Mwali: Mmiliki wa DOWANS ni huyu!

Mwali: Mmiliki wa DOWANS ni huyu!

Status
Not open for further replies.
haa, kumbe hizi hela za dowans tunazopiga nazo kelele ni za ccm. kazi yake kubwa ni kusaidia kuendesha chama, ukizingatia kwamba ruzuku ya ccm imepungua toka bil. 1.2 mpaka mil. 800 kwa sasa. Pili, wakati wa kampeni walikopa hela nyingi sana, na nyingi walikopa kwa rostam, hivyo wanataka warudishe hela zake.
wakati huo huo ccm hawana namna nyingine ya kuiba hela nyingi toka serikalini kutokana na usaliti dhidi ya chama kuongezeka, watumishi wa serikali wanatoa siri zote kama ilivyokua walivyotumia bil. 2 za ikulu kuchapisha picha za kampeni, ikajulikana. Na wana ccm wanaopiga kelele kupinga dowans ni wale ambao hawapo karibu na uongozi wa juu wa ccm na hawana habari kamili. Habari ndo hiyoooo..
hivyo basi mlie, mcheke, muandamane, muandae makongamano, mtukane. dowans lazima ilipwe.
 
VAA NGUO NYEUSI tarehe 05 February kama ishara yako ya kuomboleza janga linaloitwa CCM
 
Ila kwa mbinde! Hakuna tena urahisi wa kujichukulia kama zamani, hata kama wakilipwa ugumu walioupata utawapa fundisho! Hiyo ni hatua moja, baadae tutaelekea kuwa wa tunisia na wamisri ndo watajua nguvu ya umma ni nini
 
Kama Tunisia walifanikiwa kumtoa rais hakuna kitakachoshindikana. 2kiamua 2naweza...
 
RA ni mfanyabiashara, hawezi kukubali jina lake litumike kuchota fedha zote hizo halafu asiambulie kiasi kikubwa. Kama kweli ni za ccm, basi za RA na wenzake ni 90% na ccm 10%.
Hivi mnataka kunieleza kuwa ccm ilitumia 94bn/- katika kampeni! Hizi ni hela nyingi sana; nadhani kama walitumia nyingi si zaidi ya 10bn/- hivyo 84bn ni za RA na wenzake.
 
haa, kumbe hizi hela za dowans tunazopiga nazo kelele ni za ccm. kazi yake kubwa ni kusaidia kuendesha chama, ukizingatia kwamba ruzuku ya ccm imepungua toka bil. 1.2 mpaka mil. 800 kwa sasa. Pili, wakati wa kampeni walikopa hela nyingi sana, na nyingi walikopa kwa rostam, hivyo wanataka warudishe hela zake.
wakati huo huo ccm hawana namna nyingine ya kuiba hela nyingi toka serikalini kutokana na usaliti dhidi ya chama kuongezeka, watumishi wa serikali wanatoa siri zote kama ilivyokua walivyotumia bil. 2 za ikulu kuchapisha picha za kampeni, ikajulikana. Na wana ccm wanaopiga kelele kupinga dowans ni wale ambao hawapo karibu na uongozi wa juu wa ccm na hawana habari kamili. Habari ndo hiyoooo..
hivyo basi mlie, mcheke, muandamane, muandae makongamano, mtukane. dowans lazima ilipwe.

Hizi habari mbona sio ngeni?
 
Hao hawana la kufanya,kwani miradi ya kweli yoooote imekufa,sasa ni kuendeleza ufisadi kwa kwenda mbele,ila mwisho wao upo karibu,soon and very soooon !
 
Mbunge Shinyanga akoleza moto wa Dowans


Na Suleiman Abeid, Shinyanga

MOTO wa kupinga nia ya serikali kutaka kuilipa kampuni feki ya Dowans malipo ya sh. bilioni 94 umezidi kusambaa nchini ambapo mbunge wa jimbo la
Shinyanga mjini (CCM), Bw. Steven Masele ameungana na wananchi wanaopinga kulipwa kwa malipo
hayo.

Akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Shinyanga katika viwanja vya soko kuu mjini Shinyanga juzi, Bw. Masele alisema yeye binafsi anapinga vikali kusudio la serikali kutaka kulipa malipo hayo na kwamba iwapo fedha hizo zitalipwa ni sawa na serikali kuwafanyia dhuluma wananchi wake.

Bw. Masele alisema yeye kama mbunge na mwakilishi wa wananchi wa Jimbo la Shinyanga mjini kamwe hawezi kujipendekeza kwa kundi la mafisadi wanaopanga njama za kutaka kuifilisi nchi wakati wananchi wake wakiwa ni masikini wa kutupwa.

Hatua hiyo ya Bw. Masele kuelezea msimamo wake kuhusiana na malipo kwa Dowans ilitokana na wananchi katika mkutano huo kuhoji msimamo wake iwapo anaungana na wananchi kupinga malipo au anaafiki kulipwa kwake kama serikali inavyodai kuwa ni kuheshimu sheria za Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi ya Migogoro ya Kibiashara (ICC).

Ndugu zangu wana Shinyanga wenzangu, mimi napenda niwathibitishie wazi kuwa binafsi yangu siko tayari kujipendekeza kwa kundi la mafisadi kwa maslahi binafsi, sikubaliani kabisa na uamuzi wa kulipwa kwa Dowans, ninapata uchungu kulipa matapeli
hao, msimamo wangu ni huo na ninaamini nanyi ndio msimamo wenu,� alieleza Bw. Masele.

Alisema pamoja na kushitakiwa katika ICC hukumu iliyotolewa ni ya kuwakandamiza Watanzania nani ni dhuluma kwa taifa changa na maskini kama Tanzania.

Mbunge huyo ambaye ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuwahutubia wakazi wa mjini Shinyanga tangu alipochaguliwa kuwa mbunge, alishauri serikali iunde
jopo la wanasheria kwa lengo la kukata rufaa na kuepusha nchi kulipa deni hilo kwa matapeli.

"Kuna kila dalili zote zinazoashiria huenda kesi hiyo ilitokana na kupangwa na baadhi ya wajanja wachache na hivyo Dowans kupewa tuzo hiyo bila ya kuzama kwa undan, tutalipaje mabilioni ya shilingi wakati umeme hawakutoa?" alihoji Bw. Masele.

Kuhusu mikataba ya Richmond Bw. Masele alikiri kufanyika kwa makosa na kuisababishia nchi hasara na kwamba sasa inahitajika wahusika kuwajibishwa kutokana na kasoro na dosari katika mikataba iliyofungwa kiujanja ujanja.




7 Maoni:

blank.gif

Anonymous said... Wewe masele acha kuhadaa wewe mwenyewe umebebwa na kutangazwa kwa lazima na hukushinda ubunge wa shinyanga. ulikimbia nini baada ya kutangazwa mshindi pamoja na mkurugenzi wa manispaa kama kweli wewe ni halali? Acha kujikosha kwa mgongo wa richmond na dowans kwetu hatukutaki!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!maana hatujakuchagua bali umechaguliwa na hao DOWANS NA RICHMOND chini ya makamba na ridhiwani,sasa leo unawageuka kweli binadamu hawana fadhila
February 1, 2011 11:12 PM
blank.gif

Anonymous said... ni kichefuchefu kwa maselle kuongea masuala hayo coz uliona wapi ktk historia ya Tanzania mbunge anashinda kwa kura moja?????????
tafadhali nyamaza kabisaaaaaaa.

February 2, 2011 12:25 AM
blank.gif

Ngambise said... Bw. Steven Masele huwezi kukata mkono unaokulisha, labda uwe taahila. Dowans ina uhusiano wa karibu sana na CCM kilichokuingiza kwenye ubunge, pesa za mafisadi ni sehemu ya ushindi wako wa ubunge. kupinga dowans kulipwa ni kupinga CCM kuwepo madalakani. Usidsnganye wananchi wako kwa kuimba wimbo wao wa kupinga dowans na kutaka katiba mpya. Kama uko serious kweli hama 'huko' uliko nenda 'kuleee' waliko wapinga dowans wa kweli
February 2, 2011 12:37 AM
blank.gif

Mango said... kama wananchi wenye nchi hawataki kuilipa dowans wasilazimishwe kulipa na mwananchi mwenzao ama kikundi cha watu. Ngoja tusubili hatua zitakazochukuliwa na dowans kwa kutokulipwa na watanzania, tuko tayari kwa matokeo hayo kama nchi lakini CCM isitulazimishe, tusipoteze muda wetu kujadili mafisadi, sasa tujadili vitu vingine kama matokeo mabaya kwenye shule za kata ikiwezekana pesa ambazo dowans inataka ilipwe tuzielekeze kwenye shule za kata ili ziwe na ahueni
February 2, 2011 12:52 AM
blank.gif

Anonymous said... Tolerance, tolerance, tolerance Ndugu zangu. Masele ni Mbunge kama alivyo Rais wetu. Iwe isiwe hivi sasa wao ndio wawakilishi wetu. Yeye ametoa dukuduku lake. Acheni akose fadhila. ila aegemee upande wenu. Si kondoo aliyepotea amejirudi. hata kwa mara hii amewapa tafu. Tuwe na subira. Si kila kingaacho ni dhahabu. Hata huko upinzani yapo madudu, kama mungejua. Kwa hiyo Mhe. Masele ana haki ya kutoa dukuduku lake na kusikilizwa. Alichosema ni kweli na kama wana CCM wote wangechukuwa msimamo huo tungepiga hatua. Huyu ni SHibuda mwingine, msubirini. Days will tell.
February 2, 2011 3:13 AM
blank.gif

Anonymous said... NAWE SULEMAIN ABED ACHA NJAA KUSIFIA VITU AMBAVYO HAVIPO WOTE TULIKUWA KWENYE UWANJA HUO MAELFU YA WATU YAMETOKA WAPI HII HABARI UMEITENGENEZA BAADA YA KUPATA MAELEKEZO KUTOKA KWA RC BALELE AMBAYE HUWEZI KUANDIKA HABARI HADI UMUULIZE HIVI UNAANDIKIA MAJIRA AU BALELE NEWS PAPER MBONA ALIPOSHUSHULIWA NA SHIBUDA KWENYE KIKAO CHA RCC HUKUANDIKA HUYO SI MBUNGE WA SHINYANGA WEWE MWENYEWE ULIANDIKA ALIVYOTANGAZWA KINYEMELA NA KESI ATASHINDWA KUWENI WAANDISHI WASTAARABU,SISI WASOMAJI TUNAWAELEWA SANA WAANDISHI WA SHINYANGA KILA MTU NA MTU WAKE WEWE NI WA BALELE.MBUNGE WETU NI SHELEMBI.ACHA UNAFIKI ABED.
February 2, 2011 4:36 AM
blank.gif

Anonymous said... Hizo pesa mnazotaka kuilipa dowans (ambao ni mafisadi watanzania waliojificha chini ya kivuli cha dowans) si mngeweka maabara kwenye shule zenu za kata mlizozianzisha ambazo zimefelisha kuliko maelezo, na vitabu kwa ajili ya shule hizo pia mngeweza kuzitumia hizo pesa kwa ajili ya kuweka sawa mashirika mawili ya usafiri la kwanza ATC muiwezeshe kupata ndege za kutosha na pili RELI YA KATI au mnasubiri kusukumwa na NGUVU YA UMMA KAMA TUNISIA?
February 2, 2011 6:06 AM
 
PHP:
Akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Shinyanga katika viwanja vya soko kuu mjini Shinyanga juzi, Bw. Masele alisema yeye binafsi anapinga vikali kusudio la serikali kutaka kulipa malipo hayo na kwamba iwapo fedha hizo zitalipwa ni sawa na serikali kuwafanyia dhuluma wananchi wake.
 
Bw. Masele alisema yeye kama mbunge na mwakilishi wa wananchi wa Jimbo la Shinyanga mjini kamwe hawezi kujipendekeza kwa kundi la mafisadi wanaopanga njama za kutaka kuifilisi nchi wakati wananchi wake wakiwa ni masikini wa kutupwa.

Hii ni danganya toto kama kweli anakerwa basi aandae muswada binafsi wa kumshitaki JK Bungeni kwa ufisadi huu wa kimachomacho......................................
 
Wakuu wanaJF nimeona niwape nukuu chache tu za magazeti haya ya leo ili mpate uhondo kidogo.

Mwanahalisi- Title: Anayedaiwa mabilioni Dowans ni Rostam
TZ Daima: Title: Dowans vita mpya

Contents:
Mwanahalisi:

'Kampuni ya Dowans S.A ndio ilipeana kienyeji mkataba wa kufua umeme na kampuni feki ya Richmond Development Company na baadae kuunganishwa na Tanesco".

"Dowans na Richmond-kampuni iliyopewa mkataba kwa upendeleo huku ikiwa haina fedha, utaalamu wala historia ya kufua umeme zilibadilishana mkataba Desemba 23, 2006 kinyume na sheria ya nchi".

TZ Daima: Wanadai kuwa majaji walitamka kuitambua Richmond kuwa ni kampuni halali kwa mujibu wa sheria za Texas, Marekani.
Kuita Richmond kuwa ni kampuni hewa ilikuwa ni kosa la kutafsiri isivyo sheria za Texas".
..."tofauti hiyo inafanya maneno aliyoyatoa katibu mkuu wa CDM Dr. Slaa kuwa na maana kubwa . Dr. Slaa alitaka uchunguzi wa kina ufanywe kuhusu jambo hili na akafikia hatua ya kusema kuwa iwapo kamati kuu ya bunge ilisema uongo kuhusu uhalali wa Richmond basi hatua zinapaswa kuchukuliwa".

"Hata hivyo ICC katika ukurasa wa 41 inasema taratibu za kuhamishwa kwa mkataba kutoka Richmond kwenda Dowans zilizingatiwa kwani ziliridhiwa na Tanesco".

Mwanahalisi:

"Karamagi aliificha taarifa muhimu menejimenti ya Tanesco kuhusu Richmond kuhamishia mkataba wake kwa Dowans. Kifungu cha 15:12 cha mkataba kinasema kuwa kabla mkataba kuhamishwa ni lazima Richmond wapate ridhaa ya Tanesco, tena ya maandishi, Karamagi alipuuza hilo".

"Balozi Kazaura (M'kiti Tanesco) anathibitisha katika mahojiano yake na kamati teule ya bunge kuwa alimweleza Karamagi hilo linawezekana pande zote zinaporidhia. Karamagi alifanya hayo November 28, 2006 lakini kumbe tayari tarehe septemba 25, 2006 mkataba ulikwisha kuwa umehamishwa kutoka Richmond kwenda Dowans".

My Take: Hebu tuangalie japo kwa ufupi mitazamo ya magazeti hayo mawili na kile ambacho wanataka wananchi tuamini.

Karibuni...
 
masele eti apinga kulipwa dowans! mh! kweli kuna watu wanadhalau sana. wewe masele umechakachua matokeo kwa msaada wa riz1 na baba yake na kuwapiga mabomu wananchi hovyo. umeona hiyo ndo sabuni enhe? shinyanga hawakutaki kabisa, umesahau siku ile msibani?
 
According to the Tanzania Business Registration and Licensing Authority (BRELA) and the list released by the Ministry of Energy and Minerals the share holders of Dowans as: Mr Andrew James (Canada), Gopalkrishnan Balachandran (India), Hon Sung Wao (Singapore), Guy Arthur Picard (Canada), Suleiman Mohammed Yahya Al Adawi (Oman). Brigadier Yahya at sometime ago denied knowledge and being a shareholder in Dowans.

None of the listed shareholders was a Tanzanian national raising concern whether it was proper in the laws of Tanzania for a foreign company to register as a local company in Tanzania without having any single Tanzanian national as a shareholder.

Surprising further is that the records indicate that the case was between Dowans (SA) and Dowans (T) Ltd vs the United Republic of Tanzania but the beneficiaries of the award will be Dowans SA (Costa Rica) Ltd. Costa Rica is widely known as one of the safe Havens in the World, hosting a number of off shore companies whose business transactions are difficult to scrutinize.

The Costa Rican Authorities have so far said Dowans is not a registered company in Costa Rica. In a letter sent to the Tanzanian Parliament in June 2008, Mr Marianela Jiminez, the Attorney General of Costa Rica said there were no records to show that Dowans (SA) was registered in Costa Rica

The emerging question amongst the public has been why was it not clear right from the start that Dowans had an of shore subsidiary? Was this off shore subsidiary legally registered or finally registered recently, in anticipation that the award would go in their (Dowans favour) and to avoid public scrutiny and ambits of the law? Could there be some Tanzanian interests in the Company which did not want to be divulged and explaining why it had to be registered in Costa Rica? All these are questions that have caused anger and stirred further concerns about the ICC ruling and final decision for government to pay

To seal off the case, the ICC argues that Tanzania has been happy to submit to the authority of International Arbitration for the following cases

• Tanesco Vs IPTL (awarded in favor of Tanesco)
• Bi Water Gauff (Tanzania) Vs United Republic of Tanzania (Awarded in favour of United Republic of Tanzania)
• Richmond Development Company/RDevco vs Tanesco (Awarded in Tanesco’s favour)

“On the same basis of the above, the international Arbitral Awards, the Arbitral Award must also be respected”, the ICC rules

This anti corruption tracker system is supported by the Embassy of Finland and the Swiss Agency for Development and Cooperation (SDC)
You can obtain more information about AP200 by clicking on its website http://www.agendaparticipation.org/ or download more details here

People behind the Corruption Tracker System (CTS)
 
Haya Wananchi ukweli si unakuja sasa...tutaona kama Bunge alitajadili na kwanini. Hii ni criminal act thats it na watanzania twendeni Mnazi Mmoja Square kuwalazimisha wote serikali ya CCM waondoke Tanzania. Milion March Please njooni tushikane mikono na kuimba nyimbo za kuipenda Tanzania mpaka JK/Pinda na CCM waondeke....
 
Rostam Aziz has the Power of Attorney to transact on behalf of Dowans. Please get the copy of the last weeks East African.
 
Siku zote tumekuwa tunataka kumjua Mmiliki rasmi wa DOWANS hapa nchini. Mwakyembe amemtaja waziwazi katika semina ya wabunge wa ccm Ubungo Plaza. Kana kwamba haitoshi, jana gazeti la Mwana Halisi limeweka bayana kabisa kwa kuonyesha nakala ya document ya kwamba bwana RA ni mmiliki halali wa kampuni hiyo. Sasa swali ni je tumfanye nini huyu jamaa? Toa maoni hapa!
 
Kwani kama serikali imemshindwa si tuamue kuwatimua kazi kama misri na Tunisia.
 
Kwani kama serikali imemshindwa si tuamue kuwatimua kazi kama misri na Tunisia.
Wazo zuri sana, kama tulowapa kazi wameshindwa basi tuwatimue.... si jukumu letu sisi kumkabili bali serikali!!!
 
Hii story waliweka kwenye Mwana Halisi pia. Pamoja na barua ya wanasheria.:clap2: Hongera media kwa hio
 
Tuandamane kama walivyofanya Tunisia na Misri sasa hivi,ili tuondoe utawala dhalimu na dhalili wa kina JK.Ngeleja,Makamba,Tambwe,Msekwa na wengine kama hao.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom