Mributz
Senior Member
- Aug 29, 2022
- 112
- 388
Picha: Mamadou Doumbia
TANZIA: Klabu ya Yanga imepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Baba mzazi wa mchezaji wake beki, Mamadou Doumbia, kilichotokea jana, nchini Mali.
Mamadou Doumbia anatarajia kusafiri asubuhi leo kuelekea Mali kwa ajili ya kushiriki taratibu za mazishi.
“Kwa niaba ya Wanachama, Wapenzi na Mashabiki wa Yanga, Uongozi wa Klabu ya Yanga unatoa pole kwa mchezaji wetu Mamadou Doumbia na familia yake yote kwa msiba huu na Mwenyezi Mungu awatie nguvu kwenye kipindi hiki kigumu.” imesema Yanga SC kupitia taarifa yake kwa umma.
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi. Amina.