KERO Mwanajeshi mstaafu afunga barabara ya mtaa akidai ni kiwanja chake

KERO Mwanajeshi mstaafu afunga barabara ya mtaa akidai ni kiwanja chake

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kuna kitu kinaitwa mipango miji ukiitizama hiyo picha mbele kule kuna watu zaidi ya mmoja wanahitaji barabara so kisheria hapo atake asitake lazima atoe barabara.

Ingekuwa ni mtu mmoja tu anahitaji hiyo njia angeweza kufanya hivyo ila hapo wahitaji ni wengi ni vile tu hawa watu wakishakuwa kwenye mamlaka wanajiona wapo juu ya sheria zote
Hiyo ndio lugha ya kibabe inayotumiwa na wanasiasa na watumishi wa Serikali, sheria mbona iko wazi tu kuwa pale Serikali inapotaka kutwaa ardhi kwa ajili ya maendeleo, inawajibika kumlipa fidia inayolingana na thamani, kwa ukamilufu babu au bibi mwenye eneo lake analopaswa kuliachia... Sio janja janja ya kupima miguu ambayo ndio ulaghai halisi wa Serikali za mitaa.
 
Hii ndio awamu ya hovyo kutokea kuliko kipindi chochote tangu tanganyika tupate uhuru. Watekaji, wauaji na mafisadi wako n mguvu kuliko mamlaka ya juu.
Kazi ni kipimo cha utu
 
Inavyonekana eneo mbele hapo aliacha kwa ajili ya hizo frem...
Sijajua nini kimetokea...
Kaona hakuna biashara au!?
 
Wanasema ni komandoo.kamwambia mwenyekiti akimwondoa atakinukisha nchi nzima inuke.
 
Back
Top Bottom