Mwanafunzi wa Chuo afariki katika mazingira tata!

Mwanafunzi wa Chuo afariki katika mazingira tata!

Dah, poleni wafiwa. But Polisi nao waangalie huo utaratibu wa kutoa fomu zao (PF 3) kwani muda wote huo wa kuhama vituo huenda ungetumiwa na madaktari kumuongezea bint wa watu siku za kuishi!
 
Mtu anasemwa kapewa sumu, badala ya kukimbizwa hospitali awahishwe tiba, anatakiwa apelekwe polisi kwanza apewe PF3, ndio arudishwe hospitali.

What a bunch of bloody bollocks and vogon verses!

Somebody ought to sue whoever instituted this shitty bureaucratic procedure.
 
Watu wa psychology inabidi waanze kuajiriwa vyuoni na shule za sekondari, kwani chanzo chawezekana kikawa ni msongo wa mawazo kilichompelekea kujihusisha na utumiaji wa pombe kwa wingi. Swala la msongo wa mawazo halina tiba zaidi ya counselling au ushauri nasaha. Lala pema peponi dada Neema.

ndugu yangu, tulishafika hadi bungeni na kuonana na waziri mkuu na waziri wa afya kuwakilisha mahitaji ya kuunda idara ya ushauri nasihi (counselling) tukitokea Tumaini University Iringa wakawa wanajiumauma tu na ahadi nyingi hadi sasa hakuna kilichofanyika. Badala yake wanasema waendelee kuwatumia maofisa ustawi wa jamii waliopo wilayani. Sijui hawajui umuhimu wa hawa washauri kuwekwa kila mahali?. Au walitupuuza na kutuona kama wapinzani. Na huenda wanafurahia kuwaongoza watu waliosongwa na shida nyingi ili wawatawale kirahisi. Inakera sana kwa kweli.
R.I.P dada huenda hawakuijua thamani yako kwa uchumi wetu.
 
PF3 inakuwaje na thamani kuliko uhai wa mtu????! Huo ni upumbavu usiohitaji muwekezaji kung'amua...
Nimewahi kupata ajali ambayo pia ilihitajika PF3 kabla sijatibiwa. Pona yqngu ilikuwa tu kwa sababu kati ya walionipeleka hospital unconcious ni afisa kiaina, nikatibiwa na PF3 ndo ikafuata ila kwa mlolongo kama huo nadhani yangenikuta pamoja na ndugu, jaamaa na marafiki zAngu....
Tutumie akili tuokoe uhai wa wenzetu.
 
Hivi kweli ni sawa kabisa mtu kunyimwa tiba, hata alipohitaji huduma za haraka hadi azungushwe kutafuta PF 3? Pengine huyu binti kama angewahi kupatiwa huduma haraka asingekufa. Kuzunguka huko kote na mtu anasumu mwilini, sindiyo inazidi kummaliza? Hiyo PF3 kwa nini ipewe kipaumbele kuliko kuokoa maisha?

Mara nyingi sana hata waliojeruhiwa kiharifu, wamepoteza maisha kwa ucheleweshwaji wa huduma unaoambatishwa na pf 3.

Kama hiyo PF3 ni ya muhimu kuliko maisha ya mhanga, basi utaratibu ufanyike ziwe zinapatikana katika kila hospitali au taarifa ya PF 3 itumwe hata kwa njia ya simu wakati huduma kwa mgonjwa zikiendelea.

Si haki kumzungusha mgonjwa anayehitaji huduma ya haraka kutafuta PF3 ambazo zinategemeana na uwepo wa kituo cha polisi ambavyo si lazima kiwe karibu na hospitalini. Mara nyingine pia hata kule polisi mgonjwa yuko mahututi o lakini anakuta polisi wana vipaumbele vyao ama wako wachache zamuni na hivo kuhatarisha maisha ya raia ambayo yangeokolewa kama si hizo bureaucratic procedures.
 
PF3 inakuwaje na thamani kuliko uhai wa mtu????! Huo ni upumbavu usiohitaji muwekezaji kung'amua...
Nimewahi kupata ajali ambayo pia ilihitajika PF3 kabla sijatibiwa. Pona yqngu ilikuwa tu kwa sababu kati ya walionipeleka hospital unconcious ni afisa kiaina, nikatibiwa na PF3 ndo ikafuata ila kwa mlolongo kama huo nadhani yangenikuta pamoja na ndugu, jaamaa na marafiki zAngu....
Tutumie akili tuokoe uhai wa wenzetu.

Niliwaza hivyo, kama katika kituo cha polisi mwenye funguo za kabati lenye PF3 ameenda kunywa chai basi polisi mmoja aandamane na majeruhi mpaka hospitali na kuwafahamisha madaktari na wauguzi kuwa wanaelewa kinachoendelea PF3 itafuata.
 
Duh! Apumzike kwa amani yake Bwana wetu!
Tumempoteza mpiganagi wa Taifa la kesho!
 
Taarifa ya sababu za kifo chake ikitolewa sidhani kama watajumuisha na huo mlolongo wa kusaka PF3...

Ukitaka kujua nchi za kishenzi, tazama tu mambo yake yanavyoendeshwa kishenzi shenzi tu...

Pia huu ujinga wa kupoteza mawazo kwa kunywa pombe sijui kwa nini watu hupenda sana kuutukuza...
 
Isingekuwa mlolongo wa PF3 labda wangeweza kumuokoa!
Kwa nini wasi control hali ya mgonjwa kwanza?

Very bright you are mkuu. Mlolongo wa pf3 ndio umemuua huyo binti innocent. Kunahitajika bunge kurekebisha sheria au kusaidia kurekebisha utaratibu huu. Yaani mgonjwa anazidiwa watu wanawaza pf3!! This is sh.it.
 
Utaratibu wa kijuha umepelekea kumpoteza mpendwa wetu!
RIP Neema
 
hapo maswala ya pf3 jamani mgonjwa kama anaumwa sana atibiwe kwanza jamani hii nchi hi
lakini pia kuna mtu aliwahi kusema kama una kiasi kikubwa cha pombe ukienda kutibiwa mafactar wanashindwa kukupa ,saada maana kama kidonge ukipewa kinaeza kikakumaliza

by the way she is cute


R.I.P ney...pole baba neema

Ukifuata beurocracy basi mambo kama haya yanatokea na usipo fuata mambo kama ya ESCROW yanatokea. Pf3 ni lazima itolewe ndio mgonjwa atibiwe. La sivyo watatibu na wahalifu. Sema wengi wetu tunasahau kwamba kunakitu inaitwa contigency.

Ingetumika hii basi binti angepona.

R. I. P.
 
Nyie misiba hii sijui tufanyaje jaman... Mungu atulinde
 
Bila shaka pf3 ni moja sababu ya kifo cha binti, shame
 
Back
Top Bottom