Mwanza City: The Photo Gallery

Mwanza City: The Photo Gallery

Maendeleo ni kama Mwanga Boss, Jiji haliwezi ng'arishwa Ilemela ikabaki imepauka. Nimegusa Metropole kwa sababu ndio taswira ya JIJI.
Sura ya jiji ni ilemela na nyamagana... huwezi kusema mwanza jiji . ilemela isiwemo ..na ndio maana nimesema bado Kuna mgogoro wa namna Gani ya kuiita halmashauri inayosimamia nyamagana...jina inatakiwa iiitwe nyamagana municipal council.lakin changamoto ilionekana kuwa kama tutaita hv bas kwenye orodha ya majiji mwanza haitakuwemo ..ndipo waliazimia ibaki tu na Hilo jina la zamani
 
Ndio maana napinga mji kupanuka, bora tuuboreshe, tunashabikia frame, huko dodoma sehemu mpya zinazojengwa unaona frame za maduka hovyohovyo kama mza?

Hivi kusimamia watu kwamba eneo hili ukinunua kiwanja jenga hivi na ezeka vigae au bati jekundu, huwezi acha nenda kajenge Sengerema.
Je hii nayo ni kazi ngumu kwa viongozi halafu mnakuwa mnapita kila baada ya mwezi kuona maendeleo ya ujenzi, aliyekiuka piga faini na kuvunjiwa, tutashika adabu ila rushwa imetujaa sana kuliko kusimamia haki
Dodoma..maframe yapo . nkuhungu,mnada Mpya ,maili mbili ,kisasa ,mkonze n.k
 
Na haitawezekana kuiunganisha Ilemela na Nyamagana, hilo baraza la madiwani litakuwa kama darasa la shule ya msingi na atatakiwa awepo Mbunge mmoja tu.
 
Kukua Kwa mji hakuzuiliki kaka ,.....Hilo linawezekana tu Kwa kuboresha miji ya pembeni au wilaya .Ili watu wasivutiwe sana kuhamia miji mikubwa wabaki kwenye miji midogo ... other wise watu wataendelea kuhamia kwenye majiji...... marekani wameweza kutengeneza miji mingi ya siZe ya kati ,,,,hivyo watu hawaoni haja ya kukimbilia new York au Los Angeles
Hahaha, mambo ya Chicago, Dalas Texas, Washington, Atlanta Georgia, nadhani wale jamaa miji yao yote ni ya maana maana tu kwa hiyo kunakuwa hamna immigration zisizokuwa za msingi au kutambiana
 
Mzee baba angemaliza mda wake mwanza ingekuwa kama paris aisee
Yule jamaa alikuwa anaibadilisha hii nchi sio mza tu,
Hakuna anayeongelea treni za mjini na tram/metro kwa sasa ila yeye alitaka ziwepo.

Hizi barabara tunazopiga kelele yeye plan ilikuwa barabara zote zinazoingia na kutoka kwenye majiji zipigwe njia nne kwa 50km.
 
Achana na mabarabara ya tarura naomba uangalie barabara zilizojengwa chini ya miradi ya world bank kama ya sabasaba, miji mwema, mwaloni na mjini kati kama ile ya thaqaafa, nyakahoja, sukuma, na isamilo ni nzuri na zipo standard ata huu mradi wa sasa wa bank ya dunia nadhani zitakuwa bora na zenye viwango🙏🙏🙏
Kwa nini tarura wasiige?
 
Mi naomba hii miradi ya kimkakati ambayo kila siku wanajinasibu nayo kuhusu Mwanza ikamilike haraka (Stand ya Nyegezi, Nyamhongolo,Soko kuu pamoja na Damp la Buhongwa)...
Baada ya hapo tuone watajinasibu na miradi ipi mikubwa Mwanza, mi naamini baada ya miradi hii kukamilika ambayo nafkri hadi kufika mwakani yote itakua imekamilika, wataleta tu miradi mikubwa hawawezi pindua Kwa ukuaji wa Mwanza inawalazimu kuleta miondombinu...
Kuna miradi ya tactic inaanza mwakani so watapiga kelele Humo balaa, barabara kubwa hazimo kwenye tactic.
 
Emirates wanautaka sana huu uwanja Toka enzi za mkapa.

Kitu kingine kinachonipa wasiwasi kwa nini wanachelewesha huu uwanja ni kwamba watu wengi hutoka mikoa ya kanda ya ziwa kuunganisha flight za nje dar,

Kukiwa na flights za kuja mza kutapunguza abiria dar,
Strategically Airport ya mza iko katikati ya miji yote mikubwa ya East africa so ni rahisi kufanya hub.
 
Mimi kwa upande wangu kutanuka kwa mji sio deal tena, Mwanza tayari ni jiji kubwa mpaka limeanza kuingia kwenye Halmashauri nyingine, yaani kutanuka kwa jiji la Mwanza sio kwa kulazimisha kama wanavyofanya Dom. Muhimu waboreshe miundo mbinu yote ndani ya metropole, na ikiwezekana wazuie uendelezaji wa maeneo ya pembezoni.
Na mimi ndio idea yangu.
Kuna maeneo lazima tuyashike for future development.
Mtu mwenye akili angepima viwanja nyamhongolo au sangabuye au popote then kuna viwanja unahifadhi kwamba kuna wakati nhc au kampuni yoyote itataka kujenga apartments viwanja vina kuwepo.
Sio wakija mnawaambia viwanja viko kayenze
 
Hii concept tayari ilikuwepo kabla ya mwaka 2012 . ilemela na nyamagana zilikuw chini ya chombo kimoja .MCC Hadi zilipovunjwa ,Kwa mujibu wa taratibu za ugatuzi wa madaraka Kila wilaya inatakiwa isimamie shughuli zake za maendeleo yenyewe chini ya Chombo chake ..na ndio maana halmashauri ikavunjwa ,hata hvyo bado Kuna mgogoro wa namna ya kuita nyamagana.either iwe manispaa au ibakj na kuwa jiji la mwanza.....
Cha muhimu hapa nashauri kuwepo na miradi ya ubia kati ya halmashauri mbili ili kutengeneza win to win situation.otherwise migogoro katika miradi ya maendeleo haiwezi kuisha hapa Tanzania
Hii mambo ya halmashauri kujikusanyia mapato ndo shida ilipo.
Kwangu mimi nafikiri serikali kuu iwe inakusanya mapato then halmashauri zinapendekeza miradi kama tactic ilivyo zinazokidhi zinapewa mpunga.
 
Yes
IMG20221012183047.jpg
 
Back
Top Bottom