambazo hazieleweki
4.mikakati ya kusajili stoo
5.TRA kwa ujumla wake wanafanya mazingira ya kufanya biashara kuwa magumu sana kwa wafanyabiashara Kariakoo na Tanzania kwa ujumla.
Je mapendezo yao ni nini kwa serikali.
Natamani kujua wafanyabiashara wa kariakoo na wafanya biashara wa tz kwa ujumla mapendekezo yao ni nini?????
 
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Kariakoo, Martin Mbwana amesema mgomo unaoendelea leo unasababishwa na kikundi cha watu wachache wenye maslahi yao binafsi huku akiomba wachukuliwe hatua na kuahidi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya usalama.

Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 16, 2023 wakati akizungumza na Mwananchi kufuatia baadhi ya maduka kuendelea kufungwa, licha ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jana kuwataka wafanyabiashara hao kusitisha mgomo huku akiahidi kushughulikia kero zao kikao cha kesho Jumatano ya Mei 17, 2023.

Mbwana amesema kilio chao kama wafanyabiashara ilikuwa ni kusikilizwa na Rais Samia Suluhu Hassan, na katika kuonyesha kuwa amewasikia alimtuma Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

"Alipokuja aliwaomba wafanyabiashara wafungue maduka na kuahidi kuwasiliza siku ya Jumatano. Nashangaa wafanyabiashara kuwa hawana imani na Waziru Mkuu," amesema

Amesema shida ni kikundi cha watu wachache wanaoonekana kuwa na manufaa na mgomo huo huku akieleza kuwa ameomba msaada kwa vyombo vya usalama kuwachukulia hatua na kusema yupo tayari kutoa ushirikiano.

POLISI WATOA TAMKO
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema wapo tayari kuimarisha usalama kwa wafanyabiashara wa soko la Kariakoo watakaofungua maduka yao huku akiwatahadharisha watakaoleta vurugu.

Muliro ametoa kauli hiyo leo Jumanne Mei 16, 2023 alipotembelea wafanyabiashara wa Kariakoo.

“Tupo kuimarisha usalama watakaofunga wafunge nasema ole wake atakeyekwenda kumsumbua atakayefungua tayari Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Jana alitoa maagizo na maelekezo yake yameeleweka” amesema Muliro na kuongeza,

“Watu wanaofungua maduka tunawahakikishia usalama, tumeshaweka askari mbalimbali mtu anayetaka afunge lakini anayetaka kufungua afungue usalama upo.

“Mtu yeyote atakayefungua biashara wafanye na natoa onyo kali atakayekwenda kufanya fujo hatua kali zitachukuliwa.”


Chanzo: Mwananchi
Leo hii nimekutana na polisi mtaa wa Nyamwezi na mitutu.. na watu hawajafungua
 
Back
Top Bottom