Mwanafunzi wa Chuo afariki katika mazingira tata!

Mwanafunzi wa Chuo afariki katika mazingira tata!

Ana kaka yake anaitwa Adam Malimbwi ana Albinism ni Mhasibu Wa UNDER THE SAME SUN huyu pia ana msongo mkubwa Wa Mawazo kwani akipokea salary lazima afunge bar mpaka uishe.
 
View attachment 213331

Binti mbichi aliyejulikana kwa jina la Neema Malimbwi (pichani) ambaye alikuwa mwanafunzi wa Chuo cha Kodi Tanzania (ITA) ambacho kipo chini ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kilichopo Mikocheni jijini Dar amefariki dunia kwa madai ya kulishwa sumu kwenye kinywaji.

Marehemu Neema alikuwa binti wa profesa wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro (Sua), Rogers Malimbwi.

Tukio hilo la kusikitisha linatajwa kutokea usiku wa Alhamisi, Desemba 18, mwaka huu wakati Neema anarudi hosteli maeneo ya Kijitonyama, Dar ambapo alikuwa akiishi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, siku ya tukio, Neema alikuwa na marafiki zake wavulana kwa wasichana kwenye onesho la muziki wa B Band inayomilikiwa na Banana Zorro ambapo akiwa huko saa 7 usiku aliendelea kuchati na marafiki zake waliokuwa hosteli akitumia ukurasa wake wa Facebook akiwaambia kuwa alikuwa ‘kiwanja' akiponda raha.

Habari zinadai kuwa, marehemu Neema usiku huo alikuwa akihama maeneo mbalimbali akiwa na vijana ambao baadhi ya marafiki zake wanadai huenda walihusika na kumtilia sumu kwenye bia alizokuwa akinywa.

View attachment 213332

Habari zaidi zinasema kuwa, Neema akiwa na wenzake wakirudi hosteli, njiani alianza kulalamikia kutojisikia vizuri.

"Alikuwa njiani na wenzake wakirudi kulala, akaanza kulalamika kwamba hajisikii sawasawa, ikabidi wenzake wamkimbize Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu wa Kinondoni, Palestina, Sinza, Dar ambako waliambiwa kuwa kutokana na hali yake kuwa mbaya wampeleke kwanza Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini' jijini Dar ili kupata hati ya matibabu (PF3)," kilisema chanzo kimoja.Chanzo hicho kikaendelea kudai kwamba, walipofika Mabatini waliambiwa waende Kituo cha Polisi Oysterbay.

Ikazidi kudaiwa kuwa, Polisi Oysterbay walitoa msaada kwa haraka ambapo sasa ikabidi Neema akimbizwe Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu Kinondoni, Mwananyamala ambako alifariki dunia.

Mwili wa Neema ulihifadhiwa kwenye mochwari ya Mwananyamala kabla ya kusafirishwa juzi kwenda Morogoro kwa mazishi yaliyofanyika jana.

Kumbukumbu zilizopo kwenye makabrasha ya gazeti hili zinaonesha kuwa, Juni Mosi, mwaka jana, mama mzazi wa Neema, Elizabeth Malimbwi alifariki dunia kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar na mwili wake kwenda kuzikwa Morogoro.

Tangu kifo cha mama yake, baadhi ya madenti wenzake wanasema, Neema amekuwa akiishi maisha ya mawazo sana na muda mwingi alikuwa akiutumia kunywa pombe kiasi kwamba, darasani ilikuwa mara chache sana kuhudhuria.

Akizungumza na gazeti hili juzi, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Camillius Wambura alikiri kuwa na taarifa hizo."Ni kweli taarifa za kifo cha mwanafunzi huyo ninazo, mpaka sasa jeshi la polisi linasubiri ripoti kamili ya uchunguzi wa madaktari kuhusiana na kifo chake," alisema Kamanda Wambura.


Chanzo: GlobalPublishers


---Gone too soon, Poleni wafiwa....

Mapendo,
TANMO.
Taarifa ya polisi ni muhimu sana kuliko maisha, badala ta tiba kwanza wanahangaika toka kituo kimoja cha polisi kwenda kingine! Sasa, hiyo taarifa itamsaidiaje huyo binti?
 
Isingekuwa mlolongo wa PF3 labda wangeweza kumuokoa!
Kwa nini wasi control hali ya mgonjwa kwanza?
Huu utaratibu wa PF3 inabidi upitiwe upya,mtu yuko taabani unaulizia PF3 utazani ndo chanjo ya kumponya.
Mtu atibiwe kwanza mengine baadae,sasa mtu anakaa anazunguka kwenye vituo vya polisi mda wote,kufa ni kugusa tu na wengi walishakufa kwa style hizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana kaka yake Adam yupo tulimuozesha mwezi uliopita ila Joshua ndiyo alifariki alizikwa kwao huko Lushoto Vuga

Sent using Jamii Forums mobile app
Acheni Hii familia itulie jamani mwacheni prof malimbwi atulie familiar imeondokewa na mama mzazi Joshua malimbwi na huyo binti yao bado mnataka Kuisimanga plz stop that acheni wapumzike

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mgonjwa hajisikii vizuri Hana jereha kwa mujibu wa mtoa mada .....Nini kilichofanya daktari aombe PF3?
 
R.I.P lakini pia angebaki nyumbani kujisomea na kujiandaa na mitihani au hata kupumzisha akili kwa kupata usingizi mzuri hayo yote yasingetokea.

Watoto hasa wanafunzi mkiwa shuleni mzingatie nini kinachowapeleka huko. Mnawatia simanzi wazazi
 
Hosp wanajua kabisa mgonjwa akizidiwa wanatakiwa kwanza kumwahisha matibabu na sio kumpeleka polisi
Huku ni kukosa busara na weledi. Pf3 ingejazwa wangeileta polis badae wangeokoa maisha yake
 
izo PF 3 kwann zisitolewe maospitalini kuwe na dawati la hao wanaotoa ili mgonjwa apate matibabu kwa uharaka? kuliko kumzungusha zungusha mwisho ni maafa


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu anasemwa kapewa sumu, badala ya kukimbizwa hospitali awahishwe tiba, anatakiwa apelekwe polisi kwanza apewe PF3, ndio arudishwe hospitali.

What a bunch of bloody bollocks and vogon verses!

Somebody ought to sue whoever instituted this shitty bureaucratic procedure.
Kwani watu kama nyie ambao bado nyeupe mnaona ni nyeupe mpo wapi??nlidhani mmeashaisha kumbe mpo...BIG UP .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom