Bramo
JF-Expert Member
- Oct 21, 2009
- 13,242
- 10,227
- Thread starter
- #81
Mkuu TCRA, Nina Ushauri/ Wazo ambalo mie naona ni la Mbolea sana kuhusu Digitally.Kwa nini Msi Regulate tukawa na Ving'amuzi Universal na Smart Cards tofaut tofaut, Mtu hatalazimika Kumiliki Zaid ya King;amuzi Kimoja, unakuwa na Decoder Moja ambayo ina accept Smart Card tofaut tofaut zinazomilikiwa na Vendor tofaut kama vile Star Times etc etc.Siku Nikienda China, nanunua Decoder nikiileta Tanzania iwe inapiga Mzigo kama kawa, ni kama vile Simu, Operator anamiliki SIM Card, lakini Handset ni Chaguo la Mteja.Hili linawezekana sana WakuuKamanda Kazi, ZUKU hawako kwenye kuwajibika kuonesha local channels. ZUKU Na DSTV wako kwenye mfumo tofauti Na Mabadiliko ya kutoka Analojia kwenda Dijitali. ZUKU Na DSTV wako katika mfumo Wa Satelite ambao ni Wa dijitali tangu zamani. Mfumo huu ni Wa Malipo, ili uone channel local, kwanza lazima yawepo makubaliano kati ya Content Service Providers (mtengeneza maudhui) pamoja na Mtoa huduma. Lazima kulipia huduma hii kuona kwani ni ya malipo (subscription service).
Channel ZA bure zinatakiwa kuonekana katika mfumo Mpya Wa Utangazaji Wa dijitali Wa Terrestrial Digital Broadcasting ambao, channel zote zilizokuwa zinapatikana kupitia Terrestrial Analogue Broadcasting bure zinapaswa kuwa katika kila kingamuzi Cha watoa huduma watatu wanaotoa huduma hii (Multiplex Operator) yaani Agape Associates, Basic Transmission pamoja Na Star Times, na hii ni Kwa mujibu Wa Sheria. Watoa huduma wote watatu wametekeleza matakwa haya ya sheria.
Aidha ifahamike kuwa hata katika mfumo Wa tatu Wa Utangazaji (Digital Cable TV Broadcasting) maarufu maeneo mengi nchini pia ni wa Malipo Na Channel local kuonekana pia kuna utaratibu wake na haihusiki Na mabadiliko ya kuhamia dijitali Na matakwa ya kuwa local channel zote. Huu ni utaratibu kama ilivyo katika mfumo Wa leseni ZA Utangazaji. Ni kama kuhoji kwa nini mwenye leseni D ya udereva haruhusiwi kuendesha bus la abiria.
Tafadhali pitia katika website yetu www.tcra.go.tz upate taarifa zaidi kuhusu leseni Na maelekezo yake. Aidha angalia ukurasa wetu wa FB www.facebook.com/TCRA1 Kwa maelezo zaidi.
Ni vizuri kuielewa sekta, mfumo Wa leseni, masharti pamoja Na kanuni zinavyoiongoza sekta ili kutokuchanganya hii mifumo. Aidha kuhusu TCRA kama unavyohisi iko, tunaheshimu mawazo yako na Asante kwa ushirikiano Na mawazo yako.
Last edited by a moderator: