Mwandishi APIGWA risasi na Polisi

Mwandishi APIGWA risasi na Polisi

hivi police wana ninio na waandishi wa habari? sasa hv imekuwa ni mchezo......ni kama wanatafutwa sana ili kuuawa. risasi ya kifiani maana yake walitaka kumwua huyu. inauma sana.
 
Jamani tumekuwa kwenye maandamano ya mwangosi mda si mrefu,hivi hawa polisi vipi,wanafikiri hii nchi ya familia zao.naamini mtalipwa kutokana na kazi yenu 2015 is not far,mtu mmoja risasi za nini?pole sana kamanda na hawa ndege wa chichidodo
 
Lilikua likipambana na polisi....... tukalishinda! kamanda wa kinondoni atasema wananchi sio watiifu ndio maana matukio ya raia kupigwa risasi yameongezeka.
 
:kev:Aroooooooooooh......JESI RA PORISI.... bado tunaenderea kuraani kwa nguvu setu sote ......matumizi ya nguvu pasipo sababu yanayofanywa na JESI RETU LA PORISI ..... ...Bira shaka kuna chanzo chake mutatuarifu kwa kirefu tunaenderea tunasubiri......:llama: :help:
 
:llama: :kev:.....Aroooooooooh Jesi Ra Porisi ............... Tunaenderea kuraani kwa nguvu zetu zote .... matumizi ya nguvu yanayofanywa na Jesi ra Porisi..... Get well soon Shaban :llama: :llama: :llama:
 
abdull kazi Hebu wahini mahakamani haraka (marafiki/ndugu zake) Huu ugaidi wa wazi unafuata mtu nyumbani kumchanganya na jambazi.
Iko siku polisi watashindwa kuzuia nguvu ya UMMA tutakapochoka!! Polisi ni majambazi period!! Narudia iko siku risasi hazitatosha kuzuia nguvu itakayowasagasaga msiwepo tena!! Wapo wengi wanauawa kwa kuchanganywa ukianzia na kina General Kombe!!
 
Last edited by a moderator:
EMT Ukisoma vizuri, kuna mama Jay wawili. Mama Jay (Mama Juma) ambaye ndiye mke wa Shabani na mama Jay (mama Juma) ambaye ndiye polisi wanadai walikua wanamtafuta ambaye kuna mwizi alikimbilia kwake, lakini baada ya tukio la risasi, issue ya mama Jay ikawa tena haina maana, mambo yalishaharibika na hata kama kweli mwizi alikimbilia huko baada ya risasi kulia, hawezi tena kuwapo eneo hilo, na ndio maana polisi hawakua tena na shida na mama Jay waliyekua wanaenda kwake.

Still tunaweza kuwa na uhakika gani kuwa polisi walielekezwa kwa Mama Jay (aliyekuwa anatafutwa na polisi) na siyo kwa Mama Jay (mke wa Shaban).

Siungi mkono kitendo cha polisi, lakini haya majina yanaleta contradictions.Heri hata tungeambiwa majina yao kamili kuepuka mgongano wa aina yoyote.
 
Ni safari wameanza. Ngoja niwaambie ukweli kidigo kuhusu hawa Polisi, Fuatilia historia zao za maendeleo ya darasani wakiwa shuleni kwa wale waliopata kusoma japo mpaka form four tu. Ni wale ambao walikuwa hawawezi kupata swali kwa mara ya kwanza mpaka masahihisho. Au la, lazima waibie kwa mjuaji mmoja. sasa leo wako wao kwa wao wataibia wapi kama si mwendo wa makosa tu? Ukweli huu haufutiki kirahisi, ni historia imeshaandikwa.


Acha uongo huo wa mchana tena bila aibu. Polisi ni ndugu zenu tunawajua na bado wapo wengi tu wenye taaluma zao nzito na wameenda shule. Pale wanapopotoka tuseme ukweli kwamba wamepotoka, lakini pale ambapo mtu hana data asitake kuaminisha umma kama huyu salosalo anavyotaka kutuaminisha. Kumpiga mtu risasa si kitu kizuri waliohusika wachukuliwe hatua
 
Wanasema kirahisi kuwa walikuwa wanasaka majambazi, walitonywa kuna majambazi wakavamia nyumba ya Mwandishi eti katika kusukumana ndio bastola ikafyatuka risasi ikampata Mwandishi, polisi hawasemi majambazi yapo wapi waliyokuwa wanayasaka, hawakupita kwa mwenyekiti wa mtaa, walivamia nyumbani kwa mwandishi. wanasema Mwandishi alijilinda kwa panga akamjeruhi Askari, hawaonyeshi Askari huyo yuko wapi? amejeruhiwa vipi? Jamani Maswali kibao mimi nimechoshwa na Ujinga wa Polisi na Ujambazi wanaofanya.
Huu ni zaidi ya ujinga
 
Nadhani hakuna jeshi katili na la majuha kama Jeshi la Polisi la Bongo. Wao kuua na kudandia lift kwenye magari ya watu. Uzuri ni kwamba wakistaafu wanasota kweli kweli hasa wale waliozoea vya dezo. Badilikeni nyie ndata.
 
Hapa kikosi cha lnterejinsia kinapaswa kulaumiwa hakikunusa vizuri mhalifu
 
Acha uongo huo wa mchana tena bila aibu. Polisi ni ndugu zenu tunawajua na bado wapo wengi tu wenye taaluma zao nzito na wameenda shule. Pale wanapopotoka tuseme ukweli kwamba wamepotoka, lakini pale ambapo mtu hana data asitake kuaminisha umma kama huyu salosalo anavyotaka kutuaminisha. Kumpiga mtu risasa si kitu kizuri waliohusika wachukuliwe hatua
Hakuna anayekataa kuwa polisi si ndugu zetu,labda tu unataka kubisha, lakini ukweli ni kuwa asilimia kubwa ya wanaoenda polisi na uwalimu ni wale wa div 1v au 111 ya mwisho,hata mitaani uwa kauli za namna hii hazikosekani 'ina maana mwanao amekosa hata ualimu au upolisi?',jaribu kufuatilia kauli hizo pindi matokeo ya mitihani ya form 4 au 6 yanapokuwa yametoka na selection imeshafanyika,kama wewe ni miongoni mwa wale wanaokandamiza keki ya taifa wenyewe sitashangaa kama hujui hili.
 
Wanasema kirahisi kuwa walikuwa wanasaka majambazi, walitonywa kuna majambazi wakavamia nyumba ya Mwandishi eti katika kusukumana ndio bastola ikafyatuka risasi ikampata Mwandishi, polisi hawasemi majambazi yapo wapi waliyokuwa wanayasaka, hawakupita kwa mwenyekiti wa mtaa, walivamia nyumbani kwa mwandishi. wanasema Mwandishi alijilinda kwa panga akamjeruhi Askari, hawaonyeshi Askari huyo yuko wapi? amejeruhiwa vipi? Jamani Maswali kibao mimi nimechoshwa na Ujinga wa Polisi na Ujambazi wanaofanya.

Unafikiri sisi(wananchi)kama tungekuwa tunajitambua tungekuwa tunapewa majibu ya kipumbavu (kama haya) na vyombo vinavyopaswa kutuhakikishia ulinzi wetu ?
 
Back
Top Bottom