Mkuu CHADEMA bado ngangari ndani na nje ya Bunge ndiyo sababu wameamua kuongoza nchi kwa mtutu wa bunduki kwa woga mkubwa waliokuwa nao dhidi ya CHADEMA.
Hawana sera hawana hoja sasa wamebaki kukurupuka na mwendo kasi huku nchi ikienda Alijojo. Nadhani umewasikia wazee wa CCM akina Mwinyi, Warioba na Butiku kuhusu huyu dikteta uchwara.
CHADEMA iliitwa chama cha Wachagga na wakristo lakini ikaendelea kupendwa na Watanzania wengi, ikafanyiwa kila hila na manyanyaso dhidi ya viongozi na wanachama lakini bado ikaendelea kukua tu. Ikatabiriwa kufa mara chungu nzima na wale waliojivalisha majoho ya Sheikh Yahya lakini utabiri wao ulikuwa ni utabiri uchwara. CHADEMA ngangari daima.