Mwalimu wangu kasema Magufuli bure kabisa

Mwalimu wangu kasema Magufuli bure kabisa

Hahaha, Kweli Magufuli Bure kabisa! Kwa Vilaza ni ngumu kuelewa maana ya Magufuli ni Bure kabisa
 
Nimekutana na mwalimu wangu, mtu mzee kiasi kwani kanifundisha sekondari. Kasema oho, unaona Magufuli anayofanya?

Nikamuuliza anafanya nini, akanijibu kazuia safari za nje, kakamata wezi bandari, katimua TRA, nk. Nikasema BURE KABISA. Mwalimu akanishangaa, akaniuliza we ya Magufuli huyaoni? Nikasema nayaona, lakini bure kabisa.

Akasema we ulikuwa mwanafunzi mbishi tokea zama zile. Nikamuuliza kwani unafanya kazi gani siku hizi? akasema, bado mwalimu. Nikamuuliza umewahi kumsifia mwanafunzi wako yoyote, achilia mimi niliyekuwa naongoza na bado hukunisifia. Akasema, ningekusifia ungevimba kichwa.

Nikamuuliza, sasa mbona unamsifia Magufuli? Aha, akajibu. Sasa nimekupata mwanafunzi wangu. Magufuli bure kabisa.

Unasemaje na wewe. Maana hadi sasa tumeona pasi na chenga nyiiiingi. Je, kuna goli? Magufuli bure kabisa. Unamuunga mkono mwalimu wangu?


Mwalimu wako alifeli sekondari, nawe akakufelisha. "BURE KABISA HAPO"
 
Kweli vyenga vingi lakini magoli siyaoni?
1.Ajira mpya hakuna
NB:
Hata zile zilizojengwa zimepunguzwa
2.Ushuru bado upo palepale.
NB:
Wameshaanza kukusanya ushuru nyumba kwa nyumba.
3.Nadhani tutangaziwe hazina ina kiasi gani na amefanikiwa kukusanya kiasi gani ndipo tuweze kwenda na kasi pamoja.
4.TULIJUA BAKHARESA ALIKWEPA ALILIPA NINI:
Vipi UDA ALIKWEPA NA AMELIPWA NINI.
ISIWE NI KILINDANA HAPA!!TULIONA YAMEKAMATWA KWA MAELEZO YA KUKWEPAKODI,YAACHIWA BILA MAELEZO.
5.TUNASEMA HIVI UKIMYA WA WENGI UNAJIBU KUBWA LA KUSHANGAZA DUNIA!!!!

Well Said. NYUMBU Hawatakuelewa, Manake Wao Ni Chambo Siku Zote Wakiwa Mbugani.
 
huyu mwalimu wako atakuwa ameshind kukufundisha kwani elimu ya kisomo cha watu wazima alipata ziro kabisa nawe ni bwererere kabisa
 
Ukitaka kujua magamba mengi ni vilaza utaona michango yao kwenye huu uzi,inahitaji uelewa wa hali ya juu kukuelewa mtoa uzi

ndio maana vipaumbele vya el vilikuwa ni eleimu,elimu,elimu
 
mleta uzi thrd za kijinga kama hizi zinatakiwa zipelekwe fb na sio hapa...hapa si mahala pake
 
Back
Top Bottom