TANZIA Mwana JamiiForums mwenzetu Kanungila Karim amefiwa na baba yake mzazi

James Hadley Chase

JF-Expert Member
Mar 25, 2020
1,571
2,652
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania.

Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu mwenzetu, rafiki, Kanungila Karim amefiwa na baba yake mzazi! Msiba upo Morogoro, Kilombero.

Binafsi nachukua nafasi hii kumpa pole sana sana, Mwenyezi MUNGU akawape subra na wepesi katika kipindi hiki kigumu cha majonzi kwa familia yenu.😢😢😢

POLE SANA RAFIKI!

ILIVYOKUWA:
Jana majira ya saa 7 usiku mzee wake alikuwa safarini kwa usafiri wa trekta akitoka nyumbani kwake Kilombero na kuelekea mashambani Mang'ula kwa ajili ya kuvuna mpunga.

Akiwa pamoja na dereva wake yeye(mzee wake) alikuwa amekaa pembeni ya trekta. Trekta ilipofika karibu na daraja la Ruaha Mkuu lilitikisika na kumtupa pembeni mzee wake na kupelekea umaiti.😭😭😭

Huuu ni msiba mkubwa wa pili kwake ndani ya muda wa miaka mitatu(3) tangu ampoteze mama yake kwa presha mwaka 2020.


Dedication🙏🙏
Nionapo amani kama shwari,
Ama nionapo shida;
Kwa mambo yote umenijulisha,
Ni salama rohoni mwangu.
Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

Ingawa Shetani atanitesa,
Nitajipa moyo kwani;
Kristo ameona unyonge wangu,
Amekufa kwa roho yangu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom