Mwana JF aukwaa uongozi wa watanzania huko Uholanzi

Status
Not open for further replies.
a. Ubalozi/Balozi hashiriki kwa namna yoyote ile si kuwa mlezi, mjumbe n.k awe nje kabisa ya mfumo wa CCM kwani yuko huko kuwakilisha Tanzania na si CCM. Hili binafsi ningependa Ikulu watoe tamko la kuwakataza mabalozi wake kujihusisha na shughuli za chama.

b. Jumuiya za Watanzania zikatae kabisa kuwa sehemu ya vyama vya kisiasa moja kwa moja au kwa implication. Kwa mfano, Kiongozi wa Jumuiya ya Watanzania wote anapokuwa mjumbe wa tawi la Chama chochote cha kisiasa na hivyo kuweza kuleta mgongano wa kimaslahi.

c. Endapo inatokea kuwa wanachama wa chama fulani ndio wengi katika jumuiya zetu basi utaratibu uwekwe wazi na ukubaliwe kabisa kuwa mikutano ya Jumuiya kamwe haitatumika kuzungumzia, kutoa taarifa, kujadili au kwa namna yoyote ile kuyapa nafasi mawazo na hoja za chama hicho hata kama wanajumuiya wote kwa muda huo ni wanachama wa chama hicho.

Vinginevyo, mgongano wa kisiasa utaanza kutokea na kujionesha hasa shughuli za vyama vya kisiasa zitakapoanza kuingiliana na maslahi ya jumuiya nzima ya Watanzania.

Mkuu kale kaibara ka 15 ka chama chetu umekasahau? Au hakatumika ughaibuni?
 
Mkuu kale kaibara ka 15 ka chama chetu umekasahau? Au hakatumika ughaibuni?

Balozi hatakiwi kutekeleza ibara ya 15:1 kwani yeye hakwenda huko kama mwakilishi wa CCM bali mwakilishi wa nchi, ndo maana ni makosa balozi kujiusisha na mambo ya cha kimojawapo anapokuwa ughaibuni hata kama anatetea CHADEMA, TLP au CUF anafanya makosa.
 
Balozi hatakiwi kutekeleza ibara ya 15:1 kwani yeye hakwenda huko kama mwakilishi wa CCM bali mwakilishi wa nchi, ndo maana ni makosa balozi kujiusisha na mambo ya cha kimojawapo anapokuwa ughaibuni hata kama anatetea CHADEMA, TLP au CUF anafanya makosa.

Mkuu ni makosa ya wapi? Anakosea sheria zipi? Kama yeye ni mwanachama wa Sisiem (kitu ambacho mara nyingi ni kweli) hawajibiki kutekeleza ibara ya 15.1? Nini kinamzuia? Kama ni sheria, ni zipi?
 

Mkuu ni makosa ya wapi? Anakosea sheria zipi? Kama yeye ni mwanachama wa Sisiem (kitu ambacho mara nyingi ni kweli) hawajibiki kutekeleza ibara ya 15.1? Nini kinamzuia? Kama ni sheria, ni zipi?

Kwa sheria za tanzania mwajiriwa wa serikalio hatakiwi kujiusisha na siasa sehemu ya kazi, balozi ni mwakilishi wa raisi kwa nchi husika haiwezekani hafanya shuguli za chama wakati anajua yeye anawakilisha watanzania wote, inakuwa ni vigumu kutofautisha muda wa serikali na muda wa chama au resources nyingine za serikali zinaweza kutumiwa kwenye shuguri za chama.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom