Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Tatizo watu wanamuona nyerere kama mungu wao. Sishangai kusikia watu wana abudu mizimu na sanamu kwa hali hii.
 
Jaji warioba wakati anawasilisha rasimu,aliwaasa wajumbe wa bunge maalumu la katiba kuwa,ili katiba mpya ipatikane,MAONI ya wananchi yalimo yenye kwenye Rasimu ni la lazima yaheshimiwe. Tunachokiona sasa ni janja ya kutunga katiba ya watawala badala ya katiba ya wananchi
 
Mleta mada anataka muyataje hayo maneno nyie mnakuja na ngonjera zile zile, NAOMBA UTUAMBIE LISSU AMETUKANA VIPI AU MANENO GANI MABAYA ALIYOYATAMKA JUU YA NYERERE. kwa hiki ulichokiandika bado haujajibu swali la mleta mada

hawana hoja haoo,wanaogopa ukweli mchungu
 
Hivi Nyerere ni malaika hata asikosolewe??
 
Nyerere ni sawa na mtanzania yeyote, kwa mazuri aliyofanya alisifiwa na kwa mabaya aliyoyakosea lazima akosolewe, yeye sio Mungu na wala hatokuja awe mungu.
 
kwa upande mwingine kumbe tafsiri ya msikilizaji inaweza kufanya hayo maneno kuwa matusi ama la,sasa basi ili kumuaminisha mwingine aamini unachoamini ni kumshawishi kwa hoja na mifano au nukuu toka ktk hayo maneno,tukirudi kwa lissu ninyi mnaoamini kuwa ametukana tunaomba nukuu ya yale unayoamin kuwa ni matusi ili tukikubaliana nanyi tuungane ktk kumkemea bwana lissu,lakini kinyume na hayo tutaendelea kuamini kuwa hizo ni siasa za majitaka ambazo hazina nafasi leo.

Hawana hoja,kazi kubwabwaja maneno

CCM waache unafiki(pretenders are worse than murderers
 
Wanaosema tundu lisu amemtukana mwalimu nyerere hawana hoja nyerere hakuwa MUNGU hivyo basi ana mazuri yake na mabaya yake.
 
Hata akitukanwa ni haki yake mbona Mungu alitukanwa na anaendelea kutukanwa wala halalamiki
 
Mimi namshangaa hata rais anaicheza ngoma asioijua,je!warioba kutukanwa hadharani kwake ni halali?kwa nyerere ndio kosa,
 
Kama Nyerere hakuwa mwongo huo ujamaa aliokuwa anutetea na kutufanya wote maskini uko wapi?Yeye alidanganywa ba Wachina halafu akaja kutudanganya sisi,sasa huo ni ukweli? Na kama Intrahamwe inampenda sana kwa nini walimtema? Enyi mnaokurupuka eti Nyerere katukanwa, mwuulizeni Mkapa maujanja ya mzee wetu atawapa full story. Tuliishi kiungo ongo tuuu kama tunavyoishi kidhaifu dhaifu sasq hivi. Tukisema Kikwete sio rais wa Zanzibar mnasema ni uongo. Hebu Ikulu wapinge na hili. Huu si uongo? Kujifanya Rais wa Tanzania wakati sio kweli. Kikwete ni Raisi wa Tanganyika period. Kwa kuwa kuna uongo uongo kila mwongo atasema ni Rais wa wote ... Tanganyika na Zanzibar. Feki kabisa.
 
duuh hili ni jipu la pua kwa wazee wa kijan manake walikuwa washazoea kumtumia mwl Nyerere kupata kura vijijin.sasa ikitokea mtu kuanika mapunguf ya mwl ni kama kuwaamsha waliolala na kujua kuwa mwl alikuwa mwanadam kama wao. ni shida kwel anywayz wacha muv iendelee
 
Nadhani kwa mtu mwenye akili timamu anajua kua tanzania iko huru kwa juhudi za mwlm nyerere,nanikweli kafanya mengi mazuri sana sana ila sidhani kama hakuwahi danganya au kukosea sababu sifa kuu ya mwanadam mapungufu as we know no body is perfect,,anaetukanwa ni mzee warioba na si nyerere tuache kulishwa sumu kama atukumskia lissu someni iko jf ndipo tutajua ukweli
 
hakuna matusi mkuu , hiyo ni tafsiri ya kiwango cha chini ya walioshindwa hoja .
 
hadi leo magamba yameshindwa kutaja matusi.yamebaki na propaganda zao tu.shame!
 
"Aliyezoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi" au "aliyezoea kuishi kwa uongo/ulaghai kamwe hawezi kuwa mkweli" by Tundu Lissu on Dr. Mwakyembe, Prof. Issa Shivji ad Mwl. Nyerere.
 
no body is perfect xo mwalimu ni binaadamu xaxa wanaodai katukanwa pliz mention those insults which nyerere ambapo ametukanwa xio kutoatoa porojo ambazo hazina msingi
 
Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.

Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.

Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?

Acahana nao hao ndugu, kuna watu kazi yao ni kufanya kizuri kionekane kibaya na kinyume chake!
 
Last edited by a moderator:
Jaji warioba wakati anawasilisha rasimu,aliwaasa wajumbe wa bunge maalumu la katiba kuwa,ili katiba mpya ipatikane,MAONI ya wananchi yalimo yenye kwenye Rasimu ni la lazima yaheshimiwe. Tunachokiona sasa ni janja ya kutunga katiba ya watawala badala ya katiba ya wananchi

umeandika UKWELI sana !
 
Back
Top Bottom