2019
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 2,982
- 4,458
Bila shaka huyu ni kigogo mzito sana, anajenga frem kwenye hifadhi ya barabara, ndani ya kituo cha mwendokasi Mbagala, kibali amepata wapi? Ilikuja Tanroad ikasimamisha ujenzi na kupiga X jamaa akafuta kwenye x za kijivu ujenzi unaendelea, wakaja tena wakarudia kupiga X bado mafundi wanapaua kwwa kasi. Idadi ya frem ni nyingi sana.
Ni nani huyu ambaye ni mkubwa kuliko serikali?
Mkuu wa mkoa amemshindwa?
Meneja wa Tanroad amemshindwa?
Dar wamemshindwa?
Wizara ya ardhi imemshindwa?
Je Jery Silaa anajua hii?
Nikitazama najisemea hakuna kikubwa duniani kama pesa na madaraka. Utafanya unavyotaka.
Madhara ya ujenzi huu yatakuwa makubwa sana sababu zitabinya upana wa barabara kwa magari na wateja wanaofanya manunuzi, hivyo kuongeza kero nyingine kwa watumiaji.