Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Siko tayari kutukana, ila jua kua maneno aliyoyasema hakustahili kuyasema dhidi ya Nyerere.

ndugu bado upo zama zile za zidumu fikra za mwenyekiti!.kwa maelezo yako unaonekana mshabiki kama wale wasio na hoja kwenye bunge la katiba,wamebaki tu kusema mara ooh tumeoana sababu ya serikali mbili na muungano,nimezaa huku ilhal mimi ni wa upande ule,swali hakuna wazungu,waarabu,wachina nk waliooa au kuolewa hapa?,au nao nchi zao zimeungana na tz?.hebu jitafakari achana na siasa nyepesi.
 
Ndipo tunapokosa direction kama taifa iwapo sifa ya kisiasa ni kumwaga matusi tu.

Nyerere aliandika kitabu "tujisahihishe"
kwa mintaarafu wali/alikosea, tunapoyataja makosa yake hatumdhalilishi, wala hatujamtukana.

ikiwa unadhani Nyerere ametukanwa basi nakujulisha kuanzia sasa ujue Nyerere amejitukanisha.

Nyerere ametudanganya kuhusu UJAMAA NA KUJITEGEMEA.
Nyerere ametudanganya kuhusu AZIMIO LA ARUSHA.
 
kweli nimeamini watu wanafuata upepo ila sio uhalisia wa hoja, basi mpelekeni mahakamani kama alimtukana nyerere
 
Kwa akili zenu, na u CDM wenu bado mnaona kabisa Lissu alikuwa sahihi kutumia lugha zile na kumwita Mwalimu Nyerere mwongo! Kwa hiyo unataka kuwaambia watanzania kuwa mwasisi wenu wa CDM ni bongo lala kwa kuwa Lissu hakutoa tusi lolote? Kweli CDM sasa siasa zimewashinda!

Thibitisha pasipo shaka hapa jukwaani, ni kweli kwamba ktk maisha ya uongozi wa mwalimu hakuwahi kusema uongo?
 
Na wewe una matatizo ya kujua maana na matumizi ya meneno; umetafuta majina badala ya maneno. Nitakusaidia kwa kuanza hivi: " Maneno ni upanga wenye ncha mbili zinazokata pande zote. Maneno yako yanaweza kukufanya uwe na hatia na vile vile yanaweza kukuondoa kwenye tuhuma za hatia. Yote inategemea na jinsi unavyotumia maneno yako."

Halafu nitakurahishia hivi:

MANENO yote yaliyowahi kutoka mdomoni mwa Lissu yanatakiwa yaangaliwa kwa makini, mfano yakiwa yale maneno yake dhidi ya Zitto na Kitila.

kwa upande mwingine kumbe tafsiri ya msikilizaji inaweza kufanya hayo maneno kuwa matusi ama la,sasa basi ili kumuaminisha mwingine aamini unachoamini ni kumshawishi kwa hoja na mifano au nukuu toka ktk hayo maneno,tukirudi kwa lissu ninyi mnaoamini kuwa ametukana tunaomba nukuu ya yale unayoamin kuwa ni matusi ili tukikubaliana nanyi tuungane ktk kumkemea bwana lissu,lakini kinyume na hayo tutaendelea kuamini kuwa hizo ni siasa za majitaka ambazo hazina nafasi leo.
 
Siko tayari kutukana, ila jua kua maneno aliyoyasema hakustahili kuyasema dhidi ya Nyerere.

We naona hujailewa mada hebu ongelea ni maneno gani yaliyotolewa na tundu kumtukana nyerere na sio kubakia tu ati kamtukana..
 
Kwa akili zenu, na u CDM wenu bado mnaona kabisa Lissu alikuwa sahihi kutumia lugha zile na kumwita Mwalimu Nyerere mwongo! Kwa hiyo unataka kuwaambia watanzania kuwa mwasisi wenu wa CDM ni bongo lala kwa kuwa Lissu hakutoa tusi lolote? Kweli CDM sasa siasa zimewashinda!

Acha kwenda nje ya mada hebu ongelea maneno ya matusi yaliyotolewa na tundu na kwani nyerere hawezi kuwa mwongo au unadhani yale yote yaliyotolewa naye yalikuwa ya kweli.???
 
kama maneno gani kwa mfano hayakumstahili Baba wa Taifa na yalimstahili nani?
 
kwa mada hii,wanapropaganda wameshikwa pabaya.tajeni sasa.msikariri kama kasuku
 
Matusi ni maneno ya kawaida. Yanakuwa matusi tu pale yanapotumika kudhalilisha (discredit) watu wengine, vinginveyo siyo matusi. Nimeuliza iwapo muuliza swali ana threshold yoyote inayotofuatisha matusi na maneno mengine, hajanijibu ila wewe umeingia kumsaidia. Msioona matusi katika maneno ya Lissu ina maana kuwa hamuoni udhalilishaji katika maneno yake, na inakuwa ni vigumu kuwaridhisha. Nyie wanasheria nadhani mnajua sheria za Defamation of Character ambazo kwa lugha rahisi ni sheria dhidi ya kutukana. Ni mnajua ni mambo gani yanayotumika kutukana na ni yapi; na vile vile mnajua kuwa kuna hata sheria dhidi ya kutukana mtu aliyekiwsha fariki?

Je ulimsikia Lisu kwa masikio yako?nirudi kwenye hoja yako, defamation unayosema ni Sawa. Lkn with evidence kwamba aliwahi kusema uongo bado mtu huyo atakuwa convicted?
Watu wengi tunaongozwa na mapenzi ya kumpenda Nyerere, hata mimi ni namkubali sana , lkn siamini hata kidogo kwamba hakuwahi kusema uongo,
 
Kwa akili zenu, na u CDM wenu bado mnaona kabisa Lissu alikuwa sahihi kutumia lugha zile na kumwita Mwalimu Nyerere mwongo! Kwa hiyo unataka kuwaambia watanzania kuwa mwasisi wenu wa CDM ni bongo lala kwa kuwa Lissu hakutoa tusi lolote? Kweli CDM sasa siasa zimewashinda!

Kwani MWONGO ni tusi???
 
......Lissu aliwahi kuzungumzia issue za majaji walioteuliwa na JK......ukisoma kw amakini utaona uchambuzi wake ulikuwa una walakini fulani.......washabiki wa siasa wakabaki kushangilia!!........nakubaliana na wewe kuwa ni muhimu tuwe makini na maneno yatolewayo na watu mbali mbali..........

Moja ya jambo ambalo limeijengea Sifa sana JF ni kutokana na baadhi ya wanachama wake kuwa na uchambuzi mahiri........Umaarufu wa JF....Ni utamaduni wa kuchambua.......siku hizi kumetokea wanasiasa wengi wanataka kuivuruga JF yetu hapa....i.e. hapa pumba zinawekwa mchana kweupe na mchele vivyo hivyo.....

TUNDU LISSU namfananisha na "tanganyika jeki"
sifa kuu ya hii jeki ni kuwa hunyanyua gari pamoja na mzigo wake.

JK alinyanyuliwa pamoja na mizigo ya majaji wake.
Nyerere kanyanyuliwa na mizigo ya uongo wake.

Jk aliteua baadhi ya majaji ambao hawakuwa na sifa za uteuzi ndio maana kuna baadhi ilibidi wajiunge open university kuchukua LLB ili wakidhi matakwa ya sheria waliyokwisha ikiuka. "tanganyika jeki imewanyanyua"

Huyu Nyerere sasa kanyanyuliwa juu zaidi muuone uongo wake, kwa kuthibitisha uongo wake jiulize,
uko wapi ujamaa na kujitegemea!!!!!
Liko wapi azimio la arusha!!!!!!

muungano nao magumashi.

Msipanick huu ni ukweli hamkuujua kabla.
 
Mi nasema mtu yeyote akikosea atakosolewa na akifanya vizuri atasifiwa na kwa mujibu wa imani yangu ni Mungu tu hakosolewi kwa sababu yeye ni PERFECT. Kutotaka Nyerere akosolewe ni kujidai eti alikuwa PERFECT katika maamuzi yote aliyofanya. Hii si Kweli lazima tubadilike tumweke binadamu yoyote kwenye mizani bila kujali umaarufu wala hekima ya kibinadamu aliyo nayo. tukijidai eti kumkosoa nyerere ni Dhambi inayostahili adhabu kubwa tutakuwa tumefisha uhuru wa fikra na hivyo kujifungia kwenye blanket la umbumbumbu wa hali ya juu. Nyerere was not God na hatakaa awe Mungu kwani kuna aliyofanya mazuri na kuna aliyokosea kama binadamu. Tumemsifia miaka yote kwa mazuri aliyofanya na kama alikosea basi anastahili kukosolewa. inakuwaje kukosoa mawazo na matendo ya nyerere eti ni MATUSI ;huu ni unafiki mkubwa wa kuzima mawazo chipukizi yenye mtazamo wa mawazo huru

Kama hakuwa mungu ni lazma akosolewe kwan nyerere jaman aliumbwa tofauti na binadamu wengne shida yote ya muungano tunaipata ni kwasababu waasisi wa muungano hawakuwa wazi
 
Hoja hapo ni kutaja hayo matusi kwani ccm mumezoea uzushi mpaka sasa muko makanisani kueneza kwamba serikali tatu jeshi litapindua nch basi bola tupinduliwe na jeshi kuliko kutawaliwa na ccm
 
Namkubali sana Nyerere, lakini hiyo haitamaanisha kuwa pale alipokosea iwe dhambi kumkosoa! Naungana na mtoa mada: kama tumeshindwa kutaja makosa ya Tundu Lissu, kama tumeshindwa kuyataja matusi aliyo tukana, basi tukae kimya. Nilichokiona mimi ni mtu kukosolewa alipokosea na mkosoaji alikuwa sahihi!

Anayetaka kueleweka aje na hoja yenye ushahidi kwamba aliyosema Lissu siyo kweli na hayakusemwa na Mwalimu, hayakufanywa na mwalimu na hayakuandikwa na mwalimu!

Napenda kusisitiza, ni katika jamii ya wendawazimu na wasanii wa kisiasa tu, ambapo watu watajidai kupenda kujali na kumtetea marehemu, huku tukishindwa kuwaheshimu wazee wetu walio hai kama kina Mzee Warioba, kina Mzee Aboud Jumbe na wengineo. Halafu tusubiri mpaka nao wafe ili tujidai tunawaheshimu. Tuache unafiki!
Umenena mkuu, lakini umemsahau pia Lyatonga Augustine Mrema mzee wa Kiraracha ambaye aliimarisha usafi wa jiji la DSM na kuleta vivuli vya miti na pavements katikati ya jiji kwa amri ya siku 7, ingawa fadhila za JK zimemfanya aonekane kutikiswa siku hizi kimsimamo na kuegemea lolote la ccm hata bila kuchuja kama zamani. mnyonge myongeni lakini haki yake mpeni. Kaifanyia nji hii mambo mengi sana mazuri ambayo hapaswi kusubiri afe ndo tumsifu.
 
Mimi ninafikiri waliomtukana Nyerere tusi kubwa ni wale walioua AZIMIO lake la ARUSHA na kuweka AZIMIO la Zanzibar badala yake. Hawa mahayawani wanatetea maslahi yao na familia zao. Walijua Azimio la Arusha lilikuwa linawabana kwa hivyo hawakuona haja ya kuwepo mjadala wa kitaifa kuhusu hilo. Lakini kwa vile wanajua Muungano wa serikali mbili ni lulu kwao kuendeleza usultani mamboleo basi ndo unaona wanahahaha kila kuchapo kutafuta vihoja mshenzi kulinda status quo. Washenzi sana hawa.
Haya Matusi kwa Nyerere hamuyaoni?muungano sasa umevurugwa Zanzibar imekuwa Nchi bila lidhaa ya Watanganyika, hili ni Tusi kubwa kwa Nyerere kwani Muungano aliotuachia ulikuwa ni kuelekea Kuwa na Serikali moja na Kuwa Taifa moja,Matusi yapo mengi sana ,huu Ufisadi ,rasilimali kutoroshewa nje ya Nchi,Uwekezaji wa kimagashi,Tamaduni zetu na Maadili kuporomoka kwa kasi Haya ni matusi kwa Nyerere , Siku hizi imekuwa ni Kawaida Vijana kuvaa Nguo chini ya makalio imekuwa kawaida hata wanawake wanavaa nguo za utata Hakuna wa kuthubutu kuwakemea , haya ni matusi makubwa kuliko hayo ya Lisu.
 
Nyerere Kama binadamu wengine alikuwa na Mapungufu yake japo si mengi sana kuliko Mazuri aliyofanya,tuendelee kumpongeza kwa Mazuri yake Pia isiwe dhambi kuyakosoa Mabaya kisha kumsamehe na kumwacha apumzike kwa Amani.
 
Back
Top Bottom