Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,892
MWANAMKE KUPATA MIMBA PASIPO RIDHAA YA MWANAUME LIWE KOSA LA JINAI.
Anaandika, Robert Heriel
Sisi kama wanaume tumekubali kabisa kuwa Kufanya ngono na Mwanamke Chini ya miaka 18 hiyo itahesabika kama Kosa la JINAI, Kwa jina la Ubakaji, bila kujali hiyo Binti alifanya Kwa ridhaa yake au Kwa kulazimishwa. Tumekubali.
Pia kesi ya ubakaji inaweza kuwa hata Kwa Mwanamke mwenye zaidi ya miaka 18 ikiwa tuu hakukuwa na makubaliano ya ridhaa Kwa Mwanamke. Na adhabu yake sio mchezo, ni Mvua ya miaka 30, yes miaka thelasini. Sawasawa! Tumekubali.
Sisi kama wanaume tunafanya Mapenzi Kwa sababu kuu ambayo ni Starehe Kwa 99%, kufurahisha Nafsi na mioyo yetu. Hiyo asilimia 1% iliyobaki ndio inahusu mambo ya Kupata Watoto ikigawana na kutafuta heshima Kwa wanaume wasio na Pesa.
Wakati wenzetu Wanawake, Dada zetu, Mama zetu hufanya mapenzi Kwa sababu nyingi Sana ikiwemo
I)Kuturidhisha Sisi wakitaka kupendwa, 25%
ii) Kupata Fedha na mambo ya kiuchumi 50%
iii) Kustarehe, 24%
iv) Kupata Watoto. 1%
Wanawake lazima waelewe Sisi tunapowatongoza tupo kwaajili ya Jambo moja kuu nalo ni Starehe tuu. Yaani ukiona mwanaume amekutongoza au anakukodolea macho basi elewa hapo anachotaka ni Starehe tuu. Tena akiwa ameoa ndio kabisa.
Serikali lazima itutendee Haki wanaume, Kustarehe sio kosa kisheria, na kisheria hakuna kosa la Kustarehe na Wanawake ikiwa tuu sio Wake za Watu, au Watoto Chini ya miaka 18.
Haiwezekani unakutana na Mwanamke kwaajil ya Kustarehe alafu anakuletea mambo ya Mimba, huo ni uhuni. Ushenzi na sio uungwana.
Serikali iweke sheria kuwa Mwanamke kubeba mimba ya mwanaume pasipo ridhaa ya mwanaume ni kosa la jinai, na adhabu itungwe. Huo ni uhuni.
Najua kuna Watu wataniona hamnazo au nimechanganyikiwa, au ninatabia za kishenzi lakini Kwa upande wangu nipo Mbele ya Muda. Ninazingatia Haki za Pande mbili, yaani Mwanamke na Mwanaume.
Mwanamke kwenye Hii Dunia ana-control mambo makuu mawili natural, ambayo ni Sex na reproduction. Mwanamke ndiye anatawala tendo la Ndoa pamoja na ishu ya Uzazi. Hayo mambo mawili.
Ni jukumu la Mwanamke kudhibiti suala la mimba. Na ikiwa anataka kubeba mimba ni lazima aongee na Mwanaume wakubaliane. Huo ndio uungwana, hiyo ndio HAKI.
Sheria Hii ya Mwanamke kubeba mimba pasipo ridhaa ya mwanaume italeta tija ndani ya jamii yetu. Kama ifuatavyo;
1. Itapunguza migogoro ya kijinga ambayo haina maana.
2. Itawafanya Wanawake wasikubali kubeba mimba bila ya Ndoa au pasipo kuandikishana(makubaliano maalumu) iwemo sahihi ya Mwanaume, ikiwa Mwanamke hajaolewa.
3. Itapunguza single mother ambao wengine Kwa Makusudi hujibebesha mimba Kwa maamuzi Yao wajitegemea liwalo na liwe, au wakidhani watapata huruma au mapenzi ya wanaume.
Kuzaa Watoto hakuna uhusiano wowote na kuongeza hisia za mwanaume kama hakupendi. Acha niseme ukweli WA moja Kwa moja.
4. Itapunguza Wanawake wanaoingilia ndoa za Watu na kujibebesha mimba na kuharibu ndoa za Watu. ATI kisingizio mwenye kosa ni Mwanaume Kwa sababu alimfata. Ni Kweli mwanaume alikufata lakini alifuata Starehe lakini sio Watoto. Zingatia makubaliano yenu, Kabla hujalala na Mwanaume muulize swali ikitokea Umepata mimba nini kitatokea, uone atakujibu vipi, majibu hayo muandikishe aweke sahihi. Uone kama hataghairi.
5. Itapunguza Watoto kuzaliwa bila ya Ndoa, makubaliano.
Ndoa ndio sehemu pekee mtoto anazaliwa Kwa ridhaa. Ukishaolewa jua tayari umesaini makubaliano ya kuzaa Watoto.
Lakini kama haujaolewa hiyo sio kazi yako. Kazi yako ni Starehe na unatakiwa kulipwa.
Haiwezekani umetoka zako kwenye Starehe na Mwanamke na lengo likiwa ni Starehe alafu mtu akuletee vitu visivyoeleweka.
Serikali hasa watunga sheria wajue kuwa ni ukiukwaji wa Haki za binadamu hasa Kwa wanaume kumbebea mimba pasipo ridhaa yake. Ni jinai ambayo haijawekwa kwenye sheria. Iwekwe.
Ooh! Wakati unafanya hukujua mimba inaweza kutokea? Wanaouliza maswali haya sijui wanatumia Akili ipi, ni uhuni, Utapeli na unyanyasaji Kwa wanaume. Kumpa kazi isiyomhusu.
Kama lengo ni kuwapendelea Wanawake Kwa kubinya Haki za Wanaume ni Sawa, lakini hiyo kamwe haiwezi kuwa Haki.
Unakuta kijana wa Watu Hana Mpango WA kuwa na Watoto lakini hiyo haimaanishi hapaswi kufanya ngono/mapenzi. Mapenzi yapo sio kwaajili ya Uzazi tuu Bali pia ni Starehe.
Wataalamu washeria na mnaopenda Haki liangalieni Jambo hili, mlifanyie kazi.
Nimemaliza! Mnaochukia mchukie, wenye matusi mtukane. Ila Sio HAKI kubeba mimba ya mwanaume pasipo ridhaa yake. Huo ni ukatili wa kijinsia.
Nawatakia Sabato NJEMA.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel
Sisi kama wanaume tumekubali kabisa kuwa Kufanya ngono na Mwanamke Chini ya miaka 18 hiyo itahesabika kama Kosa la JINAI, Kwa jina la Ubakaji, bila kujali hiyo Binti alifanya Kwa ridhaa yake au Kwa kulazimishwa. Tumekubali.
Pia kesi ya ubakaji inaweza kuwa hata Kwa Mwanamke mwenye zaidi ya miaka 18 ikiwa tuu hakukuwa na makubaliano ya ridhaa Kwa Mwanamke. Na adhabu yake sio mchezo, ni Mvua ya miaka 30, yes miaka thelasini. Sawasawa! Tumekubali.
Sisi kama wanaume tunafanya Mapenzi Kwa sababu kuu ambayo ni Starehe Kwa 99%, kufurahisha Nafsi na mioyo yetu. Hiyo asilimia 1% iliyobaki ndio inahusu mambo ya Kupata Watoto ikigawana na kutafuta heshima Kwa wanaume wasio na Pesa.
Wakati wenzetu Wanawake, Dada zetu, Mama zetu hufanya mapenzi Kwa sababu nyingi Sana ikiwemo
I)Kuturidhisha Sisi wakitaka kupendwa, 25%
ii) Kupata Fedha na mambo ya kiuchumi 50%
iii) Kustarehe, 24%
iv) Kupata Watoto. 1%
Wanawake lazima waelewe Sisi tunapowatongoza tupo kwaajili ya Jambo moja kuu nalo ni Starehe tuu. Yaani ukiona mwanaume amekutongoza au anakukodolea macho basi elewa hapo anachotaka ni Starehe tuu. Tena akiwa ameoa ndio kabisa.
Serikali lazima itutendee Haki wanaume, Kustarehe sio kosa kisheria, na kisheria hakuna kosa la Kustarehe na Wanawake ikiwa tuu sio Wake za Watu, au Watoto Chini ya miaka 18.
Haiwezekani unakutana na Mwanamke kwaajil ya Kustarehe alafu anakuletea mambo ya Mimba, huo ni uhuni. Ushenzi na sio uungwana.
Serikali iweke sheria kuwa Mwanamke kubeba mimba ya mwanaume pasipo ridhaa ya mwanaume ni kosa la jinai, na adhabu itungwe. Huo ni uhuni.
Najua kuna Watu wataniona hamnazo au nimechanganyikiwa, au ninatabia za kishenzi lakini Kwa upande wangu nipo Mbele ya Muda. Ninazingatia Haki za Pande mbili, yaani Mwanamke na Mwanaume.
Mwanamke kwenye Hii Dunia ana-control mambo makuu mawili natural, ambayo ni Sex na reproduction. Mwanamke ndiye anatawala tendo la Ndoa pamoja na ishu ya Uzazi. Hayo mambo mawili.
Ni jukumu la Mwanamke kudhibiti suala la mimba. Na ikiwa anataka kubeba mimba ni lazima aongee na Mwanaume wakubaliane. Huo ndio uungwana, hiyo ndio HAKI.
Sheria Hii ya Mwanamke kubeba mimba pasipo ridhaa ya mwanaume italeta tija ndani ya jamii yetu. Kama ifuatavyo;
1. Itapunguza migogoro ya kijinga ambayo haina maana.
2. Itawafanya Wanawake wasikubali kubeba mimba bila ya Ndoa au pasipo kuandikishana(makubaliano maalumu) iwemo sahihi ya Mwanaume, ikiwa Mwanamke hajaolewa.
3. Itapunguza single mother ambao wengine Kwa Makusudi hujibebesha mimba Kwa maamuzi Yao wajitegemea liwalo na liwe, au wakidhani watapata huruma au mapenzi ya wanaume.
Kuzaa Watoto hakuna uhusiano wowote na kuongeza hisia za mwanaume kama hakupendi. Acha niseme ukweli WA moja Kwa moja.
4. Itapunguza Wanawake wanaoingilia ndoa za Watu na kujibebesha mimba na kuharibu ndoa za Watu. ATI kisingizio mwenye kosa ni Mwanaume Kwa sababu alimfata. Ni Kweli mwanaume alikufata lakini alifuata Starehe lakini sio Watoto. Zingatia makubaliano yenu, Kabla hujalala na Mwanaume muulize swali ikitokea Umepata mimba nini kitatokea, uone atakujibu vipi, majibu hayo muandikishe aweke sahihi. Uone kama hataghairi.
5. Itapunguza Watoto kuzaliwa bila ya Ndoa, makubaliano.
Ndoa ndio sehemu pekee mtoto anazaliwa Kwa ridhaa. Ukishaolewa jua tayari umesaini makubaliano ya kuzaa Watoto.
Lakini kama haujaolewa hiyo sio kazi yako. Kazi yako ni Starehe na unatakiwa kulipwa.
Haiwezekani umetoka zako kwenye Starehe na Mwanamke na lengo likiwa ni Starehe alafu mtu akuletee vitu visivyoeleweka.
Serikali hasa watunga sheria wajue kuwa ni ukiukwaji wa Haki za binadamu hasa Kwa wanaume kumbebea mimba pasipo ridhaa yake. Ni jinai ambayo haijawekwa kwenye sheria. Iwekwe.
Ooh! Wakati unafanya hukujua mimba inaweza kutokea? Wanaouliza maswali haya sijui wanatumia Akili ipi, ni uhuni, Utapeli na unyanyasaji Kwa wanaume. Kumpa kazi isiyomhusu.
Kama lengo ni kuwapendelea Wanawake Kwa kubinya Haki za Wanaume ni Sawa, lakini hiyo kamwe haiwezi kuwa Haki.
Unakuta kijana wa Watu Hana Mpango WA kuwa na Watoto lakini hiyo haimaanishi hapaswi kufanya ngono/mapenzi. Mapenzi yapo sio kwaajili ya Uzazi tuu Bali pia ni Starehe.
Wataalamu washeria na mnaopenda Haki liangalieni Jambo hili, mlifanyie kazi.
Nimemaliza! Mnaochukia mchukie, wenye matusi mtukane. Ila Sio HAKI kubeba mimba ya mwanaume pasipo ridhaa yake. Huo ni ukatili wa kijinsia.
Nawatakia Sabato NJEMA.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam