KERO Mwanajeshi mstaafu afunga barabara ya mtaa akidai ni kiwanja chake

KERO Mwanajeshi mstaafu afunga barabara ya mtaa akidai ni kiwanja chake

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,922
Reaction score
6,531
Mzee huyu ameongeza mawe na kuyamwaga barabarani kwa madai kwamba barabara imepita kwenye kiwanj.jpg
Mzee huyu ameongeza mawe na kuyamwaga barabarani kwa madai kwamba barabara imepita kwenye kiwanja chake.

Cha kushangaza ni kwamba mbele kuna nafasi ambayo inaonekana ndiyo mpaka wa kiwanja chake, lakini sasa anaziba barabara kabisa. Swali linajiuliza, kama kweli hiyo ndiyo mipaka ya kiwanja chake, ile nafasi ya mbele aliacha kwa matumizi gani?

Kitendo hiki cha kumwaga mawe kimezuia shughuli za wananchi na matumizi ya barabara hii muhimu. Ni vyema mamlaka husika zifike eneo hilo, zihakiki mipaka halali ya kiwanja na kuchukua hatua stahiki ili barabara irejeshwe katika hali yake na wananchi waendelee kuitumia bila usumbufu.

 
Huwezi kujua haiwezekani akurupuke tu, ukweli utakuwepo
Sio kweli haiingii akilini huyo mzee atakuwa amevurugwa tu maana ukiicheki hiyo ni barabara kubwa na ukiangalia imetokea mbali haijapita kwenye usawa wa nyumba yake peke yake ni mtaa wote.
Ingekuwa ni njia ndogo ya uchochoroni hapo sawa ningemtetea.
Na kama si hivyo basi viongozi wa mtaa na wananchi itakuwa walikubaliana kila mtu atoe hatua kadhaa kwa ajili ya kuchangia eneo la barabara huwa inafanyika pia.
 
... hiyo barabara ifungwe, ibakie chocho ya watembea kwa miguu! ... Hii ni kama malalamiko yake yana kaukweli!
NB: Hapo mbele ya kibao kuna barabara inakatiza, na mbele tena kidogo baada ya hizo fremu kuna barabara ingine tena inakatiza, ... kwahiyo unaweza kupatikana ufumbuzi, BUSARA IKITUMIKA!
 
View attachment 3645904Mzee huyu ameongeza mawe na kuyamwaga barabarani kwa madai kwamba barabara imepita kwenye kiwanja chake.

Cha kushangaza ni kwamba mbele kuna nafasi ambayo inaonekana ndiyo mpaka wa kiwanja chake, lakini sasa anaziba barabara kabisa. Swali linajiuliza, kama kweli hiyo ndiyo mipaka ya kiwanja chake, ile nafasi ya mbele aliacha kwa matumizi gani?

Kitendo hiki cha kumwaga mawe kimezuia shughuli za wananchi na matumizi ya barabara hii muhimu. Ni vyema mamlaka husika zifike eneo hilo, zihakiki mipaka halali ya kiwanja na kuchukua hatua stahiki ili barabara irejeshwe katika hali yake na wananchi waendelee kuitumia bila usumbufu.

View attachment 3645903
Asije akasema "unanijua mimi ni nani?"
 
Huwezi kujua haiwezekani akurupuke tu, ukweli utakuwepo
Kuna kitu kinaitwa mipango miji ukiitizama hiyo picha mbele kule kuna watu zaidi ya mmoja wanahitaji barabara so kisheria hapo atake asitake lazima atoe barabara.

Ingekuwa ni mtu mmoja tu anahitaji hiyo njia angeweza kufanya hivyo ila hapo wahitaji ni wengi ni vile tu hawa watu wakishakuwa kwenye mamlaka wanajiona wapo juu ya sheria zote
 
Mpaka barabara ya mtaa inatengenezwa kwenye hicho kiwanja chake alikuwa wapi? Ana hati miliki ya ya Wizara ya hicho kiwanja, na inayo onesha hakuna barabara mpaka alete hiyo jeuri?
 
Kuna mwingine huku kwetu alikua kanal, yeye amefunga kwa maadai anairekebisha, sasa watu inabidi wazunguke km kama 6 kupisha hiko kipande alicho funga.
 
... baadhi ya wastaafu wa jeshi wamekuwa na kero ya kuanzisha uvamizi wa maeneo ya kambi za jeshi, hasa pale wanapostaafia. Matokeo ni kukuta kambi za jeshi zilizokuwa zimetengwa vizuri na makazi ya raia kuwa CHANGANYIKENI!
TUSISAHAU MBAGALA NA GONGOLAMBOTO!
 
Inawezekana wakati hiyo barabara inachongwa ilimega eneo la huyo mwanajeshi na hakulipwa fidia. Hiyo barabara ni ya mtaa ndio lakini kulikuwa na shamba la mtu hapo, hivyo kama Serikali ya mtaa ilitwaa ardhi yake bila kumlipa fidia ni haki yake kuziba barabara.
 
Ujuaji wa kijinga na selfishness, mtu wa aina hiyo akipata tatizo lolote la kijamii ni kumuangalia tu ateseke mwenyewe.
 
Back
Top Bottom