Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Hivi kumbe kumwambia baba yako "MWONGO" ni tusi? nimeamini usanii ni kazi mbaya kumbe, unahitaji limbwata kuwa msanii makini. Siku moja Mwalimu Nyerere alipokuwa analitangazia Taifa habari za vita dhidi ya Nduli Iddi Amini aliwaahidi watanzania kwamba atalitangazia Taifa kila kitu kinachoendelea wakati wa vita hivyo. Haikuchukuwa muda Amini alipowatandika baadhi ya vijana wetu akiwemo mpwa wake Nyerere mwenye kuongoza ndege ya kivita, watu tukasubiri mwalimu atasema nini. Waandishi wa habari walivyo wachokozi walimuuliza siku nyingine mbona wanasikia hivi na vile naye hawaelezi wananchi kila kitu kama alivyoahidi? Alicheka kwanza halafu akajibu, "Sio rahisi kueleza kila kitu hasa katika mazingira kama ya vita....ukiumizwa ukalalamika unampa turufu adui yako, kwa hiyo unatakiwa kuchambua nini useme kweli na nini usiseme kweli...."

Sasa kama hapo utamsemaje baba yako, hakukuongopea katika ahadi yake? Tusi sio tusi tena kama utaliangalia mazingira yake ambamo limetolewa. Hata mambo ya chumbani saa nyingine huitwa matusi, sasa ni matusi kweli? Kwamba baba na mama wanatukanana kila siku chumbani na walifunga ndoa ili watukanane kila mara ili watoto wapatikane?

Mtu mwingine atakuambia, "Unapendeza kama huna akili nzuri dah!" Je, utampeleka mahakamani kwamba amekutusi? Au utajidhalilisha mwenyewe kujionyesha kwamba wewe ni mshamba kutotumia akili ya kawaida kupambanua sifa na matusi? "Huyu kijana chizi sana yaani, amewajengea ghorofa wazazi wake hadi nammaidi kinoma..." Jamani kuna namna nyingi za kuelezea kitu ilimkuvuta akili za wanaokusikiliza wakuelewe haraka kwa kutumia lugha ya kawaida. Hata wakati mwingine Nyerere aliwatukana wanaomsikiliza nao wakapiga makofi kumshangilia, baadaye wakagundua kumbe walikuwa wanatukanwa. Mwalimu Nyerere kwa wakati wake alikuwa na akili za ushawishi sana na ilimchukuwa mtu kuwa mchambuzi makini ili kuelewa sawasawa anachokiongelea, ndio maana kina Kambona ilibidi wakae kando maana walishatambua mapema anachokimaanisha na kisha wakampinga waziwazi, lakini yeye hakutaka apingwe moja kwa moja pasipo kutumiaa mbinu ya ushawishi hasa kwa wasaidizi wake, alitaka watu makini lakini wanaotambua kwamba yeye ni boss.

Mbona mwingine aliwaambia watanzania wana akili za kijinga na ufinyu wa kufikiri na wivu wa kike na mkabaki kunung'unikia mvunguni hadi leo? Mbona JK anatukanwa hadharani naye anacheka tu ila wapambe wake wanaojishauwa kwake ndo wanayafanya makubwa wakati yeye anayetukanwa ana-enjoy? Nampenda JK kwa style yake ya kupuuzia mambo yasiyo na tija anayorushiwa hata ya nguoni, ambayo angekuwa mtu mwingine ingekuwa patashika. Acha uhuru wa kujieleza aliouasisi JK uendelee kujitanua ili mradi hadhuriki mtu. Watu wengine wanataka kutufanya watanzania wote ni punguani katika kutafakari mambo ila wao tu wanataka kututafsiria. Acha tujichambulie mambo kwa kadiri tunavyoweza, wala msiturubuni kama CCM wanavyotaka Katiba ya chama chao ndoyo iwe katiba ya nchi hata kwa kumwaga damu wakiweza. Mwizi hapendi kuibiwa, akigundua unamwibia atataka kukuua.

Hao wanaosema Tundu Lisu kamtukana Mwalimu ndio wenyewe wanaomtukana kila siku kwa kuyapiga chini yale aliyoyapigania hadi kifo chake, sasa kwa kuwa Lisu ni Mpinzani wao wanaitumia nafasi hiyo kumgeuzia kibao Lisu wanayemwona anawazidi kete, ili waonekane wenyewe wanamjali sana Mwalimu kuliko kina Lisu na kuwafunika wanaoitaka Tanganyika. Mbona mliliua Azimio la Arusha hata kabla hajafa, tena mkalinyonga akiwa anaona nanyi mkimkodolea mimacho kuona atafanya nini? Hivi hamjui kwamba mlimchefua sana Mwalimu kiasi kwamba huenda mlichangia kuiharibu afya yake kwa msongo wa mawazo mlipokanyaga kila kitu kizuri alichokipigania na kuchukuwa kila alichokipiga vita? Nani anamuenzi zaidi Mwalimu ninyi wanafiki na wale wanaosema kweli waionayo?

Nene mvifile hilo! Swela Mwagito.
 
Petro E. Mselewa kujua matusi ni mpaka mama yako akuambie kuwa wewe baba yako ni aliyekuwa mchunga ng'ombe wenu.
 
ukweli nyerere walikuwa muongo na mnafiki, amedhulumu sana, sasa mkiambiwa mnaona katukanwa, mbona wengine mnawatukana kwa kukashifu .....?

Hayo maneno hebu kamwambie baba au mama yako hata kama yana ukweli, kisha tuletee mrejesho juu ya reaction yao.
 
95% ya Wabunge sasa Wanaishi Dsm,wanaenda kupora Ubunge huko majimboni kisha wanahamia kuishi Dsm,hawataki kuishi majimboni kwao wameng'ang'ania kuishi Dsm,kila kiongozi hata akiwa Mkuu wa mkoa,wilaya nk wengi ni wakazi wa Dsm , mda mwingi wanautumia wakiwa Dsm,Maendeleo yamechelewa kwa Sababu watu wanabanana Dsm na kusahau majukumu Yao ,huu Ulimbukeni wa kupenda kuishi Dsm Ndio umepelekea Zoezi la Serikali kuhamia Dodoma Kuwa gumu sana, matokeo yake Dsm sasa imekumbwa na kubanana na foleni zisizokwisha kisa Serikali Wamegoma kuhamia Dodoma , Nyerere aliona mbali sana alijua ipo siku Dsm itakuwa Majanga kwa kufurika watu na magari, kutokutekeleza Mazuri ya Nyerere Pia ni Matusi kwake.
 
Matusi aliyo tukana TL ni kusema ukweli.Ukweli ni matusi makubwa sana kwa CCM kuzidi hata yale ambayo kada wa CCM Salmin wakati alipokuwa rais wa Zanzibar alisha wahi kuyasema tena kipindi hicho baba wataifa alikuwa hai.Salimin alisema kuwa WEE MZEE UMESHAZEEKA KACHUKUWE JEMBE NENDA KULIMA USIJARIBU KUTIKISA KIBERIT KILICHO JAA NJITI.
 
Kitendo cha Serikali kugoma kuhamia Dodoma na kulinusulu jiji la Dar na foleni ni Tusi namba moja kwa Nyerere .
 
Hao serikali mbili wameshindwa hoja ya kwa nini kusiwe na na serikali tatu,wana tapa tapa.Serikali tatu..Period........
 
UWONGO WA NYERERE, kama nakumbuka vizuri tLisu alitoa nukuu moja ya gazeti la Observer la Uingereza Nyerere alipokuwa akihojiwa kuhusu Wazanzibar na muungano (mtanisahihisha baada ya kurejea maneno ya Lisu kwenye You Tube), Nyerere alisema kama Wazanzibar wakiamua kuwa hawataki muungano HATOWAPIGA MABOMU. But UWONGO wake ni kuwa mwaka 1984 Aboud Jumbe alipohoji kuhusu muundo wa muungano aliwekwa kizuizini Mjimwema mpaka leo. HUO SIYO UWONGO WA NYERERE?
 
Tusi kubwa alilotukana Lissu, ni kuuliza uhalali wa kumuweka kizuizini Mzee Jumbe kule Mjimwema.
Naungana na wewe, huyu mzee alijiuzulu nyazifa zake wakati wengi wetu tukiwa mashuleni, hatukujua ni nini hasa kilimpata hadi kufikia uamuzi huo, ala kumbe kosa lake kubwa ilikuwa kuhoji uhalali & mfumo wa muungano huu huu unaojadiliwa ndani ya Bunge la katiba!!

Ni kweli kosa la Lissu ni kutoboa zile zinazoitwa SIRI za nchi - hili ndilo kosa lake na si eti kamtusi baba wa taifa.
 
Hao serikali mbili wameshindwa hoja ya kwa nini kusiwe na na serikali tatu,wana tapa tapa.Serikali tatu..Period........
Ni vigumu mno kuutetea hoja isiyo na haki ili ipate haki stahiki na ikubalike. ni kweli ni kazi ngumu mno ndiyo maana mara wanahamia kwenye matumizi, ulinzi na jeshi, vita nk
 
Siko tayari kutukana, ila jua kua maneno aliyoyasema hakustahili kuyasema dhidi ya Nyerere.

Ni maneno gani ambayo hakustaili kusema? Tiririka nayo tujuwe? Acha ushabiki wa kisiasa.
 
Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.

Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.

Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?
......Lissu aliwahi kuzungumzia issue za majaji walioteuliwa na JK......ukisoma kw amakini utaona uchambuzi wake ulikuwa una walakini fulani.......washabiki wa siasa wakabaki kushangilia!!........nakubaliana na wewe kuwa ni muhimu tuwe makini na maneno yatolewayo na watu mbali mbali..........

Moja ya jambo ambalo limeijengea Sifa sana JF ni kutokana na baadhi ya wanachama wake kuwa na uchambuzi mahiri........Umaarufu wa JF....Ni utamaduni wa kuchambua.......siku hizi kumetokea wanasiasa wengi wanataka kuivuruga JF yetu hapa....i.e. hapa pumba zinawekwa mchana kweupe na mchele vivyo hivyo.....

Mkuu Ogah, tunaomba utoe jibu la swali la aliyeanzisha uzi. Vinginevyo utakuwa unaendeleza uzushi kama hutaweka hizo kauli za Lissu mnazodai ni mbovu.
Ndipo tunapokosa direction kama taifa iwapo sifa ya kisiasa ni kumwaga matusi tu.

Hayo matusi ni yepi?
Maneno ni upanga wenye ncha mbili zinayokata pande zote. Maneno yako yanaweza kukufanya uwe na hatia na vile vile yanaweza kukuondoa kwenye tuhuma za hatia. Yote inategemea na jinsi unavyotumia maneno yako.

Sidhani kama Lisu alitumia maneno yake vizuri, na ndiyo maana nimekuwa na wasiwasi na uhakika wa maneno yote aliyowahi kutuambia kuhusu Zitto na Kitila huko nyuma.

Mkuu Kichuguu, mbona hutaji hizo kauli? Tunawashukuru kwa kutukumbusha ya Zitto, Kilita, Majaji n.k. Ila unaendelea kuharibu badala ya kusaidia kwa kushindwa kuandika hizo kauli. Kama huwezi kufanya hivyo ni bora ukakaa kimya.
 
Kama nyerere kakosea,yap inawezekana. Sasa yasipowekwa wazi hayo makosa ,tutajirekebisha Vipi ili yasirudiwe. Mara nyingi ukweli unauma.
 
Nyerere alikuwa muongo kweli na Lissu kabainisha hilo.
 
Siko tayari kutukana, ila jua kua maneno aliyoyasema hakustahili kuyasema dhidi ya Nyerere.

Mkuu aliongea reality hakutukana, aliongeliea amri ya raisi ambayo tume ya nyalali iliona ni amri kandamizi! that is reality sio matusi! au wewe unaona ni matusi kusema mtu aitumia sheria kandamizi?? ilikuwepo na ilitungwa na wakoloni na ni sheria kandamizi msimuonee lissu bule!
 
Kwa akili zenu, na u CDM wenu bado mnaona kabisa Lissu alikuwa sahihi kutumia lugha zile na kumwita Mwalimu Nyerere mwongo! Kwa hiyo unataka kuwaambia watanzania kuwa mwasisi wenu wa CDM ni bongo lala kwa kuwa Lissu hakutoa tusi lolote? Kweli CDM sasa siasa zimewashinda!

Litaje.
 
Back
Top Bottom