MwanaJF gani unapenda topics na comments zake?

MwanaJF gani unapenda topics na comments zake?

Nawakubali wote wenye hoja za kujenga na panapostahili kukosoa wanakosoa sio bendera kufuata upepo. Bora liende tu kisa hoja ametoa fulani hao siwafagiliii.

Big up to my Bro Mr Rocky, asakuta same, ngalikihinja. Thumb up to Heaven on earth, Evelyn Salt, Charming Lady....
 
Mbona mimi hakuna alienitaja? Au mchango wangu hauonekani?

mambo ya kujuana tu mkuu yametawala hapo wala usipate hasira! watu wametaja mademu zao,wanachama wenzao,maclassmates wao,madada zao,wafanyakazi wenzao,etc. so take it easy!
 
hahaaa kama ni mwelewa he will surely understand this

Aaargh kama mtu huoni sababu ya kuwa kundi fulani unachapa lapa tu sio unahoji as if kazi ya seremala kapewa mpishi!!!!!!!!

Huku ni stress free "Jf" haswa uzi kama huu sasa mtu analeta habari ya seminar room kuwa hii theory sio ya Rostow ni A.G.Frank ya nini yote haya!!!!

Kuna thread ya uwepo wa Mungu aende kule kuna theology,philosophy na empiricism akaweke michango huko,watu wanajadili katiba sijamuona kule,wanauliza kama orgasm kwa mwanamke ni real experience yake sijaona!!!!!!
 
Interaction makes meaning to those who interacts and they can change those attached meanings as they keep interacting!!!!!!

Failure to attach meaning is an indicator that you are not among them...suit youself! !!!!!!!!

Sijaelewa!
 
Mmh ukingojea kutajwa hapa inaweza kula kwako mimi nampenda sans Mshana Jr. Raha jipe mwenyewe
 
Kwa idadi ya Likes nilizopata na zile quotations mlizonipa japokuwa si nyingi sana ila zinaonyesha ni kwa kiasi gani nakubalika na jamii hasa ukizingatia wengi hatufahamiani kwa sura.
Nawapenda wote,tumepeana changamoto na kurekebishana...
Wote napenda comments zao,kuna wale wenye comments za kuchekesha wananifanya siku yangu iende poa.
Wale wenye comments zenye uzito zaidi,najifunza kutoka kwao.

"Nlikuwepo":bolt:
 
nyumbakubwa-huyu anaongea kama mwanamke kamili aliyekamilika,wanaume wote wangependa kuwa na mke wa mtizamo wake,
gezaulole-anavyowakimbiza wakenya na majivuno yao utampenda,
nyani ngabu na kiranga-hawa ni mabingwa wa kusimamia misimamo yao,hawatikisiki ktk kutetea hoja zao na wanachokiamini,
kaunga na ashadii-wadada wenye staha,wana busara za kweli na hakika,kuna wakati natamani ningekuwa nafahamiana nao in the real world sio ki-jf,
asprin-anapenda sana kukagua vibinti vinapoingia jf,siku hizi ananichekesha sana na mikwara yake ya kubadili dini,hata hapa anaweza kuja na kusema nisingemtaja angebadili dini!lol,
the boss-huyu jamaa yeye ni mfalme wa kuongea maneno ambayo wanawake wanapenda kusikia,huyu jamaa ktk dunia ya kweli atakuwa hataree sana kwa wadada,
nzi-shabiki nguli wa man utd,watu wote watakimbia uzi wa man utd yeye atabaki pale daima
emt-jamaa ukisoma hoja zake utafikiri unasoma kitabu cha kitaaluma,nakukubali sana bro
mzizimkavu-amejaa maarifa mengimengi ya kila aina kila pande

aisee, Kiranga na Nyani Ngabu wana misimamo balaa , mpaka natamani siku moja niwaone laive hawa watu hawatikisiki kabisa hata uwatingishe vipi! Kuna mwingine Pasco ,hata umkasirishe vipi ndo kwanza ata like post yako..Nawa admire sana hawa watu
 
Last edited by a moderator:
Naona MMU na Chit-Chat wanapeana mashavu tu.

teh teh teh
Ritz hujatajwa sababu wewe unapenda ku - attack watu binafsi badala ya kujadili hoja japo una ufahamu mkubwa wa mambo
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom