Mwanza jiji zima hakuna Brown Bread?

Ok .... Kwamba Mwanza bado sana hata mikate ya brown hakuna!.😳
Mwisho wa mwaka huu asubuhi sana naamkia Mwanza! ....Wenyeji wa mji ule walioko humu, naomba uzoefu wenu, kuhusu nyumba za wageni, maeneo salama ya kuvinjari, mambo ya kula kula na kumwagilia roho.πŸ˜€
Natanguliza shukurani.
 
Ungeenda Uturn pale mtaa w mviringo ipo supermarket ya maana
 
Ondoa shaka Mkuu,Mwanza utakaa na kufurahia maisha vizuri sana,wenyeji ni wakalimu sana,rate ya uhalifu ni ndogo so utatembea kila mahari bila kashi kashi kabisa.Viwanja vya kuvinjari vipo kina The Cask na wenzie unakula bata hadi majogoo.Sehemu ya kufikia inategemea na bajeti yako tu kuna sehemu ya $150 per night na kuna sehemu ya Chumba 20,000-35,000.Ni wewe tu na bajeti yako.
 
Du!. Nimeipenda hiyo, usingizi kuulipia Biden 150 hapana, bora nipate viwanja vilivyochangamka hadi machweo....@Nyamizi nitakutafuta humu humu nitua Mwanza.
 
Mimi nilitaka kununua Pound sterling ilinichukua siku tatu kuzipata,Mwanza naipenda sana ukiondoa issue ndogondogo kama za Brown bread Mwanza patamu alafu bata bei poaaaaa tu.
Du! πŸ€” Nikusanya data!.
 
Sasa kwa akili yako unaona mwanza nalo ni jiji la maana?😁😁😁......juzi nilikuwa sehemu nimekaa nikaagiza maji ya kunywa madogo bei mimi nafahamu ni 500 .....nikaagiza maji ya moto eti naambiwa bei ni sh 600 nilishangaa sanaπŸ€”πŸ€”πŸ€” maji ya moto nauziwa 600 kwa lipi hasa
 
Hata watu wake ni washamba bado compared na wa Arusha!!
Kwa hiyo wa Arusha ndiyo wajanja? Hii hii Arusha ambayo nimeishi 8yrs au kuna Arusha nyingine.Tena tunaishi Njiro unaonekana wa kishua kumbe michosho tupu.Ipeni Mwanza heshima yake,wanaweza kuwa wanakandamiza kiswahili but Mwanza kuna watu wana exposure kubwa wanasafiri kila mara tu na route zao ni Mwanza Nairobi kisha hao nnje ya Nchi na Dar hawapajui na wala hawahitaji kupajua.Nyinyi wa Arusha kaeni na ujanja wenu wa kuvuta bangi ndiyo mnachoweza.
 
Ushamba wa Arusha upo kwy ulimbukeni wa vitu. Na kujifanya wahuni. Kila muarusha anajifanya muhuni mvuta bange
Yani kuvuta bangi ndiyo wanajiona wajanja [emoji3][emoji3]
 
Acha Ushamba, huwezi uliza jiji Zima la mwanza. Mwanza hawakai wasukuma pekee Yao ni jiji la kimataifa wewe kumuuliza huyo mshamba wako unaona umeuliza jiji Zima..
 
Sasa wewe unalalamika kwakuwa ulienda sehemu si yako,ulipaswa kwenda sehemu inayoendana na bajeti yako Mkuu.Hata Dar beer local inauzwa 1500-2000 lakini kuna sehemu inauzwa 9,000.Ni wewe tu unataka kwenda wapi.Wallet yako ndiyo ilipaswa ikuongoze.Siyo una pesa ya mawazo halafu unataka kwenda sehemu za wenye nazo utaishia kulalamika hata tofauti ya shs 100 tu [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Du!... Kumbe Bugarika nako ni noma? πŸ€” 😳
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…