Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Mwalimu Nyerere ametukanwaje hasa?

Maziwa Lala kwelikweli wewe na uanasheria wako wa kwenye JF...yaani matusi kwako ni yale ya nguoni tu...kama baba yako ni marehemu akatokea mpuuzi miaka kadhaa baadaye akasema baba yako alikuwa gaidi wewe hutaona kuwa ni matusi...acha ushabiki wa pesanane...
Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.

Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.

Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?
 
Nyerere alikuwa binadamu tuu,ukweli utabaki palepale kuwa kila binadamu hukosea na kukosolewa.
 
Umenena mkuu, lakini umemsahau pia Lyatonga Augustine Mrema mzee wa Kiraracha ambaye aliimarisha usafi wa jiji la DSM na kuleta vivuli vya miti na pavements katikati ya jiji kwa amri ya siku 7, ingawa fadhila za JK zimemfanya aonekane kutikiswa siku hizi kimsimamo na kuegemea lolote la ccm hata bila kuchuja kama zamani. mnyonge myongeni lakini haki yake mpeni. Kaifanyia nji hii mambo mengi sana mazuri ambayo hapaswi kusubiri afe ndo tumsifu.

Nakubaliana na wewe ndugu yangu. Ila tatizo ni kuwa hawataki kujifunza hawa. Na kama unavyosikia inavyokuja kwa Muasisi wa siasa za taifa letu, kuna siku itafika kwake( sijui kama atakuwa hai au watngojea awe ameondoka). Wakati huo watasema " alichapa kazi sana, akakamata madini uwanja wa ndege, halafu wakamtenda (siyo kweli) akawa mpinzani wao. Akwaponda jukwaani na akawakumbatia sirini"! Hiyo ndiyo historia yake asipobadilika.

Kumbe inaonekana wabongo wana matatizo ya kuendekeza njaa na unafiki bila kujali wanaandika historia!
 
mkuu big up sana mkuu,nawashangaa sana ccm jk alipokuwa hai hawakutimiza wala kuyaishi yale sahihi aliyosema..walisema yamepitwa na wakati,leo ni marehemu wanajifanya kumtumia kama nukuu za biblia,wanafiki hawa tulione hili...wanatafuta tonge tu

Mbaya zaidi pamoja na uchungu wote wa kinafiki walionao juu ya mwalimu, matendo yao na maneno yao hayaonyeshi kama hata wanamjali kwa lolote!

Kipindi cha uhai wake, usingekuta viongozi wezi bado wako madarakani tena wanainuliwa mikono hadharani wanapigiwa na kampeni na Marais! Ni aibu!...Wala usingesikia mtu anakwiba mabilion benki halafu anaambiwa arudishe tu aende zake!.Eti mafisadi wanajulikana kwa majina, ushahidi upo, kuwashitaki unajiumauma.Mara umewashitaki kesi zinaendeshwa kama hawataki! Zinamaliza miaka! Mara Wananchi wamesahau, wathumiwa haoooo wanapeta uswahilini..Wala usingeona chama cha wakulima na wafanyakazi kimekuwa chama cha wafanyabiashara na majambazi, tena kienyeji!

Lakini naamini hata yeye alijua kuwa mbegu anazopanda, kuna watu watavuna! Imekuwa bahati mbaya wale watu tumekuwa sisi!

Halafu sikia walivyo wanafiki na kudai inawauma sana! Mwalimu katukanwa! Wapi? Matusi gani? Hivi katika akili ya kawaida ni nani anayepata laana? Lissu aliyesema Mwalimu alikuwa na "tabia za tofauti"? au Wao wanaodai kuwa watoto wa Mwalimu halafu wanayofanya na kusema yanamtukana mwalimu?

Siamini kama marehemu wanasikia wala kuona, lakini tuache unafiki na kulichafua jina la Mwalimu kwa kudai utakatifu wakati tunajua wazi uchafu wetu.
 
TUNDU LISSU namfananisha na "tanganyika jeki"
sifa kuu ya hii jeki ni kuwa hunyanyua gari pamoja na mzigo wake.

JK alinyanyuliwa pamoja na mizigo ya majaji wake.
Nyerere kanyanyuliwa na mizigo ya uongo wake.

Jk aliteua baadhi ya majaji ambao hawakuwa na sifa za uteuzi ndio maana kuna baadhi ilibidi wajiunge open university kuchukua LLB ili wakidhi matakwa ya sheria waliyokwisha ikiuka. "tanganyika jeki imewanyanyua"

Huyu Nyerere sasa kanyanyuliwa juu zaidi muuone uongo wake, kwa kuthibitisha uongo wake jiulize,
uko wapi ujamaa na kujitegemea!!!!!
Liko wapi azimio la arusha!!!!!!

muungano nao magumashi.

Msipanick huu ni ukweli hamkuujua kabla.

Ushabiki wa kisiasa ni kitu kibaya sana.....ni baadhi ya mambo yanayorudisha nyuma sana harakati za mageuzi nchini........



Mkuu Ogah, tunaomba utoe jibu la swali la aliyeanzisha uzi. Vinginevyo utakuwa unaendeleza uzushi kama hutaweka hizo kauli za Lissu mnazodai ni mbovu.


Hayo matusi ni yepi?


Mkuu Kichuguu, mbona hutaji hizo kauli? Tunawashukuru kwa kutukumbusha ya Zitto, Kilita, Majaji n.k. Ila unaendelea kuharibu badala ya kusaidia kwa kushindwa kuandika hizo kauli. Kama huwezi kufanya hivyo ni bora ukakaa kimya.

Mkuu ni uzushi gani uliouona kwenye maandishi yangu?........ukitaka kujua kuwa baadhi ya maandishi ya Lissu yalikuwa na walakini kuhusu uteuzi wa majaji.....rejea mada husika......

Nilichosisitiza kwenye post yangu huko juu ni kwamba inabidi wana JF tuwe makini wakati wa kusoma maandishi/maneno ya watu mbali mbali....hapo uzushi uko wapi?

Lissu hakuwa anaiwakilisha JF bali alikuwa anawakilisha maoni wa Wachache katika kamati yake kwa hiyo waliyoyaleta hapa JF ndio wanatakiwa watuletee uchambuzi wa kina ni katika maneno yapi au maandishi yepi yanayoonyesha LISSU amemtukana Nyerere (R.I.P) tofauti na hayo mtakuwa bado mnaimba ngonjera na hamjajibu kinachotakiwa kujibiwa na mleta mada.

Well, all the best na mtizamo wako........
 
Ukweli utabaki kuitwa ukweli na kamwe uongo hautoitwa ukweli,Lisu alyatoa ambayo weng huwa wanayajua ila wanakosa ujasir wakuyasema
 
Maziwa Lala kwelikweli wewe na uanasheria wako wa kwenye JF...yaani matusi kwako ni yale ya nguoni tu...kama baba yako ni marehemu akatokea mpuuzi miaka kadhaa baadaye akasema baba yako alikuwa gaidi wewe hutaona kuwa ni matusi...acha ushabiki wa pesanane...

Nikisema OSAMA gaidi ni tusi au sifa?
Tundu Lissu amemsifu hayati J.K.Nyerere kwamba aliongoza nchi
1.Kibabe
2.Kiujanjaujanja
3.Kidikiteta
4.Uongouongo
Sasa hizo zote ni sifa za Baba wa taifa. Tusi hapo ni lipi mbona ccm munakuwa wanafiki. hata mukisifiwa kwa natendo yenu bado munanuna!!!.
 
Maneno ni upanga wenye ncha mbili zinayokata pande zote. Maneno yako yanaweza kukufanya uwe na hatia na vile vile yanaweza kukuondoa kwenye tuhuma za hatia. Yote inategemea na jinsi unavyotumia maneno yako.

Sidhani kama Lisu alitumia maneno yake vizuri, na ndiyo maana nimekuwa na wasiwasi na uhakika wa maneno yote aliyowahi kutuambia kuhusu Zitto na Kitila huko nyuma.

Kumbe watu ni wanafiki na kusikiliza propaganda bila kuchambua. hapa mtoa mada kasema tajeni matusi aliyosema Tundu dhidi ya Nyerere wote mnaishia kuanyaanya tu. basi nyinyi mnaomtuhumu ndiyo wenye matusi tena makubwa kwa sababu mnafanya mambo ya ajabu kwa kujificha katika maneno ya Mwl. na mtalaaniwa mpaka mbinguni
 
Nikisema OSAMA gaidi ni tusi au sifa?
Tundu Lissu amemsifu hayati J.K.Nyerere kwamba aliongoza nchi
1.Kibabe
2.Kiujanjaujanja
3.Kidikiteta
4.Uongouongo
Sasa hizo zote ni sifa za Baba wa taifa. Tusi hapo ni lipi mbona ccm munakuwa wanafiki. hata mukisifiwa kwa natendo yenu bado munanuna!!!.

Lissu n mwanasheria anajua kitendo cha kutoa lugha inayoashiria kumdhalilisha mtu n makosa.
kumwita mtu muongo kisheria n kumdhalilisha.
kumwita mtu dikteta kisheria n makosa( defamesheni).
Kwa vile kauli kaitolea bungeni hakuna chombo chochote kitahoji kasoro bungeni tu.(kinga ya bunge kwa mbunge) .
Nje ya bunge anajua madhara yake hawezi kuyasema hayo.
Hata kama sio nyerere, sio busara kutamka" nyerere ni muongo, alizoea vya kunyonga, alitawala kijanjajanja. laghai nk" hayo sio matusi ni kashfa.
 
Lissu n mwanasheria anajua kitendo cha kutoa lugha inayoashiria kumdhalilisha mtu n makosa.
kumwita mtu muongo kisheria n kumdhalilisha.
kumwita mtu dikteta kisheria n makosa( defamesheni).
Kwa vile kauli kaitolea bungeni hakuna chombo chochote kitahoji kasoro bungeni tu.(kinga ya bunge kwa mbunge) .
Nje ya bunge anajua madhara yake hawezi kuyasema hayo.
Hata kama sio nyerere, sio busara kutamka" nyerere ni muongo, alizoea vya kunyonga, alitawala kijanjajanja. laghai nk" hayo sio matusi ni kashfa.

Tunashuhudia wanaCCM wengi humu JF pamoja na Masalia ya CHADEMA majukwaani yakiwa upande wa CCM wakitamka kuwa CHADEMA ni chama cha Kilaghai, Viongozi wa CHADEMA ni madikteta, CHADEMA ni chama cha KIHUNI sasa kama nyie mmeweza kuyasema hayo kama wewe unasema ni kosa vipi kwa upande wenu kuyatamka hayo kwa viongozi wa CHADEMA ni sahihi kwa kuwa ni nyie mmeyasema ila akitamka mwana CHADEMA kwenda upande mwingine ni kosa na tusi?
 
Mwalimu aliwahi kukiri hadharani kuwa haiwezekani kwa mtu kukaa madarakani miaka yote takribani 25 bila kufanya makosa. Na kwamba yeye siyo Mungu hivyo alifanya makosa! Na akafafanua kwamba tatizo ni watu kuacha kuenzi yale mazuri na kung'ang'ania mabaya. Mwenye clip ya hotuba ile tafadhali atuwekee hapa ili hawa wakina Tomaso wajue Nyerere hakuwa Mungu bali alikuwa muungwana anayekiri kuwa kuna mabaya alifanya wakati wa utawala wake.

Naunga mkono hoja ya mleta mada.....orodhesheni matusi aliyotukanwa Mwl Nyerere
 
Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.

Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.

Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?
sidhani kama Lisu katukana ila naona kuna upotoshwaji wa hali ya juu kwani nyerere ni binadamu lazima kuna sehemu amekosea na hatutakiwi kurudia yale yale makosa tunapoelekea kuandaa hatma ya vizazi vya leo,kesho na kijacho.
 
[h=2]Edwin Mtei asikitishwa na alaani kitendo cha Tundu Lissu kumtukana Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere[/h]
Nilimsikiliza Mheshimiwa Tundu Lissu na nasikitika kwamba sikubaliani naye jinsi alivyoeleza shutma juu na dhidi ya Mwalimu Julius Nyerere, Baba na Muasisi wa Taifa letu.

Inajulikana na umma wa Watanzania, kwamba mimi binafsi, kama Waziri wa Fedha, nilitofautiana na Mwalimu, nikajiuzulu Uwaziri Decemba,1979, nikimwomba ateuwe Mtanzania mwingine atakayeshauri mambo ya Uchumi na Fedha. Lakini tuliendelea kuwasiliana kwa maelewano bila chuki, na hata aliniteuwa niwe Mwakilishi wa Tanzania na Afrika inayoongea Kiingereza katika IMF (Shirika la Fedha Duniani) chini ya miaka mitatu baadaye Novemba, 1972.

Nimekuwa na mawasiliano na maelewano mazuri sana na Mwalimu hata baada ya kuasisi CHADEMA, Julai 1992 na tulipokamilisha Katiba na Sera za Chadema, nilimtembelea Nyumbani kwake Butiama nikampa azisome ajionee jinsi tulivyonuia kuwahudumia Wananchi wetu. Hata siku moja siwezi kumtusi Muasisi wa Taifa letu. Iwe ni mwiko pia kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo kumtusi Baba wa Taifa.

Ningewashauri uongozi wa Chadema na hasa Vijana wa M4C (Vuguvugu la Mabadiliko) tuendelee na uhamasishaji : kwa umakini, tukiwa na huruma kwa wanyonge maskini wa kutupwa, tukijiandaa kwa umakini na kiutaalamu Sera na Mikakati ya kuwakomboa toka katika umaskini wa kutupwa kwa kutumia nguvu ya umma (Peoples Power) tukitumia mikakati sahihi: kwani Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke:

Mikakati na Sera sahihi ikiwa ni kutumia misingi ya Uchumi na Miundombinu tulionayo licha ya uhalisia dhoofu tulioridhi; tukiwaenzi walioijenga na kuturidhisha kwa unyofu wao.

Roho ya Julius Nyerere ilale mahala pema Peponi. Amen!

With all due respect to Hon. Tindu Lissu, this smacks BAD TASTE.


Edwin Mtei,

Founder Chairman of CHADEMA.

Umenikumbusha jambo; Mwalimu aliwahi kuwaoji wakenya-kwamba kama mtu atapita hapa na kukuambia yule bwana yule unayemuona ndo baba yako. Je, utakubari?
Mleta mada anakiu ya kujua matusi alotoa TL dhidi ya Mwl; wewe unacopy maoni ya Mtei unaweka hapa. Duh! Kaaazi ipo
 
Kuna uvumi (binafsi naziita propaganda) kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum na Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M.Lissu 'amemtukana' Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 'Matusi' husika yanadaiwa kuporomoshwa na Tundu Lissu alipokuwa akiwasilisha Maoni ya Wachache katika Kamati Nambari Nne ya Bunge.

Inasemwa kuwa Tundu Lissu amemtukana na kumdhalilisha Baba wa Taifa. Propaganda hizi zinazosambaa haraka na kwa kishindo zimemkumba hadi Mzee Edwin Mtei ambaye ni Mwenyekiti wa kwanza wa CHADEMA. Nikumbukacho ni kuwa Lissu alipokuwa akitetea na kufafanua Maoni ya Wachache,alitoa mifano minne akiwataja watu mbalimbali wakiwemo Mwalimu Nyerere,Profesa Issa Ghulamhussein Shivji na Dr.Harrison Mwakyembe.

Kwanza,tufahamishane hasa matusi yaliyoporomoshwa na Wakili Lissu dhidi ya Mwalimu Nyerere. Tukiyajua na kutambua kuwa ni matusi na dharau kweli,tuungane kumkemea Wakili Lissu na kumuonya asirudie tena. Karibuni tutaje matusi au dharau za Wakili Tundu Lissu kwa Mwalimu Nyerere. Halafu,kwanini wengine waliotajwa hawaonekani kama wametukanwa au kudhalilishwa?

cjui niseme ni upuuzi au nini,vitabu vya dini vinasema hakuna binadamu aliekamilika na ndo maana kuna kutubu,nimeshangaa hata yule babu anaejiita askofu halijui hilo mpaka kusema eti nyerere hakuna wa kumkosoa,eti anatarajiwa kutangazwa mtakatifu na kanisa katoliki,kama kuna mtu ana mawasiliano na yule babu hebu amwambie asome vizuri historia ya watakatifu aone walikuwa na maisha gani kabla ya kuja kubadilika na kutubu dhambi zao,wengine walikuwa wauaji,wanyang'nyi nk lakn leo hii ni watakatifu,kwa hili babu hastahili kuitwa askofu kama hata maandiko anayapotosha.
kwa mwenye akili ya kufikiri atajua pale swala sio kumtukana nyerere wala kumkosoa hapa ni agenda ya kutafuta pa kushika kwa sababu hata mfa maji haishiwi kutapatapa,kila mjumbe anaesimama analifanya hilo kama ndo kipengele cha kujadili bungeni kwa sababu binafsi nadhani wajumbe wameambiwa bila kuliweka hilo hatuna jambo jingine la kutumia kuwalaghai wananchi,na atakaekiuka hana ulaji ndo maana wanaangaika sana ili waonekane waendelee kupata fadhila.
 
Back
Top Bottom