Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 970
- 1,942
Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Bishop Bikira iliyopo Kata ya Nyakato Tarafa ya Bugabo Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, amekutwa amefariki dunia, baada ya kujinyonga kwa kutumia shuka.
Akizungumza na Waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Blasius Chatanda amesema kuwa Mwanafunzi huyo, Jovan Revelian Justinian alijinyonga kwa kutumia shuka,aliyoifunga juu ya dali ndani ya bweni,baada ya kuwa na msongo wa mawazo, uliotokana na kubakishwa shuleni.