Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

......Lissu aliwahi kuzungumzia issue za majaji walioteuliwa na JK......ukisoma kw amakini utaona uchambuzi wake ulikuwa una walakini fulani.......washabiki wa siasa wakabaki kushangilia!!........nakubaliana na wewe kuwa ni muhimu tuwe makini na maneno yatolewayo na watu mbali mbali..........

Moja ya jambo ambalo limeijengea Sifa sana JF ni kutokana na baadhi ya wanachama wake kuwa na uchambuzi mahiri........Umaarufu wa JF....Ni utamaduni wa kuchambua.......siku hizi kumetokea wanasiasa wengi wanataka kuivuruga JF yetu hapa....i.e. hapa pumba zinawekwa mchana kweupe na mchele vivyo hivyo.....

Lissu hakuwa anaiwakilisha JF bali alikuwa anawakilisha maoni wa Wachache katika kamati yake kwa hiyo waliyoyaleta hapa JF ndio wanatakiwa watuletee uchambuzi wa kina ni katika maneno yapi au maandishi yepi yanayoonyesha LISSU amemtukana Nyerere (R.I.P) tofauti na hayo mtakuwa bado mnaimba ngonjera na hamjajibu kinachotakiwa kujibiwa na mleta mada.
 
Kwa akili zenu, na u CDM wenu bado mnaona kabisa Lissu alikuwa sahihi kutumia lugha zile na kumwita Mwalimu Nyerere mwongo! Kwa hiyo unataka kuwaambia watanzania kuwa mwasisi wenu wa CDM ni bongo lala kwa kuwa Lissu hakutoa tusi lolote? Kweli CDM sasa siasa zimewashinda!

Kwa hiyo kama alidanganya asiitwe mwongo kisa.
 
Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.

Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.

Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?

Inaonekana ni tusi kwa sababu Mh. Tundu Lissu ameongea udhaifu wa Baba wa Taifa hadharani. Maana yake ni kwamba Baba wa Taifa hata angefanya nini haruhusiwi kukosolewa. Hii ni imani ya watu wengi haswa wenye heshima za unafiki. Na ni dhambi kubwa kwa Mwenyezi Mungu kuwa mnafiki. Mh. Lissu kajitoa mhanga kuusema ule anaoona ni udhaifu wa utawala wa Baba wa Taifa, sidhani kama amekosea hata kama anachoita udhaifu kwa wengine wataona ni ubora. Yeye kasema bila unafiki kile alichokiona na kukitathmini. Kama ni kumkosoa Bw. Lissu iwe aidha anachodai kufanywa na Mwl Nyerere kisemwe kuwa sio kweli au kama ni kweli kafanya ionekana ni ubora na sio udhaifu. Hapo tutaelimishana na nchi yetu itasonga mbele na itapata baraka kutoka Mbinguni.
 
Lissu hakuwa anaiwakilisha JF bali alikuwa anawakilisha maoni wa Wachache katika kamati yake kwa hiyo waliyoyaleta hapa JF ndio wanatakiwa watuletee uchambuzi wa kina ni katika maneno yapi au maandishi yepi yanayoonyesha LISSU amemtukana Nyerere (R.I.P) tofauti na hayo mtakuwa bado mnaimba ngonjera na hamjajibu kinachotakiwa kujibiwa na mleta mada.

Hakuna mtu atakae weza kuainisha hayo matusi na kashfa za Lisu dhidi ya JKN wanazodai.WTz hana kawaida ya kuhukumu nini kasema mtu kawaida yao wanahukumu mtu alie sema.
 
Maccm ndio sasa wanamtukana yeye JKN aligundua sehemu nyingi alikosea nae akatunga kitabu cha Tujisahihishe hivyo anaonyesha kuwa hakuwa malaika hivyo rhuksa kukosolewa.
 
Hayo maneno hebu kamwambie baba au mama yako hata kama yana ukweli, kisha tuletee mrejesho juu ya reaction yao.

lisikupe shaka, pale kwenye tatizo huwa simumunyi maneno, sio nyumbani wala kibaruani jamaa!
 
Lissu kalenga kwenye hotuba yake kumwita baba wa taifa mlaghai, ina maana ni mtu muongo, tapeli,asiefaa kuaminiwa na pengine kuenziwa. Maana hizo ndio sifa za mtu muongo kama alituongepea kuhusu muungano ina maana kuna vingi atakuwa aliongopa. Hiwapo kila kitu kiko wazi kuhusu muungano na hati wamepewa uoni kama aliamua kumchafua baba wa taifa.

Huyu Lissu katukosea sana watanzania inabidi atuombe msamaha, wafuasi wenzake wa serikari tatu kutokana na kauli za Lissu wanaendeleza lilelile la kumzihaki Mwalimu JKN kupitia kauli za Lissu. Ni kama vile Lissu kiongozi wa taifa kupitia bunge akijua wazi lina angaliwa na watanzania live kaamua kutuambia watanzania ni sawa kumzihaki baba wa taifa, unaweza kuona kwanini Tanesco waliona umuhimu wa kukata umeme kama akukuwa na itilafu it was shocking for most of us too.

Huyu bwana arudi kwenye taaluma tu huko ndio kunako mfaa inaonekana, lakini kwa sasa alipofikia ubabaishaji wake umekuwa dhahiri kwenye siasa anaweza sema lolote kimaslahi ya siasa.
 
Tusiwe watumwa wa mawazo .Nyerere hakuwa malaika ni binadamu anamapungufu yake. na kukosolewa isiwe kosa CCM hawana hoja wamebaki kusema amemtukana baba wa taifa ametukana nn? CCM wanafiki wakubwa
 
Kauli za Lissu dhidi ya Baba wa Taifa ni kweli zimeshtuaa baadhii ya wauminiii safii wa Baba wa Taifa ila bahatii mbayaa zinatumikaa vibaya na wauminiii wengii WANAFIKI wa Baba wa Taifa.
CCM imekuwaa inamdhalilishaa sanaa Baba wa Taifa kwa kipindiii kirefuu kwa matendo yao ya kulea na kuhamasisha rushwa, ufisadi, ujangili, uporaji, wizi, dhuluma, unafiki, uzembe katika Taifa hili.
 
Nmshangaa sana lisu, kaka yake Alute mbona nabusara sana?? ni kwabahati mbaya tu alishindwa kupita kura za maoni CCm jimboni kwake, lakini kama angechuana na mdogo wake angemshinda, nadhani atagombea tena 2015, nitafurahi akimbwaga mdogo wake
 
Nyerere alikuwa muongo kweli na Lissu kabainisha hilo.

Mkuu Faizafoxy umeguswa kweli na Mhs Tundu Lisu, ni kweli Raisi Nyerere hakuwa muwazi saana, nadhani nia yake kubwa alitaka kulinda taifa letu la Tanzania lisiparaganyike!!
Kwa maana hiyo TL hajakosea kusema ukweli ulio wazi, shida ya MaCCM hawataki kuambiwa ukweli!!
Wana ngangana na kushikilia uzushi ili kuhalalisha dhuluma kwa Watanzania hadi basi!!
Wazenji sasa hawataki uongo huo wa MaCCM, wakubwa wanapanick wanashikilia kila straw ili wasizame!!

 
Acha kwenda nje ya mada hebu ongelea maneno ya matusi yaliyotolewa na tundu na kwani nyerere hawezi kuwa mwongo au unadhani yale yote yaliyotolewa naye yalikuwa ya kweli.???

Kwa hiyo kwa akili yako wewe ndo unamwona Tundu Lissu kasema ukweli? yeye si mwongo?
 
Thibitisha pasipo shaka hapa jukwaani, ni kweli kwamba ktk maisha ya uongozi wa mwalimu hakuwahi kusema uongo?

Mna uthibitisho gani kwa kusema alikuwa mwongo?? Kwa mfano upi alioutoa Lissu?? Acheni kujitoa faham kwa kutetea ujinga!
 
Nyerere alikua kiongozi mzuri, Lakini alikuwa na mapungufu jamani hakuwa Mungu alikuwa na mapungufu mengi tu ukiachana na huo uwongo,

Ni kweli mkuu, lakini mapungufu yake huwezi kuyalinganisha na ya Lissu!
 
Lisu alichofanya ni kunukuu maandiko ya watu wengine kuonyesha namna walivyomsema Nyerere, hivyo si kweli kuwa limtukana bali alionyesha kuwa amewahi kukosea. Mfano mzuri ni Kitabu cha Msekwa kilichochapiswa mwaka huu januari. inamaana kosa la Lisu ni kukisema hicho kitabu, magazeti na maandiko mengine?
Uiwa na aili kama za ccm, kilakitu ni tusi, walizoea vya kunyoga?!!!
 
Kwa hiyo kama alidanganya asiitwe mwongo kisa.

Alidanganya nini? Mnatakiwa kuthibitisha, siyo kuongea ongea tu kama Lissu! Yaani chuki zenu za CCM mnazifanya Lissu na CDM members hata wakiongea utumbo mnaona sawa tu! Hamna tofauti na waliomtukama Jaji Warioba! Waanasiasa watu wa ajabu sana, na nyie mnashangilia kama mazuzu kisa kaongea mtu wa CDM, au CCM walivyoshangilia kwa kuwa kaongea Kikwete! Ni Mpuuzi tu ndo anaona hii ni sawa!
 
Mh. Tundu Lisu ni miongoni mwa wabunge ninaowaheshimu sana tena sana. Japo sina chama cha siasa lakini nimekuwa nikikunwa na siasa za chadema. Lakini kwa hili kwakweli napenda kutofautiana na Mh. Lisu na chama cha chadema kwa kuendelea kukaa kimya kwa jambo kubwa kama hili na linalogusa hisia za watu wengi kwa namna tofauti. Naamini kuna watu wengi waliosikitishwa na tukio hilo na kupelekea kupunguza imani kwa Lisu napengine Chama kwa ujumla.

Ni ukweli Mwl. amefanya mambo mengi mazuri na mabaya pia na hata mimi kuna mbambo ambayo kimtizamo ninatofautiana naye mfano hili la Muungano. Tatizo langu kubwa kwa Lisu ni namna ya utumiaji wa maneno katika kufikisha hoja yake nzuri. Lisu inawezekana kabisa kutoa hoja yako na ikaeleweka pasipo kutumia lugha kali namna hiyo na pengine kutafsiliwa kama matusi. Mimi binfsi nayatafsiri maneno hayo kama matusi kulingana na nilivolelewa jinsi ya kuongea na kufikisha ujumbe kwa watu hasa wanaonizidi umri.

Kumbuka kuna watu wanamheshimu Mwl. kulingana na mambo aliyoyatenda na wengine mwalimu ni mtu wa level nyingine kiimani (Kulingana na imani zao za kidini) Hivyo muda mwingine matumizi mazuri ya maneno yanaweza kujenga taifa pasipo kuleta mgawanyiko katika jamii.

NOTE: Kwangu mimi tatizo siyo aliyoyaongea Lisu ila Jinsi alivyoongea.
 
Alidanganya nini? Mnatakiwa kuthibitisha, siyo kuongea ongea tu kama Lissu! Yaani chuki zenu za CCM mnazifanya Lissu na CDM members hata wakiongea utumbo mnaona sawa tu! Hamna tofauti na waliomtukama Jaji Warioba! Waanasiasa watu wa ajabu sana, na nyie mnashangilia kama mazuzu kisa kaongea mtu wa CDM, au CCM walivyoshangilia kwa kuwa kaongea Kikwete! Ni Mpuuzi tu ndo anaona hii ni sawa!

Yaani ina maana facts za Lisu kuhusu uongo aliosema hujaziona, inawezekana tunabishana na mtu ambaye hujui unaongea nini. Ndio ubaya wa JF huu. karudie post yenye hotuba ya Lisu ukasome duh
 
Back
Top Bottom