I got a question for you guys,
Katika mazingira yetu ya kibongo bongo bado hakikubaliki sana kwa mwanaume kuingia jikoni na kupika, haswa na wanaume wengine. Akifanya hivyo basi ataitwa majina kibao na yatasemwa mengi juu yake mf.mume bwége,kakaliwa, kalishwa limbwata, sio mwanaume kamili n.k.
Sasa swali langu ni kama hayo hapo juu yanamhusu mwanaume ambae anaishi na mwanamke , vipi yule asieishi na mwanamke(mpenzi/mke)?Pengine anaweza akawa anaishi na ndugu, dada wa kazi au hata mwenyewe.Huyu tumwite nani? Maana kama kukaliwa kakaliwa na nani?Limbwata kapewa na nani?Ubwége kavishwa na nani?Uanaume kavuliwa na nani?
Nadhani ni muda sasa tuanze kukubali wanayofanya wengine na kuwaacha wajihukumu wenyewe.Kama wewe hutaki/huwezi hamna haja ya kumwita anaefanya majina ya ajabu.Baki tu ukishangaa!!
Lizzy, hivi kazi ya mwanamke na mwanaume ndani ya nyumba ni nini?
Mi ninachojuwa kazi ambayo mwanamme hawezi kuifanya na ni katika vitu vya asili ni kuzaa na kutumia manyonyo yake kunyonyesha mtoto... Lakini kazi zote za nyumbani sioni tabu mwanaume akizifanya...!
Sasa ikitokea mwanamke ndiye mwenye kazi na mume kwa bahati hana kazi kwa sababu hizi na zile, na hapo nyumbani kuna Mtoto/watoto, je baba hata weza kuwapikia, kuwabadilisha nepi, kufua nguo za mtoto na kuwakogesha.
Je ikitokea nyote wawili mnafanyakazi mrudipo kazini hamuwezi kusaidiana, mmoja anakata vitunguu, mwingine anatayarisha iki na kile, na mkapika mkala na watoto na hata mfanyakazi na ndugu wengine wanao kaa nayi wakala na kufurahia maisha.
Mimi biafsi nilikuwa nikiwapikia dada zangu wakubwa chakula na wakirudi kutoka shuleni wanakuta hapo ugali wa nguvu na mchuzi wa kukata na shoka, baba na ama wakirudi kazini wanakuta wali wa nazi na samaki wa chukuchuku tayari nishaandaa, na sikuwahi hata siku moja kuwasikia wazazi wangu wakisema kuwa hii si katika kazi za kiume, kiufupi ni utaratibu tu wa kila familia na mambo yake hakuna cha ajabu hapo. Ila walikuwa wakilalamika tu kuwa nikitumia vyombo vingi na kazi ya kuosha ilikuwa ikiwakabiri wao.
Hii kitu huwa inashangaza sana, kazi za kupika na kufua au hata kuonsha vyombo zikiwa zinafanyika nyumbani zinakuwa ni za mwanamke, ila zikiwa ni za kuajiriwa kama vile kwenye mahoteli na kazi za udobi basi zinageuka ni za kiume na majina yanabadirika, na kuitwa kwa kiinglishi, utasikia maneno kama chef, laundryman (huyu ni dobi) n.k.
Kwa uoni wangu mimi kazi za nyumbani ni kujipanga tu wewe na mwenza wako, haijarishi nani na nani wanaishi nanyi hapo nyumbani, kama baba na mama wamehamua kijipangia wenyewe jinsi ya kuishi basi ni nani mwingine wa kuwaingilia... Kama wakikubaliana kuwa baba ndiye hawe mwajiriwa (mtafutaji) na mama habaki nyumbani kutunza mali ya familia na watoto, hayo ni maamuzi yao, la wakiona kuwa kuna haja ya wote wawili kutafuta kazi za kuajiriwa na nyumba kumwachia mfanyakazi wa nyumba ili kutunza watoto na mambo mengine ya afya na usafi wa nyumba na kuangalia watoto ni juu yao.
Hao wengine watakao sema kuwa fulani kalishwa limbwata au kafanyaiwa ulozi hizo ni fikra zao, na wakati mwingine ni kuona gere tu kuwa wao hawafanyiwi hayo... Wakati mwingine ndoa hazina fomula mahalum vile wenyewe mnavyotaka kuishi ndio hivyo hivyo, japokuwa wengi tumeathirika na mila, desturi pamoja na imani za kdini zetu...!
Labda niseme tu kuwa mila zingine hazioni kuwa ni destiuri nzuri kwa mwanaume aliyeoa na wakati mwingine hata yule amabye ajaoa na bado anaishi kwa wazazi wake, kuingia jikoni na kupika, kuosha vyombo, kufagia au hata kumbadirisha mtoto nepi, lakini kama wenyewe wanaona kuwa ilo ni sawa kwa mwanaume kutoyafanya hayo, basi hakuna wa kuwalazimisha, lakini wakiona kuwa kusaidiana kwenye kazi za nyumbani ni wajibu wa kila mmoja basi ni nani tena wa kunyanyua mdomo na kuanza kuwasema kuwa wamelishana limbwata...!?
Basi kama kweli kuna limbwata la kutufanya sisi wanaume wote tuweze kuwasaidia wake zetu kazi za nyumbani, mimi binafsi ningependa ilo Limbwata liwekwe kwenye maji ya bomba ya kunywa, kwenye chupa za maji yanayouzwa madukani na mabarabarani, kwenye visima na ikiwezekana hata kwenye bear na pombe kali ili kila mwanaume haweze kunywa na apate kumsaidia mke wake kazi za nyumbani.... Au wewe unaonaje, si itakuwa raha ndani ya nyumba!?
Tena tangazo lake la biashara utalisikia "
...Kunywa maji safi ya kunywa yenye limbwata katika formula mpya kabisa.... Chupa moja limbwata mwezi mzimaaa...." Ah ah ah ah.