Mwanaume hawezi kukupenda kama anavyompenda mke wake, never ever!

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,883
Anaandika Robert Heriel.

Haijalishi atakuambia nini, haijalishi atakupa nini. Mwanaume hawezi kukupenda Kama anavyompenda mkewe.
Hilo wala sio siri, wanaume wote duniani tupo hivyo.

Asije akakudanganya mtu kuwa ati anakupenda kuliko mkewe huo ni uongo na amekuona hamnazo kichwa maji.

Ndio maana wanawake wote wenye akili ndoa kwao ni moja ya kipimo kikubwa cha upendo kwa mwanaume.

Elewa kuwa mpaka mwanaume anakuacha wewe anaoa mwanamke mwingine mbele ya macho yako jua hakupendi.

Hii ni tofauti na wanawake, mwanamke anaweza kuolewa na mwanaume asiyempenda. Lakini kwa mwanaume hilo haliwezekaniki na kama litawezekanika labda kwa masharti ya mganga.

Ukitaka ujue kuwa hupendwi zaidi ya mkewe, ukitaka kuhatarisha ndoa ya mwanaume yeyote hapo ndipo utaonja joto ya jiwe. Na ndio mwanzo wa kupigwa chini.

Ili mwanaume akujali sana kuliko anavyomjali mkewe basi itampasa mkewe awe hafanyi wajibu wake kama mke, awe na kisirani, hajui mahaba, hajui kutumia mdomo wake vizuri, hana manjonjo n.k. Lakini kama anatimiza wajibu wake nakuhakikishia atakuweka katika wakati mgumu kupasua ngome yake.

Kamwe usijilinganishe na mke aliyeolewa, hiyo ni dalili haujitambui. Ni sawa na mgeni kutoka nchi za ughaibuni kujilinganisha na raia wa nchi.

Ndio maana wanawake washenzi wanapoingilia ndoa za watu, huenda kwa waganga wa kienyeji au walozi kisha humloga mke ili apandishe kisirani cha ndoa ili asimpe mumewe utulivu. Hilo likifanikiwa basi mwanamke wa nje hupata nafasi ya kujivinjari na mwanaume.

Wengine huwatupia majini ya ugomvi, maradhi, uvivu, uchafu basi ilimradi kudhoofisha ngome.

Pamoja na yote hayo mke ni mke na hawara ni hawara.

Wanawake wengi wanalijua hilo ndio maana hufanya juu chini kuachanisha ndoa za watu alafu wao ndio waingie washike hatamu ndoani ili kujimilikisha Kabisa.

Wanajua mapenzi bila ndoa hayana guarantee. Muda wowote unapigwa chini na hauna haki yoyote.

Wanawake kiasili hawapendi ukiwa naye kwenye mahusiano mfanye Kwa kujifichaficha, wanaona kuwa huo sio upendo.

Ndio maana ukitoka na mwanamke hapo mtaani sio ajabu huyo mwanamke akawa anajipitisha kwa mkeo na kumfanyia visa mpaka ajue kuwa ni mke mwenza.
Wanawake hawawezagi mapenzi ya siri.

Na kamwe mwanamke asije akakuambia kuwa mapenzi yenu yatakuwa ya siri. Hakunaga kitu Kama hicho kwa hawa dada zetu. Siku zote wanaendeshwa na hisia.

Usiku mwema!

Robert Heriel,
Taikon wa fasihi,
Kwa sasa Kibaha.
 
Siyo kweli....

Ukweli ni kwamba wanaume huwa tunatumia ubongo zaidi kuliko moyo..

Wanawake wanafuata mioyo zaidi kuliko bongo zao...

Mwanaume anaweza kuupenda mchepuko mara 100 zaidi ya mke wake, ila kamwe hatokubali huo mchepuko uharibu ndoa yake au ulete sintofahamu yoyote ile kwa mke wake, na heshima kwa mke inabaki palepale..

Wakati huohuo, mwanamke akipagawishwa vizuri huko nje, basi tegemea dharau na viburi vitazidi mara 100 kwa mme wake.

Mwanaume unaweza ukawa umetoka kufanya uzinzi huko nje, na ukija ndani unampa na mkeo vizuri tuu. Ila mwanamke akitoka kupata mechi huko nje akirudi ndani mwanaume hesabu maumivu tuu..
 
Siyo kweli....

Ukweli ni kwamba wanaume huwa tunatumia ubongo zaidi kuliko moyo..

Wanawake wanafuata mioyo zaidi kuliko bongo zao...

Mwanaume anaweza kuupenda mchepuko mara 100 zaidi ya mke wake, ila kamwe hatokubali huo mchepuko uharibu ndoa yake au ulete sintofahamu yoyote ile kwa mke wake, na heshima kwa mke inabaki palepale..

Wakati huohuo, mwanamke akipagawishwa vizuri huko nje, basi tegemea dharau na viburi vitazidi mara 100 kwa mme wake.

Mwanaume unaweza ukawa umetoka kufanya uzinzi huko nje, na ukija ndani unampa na mkeo vizuri tuu. Ila mwanamke akitoka kupata mechi huko nje akirudi ndani mwanaume hesabu maumivu tuu..

Mwanaume kamwe hawezi mpenda mchepuko kuliko mkewe labda Mkewe awe cherema, kisirani au hatimizi wajibu wake kama Mke.

Lazima ujue sababu zinazomfanya mwanaume achepuke
1. Tamaa ya Mwili
Hii ni Kwa wanaume wote

2. Kupata Utulivu.
Hii ni Kwa wale wanaosumbuliwa na Wake zao.

Mwanaume akishampenda Mchepuko automatically ndoa ya Kwanza inakufa automatically.

Ukiona hataki kuvunja ndoa ujue bado anampenda mkewe sema ndio hivyo basi tuu.
 
Kuna mapenzi kabla ya ndoa pia kuna mapenzi baada ya ndoa.. Tatizo wanabadilika!,baada ya ndoa.,wenyewe wanaita kutoa mkosi.
NI NGUMU SANA KUUFAHAMU UKWELI HALISI NDANI YA MWANADAMU MWINGINE.
N.b:-Utakapooa wake wawili au watatu ni rahisi kufahamu yule akupendaye Kwa dhati.
 
Michepuko inatimiza wajibu wa mke ambayo inatakiwa watimize kwenye ndoa. Michepuko inajua nini mwanaume anataka nini anakosa kwa mumewe.
 
Hata mchepuko ukimuweka ndani kisa anakutimizia Yale apaswayo mke kutimiza akishakuzoea tu nae atakufanya utafute mchepuko mwingine. Wanawake utimiza wajibu wao kabla ya kuolewa, wakishaolewa ujisahau.
 
Unakuta mwanamke KILA kitu anamwachia dada wa Kazi kuanzia usafi chumbani,kufua nguo, kupika nk mke yeye nae kawa boss anatuma tu. Sasa umeoa mke au umeoa dada wa kazi. Dada wa Kazi anakufanyia KILA kitu isipokuwa ngono tu.
 
Unakuta mwanamke KILA kitu anamwachia dada wa Kazi kuanzia usafi chumbani,kufua nguo, kupika nk mke yeye nae kawa boss anatuma tu.
SAsa umeoa mke au umeoa dada wa kazi. Dada wa Kazi anakufanyia KILA kitu isipokuwa ngono tu.
Hii inaitwa Cash out kwa sisi wa wazee wa kubeti hapo kma unaowa mdada wa kazi tu
 
Wengine tunaoa mke mmoja Kwasababu Dini imetubana lakini sio kweli kuwa hakuna wanawake wengine wanaopendwa.
 
Anaandika Robert Heriel.

Haijalishi atakuambia nini, haijalishi atakupa nini. Mwanaume hawezi kukupenda Kama anavyompenda mkewe.
Hilo wala sio siri, wanaume wote duniani tupo hivyo.

Asije akakudanganya mtu kuwa ati anakupenda kuliko mkewe huo ni uongo na amekuona hamnazo kichwa maji.

Ndio maana wanawake wote wenye akili ndoa kwao ni moja ya kipimo kikubwa cha upendo kwa mwanaume.

Elewa kuwa mpaka mwanaume anakuacha wewe anaoa mwanamke mwingine mbele ya macho yako jua hakupendi.

Hii ni tofauti na wanawake, mwanamke anaweza kuolewa na mwanaume asiyempenda. Lakini kwa mwanaume hilo haliwezekaniki na kama litawezekanika labda kwa masharti ya mganga.

Ukitaka ujue kuwa hupendwi zaidi ya mkewe, ukitaka kuhatarisha ndoa ya mwanaume yeyote hapo ndipo utaonja joto ya jiwe. Na ndio mwanzo wa kupigwa chini.

Ili mwanaume akujali sana kuliko anavyomjali mkewe basi itampasa mkewe awe hafanyi wajibu wake kama mke, awe na kisirani, hajui mahaba, hajui kutumia mdomo wake vizuri, hana manjonjo n.k. Lakini kama anatimiza wajibu wake nakuhakikishia atakuweka katika wakati mgumu kupasua ngome yake.

Kamwe usijilinganishe na mke aliyeolewa, hiyo ni dalili haujitambui. Ni sawa na mgeni kutoka nchi za ughaibuni kujilinganisha na raia wa nchi.

Ndio maana wanawake washenzi wanapoingilia ndoa za watu, huenda kwa waganga wa kienyeji au walozi kisha humloga mke ili apandishe kisirani cha ndoa ili asimpe mumewe utulivu. Hilo likifanikiwa basi mwanamke wa nje hupata nafasi ya kujivinjari na mwanaume.

Wengine huwatupia majini ya ugomvi, maradhi, uvivu, uchafu basi ilimradi kudhoofisha ngome.

Pamoja na yote hayo mke ni mke na hawara ni hawara.

Wanawake wengi wanalijua hilo ndio maana hufanya juu chini kuachanisha ndoa za watu alafu wao ndio waingie washike hatamu ndoani ili kujimilikisha Kabisa.

Wanajua mapenzi bila ndoa hayana guarantee. Muda wowote unapigwa chini na hauna haki yoyote.

Wanawake kiasili hawapendi ukiwa naye kwenye mahusiano mfanye Kwa kujifichaficha, wanaona kuwa huo sio upendo.

Ndio maana ukitoka na mwanamke hapo mtaani sio ajabu huyo mwanamke akawa anajipitisha kwa mkeo na kumfanyia visa mpaka ajue kuwa ni mke mwenza.
Wanawake hawawezagi mapenzi ya siri.

Na kamwe mwanamke asije akakuambia kuwa mapenzi yenu yatakuwa ya siri. Hakunaga kitu Kama hicho kwa hawa dada zetu. Siku zote wanaendeshwa na hisia.

Usiku mwema!

Robert Heriel,
Taikon wa fasihi,
Kwa sasa Kibaha.
Robert umechanganya sana umeconclude halafu ukatoa exceptions na hio exception kuwa wapo wanawake wanaolewa na waume wasiowapenda basi vivyo hivyo wapo waume hupenda mcheluko kuliko mke wake, huo upekee upo na unaishi, mwanamke asiekupenda anakuwa mkosi kwenye maisha, Sasa wengine michepuko ndio imetupa riziki zetu na tunachanua kisa tu nyota Kali ya mchepuko.

Siku zote tukumbuke kuwa kuna exception katika kila jambo
 
Back
Top Bottom